Uchaguzi 2020 Wingi wa wagombea CCM ni uthibitisho kazi nzuri ya Rais Magufuli kwa taifa letu. Je, Oktoba ni kuchagua au kuthibitisha tu taratibu?

Uchaguzi 2020 Wingi wa wagombea CCM ni uthibitisho kazi nzuri ya Rais Magufuli kwa taifa letu. Je, Oktoba ni kuchagua au kuthibitisha tu taratibu?

Siasa za Magufuli ni sawa na kocha anayefundisha mfumo wa kupack basi. Mchezo wa aina hiyo unaboa sana. Ndio maana kwa sasa siasa zetu ni so boaring.

Katika mazingira haya ndio hapo unapoona kundi la kubwa la upande mmoja, maana ushindani halisi haupo. Sidhani kuwa ccm ni imara au inakubalika sana, bali siasa zenye ushenzi, uhayawani na ukatili wa wazi, umefanya chaguzi zetu kuondoa ushindani halisi, na kuleta ushindani wa kujipendekeza kwa rais. Matokeo yake, kila anayeona anajuana na rais kwa namna yake, anajitokeza kutaka kuchaguliwa kugombea uwakilishi.
 
Wakuu yaani kila ninayemfahamu anaona anaweza kuwa mbunge kupitia CCM.

Niko na mdogo wangu hapa ananiambia hata yeye anaona kama anaweza kuwa mbunge wa CCM mwaka huu akiamua wakati hajui hata Polepole ni nani au katibu mkuu wa CCM ni nani.

Maana kila mtu anaona anaweza.

NINI MAONI YAKO.

1: Je, Ubunge umerahisishwa sana wakati huu?

2: Je, CCM Imekuwa safi kiasi kwamba hakuna hata wasio na pesa nao wanaweza kupita kuwa wabunge?

3: Je, Ubunge Watu wanatamani kufanya kazi na Raisi ajaye ikiwa mwenyekinti wa CCM atashinda?

Nini maoni yako

Kwa sababu rais anatumia madaraka yake kuharibu demokrasia, na anaweza kunajisi box la kura, kila anayejua ana ukaribu na rais, au anaimba mapambio ya rais, anaona anaweza kuwa muwakilishi.
 
Siasa za Magufuli ni sawa na kocha anayefundisha mfumo wa kupack basi. Mchezo wa aina hiyo unaboa sana. Ndio maana kwa sasa siasa zetu ni so boaring. Katika mazingira haya ndio hapo unapoona kundi la kubwa la upande mmoja, maana ushindani halisi haupo. Sidhani kuwa ccm ni imara au inakubalika sana, bali siasa zenye ushenzi, uhayawani na ukatili wa wazi, umefanya chaguzi zetu kuondoa ushindani halisi, na kuleta ushindani wa kujipendekeza kwa rais. Matokeo yake, kila anayeona anajuana na rais kwa namna yake, anajitokeza kutaka kuchaguliwa kugombea uwakilishi.
Wanaandaliwa wawakilishi wa rais.
Sisi wananchi hatuna mwakilishi hata tukipiga kura.
 
Ndugu yangu Pascal Mayalla, umeshakuwa mtu mzima sasa, jalibu kusimama kwenye ukweli na siyo kuleta Siasa kwenye mambo ya msingi, ili hata kizazi chako kiweze kukukumbuka, ukweli ulio wazi ni kwamba maisha yamekuwa magumu na ajira hazipatikani ndo maana unaona foleni ya watia nia kugombea nafasi za ubunge mfano kina Gwajima hata sadaka hawapati tena.

Ndugu Pascal Mayalla,unakumbuka miaka mitatu au minne iliyopita,Uhamiaji walitangaza nafasi za kazi 80 kama sijakosea,watu walijitokeza kwenye usaili walikuwa elfu 12, ikabidi waende kufanyiwa usaili kwenye uwanja wa Taifa.

Hata wewe unashinda kwenye mitandao na kusifia chochote hata kama ni kibaya,sababu unatafuta ajira /uteuzi kutoka kwa wale unaokesha kwenye mitandao ukiwasifia.
 
Kaka ingependeza ukaweka angalizo kuwa haya ni maoni yako binafsi. Wapo wanaosema kuwa sababu za makada wengi kujitokeza kuchukua fomu nikutokana na sababu zifuatazo:

1. Khali ngumu ya maisha tofauti na siku za nyuma kabla ya JPM kuchukua nchi mfano. Manabii wengi wa makanisa walikuwa wanaokota hela tu kupitia sadaka (aliyekuwa anatoa sadaka 10,000) leo anatoa (1,00 au 500), Wakuu wa mikoa walikuwa kama wafalme hawakuwahi kuishi kwa kutegemea mishahara walikuwa wanapokea bahasha za kumwaga kutokana na mzunguko mkubwa wa pesa uliokuwepo (Ndio maana wengi wao sasa hivi pamoja na Mkwara wa Jiwe wameona ni bora kuachana na kazi hiyo kuliko kuendelea nayo). N.K...

Pia kuna Wazee wengi walishataafu baada ya "kupiga" saana kupitia miradi mbali mbali wakawa wamewekeza sehemu mbali mbali lakini kutokana na kupungua kwa mzunguko wa pesa sasa hivi miradi yao imekufa na ndio maana unaona sampuli za kina kimei, Kapuya, Wasira E.t.C zikirudi.

Kwa hiyo Mkuu kila mtu anaelewa kuwa Ubunge ukishaupata unahakika wa kupata mamilioni ya pesa bila kujali athali zozote za uchumi zitakazojitokeza. Mwisho usisemeni CCM tu angalia hata vyama vya upinzani kama chadema mwamko umekuwa mkubwa kuliko 2015 kwa mfano wanawake wametijokeza kwa winga saana.

2. Sababu ya Mwiho ni watu kutotambua hasa majukumu ya Mbunge na kuona kuwa ni kazi rahisi ambayo mtu yoyote anaweza kufanya (Chukulia sampuli za kina Msukuma, Lusinde,Martha Mlata, Lijuakali) eti nao ni wabunge....ndio maana hatak akina steve Nyererre wamechukua fomu.

3. Mwisho kabisa wengine wachache ni kutafuta umaarufu na kujipendekeza....ili wazi wakijua hakuna dalili za kupita
 
Wanaounga mkuno juhudi za Mh. Rais ni wale walioamua kufanya kazi (hasa za uzalishaji) kwa bidii, weledi na uaminifu kwa ajili ya maendeleo ya taifa. Watia nia wote ni watafuta umaarufu na wachumia tumbo tu.

Nafasi za uongozi kama Ubunge, Udiwani
Watia nia wote wanalilia matumbo yao hawaipendi CCM bali nafsi zao binafsi
 
Bwana yule kaharibu sana mifumo ya hii nchi na kajigeuza Mungu mtu,na matokeo yake sasa kila mtu anamlamba miguu maana maamuzi yote ni yake baada ya kuvuraga demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa kuanzia kwenye chama chake na nchi nzima kwa ujumla
Rais ajaye anakazi kubwa sana! Itabidi tumsamehe kipindi cha miaka ile mitano ya kwanza hata asipofanya maendeleo yoyote! Ana kazi ya kurejesha mifumo kama ilivyo kwenye kanuni za uongozi wa nchi! Watanzania tumeamua kumwachia mtu mmoja ndiye aamue mwelekeo wetu kama taifa na katika hili wala hatujiulizi je mtu huyo tunayemwamini ana akili timamu? Watz ipo siku tutatumia akili ya taahira!!
 
Back
Top Bottom