Uchaguzi 2020 Wingi wa wagombea CCM ni uthibitisho kazi nzuri ya Rais Magufuli kwa taifa letu. Je, Oktoba ni kuchagua au kuthibitisha tu taratibu?

Kwa uelewa wangu kwamba ugumu wa maisha ndio unapelekea watu wote hawa kuchukua fomu.
Wengi wamechukua fomu ili kujitafutia maisha. Siasa imekuwa Kama kazi ya kutafuta maisha.
Wengi wanajua hata wakikosa ubunge basi watapata teuzi nyingine.
 
Ni kuthibitisha na kutoahaki ya kiraia ya kupiga kura tu.mpaka sasa kwa kazi nzuri za JPM keshashinda kwa kishindo. wabunge wa CCM mwaka huu ni more than 95%.
Nadhani itakuwa vyema wabunge wote (100%) wakiwa CCM maana hapatakuwa na visingizio tena kama vile tunavyowaaminisha wananchi kuwa vyama vya upinzani vimetawala kwa zaidi ya miaka 50 na kuipisha CCM mwaka 2015. Hamna kuhoji bajeti au muswada wowote utakaoletwa na serikali. Itapendeza zaidi kama wabunge wetu watapitisha muongozo kuwa hamna haja ya kusoma bajeti kwa vile wote wanajua matokeo yake.

Amandla...
 
Urais na ubunge vinaingiliana vipi? Napatafuta sana
Urais na shughuli za serikali zinambeba rais na kurahisisha kura zake kwa wenye akili ndogo ambao ni wengi tanzania hivyo Magu atashinda
Ubunge watu hawaangalii serikali imefanya nn bali wewe umefanya au unataka kufanya nn

Mbunge kazi yake ni kuongea na rais kazi yake si kuongea bali kutenda. Hivyo kwa sasa rais wetu ni domo na mtendaji ndiyo maana bunge likakosa umaarufu

Paschal tuelewe kuwa fomu nyingi za kijan kunaonyesha kuna tatizo mahali hasa ktk mfumo wa bunge
Pia inaonekana ubunge ni ulaji kama ilivyo awamu hii ya tano kuwa uongozi ni zawadi si dertemination binafsi pamoja utumishi kwan awamu hii imetuaminisha hata elia F michael naye anafaa kuongoza watz au hassan ngoma au malaya jokate mwegelo aliyesifia uume wa hashimu kwa mapaparaz na leo ni mfano wa kuongoza
Ccm ya kale ilijua ndiyo maana wabovu walifichwa kwenye viti maalum kama malaya sofia simba nk

Bunge ni mahali pa kuzungumza changamoto za taifa si kusifia yaliyofanyika na ndiyo maana ya kutunga sheria au kupitisha bajeti au kushauri na kuisimamia serikali

Watz wenye akili ndogo ambao ni wengi wanadhan mbunge ndiye mtendaji kumbe kaz yake n kubwabwaja tu

Paschal angalizo lako linathibitisha ninyi ni mafisi ambao mmesikia upishi mahali na chakula mahali kwa uroho unataka vyote ili ulianza kupika huku ukute kule chakula hakijaisha upakuliwe ule

Mafisi ninyi nenden mkajipoteze


Kuna shida mahali binfs nimejaribu kulitafuta
 
Pole sana,
Kutokana na udhaifu uliyokomaa wa mtoto 'aliegoma kukua' kwa sababu ya kutegemea sana dola, mnaiogopa sana na kuichukia TUME huru.
Mnaogopa DEMOCRACY na uhuru wa waTz katika kuamua mambo yao/siasa kwa haki na bila aibu kujitahidi kuupulizia 'perfume' udikteta uliyo wazi kabisa.
Mmekuwa na kelele nyingi za mapambio na kuabudu kuliko kujitahidi kutoa hoja za msingi.
Kama kibatali kinachotoa joto jingi kuliko mwanga, ni dhahiri kuwa hamfai mmekosa mvuto. Na kama kisingekuwa pia kinatoa moshi mwingi labda kingeweza kuonekana kinafaa angalau kwa kupikia, wakati wa mwambo.
Tutaonana oktoba, hamtaamini yatakayowakuta.
AMEN.
 
Subiri tu ukuu wa wilaya kwa sasa bwana Mayalla.
 
Wingi wa wagombea unatokana na kuona ubunge ni dili na pia JPM ameonesha kuuchukia upinzania na kuvifanya vyombo vya dola na taasisi za serikali kuipendelea CCM. Kwa hiyo, atakayeshinda kura za maoni CCM - ana uhakika wa kufanyiwa kampeni na CCM, Polisi, Tume ya Uchaguzi!!

Paschal, umesahau teuzi katika serikali za 2016 asilimia 95% ilikuwa ni walioshindwa katika kura za maoni na uchaguzi 2015??
 
Una tatizo la ubongo...si bure dada
 
Twende na Link hii ili tujadili michakato yote majimboni kwa upana zaidi...
Karibuni.
🇹🇿MCHAKATO⚖️MAJIMBONI 2020🇹🇿
 
Bwana yule kaharibu sana mifumo ya hii nchi na kajigeuza Mungu mtu,na matokeo yake sasa kila mtu anamlamba miguu maana maamuzi yote ni yake baada ya kuvuraga demokrasia ya kuchagua na kuchaguliwa kuanzia kwenye chama chake na nchi nzima kwa ujumla
Hata yeye mwenyewe aliteuliwa na m/kiti aliyepita na kuwaacha hata marafiki zake. Hiyo siri ameitoa juzi tu. Sisi tulijua wanapita kwa kura na hoja lakini kumbe ni m/kiti ndio anateua nani ashike nafasi. Hivyo tusitegemee kura zetu katika kuchagua, kwa sababu kuna kauli na maamuzi ya m/kiti vina nguvu kuliko kura.
 
Kipimo cha kazi nzuri tungepima sisi wapiga kura kwa kuruhusu wanachama kuchukua fomu na kusubiri mchujo. Lakini fomu imetoka moja tu ya m/kiti. Hii maana yake ni kwamba m/kiti amesha pita kilicho baki ni maamuzi tu nani na nani wakae katika nafasi gani kwenye ubunge na udiwani. Na mfano wake tumeona kwenye uchafuzi wa serikali za mitaa.

"Swali ni jee uchaguzi wa October ni uchaguzi wa kuchagua kwa kushindanisha vyama au kushindanisha wagombea".
Jibu ni hapana, kwa sababu uchaguzi unafanyikia maofisini kwa wakubwa, huku nje kwa wanyonge tunaletewa uchafuzi ili wajihalalishie uovu wao.

"sio kila anayejitokeza kuchukua fomu kugombea ubunge au udiwani kupitia CCM, yuko very serious ".
Ni kweli na hilo tumeliona sio tu kwenye kuchukua fomu, bali hata waliokuwa wabunge wa CCM tumeona waliyo yafanya wakiwa mjengoni. Na watakao ingia baada ya uchaguzi hatutegemei miujiza zaidi ya kile tunachokijua.
 
Wana jamvi wasalaam!

Kumekuwepo na utitiri wa "wana CCM" kutia nia kugombea nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi huu ujao wa 2020. Tafakuli fikirishi ya hao "wana CCM" JE ni kweli wako serious au wala lao jambo?

Baada ya Uchaguzi wa 2015 kila mtu alishuhudia kilichotokea, baada ya bwana mkubwa kutangazwa kashinda kilichofuatia ni teuzi za watia nia wa wakati huo kuteuliwa haswa haswa kwenye posti za DED na DAS.

Nadhani opportunists wameshasoma mchezo wa uchaguzi uliopita hivyo wameamua kuweka CVs zao kwa bwana mkubwa ili nao wafikiriwe kwenye posti hizo.

Trend hii ya ukada kupewa kipaumbele kwenye teuzi especially watia nia ukiwa unaona mbele itakuwa na matunda yake very soon! Na nadhani dalili ya maua ni suala hili la watia nia, bado kidogo matunda yataanza kudondoka!

Walio serious kugombea huenda wapo ila waliowengi ni wa kusubmit resumes!

Tukae tusubiri
 
Pelekeni tuu CV zenu ili ziwekwe kwenye data base ya serikali ambayo itakuwa na Rais ajaye ambaye sio ccm. You know what's next? tutakapotaka kujaza nafasi za utumishi basi tuna click tuu na jina lako likitokea basi maombi yako yana hifadhiwa kwenye dustbin.
Kifupi mnapaswa kuwa blacklisted kwani msije leta utendaji wa fitina za awamu ya tano.
 
Kama demokrasia ingekuwa imekuwa wasinge print copy moja tuu ya kugombea nafasi za "kuongoza vyombo vya dola" eti kwa uhaba wa karatasi.
Wangeweza kuwaambia watia nia waje na karatasi zao wenyewe.
 
Nchi hamjapewa mshatangaza visasi....!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…