Wito kwa Serikali yetu, Huu ni Udhalilishaji wa Bullying & Intimidation. Mbona Rais Samia Hadhalilishi? Tusiruhusu Udhalilishaji Huu Uendelee!

mtu yeyote mwenye akili atakubaliana na hiki alichoandika pascal.
 
Bully iko wapi hapo...
Unajua maana ya bullying? Nimeshindwa kuelewa huu mgogoro ulitoka wapi? Mbona Injinia alikuwa anaelezea vizuri tu? Shida ya zero brain hatoi muda wa kusikiliza! Serikali iliondie hili takataka kwenye utumishi wa umma! Pasco uko sahihi, wenzetu wako mbali sana kwenye kukemea udhalilishaji. Hata mimi niliwahi kufanyakazi kwenye taasisi ya Kiingereza wako vizuri sana kwenye mambo ya safeguarding! Sasa hii punda inamdhalilisha mtumishi mwenzake mbele ya kadamnasi, halafu na watumishi wa umma nao wapuuzi tu eti wanashagilia! Kikao kilitakiwa kinune mwanzo mwisho mpaka zero ajione mjinga!
 
Watanzania inabidi wapelekwe hivi hasa huko serikalini. Ikiwezezekana zaidi ya hapo itapendeza sana. Huku private sector mziki ni mkubwa sana zaidi ya hapo na mambo yanaenda. Uliza kwenye kampuni za simu watu wanavyohenya. Maendeleo hayaji kwa kufanya kazi kimwinyi. Huko ulikofanya kazi na wazungu nina uhakika kuna namna ya kuangalia performance na goals za kila mfanyakazi. Usipokidhi vigezo utashughulikiwa kwa namna ambayo hata bullying ina nafuu. Makonda hatumkubali lakini shetani naye akisema ukweli, ukweli unabaki pale pale
 
Wewe nawe!
 
Huyo ni sikio la kufa tu.
 
Mkuu jitahidi kuandika Kiswahili angalau na sisi huku tuzielewe hoja zako vizuri. Ni ombi tu. Shukran.
 
Pascal Mayalla kwa heshima nadhani umekuwa too emotional na hujatumia muda kutafakari kabisa. Dkt Samia mwenyewe alishatukana stupid! Upande wa uongozi kuna ombwe kubwa sana hasa hivi vyeo, ndiyo maana tunahitaji katiba mpya watu washindane, na kusema eti kadhalilishwa hapa huyo manager ni boya kabisa. Makonda yupo sahihi kwa sababu tungekuwa na utaratibu wa kushindanisha the best ndiyo wangekuwa viongozi. Kwa hiyo sikubaliani kabisa na mtizamo wako and I believe wengi hatukubaliani na wewe kwa huu mtizamo.
 
mtu yeyote mwenye akili atakubaliana na pascal. alichofanya makonda ni kitu kibaya kabisa na udhalilishaji kwa mtu mzima. angelikuwa hata na adabu ya kulelewa tu asingefanya vile, ila sote tunamjua makonda alivyo, shida ndio hiyo.
 
mtu yeyote mwenye akili atakubaliana na pascal. alichofanya makonda ni kitu kibaya kabisa na udhalilishaji kwa mtu mzima. angelikuwa hata na adabu ya kulelewa tu asingefanya vile, ila sote tunamjua makonda alivyo, shida ndio hiyo.
Mi nakubaliana na Makonda huyo manager boya hata ningekuwa mimi nigefanya hivyo hivyo. Inakuwaje ashindwe kujielezea????? Tatizo inasemekana watu wanapeana vyeo either mtu wa mfumo au hela etc bila kujali vigezo. Kikubwa tuwe na katiba mpya na nafasi zote kubwa watu wafanyiwe vetting pawe na pool the waitwe interview. Lakini leo hii unakuta anatauliwa kiongozi kisa tu katoa rushwa kwa mfumo au kujuana, haya ndiyo matatizo. Mi namuunga mkono Makonda mpaka dakita ya mwisho. Ila wewe kama ni kiongozi ulihonga au ulipendelewa kupata cheo hautaelewa bosi au wewe kama ni mfumo ila sisi watoto wa masikini tunaobangaiza tunasikia tu mpaka unajiuliza hivi huyu anakuwaje kiongozi????
 
Suala la Udhalilishaji chini ya Utawala wa CCM mbona ni jambo la kawaida sana, nothing new!

Kwani hawa mawakala wao ambao wamewajaza sehemu mbalimbali mijini na vijijini kwenye Vijiwe vya Kahawa, Vijiwe vya kubrashi viatu, Vijiwe vya Kucheza Pool Table, n. k, n.k wamekuwa wakifanya kazi gani humo kwenye Vijiwe Kama siyo kueneza Propaganda za Kudhalilisha watu??? Wewe Unafikiri Serikali huwa inafanyaje Propaganda Chafu za kuwachafua watu ambao wanawaona kuwa ni maadui wa utawala uliopo madarakani? Je, Unajua kitu kitakachoitwa 'Characters Assassination and Smear Propaganda Campaign' ? Black Propagandas??
FYI: Hao watu wengi Sana ambao wamewajaza na wamezagaa kwenye Vilinge vingi sana vya Kahawa, Vilinge vya kubrashi viatu, Vilinge vya Kucheza Pool Table, n.k wamewekwa hapo makusudi ili waweze kufanya kazi hii ya bullying dhidi ya watu fulani fulani, hususani Wakosoaji wa Serikali au watu ambao wanaonekana kutishia maslahi yao.
 
kwamba hapo ungeweka tu katiba mezani projects zingejikamilisha zenyewe, right?🐒
Katiba mpya itatusaidia kuweka ukomo kwa mamlaka za hawa wanasiasa. Na pia tutaondokana na huu mfumo wa kuwa na wakuu wa mikoa,na wilaya.
Yaani katika hali ya kawaida,kwa jinsi makonda alivyokuwa anataka hao wakurugenzi waongee,inaonekana wazi kuwa anafanya siasa,anafanya kampeni..
Kwa ufupi hicho kikao hakina tija.kuna vikao vya baraza la madiwani,kazi yake ni nini?
 
watu huwa wanashindwa kujieleza kwa sababu nyingi sana. kuna siku yatakukuta na utaelewa hili. inaweza kuwa kuna siri kubwa ya serikali kuhusu ulichoulizwa na kimaadili huwezi kukisema pale kwenye kadamnasi, au kuna jambo la hivyo na ulijaribu kulificha kwa maslahi ya uma, au pengine wee ni interovert wa kuzaliwa, umeubwa hivyo, unatenda kuliko kuongea, kama walivyo extrovert wengine wanaongea kuliko kutenda. kuna mtu ukimleta hapa aongee hata jambo la uongo atakuconvince, mwingine hata jambo la ukweli atashindwa kulieleza ila ni professional, ukiweka kuongea pembeni anafanya kazi kwa ufanisi kuliko huyo mwongeaji. wanadamu tunatofautiana, wengine wanaweza sana kuongea kwasababu ya malezi, and vise verse is true.

kuna watoto wamelelewa na single mothers, au yatima, au aliugua sana akaumia moyo akawa mpole, au kuna jambo limemuumiza maishani akajikuta mpole sio muongeaji. ukiwa mtawala jua utatawala watu wa aina hizi zote, na uwachukulie kila mtu kama alivyo kwa faida ya taasisi kwasababu sio waongeaji vizuri wote ni watendaji wazuri, na sio wasiojua kuongea wabovu.
 
Ila wabongo kiboko asee dah!

Leo hata wewe NJAA unasimama kwa ukali unamsema Magu?

Kweli mtu ukifa unakufa na yako yote. We si ulikuwa mmoja wa timu chawa pro wa kusifu na kuabudu kila kitu
mbona hyo thiead ya kumuhusu magu na hyo mmama ni ya 2017 mkuu, au magu alishafariki tayar, au kuweka hyo kumbukumbu ndo shida?
 
Sidhan kama Magu angekuwa hai Mayalla angeandika hii
mbona aliandika hata kabla magu hajafa, mayalla pekee ndo alikuwa na ujasiri wa kumuuliza magu swali pale ikulu kuhusu magu kuvunja katiba kwa kuingilia utendaji wa mihimili mingine, wengine waliishia kuomba matangazo na wine walipopewa nafasi ya kuuliza swali, na magu alivokuwa mshenzi kabla ya kujibu akasema mayalla ni NJAA.
 
makonda alimdhalilishaga piere likwid pale mlimani city, akimuita mtu wa hovyo hovyo, niliyaona maumivu ya piere wakat wa ule udhalilishaji, na makonda alimdhalilisha piere kisa tu alihisi piere anapata umaarufu kwa kasi sana. sasa kama rc mzima unaweza mdhalilisha petty comedian kama piere hadharani we ni kiongozi au takataka tu? kuhusu chongolo Chakaza kaweka na clip kabisa

baada ya hapo piere alipewa nafasi ya kusafiri na wabunge kwenda misri kama sijakosea kama sehemu ya wahamasishaji (pm ndo aliomba hyo nafasi), (hli jambo pia lilimuudhi kocha fulani na akaongea shombo kuhusu piere)

hv piere aliishiaga wapi wajameni?
 
Kaka niliishawahi kukwambia huyu mtu hafai, ila hatufahamu ni kwanini anapata hivi vyeo, alipaswa apewe kazi lakini siyo mamlaka makubwa kiasi hiki. Aliisha jiona ni Mungu mtu, haonyeki hasikii la yeyote kwamba yeye yuko juu ya sheria za nchi hii.

Anatafuta kuwa kwenye national level politics lakini hana sifa hizo, anapoteuliwa na kiongozi mkuu wa nchi anajiona yeye ndiye mkuu kuliko aliyemteua.

Tulimuona tangua alipokuwa mkuu wa wilaya kinondoni, akawa mkuu wa mkoa Dar es Salaam, alikuwa ana fanya drama kila siku ilimradi tu aandikwe magazetini na mitandao ya kijamii kama hivi.

Haya anayoyafanya, angeweza kuya fanya in closed door, akaongea na viongozi wa idara zote za mkoa bila kumdhalilisha mtu yeyote, lakini aliisha dhiirisha kwamba yeye anapenda kudhalilisha watu/binadamu wenzake, aliondolewa uenezi, lakini bado anadhani yeye pekee ndiye mkuu wa mkoa. Nili uliza nchi hii ina mikoa mingapi, hajifunzi kwa wenzake?

Juzi hapa tuliona anaombewa na viongozi wa dini mbali mbali akiwemo Kardinali Pengo, nikauliza kuna tatizo gani au yeye ni special sana kuliko wakuu wa mikoa mingine?

Labda arudishwe huko chamani huku serikalini hatufai. Ingawa pia tunafahamu vyama vya siasa ni mali ya umma lakini huko wengine wasio wa chama hicho wanaweza kumpuuza.

Apewe kazi lakini asiwe mkuu wa mkoa, wilaya, hata kata. apewe kazi naye apimwe na wakuu wa mikoa,wilaya na viongozi wa idara.

Nashangaa sana kuna watu hata wana diriki kusema eti agombee urais, sijui atakuwa vipi?
 
Kuna kitu wazungu hujifunza kuhusu tamaduni ngeni.

Mfano profesa Joseph L. Mbele ktk kitabu chake cha 'kusomana tamaduni' anasema wazungu wamefundishwa kuhusu utamaduni (umuhimu wake ktk asili ya mtu) wasishangae wakiona mswahili amebeba jogoo ndani ya basi kwa kuwa mswahili naye hushangaa mzungu kupanda basi na mbwa wake

Kuna vitu tunafanya wanakuangalia tu moyoni wanatamani wakuchapa mijeledi kama alivyofanya Jerumani kwa mababu zetu ili kuturudisha katika reli jinsi wanavyofikiria wao lakini wazungu hao wanarudi hatua moja nyuma na kukumbuka huyu jamaa mswahili fikra, mazoea na matendo yake yameathiriwa sana na tamaduni zake za asili za kiafrika tumuache kama alivyo.

Peasants of the Empire. Rural Schools and the Colonial Imaginary in 1930s French West Africa​

Harry Gamble

Ila mheshimiwa Paul Makonda anafanya kitu kinaitwa a big conversation / brainstorming yaani mkutano wa wazi kabisa na waswahili wenziwe ambao ungeweza kufanyika chini ya mwembe au ukumbi wa kisasa wa AICC ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa changamoto za matatizo.

Kwa kujaribu kuongea kwa uwazi wapi tunakwama ili kutafuta 'kufahamiana' na kujenga fikra pia mtazamo mpya wa ushirikishwaji viongozi na umma tuwe tuna fikiria sawia kufikia malengo maana inaonekana viongozi na umma kila mmoja yupo ktk dunia yake tofauti na kwa namba hiyo ni ngumu kufikia malengo au matamanio kama jamii kubwa.

Dola yoyote kubwa kama ya China, Uingereza, USA, Japan, Byzantine, Ottoman, Greek Empires ziliweza kupiga hatua kwa kuwa na watu wenye uwezo wa kujiuliza wamekwama wapi kama jamii kubwa na nini kifanyike kama jamii moja.

Na ndiyo maana dola hizo zikaanzisha shule, madrasa, Sunday school n.k ili kuifinyanga akili ya watoto wa jamii yao kufikiri sawia kutatua matatizo na changamoto ktk dola zao. Shule za dola za kikweli nilizotaja hapo awali paragraph ya juu hutumia shule kama kifaa cha social engineering / kuondoa tofauti ya maono ili kwa umoja wao waweze kufikia malengo au utatuzi wa changamoto.


Paul Makonda anatumia njia hiyo hiyo ya elimu haina mwisho kwa kufanya mkutano wa wazi wote kujifunza ikiwamo yeye na kujaribu kufanya mapinduzi ya kifikra yanayokubalika kwa pamoja baada ya mjadala mpana ili mafanikio yapatikane.
 

Pasco...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…