Wito kwa Waziri wa Elimu: Shule zishindanishwe/zitengwe kulingana na mazingira ya utoaji elimu

Wito kwa Waziri wa Elimu: Shule zishindanishwe/zitengwe kulingana na mazingira ya utoaji elimu

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Sijui kama ni makusudi au uvivu wa kufikiri, au kuamua kuishi kwa mazoea. Kila mwaka baraza la mitihani wanakuja na majina ya wanafunzi na shule bora katika matokeo ya mitihani ya ngazi tofauti.

Kinachosikitisha ni kwamba kuna utofauti mkubwa sana wa mazingira ya utoaji elimu hapa nchini, hali hiyo ya utofauti wa mazingira kwa sehemu kubwa huathiri matokeo ya wanafunzi.

Hili jambo liko wazi sana kwani ukipita kwenye shule zetu utajionea utofauti mkubwa sana wa namna hali halisi ilivyo. Mf kuna shule ambazo unakuta shule ina kila kitu anachohitaji mwanafunzi, yaani idadi ya wanafunzi kwa darasa25-35 maabara yenye kila kitu, madawati ya kutosha, maktaba, waalimu wanapata kila kitu na motisha juu pamoja na wafanyakazi wengine wa kutosha.

Eti unachukua hiyo shule unataka uishindanishe na shule kama ya Goba ambayo dalasa la nne pekee kuna wanafunzi 400, hakuna cha maabara wala maktaba hao waalimu Wana madai na malalamiko hayasemeki.

Ni wazi kwamba hapo hakuna ushindani, ni sawa na kumchukua mtu ukamnyima chakula siku tano halafu unataka akapambane na bondia, kisha akipigwa uanze kumzomea na kumsifu bondia hii sio sawa.

Kama nia ni kuinua hamasa, basi hizi shule zishindanishwe kimakundi ili kila mtu au shule ishinde katika kundi la wenzie wanaofanana mazingira ya utoaji elimu.
 
Goba darasa moja (chumba cha kusomea) kina wanafunzi 400? Hii chumvi!
 
Mfumo wa kibepari ni mfumo wa kinyonyaji na kandamizi.
 
Sijui kama ni makusudi au uvivu wa kufikiri, au kuamua kuishi kwa mazoea. Kila mwaka baraza la mitihani wanakuja na majina ya wanafunzi na shule bora katika matokeo ya mitihani ya ngazi tofauti.

Kinachosikitisha ni kwamba kuna utofauti mkubwa sana wa mazingira ya utoaji elimu hapa nchini, hali hiyo ya utofauti wa mazingira kwa sehemu kubwa huathiri matokeo ya wanafunzi.

Hili jambo liko wazi sana kwani ukipita kwenye shule zetu utajionea utofauti mkubwa sana wa namna hali halisi ilivyo. Mf kuna shule ambazo unakuta shule ina kila kitu anachohitaji mwanafunzi, yaani idadi ya wanafunzi kwa darasa25-35 maabara yenye kila kitu, madawati ya kutosha, maktaba, waalimu wanapata kila kitu na motisha juu pamoja na wafanyakazi wengine wa kutosha.

Eti unachukua hiyo shule unataka uishindanishe na shule kama ya Goba ambayo dalasa la nne pekee kuna wanafunzi 400, hakuna cha maabara wala maktaba hao waalimu Wana madai na malalamiko hayasemeki.

Ni wazi kwamba hapo hakuna ushindani, ni sawa na kumchukua mtu ukamnyima chakula siku tano halafu unataka akapambane na bondia, kisha akipigwa uanze kumzomea na kumsifu bondia hii sio sawa.

Kama nia ni kuinua hamasa, basi hizi shule zishindanishwe kimakundi ili kila mtu au shule ishinde katika kundi la wenzie wanaofanana mazingira ya utoaji elimu.
Strange of you! Kwahiyo unataka wa Goba katika exam grading/ranking yake ianzie na say A=5/100 marks, while that of St Francis A yake ianzie 81/100? AU alternatively wa Goba maswali yao yawe "uji uji" na wa St. Francis yawe magumu kama "Diamond".

Kama ni hivyo Degree zetu or for that matter formal education yetu haipashwi kutambuliwa na Developed world maana Higher learning Institutios za developed world zina kila kitu , world-class materials for learning, imparting knowledge wakati za kwetu ni kama GOBA!

Unaweza ukawa na argument anyway, lkn practicality ya pendekezo lako kwa sentensi yako ya mwisho ni ngumu sana.... not doable!
I stand to be corrected!
 
... tatizo ni kupata vigezo ambavyo ni objective katika kufikia maamuzi ya hicho unachopendekeza. Kigezo pekee kinachopimika ni ufaulu (marks/grades); vingine tofauti na hicho vina a lot of subjectivity! Tutaanza kuzungumzia hali ya hewa ya mahali husika - mikoa kama Iringa na Njombe inatakiwa ipewe consideration fulani kwa sababu kule kipindi cha baridi hata kuandika vizuri wanafunzi hawawezi kutokana na baridi kali.

Wengine akina Rukwa, Kigoma, Kagera, n.k. watataka consideration kwa sababu kule Magharibi mwa nchi asubuhi ya kule bado giza hivyo wanafunzi wa kule hulazimka kuamka usiku sana kwenda shule wakati wa upande mwingine wa nchi muda huo huo kuna mwanga!

Vitakuja vigezo lukuki; hali za kiuchumi za maeneo husika, deturi na tamaduni za mahali, dini, n.k. Hebu pendekeza vigezo vinavyopimika (measurable) ambavyo wizara itaweza kuvitumia kufanya "fair assessment" kama unavyotaka.
 
Strange of you! Kwahiyo unataka wa Goba katika exam grading/ranking yake ianzie na say A=5/100 marks, while that of St Francis A yake ianzie 81/100? AU alternatively wa Goba maswali yao yawe "uji uji" na wa St. Francis yawe magumu kama "Diamond".

Kama ni hivyo Degree zetu or for that matter formal education yetu haipashwi kutambuliwa na Developed world maana Higher learning Institutios za developed world zina kila kitu , world-class materials for learning, imparting knowledge wakati za kwetu ni kama GOBA!

Unaweza ukawa na argument anyway, lkn practicality ya pendekezo lako kwa sentensi yako ya mwisho ni ngumu sana.... not doable!
I stand to be corrected!
Naunga mkono uchangiaji wako, kuwagroup kwenye kundi la shule zinazofanana na Goba nia ni nini haswa au unataka kuboreshaje. Hatuwezi kushusha standards kwa ajili za shule kama Goba wala St Francis, standards should remain the same everywhere. Ningefurahi mtoa mada angezungumzia tunaboreshaje shule zote zifikie kwenye level ya St... au Feza boys. This is challenge to the Gov. Tulipoacha kuajiri waalimu na ku-invest kwenye elimu ipasavyo haya ndio matokeo yake solution ni kuwekeza kwenye elimu period no short cut.
 
Kule chuo hii mada inaitwa Elimu linganishi
 
Sijui kama ni makusudi au uvivu wa kufikiri, au kuamua kuishi kwa mazoea. Kila mwaka baraza la mitihani wanakuja na majina ya wanafunzi na shule bora katika matokeo ya mitihani ya ngazi tofauti.

Kinachosikitisha ni kwamba kuna utofauti mkubwa sana wa mazingira ya utoaji elimu hapa nchini, hali hiyo ya utofauti wa mazingira kwa sehemu kubwa huathiri matokeo ya wanafunzi.

Hili jambo liko wazi sana kwani ukipita kwenye shule zetu utajionea utofauti mkubwa sana wa namna hali halisi ilivyo. Mf kuna shule ambazo unakuta shule ina kila kitu anachohitaji mwanafunzi, yaani idadi ya wanafunzi kwa darasa25-35 maabara yenye kila kitu, madawati ya kutosha, maktaba, waalimu wanapata kila kitu na motisha juu pamoja na wafanyakazi wengine wa kutosha.

Eti unachukua hiyo shule unataka uishindanishe na shule kama ya Goba ambayo dalasa la nne pekee kuna wanafunzi 400, hakuna cha maabara wala maktaba hao waalimu Wana madai na malalamiko hayasemeki.

Ni wazi kwamba hapo hakuna ushindani, ni sawa na kumchukua mtu ukamnyima chakula siku tano halafu unataka akapambane na bondia, kisha akipigwa uanze kumzomea na kumsifu bondia hii sio sawa.

Kama nia ni kuinua hamasa, basi hizi shule zishindanishwe kimakundi ili kila mtu au shule ishinde katika kundi la wenzie wanaofanana mazingira ya utoaji elimu.
Mchango mzuri sana huu kuhusu Elimu. Ila hiyo data ya Goba labda ithibitishwe. Lakini umesema jambo jema sana.

Hii inalingana na maneno ya Mwl Nyerere ktk moja ya hotuba zake kuhusu Biashara huru Duniani. Alisema haiwezekani ktk Mchezo wa Ngumi ukawaweka ktk ulingo mmoja kati ya Heavy Weight na Light , hii featherweight ni "UUAJI".

Nadhani Mamlaka liwafikie hili au watueleze kwanini waliamua kuweka wote pamoja?
 
Ilapswa ifanyike hivyo muda mrefu
 
... tatizo ni kupata vigezo ambavyo ni objective katika kufikia maamuzi ya hicho unachopendekeza. Kigezo pekee kinachopimika ni ufaulu (marks/grades); vingine tofauti na hicho vina a lot of subjectivity! Tutaanza kuzungumzia hali ya hewa ya mahali husika - mikoa kama Iringa na Njombe inatakiwa ipewe consideration fulani kwa sababu kule kipindi cha baridi hata kuandika vizuri wanafunzi hawawezi kutokana na baridi kali.

Wengine akina Rukwa, Kigoma, Kagera, n.k. watataka consideration kwa sababu kule Magharibi mwa nchi asubuhi ya kule bado giza hivyo wanafunzi wa kule hulazimka kuamka usiku sana kwenda shule wakati wa upande mwingine wa nchi muda huo huo kuna mwanga!

Vitakuja vigezo lukuki; hali za kiuchumi za maeneo husika, deturi na tamaduni za mahali, dini, n.k. Hebu pendekeza vigezo vinavyopimika (measurable) ambavyo wizara itaweza kuvitumia kufanya "fair assessment" kama unavyotaka.
Nashukuru kwa mchango wako ambao kwa kweli unaoneokana kuguswa na mada husika hoja yangu hapa inatokana na kwamba serikali itoe mahitaji kwa usawa kwa shule zote ndipo uzishindanishe.

Chukulia wewe ni mzazi unayewajibika kuwahudumia watoto wako kwa usawa, badala ya kufanya hivyo wewe unahudumia mwingine kwa asilimia 100 huyu mwingine hata asilimia hamsini hapati, alafu huyu anayepata kila kitu akifanya vizuri unatoka unampongeza na kumponda aliyefanya vibaya na asiyepata mahitaji kamili.
 
Nashukuru kwa mchango wako ambao kwa kweli unaoneokana kuguswa na mada husika hoja yangu hapa inatokana na kwamba serikali itoe mahitaji kwa usawa kwa shule zote ndipo uzishindanishe.

Chukulia wewe ni mzazi unayewajibika kuwahudumia watoto wako kwa usawa, badala ya kufanya hivyo wewe unahudumia mwingine kwa asilimia 100 huyu mwingine hata asilimia hamsini hapati, alafu huyu anayepata kila kitu akifanya vizuri unatoka unampongeza na kumponda aliyefanya vibaya na asiyepata mahitaji kamili.
... shule za private hazihudumiwi na serikali Mkuu. Tena kama sijakosea, wanalipa kodi tofauti na shule za serikali.
 
Kila mwaka mm imani yangu mwanafunzi anayeibuka wa kwanza kutoka shule ya serikali ndio TO wetu huyo, hawa wengine hamna ktu
 
Wakiongoza akina Mzumbe na Ilboru, hamlalamiki. Shida inakuja wakiongoza akina St. Naniliu.
 
Back
Top Bottom