Wito: Watu Wenye Uwezo, Tujitokeze Tujitolee Kumsaidia TAL na Kuisaidia Chadema to Play Real Politics, No Reforms No Election ni Utopian Politics!.

Nimeshauri mara kadhaa,CHADEMA waende kwenye uchaguzi. Utekelezaji wa NO REFORM NO ELECTION haupo kabisa. CHADEMA haiwezi kuzuia uchaguzi.. ni vioja tu vya kitoto,waende wakapambane kwenye box,na wakalinde kura. Vinginevyo baada ya uchaguzi,CHADEMA itapotea mazima
 
Wewe mtu mmoja unaweza kuvijua na kuvijadili vyote hivyo? Hakuna mtu wa namna hiyo hapa Duniani. Au hujui nini maana ya organization structure?
 
Mkuu CHADEMA ilipata mmbunge mmoja 2020 vipi ilipotea mazima? CCM iliyozoa kura 99% lakini bado inapata wakati mgumu sana kuendesha chama na serikali.
 
Mtaji namba mmoja wa chama cha kisiasa ni wanachama.
Ni watu hao hao wanatofautiana kwa hoja hizo hizo ila wanakubaliana kuheshimu mawazo ya wengine.
Lakini kujifanya inajenga chadema ya walionyoka Lissuism ,nakuapia hata miaka mia lengo hilo haliwezekani
Uongozi mpya msiwe maziwa lala fanya kazi acha mbwembwe za mufilisi.
 
Lucas Mwashambwa , Tlaatlaah , Pascal Mayalla
Natamani kuona hizi constructive criticism muwe mnazifanya na huko chamani kwenu CCM.

Muwe unakemea maovu ya huko pia kuliko Ile tabia ya kusifia kupita kiasi haipendezi.

Nawasiliana Sana pia kila lakheli kwenu.

Kwa Sasa kijijini MPUMBWI.
 
Pascally lisu hahitaji msaada wowote kwa msiomuelewa alichokisema kina baraka za chama na kimeeleweka,

Itakuwa ni ujinga miaka nenda miaka rudi kushiriki chaguzi ambazo mwenyekiti na mgombea urais kupitia ccm ndio anayeteua wasimamizi wa uchaguzi huo huo unakuwa sio utoto tu bali mnaonekana hampo seriously.

Lisu ni mwanasiasa shupavu mwenye uelewa wa hali ya juu wa siasa za Tanzania, sio mlafi wa madaraka sio mpenda rushwa hivyo kuna sehemu anataka waTz tutambue kuwa ccm imetuchezea muda mrefu ikiwemo wewe pascally ndio maana unaona kama alichokisema lisu hakiwezekani.

Vyovyote itakavyokuwa tayari lisu kupitia chama chake chadema ameshachora mstari na ameshafungua uelewa kwa Tz wafahamu tatizo lipo wapi,

Viazazi vitamkumbuka kwa msimamo huo aliouonesha aidha afanikiwe au asifanikiwe
 
Hoja yako haieleweki kabisa,mbona hoja ya Lissu inaeleweka mnaogopa nini kufanya hayo mabadiliko ili kila mtu afurahie kura yake,tunataka uwazi(kama uchaguzi wa chadema).Tunatumia mabilioni kwenye uchaguzi afu mnaleta ujanja ujanja kwenye kuhesabu kura,kuna haja gani sasa ya uchaguzi si mjiweke tu madarakani.Kama viongozi wa nchi wameshindwa kumwelewa Lissu basi tunaongozwa na vilaza sn aisee.
 
CCM ni chama imara na chenye mfumo imara wa kiuongozi. Ni Chama ambacho kwa kila jambo kuna utaratibu wake wa kulishughulikia na kulitatua kwa mujibu wa katiba ,sheria,kanuni, miongozo na taratibu za chama
 
CCM ni chama imara na chenye mfumo imara wa kiuongozi. Ni Chama ambacho kwa kila jambo kuna utaratibu wake wa kulishughulikia na kulitatua kwa mujibu wa katiba ,sheria,kanuni, miongozo na taratibu za chama
Unaona Sasa Lucas ujibuji wako haiwezekani wewe kila Mara uwe ni kusifia tuu.

Kuna muda inabidi ushauri,maoni ,kukosoa inatoa walakini ukiwa YES MAN..

Ni hatari mnoo kua na watu wa ndio..kila kitu jibu ni ndio.

Ngoja niende hapa sehemu nikachangie KODI YA SERIKALI 😊
 
Lakini ukiacha uchawa utaona Samia kabakiza kuuza mlima Kilimanjaro tu,hapo jiulize kizimkazi strategy yao kwenye eneo hili vipi.
Watumishi wanasubiri meimosi kuombaomba kimatonya yule mgogo,kilimo bado tunategemea mvua,matatizo ya kijamii yanayozalisha ukosefu wa ajira yametengenezwa na watawala. Reforms ni lazima.
 
Hakuna mahali popote ambapo Mungu aneagiza tumsamehe Shetani

Lingine usilolijua ni hili, Lowassa hakuletwa na Mbowe, ni Kamati Kuu ndio ilimkubalia kugombea Urais kupitia Chadema, Mbowe hana mamlaka hiyo wala hakuwahi kuwa nayo
 
Tatizo la Tanzania ni kukosa uadilifu, jambo la No Reforms No Election lilitakiwa lisiwe jambo la kuwekewa vikwazo. Maana ni kitu kizuri kwa mustakhabali wa muda mrefu wa taifa letu.

Ilitakiwa vyama vyote iwe CHADEMA, CCM, CHAUMMA, ACT-Wazalendo kesho vinaweza kuwa vyama vya upinzani.

Hivyo jambo hili la No Reforms No Election linatakiwa limalizwe kwa kufanyiwa kazi kikamilifu ili kwa miaka 200 ijayo lisiibuke tena kutoka kambi ya upinzani.

CCM isishangilie kutokuwepo No Reforms No Elections kwani ni suala la kijambazi, wizi, kukosa uandilifu na hali hii siyo ya kuichekelea:

Mwandishi mchambuzi Maurice Larkin katika kitabu chake hapa chini matatizo aliyoyaona nchini Ufaransa yanashabiana na ya Tanzania ya 2025 :

FRANCE SINCE THE POPULAR FRONT
Government and People 1936 - 1986
Chapter 2
'La Republic des Députés' Politics in the 1930s

.....In France the President of the Republic was still lamenting that ' it is as though political debate was not a competition between two points of view, but the confrontation of two rival and mutually exclusive truths ....its style is that of a war of religion '
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…