Wito: Watu Wenye Uwezo, Tujitokeze Tujitolee Kumsaidia TAL na Kuisaidia Chadema to Play Real Politics, No Reforms No Election ni Utopian Politics!.

Tutegemee ushauri mwingi sana wa kutaka Chadema iweke wagombea ili kutumika kama ngazi.
Kuna uchaguzi fulani walitokeza wagombea waliosema kuwa wameteuliwa na CDM ingawa CDM iliwakana. Sasa hivi kuna wabunge 19 ambao walifukuzwa na CDM wanamaliza muda wao. Hao ni pamoja na madiwani kibao waliokaidi maagizo ya chama chao. Watu walivyo na njaa kuna viongozi watakubali kusimamishwa kugombea kwa niaba ya CDM na kukubali ushindi watakaopewa. Kwa kweli hamjifunzi.

Amandla...
 
P do you mean or politics as usual?
 
Mayalla,

Naamini kabisa unaifahamu dhana ya Uongozi iitwayo, 'Situational Leadership'. Kwa faida ya wasioijua, ni dhana inayosema kuwa, 'Uongozi wenye ufanisi, ni ule unatenda kuendana na hali ya mazingira ilivyo'.

Kwa muda mrefu, chini ya FAM, Chadema imetoa 'Upinzani ambao ni so compromising'. Je, umesaidia nini? Umewapa Uraisi, 2019, 2020 na 2024 wameporwa uchaguzi kabla ya siku ya kupiga kura. CCM, si chama cha siasa tena, ni chama dola. Sina hakika kama kuna mahala duniani, Chama dola kiliweza tekeleza haki za kidemokrasia kwa hiari yake.

So, kwa dhana hiyo ya Situational Leadership, Chadema wamefanya sahihi kumchagua TAL. Ndiye kiongozi wa Upinzani anayefaa, kwa mazingira ya sasa.
 
Sheria za uchaguzi zimekaa kuibeba CCM, ngoja TAL afungue watu masikio inatakiwa ifike mahali Kura yako iwe na thamani.

Siyo hizi brah brah za Mkaza mwana , kilichotokea uchafuzi wa serikali za mitaa ni Msiba kwa Demokrasia.

Wanasema kawia ufike kwani tuna haraka gani, acha yatengenezwe mazingira mazuri kwa vizazi vijavyo.
 
Hivi mkuu kama uliweza kutia nia kwenye beseni moja kule kawe na kina Mwijaku katika kura za maoni tunapata ukakasi sana unapotoa ushauri kama huu kimsingi TAL kwa hii milio tunayosikia sasa toka kila sehemu ni kama move zake zina scary watu wengi ushauri unakua mwingi sana ambao mantiki yake haipo spinning kibao Hivi ni nani anaweza kutoka hadharani nakusema kua mifumo yetu ya uchaguzi ipo sahihi? Ni nani anafurahishwa na watu kupotea nakuumizwa? Anaeyakataa haya iwaje aonekane hayuko sawa? Kuna shida sehemu
 
Wewe ndiyo hewa kabisa. Yaani mpo 1000km away from the river halafu muanze kujadili namna ya kuvuka?? Hakuna barabara wala usafiri wa uhakika kufikia huo mto. Hakuna chakula wala maji.

Badala ya kupambana na miundo mbinu mibovu ya njia wewe mawazo yako yanakimbilia kujadili namna ya kuvuka mto.

Tupambane na njia kwanza tukishafika mtoni sasa ndipo tuanze kujadili namna ya kuvuka.
 
Utopian? Why? It's a scientific political demand. Hivi wewe kweli kwa katiba hii, tume hii ya uchaguzi na muundo wake unaweza peleka chama kwenye uchaguzi mkuu na ukatarajia kushinda kiti Cha urais? Unless labda uwe na njaa zako tu. No reforms no election ni falsafa nzuri na inapaswa kuungwa mkono na watanzania wote hasa wenye akili timamu na wasioangalia maslahi yao binafsi. Naamini katika uamzi huu chadema hawatakuwa pekee yao Bali kutakuwa na millions of civil people behind. Tuache kukatisha watu tamaa na kusema haiwezekani. Hii ni nchi yetu sote tunaweza tukiamua. Tusikubali kuchezewa akili na kikundi kidogo Cha matapeli kwa mbinu za kijinga na kuona kwamba watanzania hawana akili. Hawa jamaa wa kijani wanaamini watanzania hawana akili timamu.
 
Msen...
Msen....kweli ww
 
Kiongozi kama hujasahahu basi umejisahahulisha! Umesahahu yaliyotokea uchaguzi wa 2019 baadae uchaguzi wa 2024?! Kuna haja ipi ya kwenda na uchaguzi unaofanana na huo?!?! Ni sawa uhangahike kulima halafu kuna wizi na unyang'aji utakaofanyika kwenye shamba lako!!!! Utalima ili upate nini! Kifupi mabadiliko/ mageuzi yafanyike inavyopaswa kwenye sheria za uchaguzi!
 
Ushauri huu ulitolewa na marehemu Lowassa kuwa chama ki-graduate kutoka harakati kifanye siasa za kimkakati kama chama hili Mbowe alipokea ushauri akaachana na habari za kushupaza shingo....naunga nawe kuhusu Lissu kupewa ushauri lakini ukumbuke Lissu ni mbishi na washauri wake wanajulikana ni watu wa hovyo sitaki kuwataja wanamshauri wewe ulishapigwa risasi 16 usiogope kufa wewe fanya chochote bila kujua anaipeleka chadema shimoni sasa hoja ya kuwa hatushiriki ila hatutasusia ni hoja ya kipuuzi!
 
castigating in politics should not be an opening remarks
 
....lakini TAL kama Mwenyekiti wa Chadema, ana baadhi ya madhaifu ambayo anahitaji msaada mkubwa kusaidiwa na watu wenye uwezo, ili aweze kubadilika na kuachana nayo, abadilike kutoka TAL mwanaharakati awe transformed into TAL mwenye statemanship!.
Asante sana kwa kuukwepa unafiki. Wengi hawataki kumwambia ukweli Antipasu kuhusu madhaifu yake! Kwa hoja yako hii, unakubaliana na Mimi kuwa litakuwa janga Antipasu kupewa majukumu yoyote mazito ya kinchi achilia mbali Chadema yake kushiriki serikali ya mseto huko Zanzibar!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…