Wizara ya Afya waanza kampeni ya kumsafisha Hayati Magufuli

Wizara ya Afya waanza kampeni ya kumsafisha Hayati Magufuli

Mungu hapendi watu vuguvugu - leo uko kanisani unakula mkate na divai, kesho unatuma wasiojulika kuteka watu... Huyo alikuwa gent wa shetani tu. Kama Mungu aliisaidia Tanzania ni kwa sababu ya maombi ya Watanzania wengine. Siyo Magufuli.
Kuhusu corona alimtanguliza Mungu na Mungu aliiponya nchi yetu na corona!! Ndiyo maana uko hapa mzima wa afya!! Corona haipo hata wanaoitafuta kwa tochi na kuwatishia watu na wimbi la tatu hawajafanikiwa kuipata wala kuiona! Mungu akipewa nafasi huwa hashindwi!! Tunatishiwa na nyoka aliyekwisha kupondwa kichwa nani atatishika?
 
Watanzania wengi mno ni wanafiki wakubwa, na hata sasa wote mnaobwatuka humu, barakoa hamvai!! ni unafiki tu wa kijinga na kulaumu wengine wakati hata wewe hapo ulipo, huna barakoa wala huzingatii chochote, ajabu zaidi, upo, na korona hupati
Mkuu jikite kwenye issues sio personalities
 
Hayati Magufuli alifanikiwa sana katika kuthibiti hofu ya corona ndiyo maana mpaka sasa hivi tunadunda salama salimini. Angalia majirani zetu pamoja na lockdown zao ikiwemo kutumia chanjo bado corona inawapiga sana tu. Tutamkumbuka sana Jemedari Magufuli. Nyinyi wapinga kila kitu tumeshawazoea ingawaje kwenye mioyo yenu inawasuta sana tu.
Mkuu Tanzania ni kubwa kuliko Magufuli. Serikali lazima ilinde hadhi yake bila kujali nani ni Rais wa wakati huo. Hizi mbinu zake za kishirikina za kupambana na Corona ndio zinaleta shida sasa kwa Serikali sasa.
 
Watajijuwa mie na familia yangu najikinga
Mkuu usijidanganye kabisa Corona ni tofauti sana na HIV, hii nikuomba kila mtu ajikinge,jamii ikichafuka lazima uipate maana inaambukizwa naweza sema kizembe sana.
Elimisha marafiki ndg na jamaa.
 
Wadudu wadogo wadogo wamekwisha maliza kazi yao. Wamebakiza mifupa tu...

Ungekua na elimu ya uhai ukajua nafasi ya mwili, roho na nafsi usingeandika ulichoandika
Ila nikuache tuu wewe muumini wa amstadam
 
Tangazo lenyewe lina makosa. Unaposema "watu kabla ya kusema chochote inabidi wajidhihirishe ndio waseme" unamaanisha kwamba hawana ulazima wa kujidhihirisha kuhusu kinachozungumzwa. Hapo maneno n "hawana budi wajidhihirishe" kuonesha kwamba wana ulazima wa kufanya hivyo.
 
Mkuu Tanzania ni kubwa kuliko Magufuli. Serikali lazima ilinde hadhi yake bila kujali nani ni Rais wa wakati huo. Hizi mbinu zake za kishirikina za kupambana na Corona ndio zinaleta shida sasa kwa Serikali sasa.
Acha utopolo wewe unazungumzia nini? TZ haina shida ya corona kama majirani zetu kwa kuwa tulikuwa makini na mbinu za kibeberu au wewe uko nje ya nchi nini? Tumefaulu sana katika kupambana na corona hakuna cha lockdown wala nini wakati majiranj zetu wamehangaika sana na bado wanahangaika sasa unataka kusema TZ hajafanya vizuri kwenye kupambana na corona?
 
Ungekuwa mtu wa imani ungekubali kuwa kazi ya Mungu haina makosa. Alazwe kwa kadiri ya matendo yake (alipojichagulia) - risasi kwa Lissu, kudukuwa maongezi ya watu, kesi za kubambikizia watu, wizi wa kura za uchaguzi 2020, kula hela ya msaada wa tetemeko, matusi ya nguoni...
Ungekua na elimu ya uhai ukajua nafasi ya mwili, roho na nafsi usingeandika ulichoandika
Ila nikuache tuu wewe muumini wa amstadam
 
Ungekuwa mtu wa imani ungekubali kuwa kazi ya Mungu haina makosa. Alazwe kwa kadiri ya matendo yake (alipojichagulia) - risasi kwa Lissu, kudukuwa maongezi ya watu, kesi za kubambikizia watu, wizi wa kura za uchaguzi 2020, kula hela ya msaada wa tetemeko, matusi ya nguoni...

Ulimuona akimpiga Tundu risasi? Rais wetu Samia alishawaambia aliyepiga zile risasi sio serikali wala aliyepiga zile risasi hawezi kuwa askari wake kamwe!

Sasa wewe ulikua unamchukia JPM siku zote nilijua ameondoka ameondoka kwa mapenzi ya Mungu roho yako imetulia. Ila sasa nashangaa Gubu na hasiraaaa zinavyokupamba moto......
Pole mwaya
 
Sio tuliaminishwa, Bali ni ukweli kwamba, Zipo nchi ambazo ziliagiza barakoa ktoka nchi zingine, baada ya kufikishwa zilionekana kuwa na virusi vya Corona

mf, Us aliagiza barakoa kutoka uchina, tuliona kwa macho yetu, zikirudishwa

Ni kwa nini mtu useme waliaminishwa na wakati ni kweli kulionekana kuwepo barakoa zenye virusi?
Huu uongo, virus vinawekwaje kwenye barakoa?,wangepigana vita kali,,barakoa zilikua zinakataliwa sababu nyingine zilikua na mapungufu,,sio kwamba eti kuna watu walichota virusi na kuweka kunako barakoa,,hiyo haiwezekni
 
Maneno aliyokua anayaongea hayati na kuwakalilisha wananchi wake, sasa imekua ngumu kwa Wananchi kuelewa kila ukiwaambia kitu utasikia Mbn Magufuli alisema hivi, mbn Magufuli alisema vile!

Wananchi wamekua wagumu kuvaa Barakoa Hongera wizara Ya Afya kwa View attachment 1827811kutoa Elimu Mujarab
Tanzania kuna watu wanafiki na kwa sasa hatuaminiani!, njaa inatuponza, Magufuri hakuamini kuna Corona sababu alikuwa kwenye jumba jeupe wakati huo hakujua ana hitilafu ya afya ambayo gonjwa hilo ndilo rafiki la kuondoa uhai. Ukiwa na tatizo la blood pressure, sukari, HIV +, na hata ujauzito kwa wanawake ikikupata unaenda udongoni. Tujifunze kuacha unafiki. Oneni Viongozi wanavyobadili kauli sababu ya njaa. Mama yetu oyeeeeeee
 
Acha utopolo wewe unazungumzia nini? TZ haina shida ya corona kama majirani zetu kwa kuwa tulikuwa makini na mbinu za kibeberu au wewe uko nje ya nchi nini? Tumefaulu sana katika kupambana na corona hakuna cha lockdown wala nini wakati majiranj zetu wamehangaika sana na bado wanahangaika sasa unataka kusema TZ hajafanya vizuri kwenye kupambana na corona?
Nyie vilaza ndio mnatupa tabu.... hivi unajua uchumi wetu unategemea utalii kwa kiasi gani? Unajua jinsi gani misimamo ya Magufuli imevuruga image ya nchi kwa wageni? Hakuna anayesema ije lockdown, lakini hii ya kujifanya kama hakuna tatizo ndio tatizo kubwa. Ulaya mwaka huu ukiisha wanamaliza maswala ya chanjo, unadhani ni mtalii gani atataka kwenda kwenye nchi iliyowekwa kwenye danger zone ya Corona; ambako akienda siku anarudi kwao atafungiwa ndani kwa wiki 2 mpaka 3. Au unadhani tembo na simba wako Serengeti tu?

Huyo mtukufu wenu alikuwa mshamba, asiyejua kufanya hata SWOT analysis, yeye kila kitu anaona dawa yake ni ugomvi tu.
 
JpM sio wa kuzimwa kwa mbwembwe tu uonekane utendji uliotukuka, mengine haya hayataleta impact kwetu sisi tunaotaka kuona vitu
 
Tunamshukuru Mungu kwa vile kazi yake haina makosa. Na wewe mshukuru kwa kutuondolea udhia.
Ulimuona akimpiga Tundu risasi? Rais wetu Samia alishawaambia aliyepiga zile risasi sio serikali wala aliyepiga zile risasi hawezi kuwa askari wake kamwe!

Sasa wewe ulikua unamchukia JPM siku zote nilijua ameondoka ameondoka kwa mapenzi ya Mungu roho yako imetulia. Ila sasa nashangaa Gubu na hasiraaaa zinavyokupamba moto......
Pole mwaya
 
Ukweli ni kwamba watu tuliaminishwa kuwa Tanzania hakuna korona na kuhusu kujikinga kwa barakoa tuliaminishwa barakoa zina korona,hivyo kwa serikali hii baada ya kubadilisha gia angani wanapata shida sana kuelimisha watu kuhusu kujikinga,ndio maana mtaani watu tupo tupo tu na ukimwona mtu kavaa barakoa tunamshangaa,ndio maana kwa sasa wizara wanajaribu kurejea maneno ya mwenda zake kwa sehemu alizo jaribu kuhimiza watu kuchukua taadhari ya kujikinga na korona,wanajaribu kumtumia kwa vile yeye ndiye aliye tufanya tuamini hakuna korona.ukweli ni kwamba mzee alituondoa hofu kiasi kilichopitiliza
Kwani Tanzania tuna Corona?
 
Back
Top Bottom