Habari wakuu,
Kama ilivyo ada, ugonjwa wa Macho Mekundu (Red Eyes) unazidi kutaradadi hasa hasa jijini Daslam ambapo 86% ya wakazi wake wote wameukwaa, wengi wao wakiwa ni vijana
Kutokana na utafiti uchwara uliofanyika, wakazi wote wa Daslamu tutaukwaa. Tafiti zilianza kwa kusema unaenezwa kwa njia ya kutazamana, baadae wakasema kupitia maji maji ya kwenye macho, sasa hivi tunaambiwa ni kwa njia ya hewa, kesho tutaambiwa ugonjwa huu ni Pandemic
Wanadai hauna tiba wala kinga. Ila utaishi nao kwa muda wa wiki mbili. Wamasai wanatuambia tupakae mikojo kwenye macho yetu, jambo lililopelekea macho yangu kufumba, nilipoenda hospitali nikaambiwa macho yamejaa vijidudu vya U.T.I na Pombe kali. Wapemba wakatuambia tupakae maji ya moto yaliyotiliwa chumvi, badala yake macho ya walio wengi yametengeneza tongo tongo na mucus zisizo na mfano zilizopelekea kuvimba kwa macho na maumivu makali sana. Wabena wakatuambia macho yetu tuyanyunyizie Smart Gin, nahisi mliofanya hilo jaribio mmekipata pata hapo Mloganzila
Ingawa ugonjwa huu ni mlipuko wa Virusi, cha ajabu ukienda duka la madawa unapatiwa dawa utumie, dawa zenyewe zimeandikwa kudeal na Bacterial Infections kwenye macho, sijui wataalamu wanatuchukuliaje kwa mfano
Anyway, ni uzi maalumu kwa ajili ya kufarijiana na kuchekana