Wizara ya Fedha, BoT na TAKUKURU imulikeni Letshego /Faidika Tanzania ni majambazi

Wizara ya Fedha, BoT na TAKUKURU imulikeni Letshego /Faidika Tanzania ni majambazi

hiyo ni shida yetu wabongo, kila kitu kinajulikana kabla ya kukopa, wakati unahitaji hela akili unaweka mfukoni, hutaki kujua masharti kabisa, una saini tu
baadaye ndo unatoa akili mfukoni
kama anahisi kuna uonevu aende bot wachunguze
Sure.
Nenda benki kuu mzee hutojutia. Watatema hela yako fasta kabisa
 
Wakuu naombeni hatua za kufuata Ili huyu jamaa awasilishe malalamiko yake BOT
 
Ni hatari usijaribu mkuu wangu. Jinsi sheria zilivyo ni kwamba wanakuacha unafanya ujinga siku wakija wanakulambusha Money laundering. Very soon microfinance nyingi wamiliki wake watafungwa. Stay tuned mkuu, sheria zake ni kali mno! Ila watu wengi hawajui ingawa walifundishwa
Bora tu
 
mimi nilikopa 2,500,000 tu kwenyetaasisi furani ila nililipa 4,450,000 baada ya miezi 5 tu mzee nilipigiwa mahesabu nikaona isiwe kasi nikalipa mpaka sasa nimekoma ...kikubwa nimejifunza tukope kwenye mabenki tu huu ni uzembe wetu wenyewe kushindwa kupiga mahesabu vzr tukipata matatizo ya haraka
 
mimi nilikopa 2,500,000 tu kwenyetaasisi furani ila nililipa 4,450,000 baada ya miezi 5 tu mzee nilipigiwa mahesabu nikaona isiwe kasi nikalipa mpaka sasa nimekoma ...kikubwa nimejifunza tukope kwenye mabenki tu huu ni uzembe wetu wenyewe kushindwa kupiga mahesabu vzr tukipata matatizo ya haraka
Hakika,
Hawa faidika ni ny*ko kwakweli
 
Hii ni taasisi ya Fedha inayojihusisha na mikopo kwa wafanyakazi na wafanyabiashara
Juni 2021 mfanyakazi (sitamtaja) alikopa ths 3,500,000 kwa makato ya Tsh 126,400 kwa mwezi,

Sasa picha limeanza mwaka huu mfanyakaz akataka kuwalipa deni lao (kumbuka ameshakatwa kama miezi 20)
Toka Juni 2021,

Kwanza wakasema balance Yao mpaka uende kwenye branchi zao za mikoa na kwa kesi yake yeye ikabidi aende Morogoro mjini, Akajaza fomu kuomba kupewa deni lake Ili alipe (afute mkopo) wakamwambia balance haitoki kirahisi hivyo ni mpaka miezi mitatu! Akasema sawa akarudi zake kijijin

Tarehe 6 (alhamis) Kabla ya Pasaka wakamwambia balance yake imetoka akachukue
Kutoka siku Ile Hadi kufika Moro goro mjini ni ngumu,
Kesho yake ilikua ijumaa kuu,
Na jumatatu ikawa ni jumatatu ya Pasaka!
Akaenda jumanne akaletewa deni la 3,930,000 ( na kumbuka alishakatwa zaidi ya miezi 20 !! Makato ya 126400 ambapo ukizidisha toka Juni 2021 Hadi march (126400*21= 2,654,400) ambayo tayari ilishalipwa..

Lakini jamaa akasema potelea pote akaamua kuwalipa iyo 3.93 m!
Baada ya kusoma iyo statement wameandika pesa mwisho kulipa ni tr 14!
Kumbuka hapo wameweka siku 7 Bila kuhesabu wikiend au zile siku za pasaka!
Jamaa kajipinda kaja kulipa tar 17 (siku 3) mbele
Anapeleka risiti Letshego wanasema amechelewa kulipa na hivyo aongeze 56,000 kama faini!!

Jamaa uvumilivu ukamshinda akasema haongezi pesa!
Na wao wakasema wataendelea kumkata! Iyo 126,400 Kila mwezi kama kawaida!

Jamani huyu jamaa afanyeje hapo katika mazingira haya!

Asanteni
Kama ni mtu makini unayejuwa thamani ya pesa na unatafuta pesa kwa shida huwezi kopa hizi FINANCE njaa. Hawa si watoa huduma bali ni kukupeleka katika umasikini wa kudumu.

Ukikopa mkopo wenye makato ya miaka 7 au 8.

Riba yao ni mara 3 ya pesa uliyokopa.

Mfano ukikopa milioni 3 kwa miaka 8 jiandae kulipa 12M


Unajiuliza hapo umekopa utatue tatizo au umejichimbia shimo.


UPUMBAVU WA WATUMISHI MBALIMBAI.

Hizi finance zina tabia ya kukushawishi na kujigamba kuwa unapata MPUNGA ndani ya masaa 24, tena nyingine zinatembea na pesa Live ukijaza tu form unapewa Mzigo.

Hili watu wengi wanaona ni rahisi coz hakuna usumbufu bila kuwaza RIBA YAKE MBELE.

NMB,CRDB NA BANK NYINGINE.

Mikopo yao inachukua muda ni kweli unapambana mwenyewe inaweza chukua hata mwezi au au wiki 2 au 1.

Lakini hawa ni uhakika siyo wababaishaji kama hizi finance janja janja.

Mtu anaona kufatilia 2 weeks ni nyingi anaona bora ajilipue huko kwa wakausha damu.


Zaidi CRDB naona wako vzr sana coz CRDB Unaweza kukopa 10M hlf makato hayo hayo NMB ukaambiwa mwisho 7M
 
Chawa wa mama hii habari umetoa wapi?
Watu kama Platinum Wana miaka na miaka wanafanya huu ujinga ulishawahi ona wanachukuliwa hatua?
Huyo chawa hamna kitu anajua yeye kusifia serikali tu
 
Asanteni kwa ushauri wenu jamaa ametuma malalamiko yake BoT kupitia complaining desk na bot wanashughulikia
 
Mikopo hii huchukuliwa na watu wenye akili timamu kabisa ambao kweli huwa hawapitii kanuni za mkopo vizuri, ama kwa uharaka au kutojua. Lakini benki zote zilipaswa zitoe maelezo ya kutosha kwa wakopaji ili kuepuka migogoro. Lakini kwa huku kutojua kwetu benki zinatumia kuzidi kutukandamiza.
 
Hii ni taasisi ya Fedha inayojihusisha na mikopo kwa wafanyakazi na wafanyabiashara
Juni 2021 mfanyakazi (sitamtaja) alikopa ths 3,500,000 kwa makato ya Tsh 126,400 kwa mwezi,

Sasa picha limeanza mwaka huu mfanyakaz akataka kuwalipa deni lao (kumbuka ameshakatwa kama miezi 20)
Toka Juni 2021,

Kwanza wakasema balance Yao mpaka uende kwenye branchi zao za mikoa na kwa kesi yake yeye ikabidi aende Morogoro mjini, Akajaza fomu kuomba kupewa deni lake Ili alipe (afute mkopo) wakamwambia balance haitoki kirahisi hivyo ni mpaka miezi mitatu! Akasema sawa akarudi zake kijijin

Tarehe 6 (alhamis) Kabla ya Pasaka wakamwambia balance yake imetoka akachukue
Kutoka siku Ile Hadi kufika Moro goro mjini ni ngumu,
Kesho yake ilikua ijumaa kuu,
Na jumatatu ikawa ni jumatatu ya Pasaka!
Akaenda jumanne akaletewa deni la 3,930,000 ( na kumbuka alishakatwa zaidi ya miezi 20 !! Makato ya 126400 ambapo ukizidisha toka Juni 2021 Hadi march (126400*21= 2,654,400) ambayo tayari ilishalipwa..

Lakini jamaa akasema potelea pote akaamua kuwalipa iyo 3.93 m!
Baada ya kusoma iyo statement wameandika pesa mwisho kulipa ni tr 14!
Kumbuka hapo wameweka siku 7 Bila kuhesabu wikiend au zile siku za pasaka!
Jamaa kajipinda kaja kulipa tar 17 (siku 3) mbele
Anapeleka risiti Letshego wanasema amechelewa kulipa na hivyo aongeze 56,000 kama faini!!

Jamaa uvumilivu ukamshinda akasema haongezi pesa!
Na wao wakasema wataendelea kumkata! Iyo 126,400 Kila mwezi kama kawaida!

Jamani huyu jamaa afanyeje hapo katika mazingira haya!

Asanteni
Muombe mkataba wake kwanza wa mkopo then watu ndo tutakuwa na uwanja mpaka wa kumshauri.

Watanzania wengi huwa tunapokwendaga kwenye hizi microfinance kuomba mikopo huwa tumebanwa kweli kweli na wenyewe huwa wajanja kwa baadhi kwa kutusainisha mikataba kwa lugha ya kiingereza.

Kwaiyo ukishatajiwa mashart mawili matatu kiwepesi fasta anaanguka sahihi na kuchukua hela kilio kinakuwa baadae kama hivi
 
Ninavyojua mimi Letshego ni benki. Kwa upande wangu nina maoni tofauti kidogo. Kabla sijawalaumu Letshego lazima mkopaji asome tena mkataba wake ulikuwa unasemaje. Pia unapolipa mkopo unakatwa kupitia account yako na bank statement huonyesha kabisa jinsi ulivyokatwa. Alishindwa nini kuchukua statement na kupiga hesabu? Hata kama kulikuwa na penalties statement ingeonyesha.

Hii kauli "Lakini jamaa akasema potelea pote akaamua kuwalipa iyo 3.93 m!" ni ya kijinga sana na kushindwa kujua haki zake. Huwa najiuliza kwanini haya mambo huwakumba sana watu wa vipato vya chini? Yaani hapo kwa mtu makini ni fursa ya kesi na kujipigia mahela ya fidia. Tafuta wakili uwaburute hao watu mahakamani utapiga hela. Pia nawasihi sana watanzania wenzangu tuwe na tabia ya kusoma mikataba kabla ya kusaini hata kama njaa imekaba kiasi gani. Kama unaona huwezi kusoma mkataba tafuta kijana smart ndani ya circle yako akueleweshe.

Kingine ni kujua haki zako. Hata ikiletwa katiba kutoka mbinguni haitasaidia kama bado watu ni wajinga kiasi cha kudhulimiwa waziwazi. Hii ndo sababu hata mbunge anaweza simama na kusema tulipishwe Tsh 100 kwenye mafuta au mwingine akasema wabunge wajengewe maeneo yao maalum ya starehe.
Sijaelewa hapo alipokuwa amelipa Deni kwa miezi 20.... Then akaja kulipa pesa 3.93mil kwa kusema potelea mbali.... Mwenzetu anaokota wapi hizo pesa na wengine wakaokote pia??
 
Acha uongo wewe chawa. Hizo taarifa zinakusanywa miaka mingap? Na watu wanaendelea kuumizwa na ushahidi upo wazi kabisa
Kumbuka wanaokusanya taarifa ni wengine na wanao chukua hatua ni wengine kabisa.

Unaweza kusema hapo mtaani kwako watu hawakujui kiundani lakini kiuhalisia watu wanataarifa zako zote,siku zikihitajika wewe mwenyewe unaweza kushangaa imekuwaje

All in all vyombo vyetu vingi viko macho mno na vinafanya kazi kweli kweli sema wamenyimwa tu power ya kutake action,ila yote tunayolalaimika humu kila siku serikali inayajua na yako mezani sema wenye mandatory ya kuchukua hatua ndo hao wamekula buyu
 
Sijaelewa hapo alipokuwa amelipa Deni kwa miezi 20.... Then akaja kulipa pesa 3.93mil kwa kusema potelea mbali.... Mwenzetu anaokota wapi hizo pesa na wengine wakaokote pia??
Alilipa marejesho 20
Yaani miezi 20,

Na baadae akaambiwa kufuta mkopo ndio alipe 3.926 m cash
 
Back
Top Bottom