Wizi wa kwenye mabasi wanaswa na kamera ya bus la ABC

Wizi wa kwenye mabasi wanaswa na kamera ya bus la ABC

Yani huwezi wadhania kabisa..duuh
Wanavyong'aa utadhani watu kumbe viatu? Mungu awezeshe wakamatwe. Tatizo huyo jamaa wa ABC hajasema basi lao lilikuwa linasafiri kutoka wapi kuelekea wapi ili iwe rahisi hata kwa polisi kufuatilia.
 
Nakumbuka siku moja nimepanda basi la kampuni X nimeweka kibegi changu kwenye keria hizo. Safari ikawa inaendelea tulikuwa tunatoka dar kwenda arusha. Kufika hedaru gari likaharibika bana, abiria wote tukashuka kusubiri litengamae, lilivyokaa sawa kuja kufika moshi ishafika saa mbili usiku mi nikaona nisiendelee na safari nitalala moshi. Katika harakati za kuondoka nikabeba begi kumbe sio langu. Nikalibeba na kusepa mpaka pale kindoroko. Lakwangu lilikuwa na nguo na viatu tuu. Kufika room nakagua nakuta nguo ambazo sio zangu, kukagua kagua naona mfuko wa rambo mweusi, nikaufungua na kupekenyua nakutana na maburungutu ya pesa na kipistol. Jaribu kutafta vitambulisho hamna. Nikahesabu ile hela ilikuwa milioni 25 cash. Kesho yake nikaenda ofisini kwenye hio kampuni nikakuta tayari ripoti zipo za mtu kupotelewa na begi. Lile lakwangu lishaletwa pale na jamaa yupo ana wenge balaa ila uzuri hakusema kilichopo ndani. Nikaongea naye akaniambia alikuwa na haraka hivyo akachanganya mabegi. Nikamuhoji ndani kulikuwa na nini mule kwa bag yake. Akasema vyote, tukaongozana mpaka pale kindoroko. Ile kufika tuu naona mtu anatoka chumbani kwangu, na sa hio nliomba nisifanyiwe usafi ndani kwangu. Aiseeh to cut short hii story nlimkabidhi vitu vyake, ila yule mwamba mpaka leo yupo karanga ananyea debe.
Duh alikuwa ni mfanyakazi wa pale?
 
Angalia video hii, kama unawatambua toa taarifa upate zawadi yako ya Tsh. laki 5.

ABC na uongozi wote ni wazembe wanatakiwa wamlipe aliyeibiwa maana wao wameratibu wizi. Abood wao wanafanya monitoring live, mtu akichanganya tu basi wanapiga simu faster mwizi anadakwa. Sasa hawa ABC inakuwaje mwizi anaachiwa???
 
ila daah kwa upande fulani nashukuru kwa hii video itasaidia sana kuongeza umakini kwene safari za mabasi. kumbe wizi upo bana.
 
Ni hatua nzuri mabasi kutumia camera za ndani ipasavyo.Kongole kwa ABC. hili basi huwa natumia nikienda Mbaya Mara nyingi sikukosea kuchagua.
 
W

WApuuz sana bora wangekua vyet wanasalimisha bac polisi au ht chuo kwa kujifanya samaria mwema umeokota
Mkuu yani wakasalimishe vyeti polisi, bora tu wasiviharibu waviweke tu mahali salama hata stendi ila wasivitupe hovyo.
 
Mzee wa watu ameiba ili akamfurahishe binti wa watu gest
 
Mimi Begi la mgongoni Hata nimebeba magimbi siweki juu, Na ukiliangalia mara mbili mbili naweza nikuulize umepoteza kitu?, uchale ukizidi nalitia hata mgongoni humo humo,
 
Back
Top Bottom