Wolper anusurika Kupigwa Risasi Kituo cha Mafuta

Wolper anusurika Kupigwa Risasi Kituo cha Mafuta

Kumbe Mark X mafuta ya elfu 20 yanatosha?
 
kwa hiyo wataipa jina gani hiyo movie tujiandae kabisa kuitafuta madukani?
 
Bwana ake akisikia ataenda kudai...

Bora awasomee Albadir kama yule waziri wa Zanzibar atakachofanya... kukusanya waganga wote nchi nzima
 
Alaaniwe huyo dada kwa kuwekea mteja hewa badala ya mafuta..

Na pili pia.. mark x na mafuta ya elfu20 mpaka gari inazimika wapi na wapi...
 
Hivi "juzikati" inamaanisha nini?
Hapo ujue mwisho wa waandishi wa habari wa magazeti haya kuhesabu siku umefika.

Wao wana leo, jana, juzi na siku nyingine za karibuni zikizobaki kwao ni juzikati.

Kamusi Kuu ya Kiswahili haina neno "juzikati". Ina neno juzijuzi.

Wanamaanisha juzijuzi.
 
Wabongo bwana .. Sasa wanafhani Wolper atarudi tena hapo? Kitu kidogo sana ila kinaweza kuikost biashara.. Then wakiajiriwa wahindi basi malalamisha tele
Mhindi kwa kazi hiyohiyo angelipwa milion lakini mbongo analipwa laki hasini we unaionaje
 
wewe ni mdada mwenye mihela mingi achanana hiyo tabia ya kuweka mafuta nusunusu kwa gari bhaana yatakutokeaga puani kama ulivyoona.....the fault was urs mamaa coz kwanza huna ushahidi kma uliibiwa au lah....!
 
Wanaofanya hivyo ni wafanyakazi mkuu , ambao kwao cha muhimu ni mshahara wao si biashara inaingiza nini.

Wafanyakazi wa ibongo wengi si waaminifu, biashara nyingi sana wanaziharibu wao, hata kama management iko vizuri.

Mnatakiwa mwe mnawatest IQ wafanyakazi kabla ya kuwapa kazi. Na mwe mnawavalisha kamera ya kifuani kama polisi wa marekani wanavyovalishwa.
 
mi ndio maana nimenunua gari linatumia umeme...mafuta yanazingua sana
 
Source bongo movie? Aaah ni nilijua kweli, kumbe ni muendelezo wa upuuzi wao. Sasa gari lililozima kwa kuishiwa mafuta alirudi nalo vipi sheli, alilibeba? Kisha baada ya kuona kimenuka akatoka tena nduki na gari, mafuta ya 20000? Fuel gauge ya mark X ni mdebwedo hata ishindwe kusoma kuwa kuna wese limeongezwa? Ama huyu Wolper ni ****** kiasi ashindwe faham km anaibiwa hadi aende, arudi?
Wewe na wajuaji wenzio mnaleta ujuaji huku hamuwezi kusoma kitu rahisi na kuelewa. Kasema hivi aliona gari imepungua mafuta akaingia hapo kituoni kuongeza na kuondoka kufika mbele kidogo gari ikazima akafanya utaratibu mwingine wa kupata mafuta ndio akarudi pale kituoni. Utaratibu mwingine unaweza kuwa kutafuta bodaboda au bajaji na kumtuma akuletee mafuta.

Halafu mnaoponda mafuta ya 20,000 acheni utoto...hizo sasa hivi ni lita si chini ya 10 ambazo kwa gari kama mark x utapata km si chini ya 60. Sasa km 60 ni ndogo? siku hazilingani kuna siku unaishiwa mafuta mfukoni una 50,000 utaweka yote 50k ?
 
Mi mwenye kwenye Altezza yangu siwezi kuweka mafuta ya kimasikini hivyo. Mafuta ya 20,000? Not me.
Hongera sana. Mie huwa napenda kujaza full tank. Lakini kuna siku huwa hesabu zinagoma naweka hata ya 10,000/= ili yanisogeze kidogo. Maana siyo siku zote nakuwa na pesa za kutosha.
 
Kuna siku niliweka mafuta ya elfu 20 pale Oilcom Tazara Maghorofani. Nafika kwenye mataa Tazara kiwese kimekata. Bahati nzuri nilikuwa na mafuta kidogo kwenye dumu. Nikatia nikaenda zangu hadi kituo kingine nikajaza. Kesho yake niliwaibukia sheli. Nikatemka mkwara kwa meneja. Akasema aliyekuwa zamu anaingia kesho yake. Kesho yake nikaibuka. Nikawaambia nitawaandika magazetini hadi wakome. Jamaa wakakubali kunirudishia mafuta yangu. Wakanijazia na ya usumbufu. Jumla nikapewa mafuta ya elfu 50.
 
Hongera sana. Mie huwa napenda kujaza full tank. Lakini kuna siku huwa hesabu zinagoma naweka hata ya 10,000/= ili yanisogeze kidogo. Maana siyo siku zote nakuwa na pesa za kutosha.
Siku zipi unakuwa na hela za kutosha?
 
Hicho kituo ni pale Tegeta Kibaoni, njia panda ya kwenda Wazo, walishawahi nifanyia huo uhuni wa kuniibia mafuta. Kwa wakazi wa maeneo hayo pale sio kabisa.
 
Back
Top Bottom