Wote wameingia kibahati na kutotarajia, Rais Samia hana jipya tena

Wote wameingia kibahati na kutotarajia, Rais Samia hana jipya tena

Autodidacts

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2021
Posts
1,165
Reaction score
1,804
Hayati Magufuli a.k.a mwendazake aliwahi kukiri kuwa hakutarajia kuwa Rais wa awamu ya tano. Wengi tunakumbuka yaliyotokea, mpambano wa Membe na Lowassa ndio uliomzaa Magufuli kama suluhu ya kambi mbili pinzani ndani ya CCM wakati huo.

Mwendazake alipata heshima na makofi mengi ndani ya siku 100 kwa kauli mbiu ya kutumbua majipu, akapata na sifa nyingi bandia. Akageuza sifa, mapambio na heshima aliyopata kuwa sera ya nyongeza. Hakutaka tena kitu chochote mbadala,akalewa sifa na kuona hakuna Rais kama yeye wote waliomtangulia akawaona kama wezi na wanyang'anyi!

Kwa kawaida ya kimaumbile ya IQ ndogo, mwanadamu wa IQ ndogo anapofikia hatua aliyofikia mwendazake ya kulewa sifa huwa hataki kushuka wala kukosolewa. Matokeo ni kwamba kila anaekosoa anashughulikiwa, amri na ubabe utawala, sheria nazo uonekana ni adui mwingine ivyo mtoto anaezaliwa ni uundaji wa vikundi vya kiharifu vinavyolindwa na serikali kushughulika na wapinzani ili kulinda heshima ya Rais na sio katiba aliyoapia kuilinda. Baadae anazaliwa mtoto wa pili yaani udikteta!

Nimemsikia jana Rais Samia anaelekea kwa kasi kuumba kile kile cha mwendazake. Sasa anaona heshima yake ni bora kuliko katiba na matakwa ya wananchi. Kauli yake kuwa suala la katiba kusubiri uchumi ukue, utajiuliza je unaweza kupata maendeleo bila katiba yenye kukubaliwa na wengi? Kwa nini watu wasiwe huru kufanya mikutano kama katiba ya sasa inavyosema? Je kauli ya Rais kuweka masharti ya uhuru wa mikutano umezingtia sheria ipi inayozidi katiba au ni kauli binafsi tu kama ya mwendazake? Ni wazi ameanza kupingwa sana.

Sasa ni dhahiri mama kalewa sifa. Atapingwa. Ataanza kulinda sifa hizo na heshima aliyopewa kwa gharama, ivyo ataunda vikundi haramu kushughulika na wanaompinga, akina Sabaya wapya tuwatarajie!

USHAURI: Rais Samia aondokane na chawa wa mwendazake, achague upande wa wananchi na sio kikundi cha wachache wenye kulenga maslahi binafsi, atapata heshima ya kweli na ya kudumu badala ya hii heshima ya bandia na ya muda mfupi.
 
Rais Samia ana uwezo mdogo wa kufikiri na kupanga mambo kabla ya mambo kutayarishwa (thinking on her feet).

Ndiyo maana kajibu vibaya suala la kuruhusu mikutano, suala ambalo jibu lake limempa kesi ya kuvunja katiba.

Halafu, ana uwezo mdogo wa kuchuja habari na kujua hii uongo na hii ukweli.

Ndiyo maana kanukuu makala ya uongo kuhusu kujifukiza ili kuondoa Coronavirus.

Zaidi, hajui kutumia msaaada wa wasaidizi wake kumuandalia mambo ya kusema na kuchuja kipi ni fake news na kipi ni kweli. Hili ni jambo hatari sana kwa rais.
 
Ni viongozi wachache sana tulio nao sasa wenye sifa hii.

Kikwete aliulizwa ni kipi kinasababisha Tanzania iwe nchi maskini...

Mwalimu Nyerere na Ben tu, ndio waliokuwa na uwezo wa hayo uliyoyaeleza katika andiko lako.
Ironically, Ben Mkapa, ambaye alikuwa na uwezo wa kufikiri on his feet zaidi ya Samia, alitumia hotuba zilizotayarishwa karibu mara zote.
 
Rais Samia ana uwezo mdogo wa kufikiri na kupanga mambo kabla ya mambo kutayarishwa (thinking on her feet).

Ndiyo maana kajibu vibaya suala la kuruhusu mikutano, suala ambalo jibu lake limempa kesi ya kuvunja katiba.

Halafu, ana uwezo mdogo wa kuchuja habari na kujua hii uongo na hii ukweli.

Ndiyo maana kanukuu makala ya uongo kuhusu kujifukiza ili kuondoa Coronavirus.

Zaidi, hajui kutumia msaaada wa wasaidizi wake kumuandalia mambo ya kusema na kuchuja kipi ni fake news na kipi ni kweli. Hili ni jambo hatari sana kwa rais.
Huyu ni empty kabisa
Alianza kukosea kwenye kuteua.
Leo anateua huyu, yakipita masaa mawili anatengua.
Dawa ya yote haya ni katiba
 
Huyu ni empty kabisa
Alianza kukosea kwenye kuteua.
Leo anateua huyu, yakipita masaa mawili anatengua.
Dawa ya yote haya ni katiba
Kwenye kuteua, alimteua mpaka ndugu yake kiundugunization, bila aibu.

Kuna tatizo kubwa pale nchi ambapo kwenye makaratasi inakwenda kwa misingi ya utawala wa sheria, lakini kiuhalisi zile sheria zote za kwenye makaratasi zimewekewa figisu kubwa sana, nchi inakwenda kwa mazoea tu.

Huyu kashakaa sana chemba na dikteta uchwara, unafikiri siku zote walikuwa wanaongea nini kama si kurithishana udikteta tu?
 
Back
Top Bottom