Yaliyojiri Ikulu Dar: Rais Magufuli amtaka CAG Kichere kutojifanya Muhimili mwingine, amwambia anaweza kuondolewa hata akiwa na mwaka mmoja

Katiba yetu inasiginwa.

Magu hakumpenda Assad na Assad atafanyiwa figisu ajute
 
Mwenye serikali yake ''Yupo''.......Hakuna cha muhimili wala mihimili hapa 😀 😀
 
Kwa kauli ya Rais unajua tu kabisa alikuwa hamtaki Proffesa Assad...et we ni mdhibiti wa hesabu za serikali na mwenye serikal yupo ...mwenye serikali ni nani kama sio sisi wapiga kura (wananchi) ,usiende kujifanya mhumili Kwan aliyetoka alifanya mhimili lini?
Au ndo huyo aliyekuwa anasema "Kuna mwingine tumeshauriana sana na katibu Mkuu kumtumbua tunashindwa "

Mtu kupata division one O na I level sio kigezo cha kumpatia kazi...wakati akiwa commissioner wa TRA hukuona hizo divionsin one ,mbona wakati ulisema ameshindwa kazi Leo ndo ataweza kazi ?
Tusubiri wizi mwingine wa matrioni yakienda chato .
 
........ntailinda na kuitetea Katiba ya JMT.........
 
Magufuli kawatukana Wachaga kwamba wanapenda rushwa.
 
Inaonesha kuwa Assad alipitia vitisho vingi
 
Political interpreneur mbona anawaapisha haraka haraka kulikoni, jana uteuzi leo kuapishwa?
 
walianza na wahindi (magabacholi) wakatukawa wee
wakanyanyasika wee
wakaandamwa weee
wakafurushwa wee

Wahindi WAKAVUMILIA na Upepo mbaya ukapita..

sasa ni zamu ya wachaga na wanasemwa
ni wezi..
ila wameiba wapi?
mbona hawakamatwi?
magerezani wako wangapi?
mahakamani kuna kesi ngapi?

*wachaga wapo watumishi,wanafunzi,wakulima,mapadri,wachungaji,ma sheikh,wana JF,maaskari,na wanaccm..Je wote nao ni wezi.!?

Xenophobia ni nini.!?

jirani yangu ni mchaga... nafuga dog
 
Hii ni safi sana kwa walioteuliwa, hakika mheshimiwa kawaamini na kuwapa majukumu hayo. Good job Mr. President
 
Ivi Dodoma kashindwa kabisa kwenda uko? Nashindwa kuelewa kabisa ilikuwa ni siasa au mkakati nilitegemea mambo kama aya yafanyike Dodoma maana juzi tu kasema kashaamia uko.
Afya hairuhusu kutoka hapo nje ya nyumba. Akimaliza hayo majukumu hapo anaendelea na bed rest. Madaktari Bingwa wamehamishia ofisi zao hapo.
 
Mtu kupata division one O na I level sio kigezo cha kumpatia kazi...wakati akiwa commissioner wa TRA hukuona hizo divionsin one ,mbona wakati ulisema ameshindwa kazi Leo ndo ataweza kazi ?
Jitahidi kuwaza mbali kidogo basi...mbona majibu ya maswali yako kayajibu pale pale M. Rais! kumtoa pale TRA na kumpeleka Njombe alikuwa anapimwa 'humble' yake, uvumilivu wake katika kuchukulia mambo na maamuzi magumu juu yake na watanzania kwa ujumla. He was being tested for his patience !! Hupo ?
 
Ivi Dodoma kashindwa kabisa kwenda uko? Nashindwa kuelewa kabisa ilikuwa ni siasa au mkakati nilitegemea mambo kama aya yafanyike Dodoma maana juzi tu kasema kashaamia uko.
DSM ni DSM!
 
Mpiga kura ni mshenga tu
 
"Kwa CAG mpya nakutakia kazi njema, usije ukaenda huko ukajifanya na wewe ni mhimili, mihimili ni mitatu tu na umeiona hapa, na katika kiapo chako nilikuwa nakisikiliza nafasi yako ni Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwahiyo mwenye Serikali yupo"- @MagufuliJP #MwananchiUpdates

"Katika maisha ya Duniani hapa huwezi kupewa mamlaka ya kuteua halafu usiwe na mamlaka ya kutengua, ukishindwa hivyo hufai kuwa Rais, CAG kasimamie kazi yako vizuri, mwenzako amemaliza miaka 5 yake, inaisha leo saa sita usiku, kesho nenda pale ofisini kayatoe mauchafu yaliyopo"-JPM
#KiapoIkulu
#MillardAyoIkuluUPDATES


Na katika kiapo chako (Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali) nilikuwa nakisikiliza, nafasi yako ni Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kwa hiyo mwenye Serikali yupo, mwenye serikali yupo, kafanye kazi zako vizuri za ukaguzi bila kuonea watu.

Unapopewa maagizo na mihimili mingine kama Bunge katekeleze, usibishane nao. Ukipewa maagizo na mihimili kama Mahakama kaitekeleze, wewe ni mtumishi, wewe ni mtumishi.- Rais John Magufuli.
Kama kayasema haya hadharani je sirini kayasema yapi?

Kama anataka CAG awe upande wa serikali sasa unamkagiaje mtu uliye na maslai nae utamsaidiaje kulinda maslai ya umma?

Ivi CAG akiwa upande wa serikali nani atawasaidia umma kujua madhaifu ya serikali kwenye mapato na matumizi?

Ni kitu gani Magufuli analificha kwenye ukaguzi huru?

Kwanini mihimili yote anaifanya kuwa ya serikali?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…