Nafuatilia mnyukano wa kikatiba na kisheria unaoendelea baada ya Rais kuteua CAG mpya.
Huyo CAG mpya ni ACPA 1450 ila sio active member 1.7.2019, kama sio active member anakosa sifa. Hebu chungulia hapa ujionee:
Orodha ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu |BODI YA TAIFA YA WAHASIBU NA WAKAGUZI WA HESABU TANZANIA (NBAA).
Aliyekuwa hafai TRA Sasa ameteuliwa kuwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali! Yajayo yanafurahisha!!
Raia wanauliza sasa Mahesabu yake akiwa TRA ana uhalali wa kuyakagua?
Je, matumizi ya ofisini akiwa RAS Njombe atakuwa na uhalali wa kuyakagua?
Hakuna rangi hatutaona at this Regime
Taarifa ya Ikulu imeeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Prof. Mussa Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano kwenye nafasi hiyo. Lakini Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (ambayo ndio sheria mama) haelezi hicho kinachoitwa "kipindi cha miaka mitano"
Katiba inaeleza kuwa CAG atakoma utumishi wake atakapotimiza umri wa miaka 60. Yani akifikisha umri wa miaka 60 anapumzika bila kujalisha ametumikia nafasi hiyo kwa muda gani. Iwe miezi miwili, miaka nane, au miaka kumi.
Ndio maana maCAG wote waliotangulia wameongoza ofisi hiyo kwa vipindi tofauti. Mzee Mohamed Aboud aliongoza kwa miaka 27 tangu 1969 hadi 1996. Thomas Kiama akaongoza kwa miaka 9 tangu 1996 hadi 2005. Ludovick Utouh akaongoza kwa miaka 8 tangu 2006 hadi 2014. Sasa hii kauli ya kusema Assad amemaliza kipindi chake cha "miaka mitano" imetoka wapi?
Matakwa ya kikatiba ni umri wa miaka 60, unless aondolewe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake. Na ikitokea hivyo Katiba imeweka utaratibu wa kumuondoa kwa kuunda tume.
Lakini taarifa ya Ikulu inaeleza Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano. Je hiki kipindi cha miaka mitano Ikulu wamekitoa wapi? Kwenye sheria ipi? Kama ipo sheria hiyo ipo ni batili maana inapingana na katiba.
Na kwa kawaida unapotokea mgogoro kati ya sheria na katiba, basi Katiba ndiyo inayoshika hatamu (When a state law conflicts with a Constitution, then constitution prevails because constitution rules supreme above all state laws).
_
Prof.Assad amezaliwa tar.06 October mwaka 1961. Kwa sasa ana umri wa miaka 58. Atafikisha umri wa miaka 60 October 06 mwaka 2021. Hivyo nadhani kwa mujibu wa KATIBA Assad alipaswa kustaafu nafasi yake ya CAG akifikisha umri huo, na si kwa hiki kinachoitwa "miaka mitano". I stand to be corrected. Hoja hujibiwa kwa hoja, sio bunduki.!
1.0 Kwa mazingira haya hana sifa ya kuwa auditor kwa kuwa amesajiliwa na NBAA kama mhasibu na sio auditor. Auditor kwa sheria ilivyo anaweza akawa mhasibu ila mhasibu sio auditor. Ina maana auditor ni superior kuliko mhasibu.
2.0 Hayuko kwenye active members wa 1.7.2019 yaani (2018/2019). Hivyo hana Certificate of Practice hata ya uhasibu ya 2018/2019.
Nimeona kuna migawanyiko ya hoja, upande wa kusifu na kuabudu unaongonzwa na VIBAKA wa Lumumba wao wanatetea uteuzi huu kwakutumia Sheria iliyoanzisha hiyo Ofisi( The National Audit Act 2008) inayo-specify 5 years terms na umri ni 65 year. Na kwamba hapa Rais ndipo katumia.
Upande wa kundi jadidi lenye akili na weledi, lenye busara na hekima ya nera una hoja za kikatiba sio za kisheria. Ikulu imeeleza kuwa Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Prof.Mussa Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano kwenye nafasi hiyo.
Wakili msomi Emmanuel Chengula anafafanua kwa kusema kwamba, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (ambayo ndio sheria mama) haelezi hicho kinachoitwa "kipindi cha miaka mitano"
Katiba inaeleza kuwa CAG atakoma utumishi wake atakapotimiza umri wa miaka 60. Yani akifikisha umri wa miaka 60 anapumzika bila kujalisha ametumikia nafasi hiyo kwa muda gani. Iwe miezi miwili, miaka nane, au miaka kumi.
Ndio maana maCAG wote waliotangulia wameongoza ofisi hiyo kwa vipindi tofauti. Mzee Mohamed Aboud aliongoza kwa miaka 27 tangu 1969 hadi 1996. Thomas Kiama akaongoza kwa miaka 9 tangu 1996 hadi 2005. Ludovick Utouh akaongoza kwa miaka 8 tangu 2006 hadi 2014. Sasa hii kauli ya kusema Assad amemaliza kipindi chake cha "miaka mitano" imetoka wapi?
Matakwa ya kikatiba ni umri wa miaka 60, unless aondolewe kwa kushindwa kutimiza majukumu yake. Na ikitokea hivyo Katiba imeweka utaratibu wa kumuondoa kwa kuunda tume.
Lakini taarifa ya Ikulu inaeleza Assad amemaliza kipindi chake cha miaka mitano. Je hiki kipindi cha miaka mitano Ikulu wamekitoa wapi? Kwenye sheria ipi? Kama ipo sheria hiyo ipo ni batili maana inapingana na katiba.
Na kwa kawaida unapotokea mgogoro kati ya sheria na katiba, basi Katiba ndiyo inayoshika hatamu (When a state law conflicts with a Constitution, then constitution prevails because constitution rules supreme above all state laws).
_
Prof.Assad amezaliwa tar.06 October mwaka 1961. Kwa sasa ana umri wa miaka 58. Atafikisha umri wa miaka 60 October 06 mwaka 2021. Hivyo kwa mujibu wa KATIBA alipaswa kustaafu nafasi yake ya CAG akifikisha umri huo, na si kwa hiki kinachoitwa "miaka mitano".
Kumbuka, Kicheere alitumbuliwa June 8, 2019 baada ya kutuhumiwa na wafanyabiashara kuwafanyia bugudha na kuua biashara zao, Alikuwa kamishna wa TRA. Leo kateuliwa kuwa CAG!
Nchi ina maigizo mengi hii. Bahati mbaya wanaoigiziwa hawajui lolote. Charles Kicheere alitumbuliwa kwa tuhuma za uzembe katika usimamizi wa TRA na kubugudhi wafanyabiashara sasa ameteuliwa anakwenda kuwa Msimamizi wa uadilifu katika mifumo ya fedha na UKAGUZI.
Mtu aliyeonekana kupwaya TRA (Kicheere) anapewa sasa kwenda kusimamia UKAGUZI wa mahesabu ya serikali. Kusimamia ukusanyaji wa mapato alishindwa, tukaaminishwa hivyo, ataweza kweli kudhibiti na kukagua HESABU za umma? Anyways, tuendelee kuona maajabu!
Wakili Chengula amemaliza kwakusema, I stand to be corrected.!
Katika hatua nyingine, Mbunge Zitto Kabwe ameongeza utata wa uteuzi wa CAG mpya kuonyesha kuwa hana sifa ya kushika ofisi hiyo kubwa ya umma iliyoanzishwa na katiba ya nchi sio na sheria,
Zitto anasema, "Charles Kicheere hana sifa za kuwa CAG kwa mujibu wa Katiba. Hana record ya ku-practice Auditing. Rais Alipomwondoa Kicheere TRA alimsema kuwa hajui kazi. Leo anampatia kazi kubwa hii huku akiwaacha 4 Deputies CAG. Uteuzi huu ni wa kuficha wizi (miradi mikubwa)"
CAG Musa Asad ameonekana kushangazwa na uteuzi huo na amenukuliwa na chombo cha habari kuwa hata taarifa hizo na yeye yuko katika majukumu ya kiutendaji. Hapa ndipo mkanganyiko unapozidi.
Kwa maoni yangu, nawauliza, ni lini utawala huu uliwahi kufuata sheria na katiba ya nchi kwa 100% katika utendaji wake? Mnakumbuka kesi ya uteuzi wa AG?