Yaliyojiri katika Mkutano Mkuu wa CHADEMA Desemba 18, 2019 katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar

Yaliyojiri katika Mkutano Mkuu wa CHADEMA Desemba 18, 2019 katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar

Mikutano mikuu ya vyama vya siasa ikiwemo CCM huhudhuriwa na vyama rafiki toka nchi mbalimmbali Duniani.Chadema naona tu akina Kambaya wa CUF ndio wageni hakuna wengine toka nje ya nchi?
 
Naona umepaniki,jikite kwenye uzinduzi wa jengo chato maana pamedoda sana.Leo habari ya mjini ni mkutano mkuu wa chama la wana tu
 
Mbowe alibadili gia angani kachukua mpunga wa nguvu kutoka kwa Lowassa kagawana na mkwe wake Mtei! Sasa yuko anakula luzuku mil326 kila mwezi anawaadaa wanachama na uchaguzi uchwara! Mbona hataki kuachia kiti?
 
Chadema ndio habari..✌🏾✌🏾✌🏾💪🏾💪🏾💪🏾
Mwanza kulidoda na Chatto kumedoda leo vibaya sana. CCM imekataliwa duniani na mbinguni, Tanganyika na Zanzibar. Mbowe kiboko ya MaCCM. Umayavuruga hayapati usingizi. Yanakesha na kucheketuka wachawi hawa.

#MWAMBATUVUSHE
 
Polisi Tanzania wamefanyakazi ya kukitangaza chama jana...
Huku kwetu viongozi wa serikali za mitaa wanapata tabu sana! Wananchi wanawakataa kwa swali kwamba ni nani kakuchagua? kama ni matatizo tutaangalia sisi wenyewe namna ya kuyatatua.
 
Kipfupi Dr Slaa kaondoka na vyama vyote rafiki vya chadema vya ulaya na Marekani Lowasa kaondoka na Kenyatta na Chama chake hawajahudhuriaha Kenyatta tu hapo hawakutuma wajumbe.

Raila odinga na Odm yake waliokuwa rafiki wa Chadema zamani hawajafika.

Wamebaki na FNL ya Burundi tu .Inatisha
 
Chadema ndio habari..✌🏾✌🏾✌🏾💪🏾💪🏾💪🏾
Mwanza kulidoda na Chatto kumedoda leo vibaya sana. CCM imekataliwa duniani na mbinguni, Tanganyika na Zanzibar. Mbowe kiboko ya MaCCM. Umayavuruga hayapati usingizi. Yanakesha na kucheketuka wachawi hawa.

#MWAMBATUVUSHE
Ila wewe jamaa kilazaa
 
Kipfupi Dr Slaa kaondoka na vyama vyote rafiki vya chadema vya ulaya na Marekani Lowasa kaondoka na Kenyatta na Chama chake hawajahudhuriaha Kenyatta tu hapo hawakutuma wajumbe.

Raila odinga na Odm yake waliokuwa rafiki wa Chadema zamani hawajafika.

Wamebaki na FNL ya Burundi tu .Inatisha
Huyuhuyu dokta mihogo anayeshauriwa na mushumbusi.
 
WanaJF duniani kote,Wasalaam!

Ni asubuhi tulivu kabisa katika jiji la Dar es Salaam huku habari kubwa inayovuma ikiwa ni mkutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA chenye wanachama milioni 6 wenye kadi.

Kama ripota wa JF nipo hapa Mlimani City nimekesha kwa lengo moja tu la kuihabarisha dunia kupitia JF kila kitakachojiri.

Leo ni hitimisho la zoezi refu la uchaguzi ambapo Mkutano mkuu utamchagua Mwenyekiti mpya na Makamu wake wawili.

Hata hivyo kuna dosari kidogo ilmetokea kwenye mkesha wa mkutano mkuu ambapo Polisi wenye magari na silaha walivamia eneo la Mlimani City na kushusha bendera zote za CHADEMA zilizopambwa kuashiria Mkutano Mkuu huu.

Haijajulikana hasa sababu ni nini kwa sababu Chama Cha Mapinduzi kinapofanya Mkutano wake Mkuu jijini Dodoma Mji wote na viunga vyake hupambwa kwa bendera za CCM.

Kwa sasa asubuhi hii tayari maandalizi yote ya ukumbi utakakofanyika mkutano mkuu yamekamilika. Tunatarajia takribani wajumbe 1300 kuhudhuria mkutano mkuu huu.Pia wageni wengi wanatarajiwa kuhudhuria wakiwemo viongozi wa vyama vyote vya siasa,mashiriia ya kimataifa ya ndani na nje, viongozi wa dini nk.

Vyombo vyote vya habari vya ndani na nje vimealikwa vikiwemo CNN na BBC.

Tunatarajia kuwaletea Live updates hapa kwa kila kitakachotokea.

View attachment 1296376

View attachment 1296132


View attachment 1296101

















Updates No 2
Mkutano Mkuu umeanza rasmi na viongozi wakuu wameshaingia wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe.

Kwa sasa Meya wa DSM Issaya Mwita ameitwa kuwakaribizha wageni kwenye mkutano mkuu huu

Kwa sasa wankaribishwa na kutambuliwa wageni mbalimbali wa vyama vya siasa vikiwemo NCCR, NLD, CUF, CCK, TLP nk

Wageni wengine waliotambuliwa ni kutoka Taasisi mbalimbali kama Mtandao wa jinsia TZ,Repoa,Walemavu nk Pia wapo viongozi wakuu wa dini.Pia yupo Naibu Msajili wa vyama vya siasa Sixty Nyahoza.

Ubalozi wa Marekani umewakilishwa na wajumbe watatu ambao wamekwisha fika mpaka sasa.

Msomi Dr Azaveli Lwaitama ndiye anayetoa salaam katika mkutano mkuu.Anashutumu watu wasiopenda demokrasia.Na amesema yeye ni mwanachama wa Chadema.

Sasa anatoa salaam mbunge kutoka Burundi wa chama cha FNL aliyekuja kuwakilisha Burundi.Anatoa salaam kwa Kiswahili na kuchanganya na kiingereza.Ujumbe wake mkubwa ameomba CDM wasikate tamaa

Viongozi wa dini sasa wanazungumza ambapo Sheikh Salum Kundecha Amir wa Shura ya Maimamu ameongea kwa niaba ya waislam.Kwa upandecwa Wakristo anayezungumza ni Askofu Mkuu wa Makanisa ya Moravian Tanzania Emmaus Mwamakula.Askofu Mkuu Mwamakula ameelezea kuhusu haki na ustawi katika kuimarisha demokrasia.

Viongozi wa kanda sasa ndiyo wamekaribishwa kutoa salaam kwa niaba ya kanda zao na ameanza Mwenyekiti wa Kanda ya Pemba akifuatiwa na Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini na baada ya hapo Kanda ya Magharibi

Kwa ujumla viongozi wengi waliozungumza hasa wa vyama vya upinzani na viongozi wa dini wamemwagia sifa Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa hotuba yake aliyoitoa Mwanza na kunyoosha mkono wa maridhiano kwa serikali.

Baada ya viongozi wote wa Kanda kuzungumza ameitwa Msanii Mbunge aa Mikumi Prof Jay kutumbuiza na ameshangiliwa sana na wajumbe.

Baada ya burudani wameanza kuitwa viongozi wa Mabaraza na wameanza viongozi wa Bavicha.Mwenyekiti wa Bavicha John Pambalu amelaani kufukuzwa chuo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi na kusema Bavicha imeshaongea na wanasheria kuona namna ya kuwasaidia.

Salaam za pili za mabaraza zimetoka kwa Baraza la Wazee na katika salaam zake Mwenyekiti wa Wazee amelaani hujuma mbalimbali zinazofanywa dhidi ya kukandamiza demokrasia nchini.Ametoa wito kwa Rais Magufuli kuanza mazungumzo ya kuimarisha demokrasia nchini.

Mwisho limeitwa Baraza la Wanawake Bawacha na Mwenyekiti wake Halima Mdee ambaye ametoa wito wanawake waendelee kuheshimiwa ndani ya Chadema kwani wameonyesha uwezo mkubwa katika kuongoza Chadema na kusema chama kwa ujumla kimeamua kuwekeza kwa wanawake

Baada ya Salaam za mabaraza sasa inafuata burudani kutoka kwa Mbunge Joseph Mbilinyi ikiwa nu kuwaweka watu sawa kwa ajili ya kumkaribisha Mwenyekiti Freeman Mbowe kuhutubia.

Kabla Mwenyekiti kuhutubia Lazaro Nyalandu na Esther Bulaya wameitwa kwa dakika chache kuzungumza na wajumbe.Nyalandu amesema aliamua kuhamia Chadema baada ya kuona CCM ya sasa imeacha njia aliyoasisi baba wa Taifa Mwl Nyerere.Nyalandu amelaani dola kupokonya mamlaka ya Bunge na Mahakama na ndiyo sababu kubwa ya kuachana na chama hicho na kujiunga Chadema.Amesema anasimama katika mkutano mkuu kama Nabii Ezekiel wa Biblia kwa kuiambia CCM anguko lao limefika.Nyalandu amekula kiapo mbele ya mkutano mkuu atasimama na Chadema mpaka mwisho wa Uhai wake na atailinda Chadema mpaka mwusho wake.

Zinafuatia sasa Salaam kutoka Brussels Ubelgiji ambapo Katibu Mkuu amekuja kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Antipas Lissu azungumze na wajumbe wote.Lissu ametoa salaam kwa njia ya skype na kupongeza mno kwa kazi kubwa iliyofanyika na Chadema kuzidi kuimarika.Lissu kasema tayari amepona na amekuomba chama kiandae mazingira salama ya yeye kurejea nyumbani.

Updates No 3..
Sasa ni Mwenyekiti Freeman Mbowe anahutubia rasmi wajumbe na Taifa kwa ujumla

Mwenyekiti Mbowe ameelezea mambo mengi na kubwa ni kuomba wajumbe wa Mkutano Mkuu waridhie mabadiliko ya Katiba ili kuongeza adavya mwaka ya uanachama kutoka shilingi 1,000 mpaka shilingi 2,500.Amesema kwa Ada hiyo chama kitakuwa na uwezo wa kukusanya shilingi bilioni 15 kwa mwaka kwa idadi ya wanachama milioni 6 na laki 5 wenye kadi

Pia Mbowe amezindua rasmi mfumo wa Chadema Digital ambapo wanachama eatatumia simu zao kulipa ada na kupata Taarifa zote muhimu

Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika Mbowe ametoa tamko rasmi la chama kwamba uchaguzi ule ni Haramu na Hautambuliki.Kutokana na sababu hiyo Mbowe ameagiza waliokuwa wagombea wote wa Chadema kote nchini kuunda serikali vivuli kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Mbowe amesifu kampeni ya Chadema ni Msingi ambapo amesema walizunguka kila kijiji nchi nzima na kuandikisha wanachama milioni 6 na nusu.Kiongozi huyo amesema dhihirisho la hicho kilichofanyika ni jinsi Mkutano Mkuu huu ulivyopendeza na kufurika wajumbe

Mbowe kwa kutumia nafasi yake kama Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini amesema ataongoza mazungumzo ya kuunda umoja wwnye nguvu yatakayowahusisha vyama vyote vya siasa,viongozi wa taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
YANAYOJITI YA NN WAKATI N KUPOTEZA PESA TU MWENYEKITI MNAMJUA
MAKAMU MNAMJUA
 
Wamekwenda kupata msosi,hadi kesho saa 4 asubuhi.
 
Back
Top Bottom