WanaJF duniani kote,Wasalaam!
Ni asubuhi tulivu kabisa katika jiji la Dar es Salaam huku habari kubwa inayovuma ikiwa ni mkutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA chenye wanachama milioni 6 wenye kadi.
Kama ripota wa JF nipo hapa Mlimani City nimekesha kwa lengo moja tu la kuihabarisha dunia kupitia JF kila kitakachojiri.
Leo ni hitimisho la zoezi refu la uchaguzi ambapo Mkutano mkuu utamchagua Mwenyekiti mpya na Makamu wake wawili.
Hata hivyo kuna dosari kidogo ilmetokea kwenye mkesha wa mkutano mkuu ambapo Polisi wenye magari na silaha walivamia eneo la Mlimani City na kushusha bendera zote za CHADEMA zilizopambwa kuashiria Mkutano Mkuu huu.
Haijajulikana hasa sababu ni nini kwa sababu Chama Cha Mapinduzi kinapofanya Mkutano wake Mkuu jijini Dodoma Mji wote na viunga vyake hupambwa kwa bendera za CCM.
Kwa sasa asubuhi hii tayari maandalizi yote ya ukumbi utakakofanyika mkutano mkuu yamekamilika. Tunatarajia takribani wajumbe 1300 kuhudhuria mkutano mkuu huu.Pia wageni wengi wanatarajiwa kuhudhuria wakiwemo viongozi wa vyama vyote vya siasa,mashiriia ya kimataifa ya ndani na nje, viongozi wa dini nk.
Vyombo vyote vya habari vya ndani na nje vimealikwa vikiwemo CNN na BBC.
Tunatarajia kuwaletea Live updates hapa kwa kila kitakachotokea.
View attachment 1296376
View attachment 1296132
View attachment 1296101
Updates No 2
Mkutano Mkuu umeanza rasmi na viongozi wakuu wameshaingia wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe.
Kwa sasa Meya wa DSM Issaya Mwita ameitwa kuwakaribizha wageni kwenye mkutano mkuu huu
Kwa sasa wankaribishwa na kutambuliwa wageni mbalimbali wa vyama vya siasa vikiwemo NCCR, NLD, CUF, CCK, TLP nk
Wageni wengine waliotambuliwa ni kutoka Taasisi mbalimbali kama Mtandao wa jinsia TZ,Repoa,Walemavu nk Pia wapo viongozi wakuu wa dini.Pia yupo Naibu Msajili wa vyama vya siasa Sixty Nyahoza.
Ubalozi wa Marekani umewakilishwa na wajumbe watatu ambao wamekwisha fika mpaka sasa.
Msomi Dr Azaveli Lwaitama ndiye anayetoa salaam katika mkutano mkuu.Anashutumu watu wasiopenda demokrasia.Na amesema yeye ni mwanachama wa Chadema.
Sasa anatoa salaam mbunge kutoka Burundi wa chama cha FNL aliyekuja kuwakilisha Burundi.Anatoa salaam kwa Kiswahili na kuchanganya na kiingereza.Ujumbe wake mkubwa ameomba CDM wasikate tamaa
Viongozi wa dini sasa wanazungumza ambapo Sheikh Salum Kundecha Amir wa Shura ya Maimamu ameongea kwa niaba ya waislam.Kwa upandecwa Wakristo anayezungumza ni Askofu Mkuu wa Makanisa ya Moravian Tanzania Emmaus Mwamakula.Askofu Mkuu Mwamakula ameelezea kuhusu haki na ustawi katika kuimarisha demokrasia.
Viongozi wa kanda sasa ndiyo wamekaribishwa kutoa salaam kwa niaba ya kanda zao na ameanza Mwenyekiti wa Kanda ya Pemba akifuatiwa na Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini na baada ya hapo Kanda ya Magharibi
Kwa ujumla viongozi wengi waliozungumza hasa wa vyama vya upinzani na viongozi wa dini wamemwagia sifa Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa hotuba yake aliyoitoa Mwanza na kunyoosha mkono wa maridhiano kwa serikali.
Baada ya viongozi wote wa Kanda kuzungumza ameitwa Msanii Mbunge aa Mikumi Prof Jay kutumbuiza na ameshangiliwa sana na wajumbe.
Baada ya burudani wameanza kuitwa viongozi wa Mabaraza na wameanza viongozi wa Bavicha.Mwenyekiti wa Bavicha John Pambalu amelaani kufukuzwa chuo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi na kusema Bavicha imeshaongea na wanasheria kuona namna ya kuwasaidia.
Salaam za pili za mabaraza zimetoka kwa Baraza la Wazee na katika salaam zake Mwenyekiti wa Wazee amelaani hujuma mbalimbali zinazofanywa dhidi ya kukandamiza demokrasia nchini.Ametoa wito kwa Rais Magufuli kuanza mazungumzo ya kuimarisha demokrasia nchini.
Mwisho limeitwa Baraza la Wanawake Bawacha na Mwenyekiti wake Halima Mdee ambaye ametoa wito wanawake waendelee kuheshimiwa ndani ya Chadema kwani wameonyesha uwezo mkubwa katika kuongoza Chadema na kusema chama kwa ujumla kimeamua kuwekeza kwa wanawake
Baada ya Salaam za mabaraza sasa inafuata burudani kutoka kwa Mbunge Joseph Mbilinyi ikiwa nu kuwaweka watu sawa kwa ajili ya kumkaribisha Mwenyekiti Freeman Mbowe kuhutubia.
Kabla Mwenyekiti kuhutubia Lazaro Nyalandu na Esther Bulaya wameitwa kwa dakika chache kuzungumza na wajumbe.Nyalandu amesema aliamua kuhamia Chadema baada ya kuona CCM ya sasa imeacha njia aliyoasisi baba wa Taifa Mwl Nyerere.Nyalandu amelaani dola kupokonya mamlaka ya Bunge na Mahakama na ndiyo sababu kubwa ya kuachana na chama hicho na kujiunga Chadema.Amesema anasimama katika mkutano mkuu kama Nabii Ezekiel wa Biblia kwa kuiambia CCM anguko lao limefika.Nyalandu amekula kiapo mbele ya mkutano mkuu atasimama na Chadema mpaka mwisho wa Uhai wake na atailinda Chadema mpaka mwusho wake.
Zinafuatia sasa Salaam kutoka Brussels Ubelgiji ambapo Katibu Mkuu amekuja kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Antipas Lissu azungumze na wajumbe wote.Lissu ametoa salaam kwa njia ya skype na kupongeza mno kwa kazi kubwa iliyofanyika na Chadema kuzidi kuimarika.Lissu kasema tayari amepona na amekuomba chama kiandae mazingira salama ya yeye kurejea nyumbani.
Updates No 3..
Sasa ni Mwenyekiti Freeman Mbowe anahutubia rasmi wajumbe na Taifa kwa ujumla
Mwenyekiti Mbowe ameelezea mambo mengi na kubwa ni kuomba wajumbe wa Mkutano Mkuu waridhie mabadiliko ya Katiba ili kuongeza adavya mwaka ya uanachama kutoka shilingi 1,000 mpaka shilingi 2,500.Amesema kwa Ada hiyo chama kitakuwa na uwezo wa kukusanya shilingi bilioni 15 kwa mwaka kwa idadi ya wanachama milioni 6 na laki 5 wenye kadi
Pia Mbowe amezindua rasmi mfumo wa Chadema Digital ambapo wanachama eatatumia simu zao kulipa ada na kupata Taarifa zote muhimu
Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika Mbowe ametoa tamko rasmi la chama kwamba uchaguzi ule ni Haramu na Hautambuliki.Kutokana na sababu hiyo Mbowe ameagiza waliokuwa wagombea wote wa Chadema kote nchini kuunda serikali vivuli kwa ajili ya kuhudumia wananchi.
Mbowe amesifu kampeni ya Chadema ni Msingi ambapo amesema walizunguka kila kijiji nchi nzima na kuandikisha wanachama milioni 6 na nusu.Kiongozi huyo amesema dhihirisho la hicho kilichofanyika ni jinsi Mkutano Mkuu huu ulivyopendeza na kufurika wajumbe
Mbowe kwa kutumia nafasi yake kama Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini amesema ataongoza mazungumzo ya kuunda umoja wwnye nguvu yatakayowahusisha vyama vyote vya siasa,viongozi wa taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.