Yaliyojiri katika Mkutano Mkuu wa CHADEMA Desemba 18, 2019 katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar

Yaliyojiri katika Mkutano Mkuu wa CHADEMA Desemba 18, 2019 katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar

WanaJF duniani kote,Wasalaam!

Ni asubuhi tulivu kabisa katika jiji la Dar es Salaam huku habari kubwa inayovuma ikiwa ni mkutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA chenye wanachama milioni 6 wenye kadi.

Kama ripota wa JF nipo hapa Mlimani City nimekesha kwa lengo moja tu la kuihabarisha dunia kupitia JF kila kitakachojiri.

Leo ni hitimisho la zoezi refu la uchaguzi ambapo Mkutano mkuu utamchagua Mwenyekiti mpya na Makamu wake wawili.

Hata hivyo kuna dosari kidogo ilmetokea kwenye mkesha wa mkutano mkuu ambapo Polisi wenye magari na silaha walivamia eneo la Mlimani City na kushusha bendera zote za CHADEMA zilizopambwa kuashiria Mkutano Mkuu huu.

Haijajulikana hasa sababu ni nini kwa sababu Chama Cha Mapinduzi kinapofanya Mkutano wake Mkuu jijini Dodoma Mji wote na viunga vyake hupambwa kwa bendera za CCM.

Kwa sasa asubuhi hii tayari maandalizi yote ya ukumbi utakakofanyika mkutano mkuu yamekamilika. Tunatarajia takribani wajumbe 1300 kuhudhuria mkutano mkuu huu.Pia wageni wengi wanatarajiwa kuhudhuria wakiwemo viongozi wa vyama vyote vya siasa,mashiriia ya kimataifa ya ndani na nje, viongozi wa dini nk.

Vyombo vyote vya habari vya ndani na nje vimealikwa vikiwemo CNN na BBC.

Tunatarajia kuwaletea Live updates hapa kwa kila kitakachotokea.

View attachment 1296376

View attachment 1296132


View attachment 1296101

















Updates No 2
Mkutano Mkuu umeanza rasmi na viongozi wakuu wameshaingia wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe.

Kwa sasa Meya wa DSM Issaya Mwita ameitwa kuwakaribizha wageni kwenye mkutano mkuu huu

Kwa sasa wankaribishwa na kutambuliwa wageni mbalimbali wa vyama vya siasa vikiwemo NCCR, NLD, CUF, CCK, TLP nk

Wageni wengine waliotambuliwa ni kutoka Taasisi mbalimbali kama Mtandao wa jinsia TZ,Repoa,Walemavu nk Pia wapo viongozi wakuu wa dini.Pia yupo Naibu Msajili wa vyama vya siasa Sixty Nyahoza.

Ubalozi wa Marekani umewakilishwa na wajumbe watatu ambao wamekwisha fika mpaka sasa.

Msomi Dr Azaveli Lwaitama ndiye anayetoa salaam katika mkutano mkuu.Anashutumu watu wasiopenda demokrasia.Na amesema yeye ni mwanachama wa Chadema.

Sasa anatoa salaam mbunge kutoka Burundi wa chama cha FNL aliyekuja kuwakilisha Burundi.Anatoa salaam kwa Kiswahili na kuchanganya na kiingereza.Ujumbe wake mkubwa ameomba CDM wasikate tamaa

Viongozi wa dini sasa wanazungumza ambapo Sheikh Salum Kundecha Amir wa Shura ya Maimamu ameongea kwa niaba ya waislam.Kwa upandecwa Wakristo anayezungumza ni Askofu Mkuu wa Makanisa ya Moravian Tanzania Emmaus Mwamakula.Askofu Mkuu Mwamakula ameelezea kuhusu haki na ustawi katika kuimarisha demokrasia.

Viongozi wa kanda sasa ndiyo wamekaribishwa kutoa salaam kwa niaba ya kanda zao na ameanza Mwenyekiti wa Kanda ya Pemba akifuatiwa na Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini na baada ya hapo Kanda ya Magharibi

Kwa ujumla viongozi wengi waliozungumza hasa wa vyama vya upinzani na viongozi wa dini wamemwagia sifa Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa hotuba yake aliyoitoa Mwanza na kunyoosha mkono wa maridhiano kwa serikali.

Baada ya viongozi wote wa Kanda kuzungumza ameitwa Msanii Mbunge aa Mikumi Prof Jay kutumbuiza na ameshangiliwa sana na wajumbe.

Baada ya burudani wameanza kuitwa viongozi wa Mabaraza na wameanza viongozi wa Bavicha.Mwenyekiti wa Bavicha John Pambalu amelaani kufukuzwa chuo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi na kusema Bavicha imeshaongea na wanasheria kuona namna ya kuwasaidia.

Salaam za pili za mabaraza zimetoka kwa Baraza la Wazee na katika salaam zake Mwenyekiti wa Wazee amelaani hujuma mbalimbali zinazofanywa dhidi ya kukandamiza demokrasia nchini.Ametoa wito kwa Rais Magufuli kuanza mazungumzo ya kuimarisha demokrasia nchini.

Mwisho limeitwa Baraza la Wanawake Bawacha na Mwenyekiti wake Halima Mdee ambaye ametoa wito wanawake waendelee kuheshimiwa ndani ya Chadema kwani wameonyesha uwezo mkubwa katika kuongoza Chadema na kusema chama kwa ujumla kimeamua kuwekeza kwa wanawake

Baada ya Salaam za mabaraza sasa inafuata burudani kutoka kwa Mbunge Joseph Mbilinyi ikiwa nu kuwaweka watu sawa kwa ajili ya kumkaribisha Mwenyekiti Freeman Mbowe kuhutubia.

Kabla Mwenyekiti kuhutubia Lazaro Nyalandu na Esther Bulaya wameitwa kwa dakika chache kuzungumza na wajumbe.Nyalandu amesema aliamua kuhamia Chadema baada ya kuona CCM ya sasa imeacha njia aliyoasisi baba wa Taifa Mwl Nyerere.Nyalandu amelaani dola kupokonya mamlaka ya Bunge na Mahakama na ndiyo sababu kubwa ya kuachana na chama hicho na kujiunga Chadema.Amesema anasimama katika mkutano mkuu kama Nabii Ezekiel wa Biblia kwa kuiambia CCM anguko lao limefika.Nyalandu amekula kiapo mbele ya mkutano mkuu atasimama na Chadema mpaka mwisho wa Uhai wake na atailinda Chadema mpaka mwusho wake.

Zinafuatia sasa Salaam kutoka Brussels Ubelgiji ambapo Katibu Mkuu amekuja kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Antipas Lissu azungumze na wajumbe wote.Lissu ametoa salaam kwa njia ya skype na kupongeza mno kwa kazi kubwa iliyofanyika na Chadema kuzidi kuimarika.Lissu kasema tayari amepona na amekuomba chama kiandae mazingira salama ya yeye kurejea nyumbani.

Updates No 3..
Sasa ni Mwenyekiti Freeman Mbowe anahutubia rasmi wajumbe na Taifa kwa ujumla

Mwenyekiti Mbowe ameelezea mambo mengi na kubwa ni kuomba wajumbe wa Mkutano Mkuu waridhie mabadiliko ya Katiba ili kuongeza adavya mwaka ya uanachama kutoka shilingi 1,000 mpaka shilingi 2,500.Amesema kwa Ada hiyo chama kitakuwa na uwezo wa kukusanya shilingi bilioni 15 kwa mwaka kwa idadi ya wanachama milioni 6 na laki 5 wenye kadi

Pia Mbowe amezindua rasmi mfumo wa Chadema Digital ambapo wanachama eatatumia simu zao kulipa ada na kupata Taarifa zote muhimu

Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika Mbowe ametoa tamko rasmi la chama kwamba uchaguzi ule ni Haramu na Hautambuliki.Kutokana na sababu hiyo Mbowe ameagiza waliokuwa wagombea wote wa Chadema kote nchini kuunda serikali vivuli kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Mbowe amesifu kampeni ya Chadema ni Msingi ambapo amesema walizunguka kila kijiji nchi nzima na kuandikisha wanachama milioni 6 na nusu.Kiongozi huyo amesema dhihirisho la hicho kilichofanyika ni jinsi Mkutano Mkuu huu ulivyopendeza na kufurika wajumbe

Mbowe kwa kutumia nafasi yake kama Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini amesema ataongoza mazungumzo ya kuunda umoja wwnye nguvu yatakayowahusisha vyama vyote vya siasa,viongozi wa taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
Akili ni nywele na kila mtu anazake. Mpaka sasa sijasikia sera za wagombea kwa kuwa agenda ni uchanguzi wa Ngazi ya juu.
So far ni mipasho na mbwembwe.
Pasikali amejisemea Hata sasa Hamjui mlifanyalo,
 
Ni heri hata kampeni hiyo ingefanywa na mzee Hashimu Rungwe wa Chauma au Mbatia wa Nccr mageuzi lakini siyo hawa CUF waliosambaratisha UKAWA.

Chadema leo inalamba matapishi yake?.......ajabu kabisa.

Maendeleo hayana vyama!
 
Ubarikiwe
WanaJF duniani kote,Wasalaam!

Ni asubuhi tulivu kabisa katika jiji la Dar es Salaam huku habari kubwa inayovuma ikiwa ni mkutano mkuu wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA chenye wanachama milioni 6 wenye kadi.

Kama ripota wa JF nipo hapa Mlimani City nimekesha kwa lengo moja tu la kuihabarisha dunia kupitia JF kila kitakachojiri.

Leo ni hitimisho la zoezi refu la uchaguzi ambapo Mkutano mkuu utamchagua Mwenyekiti mpya na Makamu wake wawili.

Hata hivyo kuna dosari kidogo ilmetokea kwenye mkesha wa mkutano mkuu ambapo Polisi wenye magari na silaha walivamia eneo la Mlimani City na kushusha bendera zote za CHADEMA zilizopambwa kuashiria Mkutano Mkuu huu.

Haijajulikana hasa sababu ni nini kwa sababu Chama Cha Mapinduzi kinapofanya Mkutano wake Mkuu jijini Dodoma Mji wote na viunga vyake hupambwa kwa bendera za CCM.

Kwa sasa asubuhi hii tayari maandalizi yote ya ukumbi utakakofanyika mkutano mkuu yamekamilika. Tunatarajia takribani wajumbe 1300 kuhudhuria mkutano mkuu huu.Pia wageni wengi wanatarajiwa kuhudhuria wakiwemo viongozi wa vyama vyote vya siasa,mashiriia ya kimataifa ya ndani na nje, viongozi wa dini nk.

Vyombo vyote vya habari vya ndani na nje vimealikwa vikiwemo CNN na BBC.

Tunatarajia kuwaletea Live updates hapa kwa kila kitakachotokea.

View attachment 1296376

View attachment 1296132


View attachment 1296101

Updates No 2
Muda huu kwa sasa tayari ukumbi umefurika wajumbe na vikundi mbalimbali vinatumbuiza kusubiri ujio wa Kiongozi Mkuu wa chama Freeman Mbowe kuingia ukumbini akiwa na msafara wake.

Naam, kwa sasa Mwenyekiti Freeman Mbowe anawasili huku ukumbi ukiwa umelipuka kwa shangwe hoihoi nderemo na vifijo.Wajumbe wote wamesimama kama heshima kwa shujaa huyu wa mageuzi nchini.

Mkutano Mkuu umeanza rasmi na viongozi wakuu wameshaingia wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe na kukaa kwenye viti vyao.

Kwa sasa Meya wa DSM Issaya Mwita ameitwa kuwakaribizha wageni kwenye mkutano mkuu huu

Kwa sasa wankaribishwa na kutambuliwa wageni mbalimbali wa vyama vya siasa vikiwemo NCCR, NLD, CUF, CCK, TLP nk

Wageni wengine waliotambuliwa ni kutoka Taasisi mbalimbali kama Mtandao wa jinsia TZ,Repoa,Walemavu nk Pia wapo viongozi wakuu wa dini.Pia yupo Naibu Msajili wa vyama vya siasa Sixty Nyahoza.

Ubalozi wa Marekani umewakilishwa na wajumbe watatu ambao wamekwisha fika mpaka sasa.

Msomi Dr Azaveli Lwaitama ndiye anayetoa salaam katika mkutano mkuu.Anashutumu watu wasiopenda demokrasia.Na amesema yeye ni mwanachama wa Chadema."Hiki Chama kina maneno mawili muhimu sana, maneno hayo ni Maendeleo na Demokrasia, bila Demokrasia hakuna Maendeleo, Maendeleo yanaletwa na Demokrasia," Prof. Azavery Lwaitama amemalizia.

Sasa anatoa salaam mbunge kutoka Burundi wa chama cha FNL aliyekuja kuwakilisha Burundi.Anatoa salaam kwa Kiswahili na kuchanganya na kiingereza.Ujumbe wake mkubwa ameomba CDM wasikate tamaa

Viongozi wa dini sasa wanazungumza ambapo Sheikh Salum Kundecha Amir wa Shura ya Maimamu ameongea kwa niaba ya waislam.Kwa upandecwa Wakristo anayezungumza ni Askofu Mkuu wa Makanisa ya Moravian Tanzania Emmaus Mwamakula.Askofu Mkuu Mwamakula ameelezea kuhusu haki na ustawi katika kuimarisha demokrasia.

Viongozi wa kanda sasa ndiyo wamekaribishwa kutoa salaam kwa niaba ya kanda zao na ameanza Mwenyekiti wa Kanda ya Pemba akifuatiwa na Mwenyekiti wa Kanda ya Kusini na baada ya hapo Kanda ya Magharibi

Kwa ujumla viongozi wengi waliozungumza hasa wa vyama vya upinzani na viongozi wa dini wamemwagia sifa Mwenyekiti Freeman Mbowe kwa hotuba yake aliyoitoa Mwanza na kunyoosha mkono wa maridhiano kwa serikali.

Baada ya viongozi wote wa Kanda kuzungumza ameitwa Msanii Mbunge aa Mikumi Prof Jay kutumbuiza na ameshangiliwa sana na wajumbe.

Baada ya burudani wameanza kuitwa viongozi wa Mabaraza na wameanza viongozi wa Bavicha.Mwenyekiti wa Bavicha John Pambalu amelaani kufukuzwa chuo kwa viongozi wa serikali ya wanafunzi na kusema Bavicha imeshaongea na wanasheria kuona namna ya kuwasaidia.

Salaam za pili za mabaraza zimetoka kwa Baraza la Wazee na katika salaam zake Mwenyekiti wa Wazee amelaani hujuma mbalimbali zinazofanywa dhidi ya kukandamiza demokrasia nchini.Ametoa wito kwa Rais Magufuli kuanza mazungumzo ya kuimarisha demokrasia nchini.

Mwisho limeitwa Baraza la Wanawake Bawacha na Mwenyekiti wake Halima Mdee ambaye ametoa wito wanawake waendelee kuheshimiwa ndani ya Chadema kwani wameonyesha uwezo mkubwa katika kuongoza Chadema na kusema chama kwa ujumla kimeamua kuwekeza kwa wanawake

Baada ya Salaam za mabaraza sasa inafuata burudani kutoka kwa Mbunge Joseph Mbilinyi ikiwa nu kuwaweka watu sawa kwa ajili ya kumkaribisha Mwenyekiti Freeman Mbowe kuhutubia.

Kabla Mwenyekiti kuhutubia Lazaro Nyalandu na Esther Bulaya wameitwa kwa dakika chache kuzungumza na wajumbe.Nyalandu amesema aliamua kuhamia Chadema baada ya kuona CCM ya sasa imeacha njia aliyoasisi baba wa Taifa Mwl Nyerere.Nyalandu amelaani dola kupokonya mamlaka ya Bunge na Mahakama na ndiyo sababu kubwa ya kuachana na chama hicho na kujiunga Chadema.Amesema anasimama katika mkutano mkuu kama Nabii Ezekiel wa Biblia kwa kuiambia CCM anguko lao limefika.Nyalandu amekula kiapo mbele ya mkutano mkuu atasimama na Chadema mpaka mwisho wa Uhai wake na atailinda Chadema mpaka mwusho wake.

Zinafuatia sasa Salaam kutoka Brussels Ubelgiji ambapo Katibu Mkuu amekuja kumkaribisha Mwanasheria Mkuu wa Chadema Tundu Antipas Lissu azungumze na wajumbe wote.Lissu ametoa salaam kwa njia ya skype na kupongeza mno kwa kazi kubwa iliyofanyika na Chadema kuzidi kuimarika.Lissu kasema tayari amepona na amekuomba chama kiandae mazingira salama ya yeye kurejea nyumbani.

Updates No 3..
Sasa ni Mwenyekiti Freeman Mbowe anahutubia rasmi wajumbe na Taifa kwa ujumla

Mwenyekiti Mbowe ameelezea mambo mengi na kubwa ni kuomba wajumbe wa Mkutano Mkuu waridhie mabadiliko ya Katiba ili kuongeza adavya mwaka ya uanachama kutoka shilingi 1,000 mpaka shilingi 2,500.Amesema kwa Ada hiyo chama kitakuwa na uwezo wa kukusanya shilingi bilioni 15 kwa mwaka kwa idadi ya wanachama milioni 6 na laki 5 wenye kadi

Pia Mbowe amezindua rasmi mfumo wa Chadema Digital ambapo wanachama eatatumia simu zao kulipa ada na kupata Taarifa zote muhimu

Kuhusu Uchaguzi wa Serikali za mitaa uliofanyika Mbowe ametoa tamko rasmi la chama kwamba uchaguzi ule ni Haramu na Hautambuliki.Kutokana na sababu hiyo Mbowe ameagiza waliokuwa wagombea wote wa Chadema kote nchini kuunda serikali vivuli kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Mbowe amesifu kampeni ya Chadema ni Msingi ambapo amesema walizunguka kila kijiji nchi nzima na kuandikisha wanachama milioni 6 na nusu.Kiongozi huyo amesema dhihirisho la hicho kilichofanyika ni jinsi Mkutano Mkuu huu ulivyopendeza na kufurika wajumbe

Mbowe kwa kutumia nafasi yake kama Kiongozi Mkuu wa Upinzani nchini amesema ataongoza mazungumzo ya kuunda umoja wwnye nguvu yatakayowahusisha vyama vyote vya siasa,viongozi wa taasisi mbalimbali na wananchi kwa ujumla kabla ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Mbowe amesikitishwa na hali iliyofikia sasa ya vyombo vya Habari kuogopa kutangaza habari za Chadema ambapo amesema waliwasiliana na vituo vyote vya Telesheni ili kutangaza mubashara mkutano mkuu Lakini wote waliogopa na kusema ni vigumu kwao kutangaza mkutano wa Chadema.

Updates No 4
Sekretariati ya Chadema imeamua kutoa Tuzo kwa utumishi uliotukuka kwa wanachama wawili waliotoa muda wao kuhamasisha zoezi la Chadema ni msingi lililozaa mafanikio makubwa kwa chama.Wanachama waliopewa tuzo hizo ni Agnesta Lambert na Freeman Mbowe.Hata hivyo wakati wa kutoa shukrani kwa tuzo hiyo Mwenyekiti Freeman Mbowe aliikataa tuzo hiyo na kusema iwaendee wanachama na viongozi wote waliojitolea muda wao kufanikisha zoezi hilo.

Baada ya hapo limefuatia zoezi la kuzindua sera za chama na viongozi wote wa Kanda wamekabidhiwa nakala kwa niaba ya Kanda zao na hatimaye kupiga picha ya Pamoja na Msajili Msaidizi wa vyama vya siasa nchini kama ishara ya uzindizi.

Na hapa ndipo umefika Mwisho wa sehemu yetu ya kwanza ambapo Mkutano Mkuu umeahirishwa kwa muda kwa ajili ya chakula na baada ya hapo itafuata sehemu ya pili ya uchaguzi mkuu wa chama.

Tunawashukuru wote kwa kuwa nasi hapa tangu Alfajiri ya leo.Mungu Awabariki sana.

#NoHateNoFear

Wasalaam
Molemo wa JF
Ubarkiwe sana, nimeanza kukufuatilia toka asubuhi hapa nasubiri matokeo ya uchaguzi. Umefanya kazi kubwa ningeijua hata Tigo pesa yako ningekupa hata soda. Sisi tuliombali na DSM tungeona kwenye magazeti kesho maana vituo vyote vimetishwa ole wake ataonesha live. Pole kwa kazi nzito
s
 
..No hate.

..No fear.

..kama CUF wameamua kujirekebisha sidhani kama ni jambo baya kushirikiana nao.
 
Ni heri hata kampeni hiyo ingefanywa na mzee Hashimu Rungwe wa Chauma au Mbatia wa Nccr mageuzi lakini siyo hawa CUF waliosambaratisha UKAWA.

Chadema leo inalamba matapishi yake?.......ajabu kabisa.

Maendeleo hayana vyama!
Kigogo 2014 alivimba bichwa akasahau kuwa siasa ni mchezo wa timing
 
Ni heri hata kampeni hiyo ingefanywa na mzee Hashimu Rungwe wa Chauma au Mbatia wa Nccr mageuzi lakini siyo hawa CUF waliosambaratisha UKAWA.

Chadema leo inalamba matapishi yake?.......ajabu kabisa.

Maendeleo hayana vyama!
Bwashee piga fundo moja la mbege ulete habari kamili hiyo kampeni imepigwaje? Mbona unarukaruka kama umepiga kiroba?
 
Na bado MaCCM lazima mnye si kwa kucheketuka huko na mambo yasio wahusu.
CHADEMA imewatia dole la kati KUDADEKI.
Ukilala CHADEMA na ukiamka CHADEMA
 
Hakuna mtu wa kumtoa Mbowe kwenye kiti anachotaka na baada ya Uchaguzi kumalizika, Mwambe atafukuzwa ndani ya CHADEMA!

Yaliyomkuta Zitto mwaka 2014 yanaenda kumpata Cecil Mwambe! Baada ya Uchaguzi wa ndani aanze kutafuta chama kingine mapema!
Pamoja na Mwambe, wengine watakaofukuzwa kwenye Chama ni Komu, Kubenea +/- Prof Safari. Rejea hotuba ya mh. Mbowe wakati akihutubia mkutano wa uchaguzi kanda ya kaskazini.
 
Back
Top Bottom