Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

asante Sana kwa kutujuza mkuu, kikwete ni mtu wa visasi, lowassa Mwaga Mboga tu, wao si wamemwaga ugali
 
Acha li chama life

Nukuu ya Makongoro Nyerere

Leo Dodoma
" Kama chama mnaona ni cha wazalendo, nashauri kaeni ila kama sio cha wazalendo uamuzi ni juu yenu"
 

Udini kivipi Mkuu embu fafanua?halafu inaelekea umekata tamaa na chama chako CCM,kwanini?
 
haya maono yako ni pofu, mapenzi na tamaa zako ndo unaita uchambuzi? Kikwete si wa kuyumbishwa kiasi hicho. Me nadhani huu ulikuwa wakati wa kuangalia Ukawa unafanya nini ili kuleta bidhaa bora sokoni na sio kuwa busy kufuatilia ccm ccm.
 
kwani kikwete sio Fisadi
 
Familia ya NYERERE IMEDHALILISHWA SANA......MIKOA YA MARA,MWANZA,SIMIYU,GEITA,shinyanga hakikisheni jina la mwalimu llinalindwa na kuheshimiwa.....
 
Hakuna mjumbe wa Ccm zaidi ya lowasa mwenyewe ambaye anaweza kusema hana imani na Jk hakuna coz whatver atakaye sema hilo ana majanga makubwa hizo ni mbwembwe tuu hakuna mjumbe anayeweza kusema hana imani na Jk

We una IMANI NAE??
 
Naipa pole sana familia nzima ya baba wetu wa Taifa na mama Maria Nyerere, tumeshindwa kuienzi legacy ya Mwl. Nyerere na CCM mmetufedhesha bara na wafuasi wa miiko aliyotuachia Baba wa Taifa
 
hueleweki ndugu naona ushapanic, hatuchagui machifu hapa, Familia Familia ndo nini???
 
chama kimevurugwa...ovias...wagombea uraisi walotajwa pia wamevurugwa....long live UKAWA
 

Nadhani Wewe Utakuwa Ni Mgeni Kwangu Na Kama Siyo Basi Utakuwa Ni Bonge La POPOMA Tena LILILOTUKUKA. Hakuna Ambaye Hajui Humu JF Kuwa Mimi Si Mtu Wa Lowassa au Membe Na Tokea Mwanzo Nilikuambia Na Hadi Nikaweka Nadhiri Humu JF Kuwa Lowassa Hatopita au Kupitishwa Na Nikaenda Mbele Zaidi Kusema Kuwa Mgombea Wa CCM Lazima Atatoka Kati Ya Dr. Magufuli au Professor Muhongo au Professor Mwandosya Na Maprofesa Wawili Wameshakatwa Na Kabaki Mtu Wangu Mmoja Tu Dr. Magufuli Na Ndiyo Huyo Huyo Atapitishwa Na CCM Tena Kwa Kura Nyingi Tu. Ukitaka Kuamini Haya Jaribu kupitia Posts Zangu Ujiridhishe. Na Kumtetea Lowassa Kama Kwanini Amekatwa Yawezekana Kwakuwa UELEWA Wako Ni Ndogo Pengine Kama Punje Za Mchanga Hukunielewa ILA Nilichokuwa Nakisisitiza Katika Hoja Yangu Ni Kitu Kiitwacho Political Equilibrium Ambapo Walitakiwa Ama Wote Wabakishwe ILI Waje Kuchinjiwa Katika 5 Bora au Basi Wote Wasiwepo Ili Kuwamaliza Kinguvu Lakini Kumwacha Mmoja Akipeta Ni Kuleta Hatari Na Mpasuko Mkubwa Ndani Ya Chama. Ni Imani Yangu Kwa Maelezo Haya Ya Kiufafanuzi Basi UPOPOMA Wako Sasa Utakuwa Ni Historia Na Tutaenda Sawa.
 
Hilo zee lipumzike tu anajiaibisha tu na njaa njaa zake

Ninawalaumu watoto wake kuendelea kumruhusu kusimama na kushiriki siasa katika umri ule. Kaichafua historia yake nzuri aliyoijenga kwa umri wake wote kwa kushabikia wapuuzi katika nchi
 
Huyo Mburushi ni mtumishi wa Caspian ya Rostam Aziz. .. wanaonekana pichani wamo Fadhili Ngajiro; Ole Porokwa; Omar Ng'wanang'wala na hapo ni hotelini St Gasper kambi ya Lowassa ambapo Leo waliwaita wajumbe kuwapa pesa wasusie NEC ama kufanya fujo na plan B awe Magufuli. Same place Kingunge alifanya press
Porokwa Katibu CCM Manyara na msaidizi wa Lowassa.
HAYO NDIYO MAELEZO YA ZILE PICHA ZA MUHINDI ALIYEKAMATWA NA MIHELA. Team Lowassa wanajipanga kumsupport Magufuli. Hili movie ni kiboko.
 

Attachments

  • 1436608413089.jpg
    65.7 KB · Views: 116
  • 1436608444410.jpg
    69.4 KB · Views: 115
Ule msemo aliyoutumia Mlm.Nyerere wakati wa kipindi cha Mrema ya kwamba ,,I cant let my country goes to the dogs" sasa umetimia, kitendo cha Kikwete kumpitisha Membe ambaye kuna tetesi ya kwamba ni ndugu yake wa damu hakijawahi kutokea ktk Historia ya Chama hicho, yaani Mwenyekiti wa Chama kumteua ndugu yake kuwa Mgombea Uraisi na hili la Januari Makamba ambaye nafasi kubwa aliyowahi kuishika ni unaibu Waziri tu tena wa Muhula mmoja na kuwaacha watu wengi ambao wana uzoefu mkubwa sana kama kina Mwandosya, n.w inatia mashaka ya kwamba nchi yetu sasa ,,has gone to the dogs"!

Kwa nini nasema hivyo ni kwamba Kikwete amefungua ukurasa mpya ambao haukuwepo Membe akiwa Riais naye atafanya kama alivyofanya ndugu yake Kikwete na kuleta ndugu yake pia labda Ridhwani...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…