Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine.
Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 11/01/2021
==========
Watuhumiwa wote wamekwishawasili katika ukumbi wa mahakama tayari kuanza kwa kesi.
Jaji: Ameingia sasa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa
Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe na wenzake
Wakili wa Serikali, Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula,
3. Jenitreza Kitali,
4. Nasorro Katuga,
5. Esther Martin,
6. Ignasi Mwinuka
7. Tulimanywa Majige
Wakili Peter Kibatala anawatambulisha Mawakili Wa Utetezi
1.Jeremiah Mtobesya
2.Michael Mwangasa
3.Seleman Matauka
4.Nashon Nkungu
5.Alex Massaba
6.Michael Lugina
7.Maria Mushi
8.Hadija Aron
9.Dickson Matata
10.Jonathan Mndeme
11.Fredrick Kihwelo
12.John Malya
Jaji: anawait Washitakiwa 1,2,3 na 4 Wanasimama Kuitikia
Wakili wa Serikali: Kwa Upande wetu tuna shahidi Mmoja kwa Leo na tupo tayari Kuendelea Kwa Upande wetu tupo tayari kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari na sisi Kuendelea
Wakili wa Serikali: Mmoja anatoka Kwenda Kumuita Shahidi Nje ya Chumba Cha Mahakama Mahakama Ipo Kimya Kidogo
Shahidi anapita ni Mdada Kajitanda Buibui na Kavaa Barakoa Kubwa sana Kumziba Sura,
Jaji: Majina Yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Jaji: umri Shahidi: 45yrs
Jaji: Kabila
Shahidi: Mchaga
Jaji: Shughuli Zako
Shahidi: Nafanya Biashara
Jaji: Dini yako
Shahidi: R. C
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii Kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eeeh Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shahidi Ataongozwa na Wakili Esther Martin
Wakili wa Serikali: Esther Ikumbushe Mahakama Majina yako
Shahidi: Anita Varelian Mtali
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Moshi, RAU madukani.
Jaji: Jina lako la Tatu sijalipata Vizuri ni Mtali.?
Shahidi: Mtaro
Wakili wa Serikali: Umeishi kwa Muda gani Rau
Shahidi: Miaka 08
Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani
Shahidi: Nafanya Biashara ya Kuuza Mbege
Wakili wa Serikali: Ulianza lini Biashara yako ya Mbege
Shahidi: Miaka 08 ninayo
Wakili wa Serikali: Mbali na Biashara yako ya Mbege una bishara gani Nyingine
Shahidi: Kuna Glocery, Stationary, Banda la Tigo Pesa na Kuna Sehemu ya Kutolea Movie
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama 05 Mwezi 08 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Sehemu yangu ya Biashara, Nikifanya Usafi
Wakili wa Serikali: Saa ngapi
Shahidi: Saa Saba Kasoro
Wakili wa Serikali: Ya Muda gani
Shahidi: Ya Mchana
Wakili wa Serikali : Kabla ya Kufika eneo lako la Biashara ulikuwa umetoka wapi?
Shahidi: Nilikuwa Nimetoka Nyumbani Nikaenda Saloon Kuosha Nywele
Wakili wa Serikali: Na Ulipotoka Saloon kuelekea sehemu yako Kufanya Usafi
Shahidi: Nilikuta Wakaka Watatu walikuwa wamekaa Mbele Yangu walikuwa wanakunywa na Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Walikuwa wanakunywa nini
Shahidi: Walikuwa wanakunywa Bia
Wakili wa Serikali: Hizo laini walikuwa wanasajili wapi
Shahidi: Kuna Vijana wanapitaga Mitaani Kusajili Laini
Wakili wa Serikali: Ukiwa unafanya Usafi kitu gani Kingine ulishuhudia
Shahidi: Kuna wakaka wawili walikuwa wanapitapita wakiongea na simu, Wanaenda wanarudi wakiongea na Simu
Wakili wa Serikali: Hao wanaopita ni tofauti na wale uliposema walikuwa wanakunywa Bia
Shahidi: Hapana ni walewale
Wakili wa Serikali: Kutoka Kwako Unapofanyia Kazi Mpaka Glocery ni Umbali gani
Shahidi: Kama Hatua 10
Wakili wa Serikali: Hapo Katikati sasa, Kati ya Glocery na ulipo, pana kitu gani
Shahidi: Pana uwazi
Wakili wa Serikali: Baada ya Muda kitu gani kilitokea
Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia
Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao
Shahidi: Ni Askari
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo
Shahidi: Nafanya Usafi
Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi
Shahidi: Hatua 05
Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine
Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu
Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi
Shahidi: Wawili
Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje
Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu
Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata
Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio
Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti
Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea
Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi
Wakili wa Serikali: Ni Askari gani huyo
Shahidi: Alinitambulisha anaitwa Askari Polisi Jumanne
Wakili wa Serikali: Ulifanya nini kujiridhisha?
Shahidi: Alitoa Kitambulisho Akanionyesha
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifanyika
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kumsimamisha..?
Shahidi: Afande Jumanne alijipekua kuanzia Kifuani akatoa Mifuko Nje
Wakili wa Serikali: We ulikuwa na nani wakati huo
Shahidi: Dada Mmoja anaitwa Esther
Wakili wa Serikali: Kutoka Eneo la walioambiwa Wachuchumae Chini, palikuwa na Umbali gani?
Shahidi: Kama Hatua Mbili
Wakili wa Serikali: Kuna Kitu gani Kingine
Shahidi: Raia walikuwa wamekuja
Wakili wa Serikali: Kabla ya Raia Kusogea eneo hilo palikuwa na hali gani?
Shahidi: Palikuwa na Jua
Wakili wa Serikali: ahaa ahaaa yani hali ya pale ilikuwaje?
Shahidi: Palikuwa pametulia
Wakili wa Serikali: Ikaendelea nini?
Shahidi: Alimsimamisha Mmoja akamuuliza Unaitwa nani?
Wakili wa Serikali: Akajibu anaitwa nani?
Shahidi: Adam Kasekwa
Wakili wa Serikali: Akamwambia nini?
Shahidi: Akiwa amenyoosha Mikono Juu akamwambia Geuka, akageuka
Wakili wa Serikali: Baada ya Kugeuka
Shahidi: Askari Jumanne alianza Kumpekua Kuanzia Kichwani, Mabegani, Alipofika Kiunoni alikuta Kitu kigumu
Wakili wa Serikali: Alikikuta Upande gani
Shahidi: Kushoto
Wakili wa Serikali: Maeneo Gani?
Shahidi: Niliona ni Bastola
Wakili wa Serikali: Ulijuaje kama ni Bastola?
Shahidi: Afande Jummane alituambia ni Bastola
Wakili wa Serikali: Halafu
Shahidi: akatuonyesha namba
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni namba gani.?
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Zilikuwa kwenye nini
Shahidi: Kwenye Bastola
Wakili wa Serikali: Wakati anakuonyesha Bastola Adam alikuwa wapi?
Shahidi: Alikuwa amesimama
Wakili wa Serikali: Ukiona na nini Kingine
Shahidi: Risasi 03
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi, alipofika Upande wa Kulia akakuta Vitu vidogo vidogo Kwenye Karatasi ya Nailon akasema inasadikiwa ni Madawa ya Kulevya ila itajulikana Mbele.
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ngapi Shahidi: 58
Wakili wa Serikali: ikawaje
Shahidi: Aliendelea Kumpekua akamkuta na Simu Ndogo aina ya Itel
Wakili wa Serikali: Hiyo simu akaifanyaje
Shahidi: Akatoa laini akakuta namba akaziandika
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo aliendelea na nini
Shahidi: Akamwambia Naomba fomu, .......akaleta fomu
Wakili wa Serikali: fomu ngapi
Shahidi: Zilikuwa Mbili
Wakili wa Serikali: Akafanya nini sasa Kwenye ile Fomu
Shahidi: Kaandika Vitu alivyokuwa amempekua
Wakili wa Serikali: Umesema palikuwa na fomu Mbili, fomu ya kwanza akijaza nini
Shahidi: fomu ya kwanza alijaza Bastola, Risasi na Laini
Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni laini gani
Shahidi: Laini ya Voda na Airtel
Wakili wa Serikali: Baada ya Kumalizia fomu ya kwanza
Shahidi: alichukua fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: Kabla ya Kujaza Fomu Nyingine
Shahidi: Alipomaliza Kujaza akampa akasaini na Baadae akasaini yeye alipo maliza Kusaini.
Wakili wa Serikali: alimpa nani
Shahidi: Alimpa Adam
Wakili wa Serikali: baada ya fomu ya kwanza nini kiliendelea
Shahidi: alichukua Fomu Nyingine
Wakili wa Serikali: alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vingapi Vilikuwa Vingapi
Shahidi: Vilikuwa 58
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: akampa Adam asome alafu asaini na sisi akamtupa tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani..?
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada Kumalizia nini kilifuata
Shahidi: akamuita Mwingine
Wakili wa Serikali: huyo Mwingine anaitwa nani
Shahidi: Mohamed Abdulahi Ling'wenya
Wakili wa Serikali: akamwambia nini
Shahidi: asimame ageuke, Baada ya kugeuka akaanza Kumpekua
Wakili wa Serikali: alianzaje Kumpekua
Shahidi: Kichwani Mikononi
Wakili wa Serikali: ilikuwaje
Shahidi: Upande wa Kulia alikuta na Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: akafanyeje
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua
Shahidi: alikuta Simu aina ya Tecno
Wakili wa Serikali: Rangi gani
Shahidi: Nyeusi
Wakili wa Serikali: akafanya nini
Shahidi: akapekua akakuta kuna laini
Wakili wa Serikali: laini gani
Shahidi: Hallotel
Wakili wa Serikali: baada ya Kupata simu akafanyeje
Shahidi: akazitoa zile Laini, Akampa yule Mwingine akazishika
Wakili wa Serikali: Na Yeye Akaendelea na nini
Shahidi: Akaendelea na Upekuzi
Wakili wa Serikali: hizo laini alikuwa anafanya nazo nini?
Shahidi: Alimpa Askari wa Pembeni akazishika
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: Aliendelea na Upekuzi lakini hakukuta kitu Kingine
Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi
Shahidi: aliomba fomu Mbili
Wakili wa Serikali: fomu ya Kwanza alijaza nini
Shahidi: alijaza vile Vikete Vidogo Vidogo
Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi
Shahidi: 25
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa akasema akasaini
Wakili wa Serikali: Nani Yeye, afande Jumanne?
Shahidi: Ndiyo na Baadae Mohamed
Wakili wa Serikali: na baadae
Shahidi: tukasaini sisi
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: Ile fomu Nyingine akajaza Simu na laini Nyingine
Wakili wa Serikali: Za Mtandao gani
Shahidi: Airtel na Hallotel
Wakili wa Serikali: Baada ya hapo
Shahidi: Alimpa Mohamed asome kisha akasaini
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne alituomba na sisi tusome Kisha tusaini
Wakili wa Serikali: Wewe na nani
Shahidi: Mimi na Dada Esther
Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi
Shahidi: walivalishwa Pingu
Wakili wa Serikali: baada ya hapo
Shahidi: afande Jumanne akatuomba tuelekee Kituoni
Wakili wa Serikali: Hao walivalishwa Pingu walikuwa ni akina nani
Shahidi: Adam na Mohamed
Wakili wa Serikali: baada ya kuvalishwa Pingu..?
Shahidi: Wakaelekea kwenye Magari, Barabarani
Wakili wa Serikali: Palikuwa na Askari wangapi
Shahidi: Watano
Wakili wa Serikali: Walikuwa wamebeba nini
Shahidi: Wawili walikuwa wamebeba Bunduki
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa eneo lile ilikuwaje
Shahidi: ilikuwa imetulia
Wakili wa Serikali: Hali ya hewa ilikuwaje
Shahidi: Kulikuwa na Jua na Mwanga
Wakili wa Serikali: Mlichukua Muda gani kwenye lile eneo Mpaka Mnamaliza Zoezi
Shahidi: Kama Dakika 45
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufanya Upekuzi Kuna Vitu Vilipatikana na Kwamba Kuna fomu zilijazwa Sasa fomu ukiziona hapa utaweza Kuzitambua?
Wakili wa Serikali: sasa bada ya Kumalizia Mkaelekea kituoni, kituo gani..?
Shahidi: Central Moshi
Wakili wa Serikali: baada ya Kufika police central
Shahidi: Tuliandika Maelezo
Wakili wa Serikali: Maelezo ya nini
Shahidi: Kitu gani Kilichofanyika ......
Wakili wa Serikali: Tukianza na fomu ya Adam utaitambuaje
Shahidi: Kwa vitu vilivyoaandikwa, Jina langu na sahihi yangu
Wakili wa Serikali: Kulikuwa na nini Kingine Bastola
Wakili wa Serikali: Kingine
shahidi: Palikuwa na Risasi
Wakili wa Serikali namba gani Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba nimpe fomu aweze Kuitambua
Wakili wa Serikali: Shika hii Karatasi iangalie kwa Makini
Shahidi: Ndiyo yenyewe
Wakili wa Serikali: Yenyewe nini
Shahidi: Fomu niliyo saini
Wakili wa Serikali: Umeitambuaje
Shahidi: Kwa Jina langu na Sehemu niliyosaini
Wakili wa Serikali: Jina lipo wapi, Ni Jina gani
Wakili Peter Kibatala: ALICHOKIFANYA DADA YANGU ESTHER HAIRUHUSIWI, ANAKWEMDA KWENYE DETAILS
Wakili wa Serikali: Sawa naondoa hilo swali
Wakili wa Serikali: Ungependa hii fomu ipokelewe Mahakamani
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Fomu ipokelewe
Jaji: Wakili wa Mshtakiwa wa kwanza
MTOBESYA: HATUNA PINGAMIZI
Mallya: Hatuna Pingamizi Fredrik
Kiwhero: kwa Niaba ya Mshitakiwa.....wa tatu hatunapingamizi
Peter Kibatala: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Nne hatuna Pingamizi
Jaji: anaandika Kidogo
Jaji: Mahakama inaipokea kwa ID 1
Wakili wa Serikali: Shahidi pia ulisema kwenye huo Upekuzi pana Bastola na Risasi unaweza hapa Mahakamani ukavitambua Tuanze na Bastola
Shahidi: Ndiyo nitavitambua
Wakili wa Serikali: Bastola unazitambuaje
Shahidi: Kwa Namba A5340
Wakili wa Serikali: na Kwa Upande wa Risasi
Shahidi: namtambua, zilikuwa na Rangi ya Dhahabu
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Naona Exibit nimuonyeshe Shahidi
Afisa Wa Mahakama anafungua Bahasha ya Kaki Anamkabidhi Wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Hebu Kiangalie hiki kitu hapa, Iambie Mahakama ni nini
Shahidi: anaingilia bila Kushika, ni Bastola
Wakili wa Serikali: ambayo Imetoka wapi
Shahidi: Imetoka Kwa Adam
Wakili wa Serikali: Uliona wapi?
Shahidi: iliyotoka kwa Adam
Wakili wa Serikali: ni Kitu gani Kilichokufanya ukagundua
Shahidi: kwa namba
Wakili wa Serikali: Namba gani
Shahidi: A5340
Wakili wa Serikali: Umeeleza pia ulishuhudia Upekuzi wa watu wa wili ambao kwa Majina yao ni Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya, Je ukiwaona unaweza Kuwatambua
Shahidi: naweza Kuwatambua
WAKILI WA SERIKALI: WAPO HAPA MAHAKAMANI?
Shahidi: Wapo hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali: Wapo wapi
Shahidi: hapa Mbele, Mohammed amevaa Tshirt ya Amevaa Meupe Kijani na Nyeusi
Wakili wa Serikali: na Adam yupo wapi Shahidi: amevaa Shati lenye Rangi Nyeupe Nyeupe
Wakili wa Serikali: Yupo wapi hapa Mahakamani
Shahidi: Yupo pale
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu
Jaji: Upande wa Utetezi
Mtobesya: Ndiyo Mheshimiwa Jaji
Mtobesya: naomba Nipatiwe ID 1 Mahakama Inampatia
Mtobesya: Shahidi umeomba Mahakama Ipokee Kielelezo hiki Onyesha Sehemu ipo saini
Shahidi: Nimesaini hapa
Mtobesy: Kwa Ushahidi wako Unasema ulisaini Nyaraka ngapi
Shahidi: Nne
Mtobesya: Ushahidi wako kwamba Sahihi zako Lote zinafanana
Mtobesya: Naomba kwa Kifungu 75(1) Sheria ya Ushahidi, Shahidi asaini tena sehemu Nyingine ili Mahakama iweze Kufananisha Saini zake
Jaji: Unaweza Kutusomea.? Mtobesya: anasoma Kifungu cha 75(1) cha Sheria ya Ushahidi
Jaji: hicho Kifungu kinaitaka Mahakama shahidi asaini ili iweze Kufanya ufafananisho
Mtobesya: Ndiyo ili Mahakama iweze kufananisha, kwa sababu tuna Nyaraka Nyingine inasaini yake tofauti
JAJI: lakini hiyo Nyaraka itakuwa imetengenezwa hapa, Utakuwa umeiiingiza Mhakama .....
Jaji : Bwana Matata una jambo la Ku-she na sisi
Matata: Sheria Anayosoma Wakili Mtobesya Ni Sheria inasema kuwa Shahidi anaweza kuandika sehemu tu 75(2) Mahakama inaweza Kuagiza Mtu yoyote Mahakamani Kulingananisha.
Jaji: Je hiyo inahusiana na Mahakama kumuelekeza Shahidi asaini?
Matata: ni tafasiri yangu kuwa Mahakama Inaweza Kuruhusu Shahidi Kuandika ili Kufananisha Kama alichokiandika ni sawa
Mallya: Pale kwenye 75(2) inasema any Documents haijambana wapi kwa hiyo anaweza Kusaini popote (any documents) ili Mahakama ifanye Uamuzi iwe imepata kwa Usahihi wake....kwa usahihi Kifungu cha 75 lakini siyo kwa Kumtaja Shahidi aandike
Jaji: Upande wa Mashitaka
Wakili wa Serikali: Maombi ya Mtobesya Pamoja na Kuegemea kutoka kifungu 75 cha Sheria ya Ushahidi tunaona amekimbia Sana na siyo wakati wake Lakini pangekuwa na Nyaraka Nyingine ambayo Ndiyo Ingekuwa imekuja Rasmi Mahakamani ndipo angetumia.......Njia yako ya Kutaka Shahidi Asaini Ni sahihi Kama watapinga tutashughulikia Kupinga huko wakati huo.
Jaji: Kwa tafsiri yangu Mamlaka iliyopewa Mahakama 75(2) ni naona Mahakama inayo Mamlaka kumuelekeza Mtu yoyote Kufanya Mlinganisho wa Maneno au Namba kwa Nia ya Kuiwezesha Mahakama Kufanya Ulinganisho, ila huyu Mtu aliye na maarifa Kuliko Mahakama Yenyewe. Najiuliza kama ...Leo nilikuwa na Avoid Upande wa Utetezi Kutuzuia Kutumia Nyaraka hii ambayo sisi tumeipata kwenye Comito.
Mtobesya///; Kifungu cha 47 cha Sheria ya Ushahidi ndiyo kinaruhusu Maoni ya Kitaalamu katika Ushahidi Lakini Kifungu cha 48 au 49 Sikumbuki Vizuri kinaruhusu hata mtu asiye Mbobezi Kufanya Maoni yake Hili Kifungu cha 75 chenyewe Kinataka Mahakama Kufanya Ulinganisho.
Jaji: Na Mimi na kubaliana na wewe Lakini kwenye Document uliyonayo hatujui baada ya Kumkabidhi Karatasi at asaini Sahihi gani kati ya hizo Mbili
Jaji: Ndiyo nasema wewe endelea na Jukumu lako kama Walitokea Wakapinga tutashughulikia Pingamizi hilo wakati huo ...na Sheria ya Ushahidi wa Kifungu cha 75 Vyote Vinafanya washitakiwa Kupewa Nyaraka zinazokusudiwa Kutumika dhidi yao kwenye Makosa Makubwa Kama haya kupitia Comito Kwa hiyo watupatie
Mtobesya: Asante Mheshimiwa Jaji
Mtobesya: Naomba nikabidhi iwe Nyaraka Original ya Hati ya Kuchukua Mali iliyosainiwa tarehe 25 2020 inayomhusu Mohamed Ling'wenya Kwa sababu sisi tunayo Moja
Jaji: chini ya Sheria Gani
Mtobesya: Kifungu cha 246 na 146 ya Makosa ya Jinai ...
..Angetoa basi Maombi Rasmi lakini hata kama no Original haiwezi kuitumia kwa wakati huu Haki yake ya Kuhoji aendelee nayo na anaweza Kuitumia hata sasa Sisi tuna tatizo na Procedure jinsi gani Ushahidi huu unataka Kuletwa Mahakamani
Jaji: Jamani Mmeelewa
Wakili wa Serikali: Sisi Haja yetu ni Swala la Procedure Ni kweli Tulianika Ushahidi Tutaokuja kutumia Mahakamani lakini ieleweka Kuwa Ushahidi hi ni Wa Kwetu. Hakuna mahala popote ambapo Mteja wake anaweza Kuwa na haki ya kutumia Nyaraka hizo ......
.Ubishi ulikuwa kama Mshitakiwa Alikuwa ametahiriwa au haja tahiriwa Mahakama ya Rufani ikasema kuwa Hilo ni Kubwa sana Kwake na Isingeweza Kujiingiza katika Risk. Kwa kesi hii basi Kama anataka Mahakama Ijiridhishe. Swala ni Kama Nyaraka hiyo imepokelewa na Kama .......imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki
KESI YA buying wa John dhidi ya Jamhuri criminal appeal namba 450 ya Mwaka 2017 Mahakama iliyoketi Shinyanga Katika Ukurusa wa 11 paragraph ya Mwisho ya a Ukurasa huo wa 11 Ambapo swala Lililojitokeza tangu wakati wa Trial Court na Kesi Ilikuwa ni ya Ubakaji ........
Mheshimiwa Jaji: tunatakiwa tuzingatie Mfumo wetu wa Utoaji haki, Mahakama kwa Kutimiza Wajibu wake anakuwa ni refa na siyo kwa kukaribishwa Kutaka Kufanya Uchunguzi Zoezi kama hilo ni Kuingiza Mahakama katika riski ambazo zinaweza Kuepukika.
...imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki
Na Hilo Ndiyo Dhumuni la Comito Trial kwamba Mshitakiwa ajue anachokuja akujitetea nacho
Upande wa serikali: Sisi tunaona ni Kukiuka Procedure na Maombi hayo tunaomba uyakatae Mheshimiwa jaji Mtobesya: Tunapoteza sana Muda Mheshimiwa Jaji, Shahidi ni wa Kwao na Ushahidi ni wa Kwao Na sijui ni wakati gani tena sisi tutapata Kuwa na wasaa wa kuwa na Shahidi huyu
Na hapa swala la Copy kwa Washitakiwa halijazungumziwa wakati ni Haki kwa Mshitakiwa Kupatiwa Hiyo Nyaraka
Nashon Nkungu: Naona nisaidie Mahakama kama Afisa wa Mahakama alichosema Wakili Robert Kidando Amejieleza Kwenye Kifungu cha 76 tuh asemi kwa nini kuna Haki ya Kukabidhi wa Nyaraka za Comito Na Kingine Kifungu 30 cha Sheria inasema tupewe Copy siyo Photocopy ....
Ambapo wewe Umegundua Sahihi Katika Nyaraka hizo na Zilizopo hapa Mahakamani Sahihi zinatofautiana Kwa Maana hiyo Ukaomba Mahakama ikupatia Nakala halisi Jaji Jambo la Pili Kwakuwa wanasema Ushahidi huo watautumia basi Wahurumie Mapema ili uweze Kuutumia.
Jaji: Mtobesya
Mtobesya: naam Mheshimiwa Jaji
Jaji: hoja zako ulizijenga katika a Mazingira Matatu Haki za Mahakama Jinai hasa akatika Mahakama Kuu, amtu anasomewa na Kukabidhi wa Nyaraka Kwamba wewe Una taarifa Kwamba zipo Nyaraka wanazolenga kuzitumia Kama Ushahidi Wao
Mtobesya: Mheshimiwa nilikuwa naomba Mashauriano na Mahakama ilitusiiipe Mahakama Mzigo wa a kuandika Rulling
Jaji: mnasemaje Jamuhuri
Wakili wa Serikali: Ni Sawa Mheshimiwa
Jaji: Basi tuta Break kwa Dakika 10, tukutane pande zote pale Ofisini
Jaji: anatoka
Mawakili wamerudi
Jaji ameingia tena Saa 6 NA Dakika 24
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa tena Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe Kisha Mahakama Kimyaaaaaa
Jaji: Muda Mfupi Uliopita Tuli-break kwa Nia ya Kuweka Sawa Mambo ya Kitaaluma Baada ya Kuyaweka Sawa na Kualika Sasa Mtobesya Kuendelea
MTOBESYA: Wakati Unaongozwa na Dada Yangu Esther Ulisema Uliandika Maelezo
Shahidi: Niliandika Tarehe 05 Mwezi 08 2020
Mtobesya: aliyeandika Maelezo yako
Shahidi: Sijui Jina lake
Shahidi: anaitwa Jumanne
Mtobesya: Ulishawahi Kukutana na Askari anaitwa Detective Coplo Francis.?
Shahidi: Sikumbuki kama nimekutana naye
Mtobesya: Lakini walikupa Maelezo Ukasoma na kisha Ukaona sawa
Shahidi Ndiyo
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe Statement (Handwritten Statement) Naomba Chini ya Kifungu Cha 164 (1h) cha Sheria ya Ushahidi
Wakili wa Serikali Wapo Kimya Jaji anawasubiri
Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi la Kumpatia hii Nyaraka
Jaji: Pokea
Mtobesya: Shahidi Unajua Kusoma na Kuandika
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: Shika Karatasi zipo Mbili Soma kama Ndiyo Uliyosoma Ukasaini na Kama Kuna Majina yako na Askari aliye andika Ihakiki Kwanza
Shahidi Anaipekua, anaikazia Macho anafunua funua mara Nyingiyingi
Mtobesya: Ndiyo hiyo.?
Shahidi: Kimyaaaa anatizama tena ile Karatasi, anaipekua
Shahidi: Ndiyo Yenyewe
Mtobesya: Soma Kuanzia Juu Kwa Sauti
Shahidi: Mimi Ndiyo Mwenye Majina na anuani takwa hapo Juu Mkazi Wa Kilimanjaro Nimezaliwa Mwaka 1979 Familia ya watoto Nilikuwa naelekea Saloon Rau Madukani Na baada ya Kumalizia nilieleza Sehemu yangu ya Biashara Kufanya Usafi. Mbele Kuna Bar Na Kukikuwa na Vijana walikuwa wanakunywa Pale Sikuwa nawafahamu Kwa Maana walikuwa ni wageni
Mtobesya: Soma Kote
Shahidi: Sikuwafahamu kwa Maana walikuwa ni Wageni maeneo haya Kwa Muda Mwingi walikuwa wanaongea na simu. Kwangu Afande Mmoja akajitambulisha Jina Afande Jumanne Akaniomba niwe Shahidi huru Ambapo nilishuduia Kufanya Upekuzi Kwenye Kupekuliwa Kijana Mmoja alikuwa na Bastola Zenye nmabaA A 5340 Pia alikutwa na Kete 58 za Madawa ya Kulevya
Shahidi: Shahidi ananendelea kusoma Baada ya Muda walikuja watu watano na a Kuwafuata wale Vijana Na wakaambiwa wapo Chino ya Ulinzi Askari hao walitaka Kufanya Upekuzi ndipo walipokuka Kuni.... Kamyamaza Kidogo Askari hao walihitaji Kufanya Upekuzi ndipo walikuja.......Adam Kasekwa mbaye nilimfahamu Jina baada ya Kuulizwa Jina lake baada ya Upekuzi Na huyo Mwingine aliyekuwa naye alitaka anaitwa Mohammed Ling'wenya ambaye pia kwenye Upekuzi alikutwa na Simu Moja ya Samrt Yenye Line ya Airtel na Hallotel na Kete 21 za Madawa ya Kulevya
Watu hawa wawili nilikuwa siwafahamu Majina wala Sura niliwafahamu baada ya Kutaja Majina yao Baada ya Kukamatwa na Polisi, Askari wale nilikuwa siwafahamu Na Kiongozi wao aliyekuwa anafanya a upekuzi aliwatambulisha kwangu ASP Jumanne.
Baada ya Majina hayo Nilijaza Hati ya Upekuzi Na Kuzuia Mali Walisaini wote na Watu tulioshuhudia Na Afande Jumanne Na baada ya Upekuzi Nilijaza Hati ambayo inaonyesha Upekuzi umefanyika Ambapo tukasaini wote na tulioshuhudia Haya Ndiyo Maelezo Yangu, Sahihi Kama Nilivyoyatoa.
Mtobesya: Nitakurudisha Kwenye baadhi ya Maeneo kama Ulivyosoma
Mtobesya: Ni sahihi Katika Ushahidi wako ulisema Askari wawili walifika wakawaambia Mpo chini ya Ulinzi na Wakawatajia Makosa yao
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hapo, hayo Maneno Yapo au hayapo
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: Nilikusikia Unasema hawa Vijana waliokamatwa wao walikuwa wanakunywa wakati wewe unafanya usafi katika Eneo lako la Biashara
Shahidi: Sahihi
Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hiyo Taarifa ipo
Shahidi: Haipo
Mtobesya: Nilikusikia Ukisema Kwamba afande Jumanne alikuja kwako akatoa Kitambulisho
Shahidi: Ndiyo alitoa Kitambulisho
Mtobesya: Hayo Maelezo ya kutoa Kitambulisho yapo kwenye Statement yako
Shahidi: Hayapo
Mtobesya: kwenye Maelezo yako nilikusikia watuhumiwa Waliposimamishwa kabla ya Upekuzi walijitambulisha Majina yao kwa Polisi aliyekuwa anafanya Upekuzi Nitakuwa sahihi nikisema Statement Yako inasema Uliwajua Majina Baada ya Upekuzi
Shahidi: Niliwajua Majina kabla ya Upekuzi
Mtobesya: Soma sehemu inayosema nilishuduia wakipekuliwa........ Mpaka inaisha Jina la Afande Jumanne, Soma kwa Sauti
Shahidi: Nilishuhudia Kupekuliwa kwa Vijana hao, na Kupekuliwa Mmoja wao alikutwa na Bastola yenye namba A5340 pamoja na Magazine yanye Risasi 3 .......pia alikuwa na Madawa ya Kulevya Ambae nilimfahamu kwa Jina baada ya Kuulizwa baada ya Upekuzi.
Mtobesya: Kwa hiyo Statement Ulifahamu Kabla au Baada
Shahidi: Baada ya Kupekuliwa
Mtobesya: Nitakuwa sahihi, kwenye Ushahidi wako ulielezea ulisaini Nyaraka Nne za Kushuhudia Upekuzi
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nenda Sasa baada Upekuzi huo,
Shahidi: Nilijaza Hati ya Upekuzi na Hati ya Kuzuia Mali ilionyesha Upekuzi Umefanyika, ambao tulisaini wote tulioshuhudia pale.
Mtobesya: Ishia hapo, Nitakuwa sahihi nikisema Nyaraka hiyo Uliyosoma inaonyesha ulisaini Nyaraka Moja..? Na siyo Nne kama Ulivyosema Asubuhi ya Leo
Shahidi: kwa Mujibu wa Mstari huu ni Kweli
Mtobesya: Isaidie Mahakama sehemu nataka Usome Kwa Sauti, Soma baada ya Neno Watuhumiwa wale wawili
Shahidi: Baada ya Upekuzi huo na Kusaini Hati ya Kuzuia Mali ambapo tukisaini wote.
Mtobesya: Wakati Wakili Wa Serikali Esther anakuongoza Ulisema aliyekuongoza hapo ni Jumanne
Shahidi: Nilisema ni Afande ambaye sikujua Kwa Jina
Mtobesya: Ipo Kwenye Rekodi, Jaji ataona
Shahidi: hapana
Mtobesya: Ungependa hayo Maelezo Yawe sehemu ya Ushahidi Wako Siku ya Leo
Shahidi: Ndiyo ningependa uwe Ushahidi Wangu Siku ya Leo
Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi
Jaji: Mahakama imeyapokea Maelezo hayo Kama Kielelezo namba 02 kwa Upande wa Utetezi
Mtobesya: Kwa Ruhusa yako Mheshimiwa naomba Kuendelea
Mtobesya: Ulielezea Mahakama Ulisaini Nyaraka za Uzuiaji wa Mali, zaidi ya Nne
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: ieleze Mahakama Hati hizo zilijazwa na nani Mpaka Nyie Mkasaini
Shahidi: Zilijazwa na Askari Jumanne
MTOBESYA: na wewe Unakumbuka ulisaini kwenye Hati zote
Shahidi: Ndiyo
MTOBESYA: Unaweza Kuisaidia Mahakama Ulisaini Upande gani
Shahidi: Pale Mwisho Kwa Pembeni
Mtobesya: Naomba Nimuonyeshe Shahidi ID 1 Nitakuwa Sahihi Nikisema Nyaraka zote Nne ulisaini hapa Kwenye Jina lako
Shahidi: Siyo zote sehemu hii, Zingine Nilisaini Upande wa Kushoto na Zingine Upande wa Kulia.
Mtobesya: Unaweza Kutuambia Ulizosaini Upande wa Kushoto zinaruhusu nani na Kwaajili ya Vifaa Vipi
Shahidi: NilizoSaini Upande wa Kushoto zilikuwa zinamhusu Adam
Mtobesya: Hizo Ulisaini Upande wa Kushoto
Shahidi: Nilisaini Upande wa Kulia
Mtobesya: na Zilizomuhusi Mohammed Ulisaini Upande gani
Shahidi: Upande WA Kushoto
Mtobesya: Ulisaini Baada au Kabla ya Jina lako
Shahidi: Nilisaini baada ya Jina langu
Mtobesya: Na Ni Ushahidi wako Mbele ya Mahakama zote Ulisaini wewe Mwenyewe na kwa Mwandiko wako
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Na Kwa Ushahidi Wako Saini zako umesaini wewe Zikiwa zinafanana
Shahidi: Kuna zingine zilikuwa hazifanani kwa sababu nilikuwa na Hali tofauti
Mtobesya: Mweleze Mheshimiwa Jaji Sasa ni hali ipi Ulikuwa nayo ikapelekea Saini zako Kutofautiana
Shahidi: Kuna saa, wakati wa Ukamataji Nilisaini wakati nimesimama na Zingine nimesaini wakati nimekaa kwenye Meza.
Mtobesya: Unaieleza Mahakama Ukisaini ukiwa umesimama na Wakati Umekaa saini lazima zitofautiane
Shahidi: Ndiyo
Mtobesya: Nilisikia wakati anakuongoza Dada Yangu Wakili wa Serikali Kuwa Mlisaini wakati Wa Tukio
Shahidi: Wakati natoa Maelezo Nilisaini Nikiwa mezani lakini Zile zingine Nilisaini nikiwa nimesimama
Mtobesya: Ni Signature zipi sasa zinazofanana ukiwa Umekaa au Umesimama
Shahidi: Nikiwa Nimekaa ndiyo zinafanana
Mtobesya: Ukiwa Umekaa umesaini Mara Ngapi na Nyaraka zipi
Shahidi: Zile ambazo nilikuwa kituoni kutoa Maelezo.
Mtobesya: Zote ambazo ulisaini Ukiwa Umekaa Zina fanana..?
Shahidi: Hapana
Mtobesya: Zote ulizoSaini Ukiwa Umesimama Zinafanana au hazifanani
Shahidi: Zinafanana
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kuishia Hapo
Mtobesya: naomba Kurudisha Kielelezo
Jaji: Wakili Malya unahitaji Muda gani
Mallya: Nusu saa hivi
Mallya: Bado unauza Mbege
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Mbege unayouza wewe inalewesha
Shahidi: Kuna Inayolewesha na Isiyolewesha
Mallya: Una Ndugu au Mume ambaye ni Polisi
Shahidi: Hapana
Mallya: Ulitambuaje kuwa hiki ni Kitambulisho cha Polisi?
Shahidi: Niliona Chapa ya Taifa
Mallya: Kitu gani Kingine Uliona
Shahidi: Niliona Jina lake
Mallya: Lilikuwa limeandikwaje
Shahidi: kwa kweli hapo Sikumbuki
Mallya: Umesema Wakati Unafanya Shughuli zako za Usafi na Vijana walikuwa wanakunywa Bia, Ni hatua ngapi
Shahidi: Ni hatua 10
Mallya: Napiga hatua Mahakamani
Mallya: Hapa Kuna Hatua Saba tu
Mallya: Umbali wa Hatua 10 Macho yako yanaona Vizuri
Shahidi: Yanaona Vizuri
Mallya: hapa Kuna Umbali Wa Hatua 7 tu Unasema Mtu Amevaa Tshirt yenye Rangi Nyeusi wakati ni Dark Green Je unataka Mahakama iamini kwamba unaona Vizuri?
Jaji: umeelewa swali..?
Shahidi: ..natumiaga Miwani, Sema Leo nimesahau Miwani
Mallya: Ulielezea Kuwa siku ya Tukio ulivaa a Miwani
Shahidi: Hapana
Mallya: Siku ya Tukio ulikuwa Umbali wa Mita 10 Leo Mshitakiwa yupo hatua 10 tu hakuna aliyevaa Tshirt Nyeusi, unataka Kumwambia Mheshimiwa Jaji unaona Vizuri?
Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa
JAJI: umelielewa Swali
Shahidi: Ndiyo
JAJI: Jibu Basi
Shahidi: Kuna saa Macho yanashida.
Mallya: Wakati Unatoa Maelezo Leo Uliomba Miwani uweze Kuangalia Vizuri.?
Shahidi: Sikuomba
Mallya: Ni sahihi Kuwa Usajili wa Simu unafanya kwa Kitambulisho?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: na wewe Uliwaona watu waliopo Mahakamani walikuwa wanasajili Line za simu
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kwenye Maelezo Yako kuna sehemu umesema Wanasajili lini?
Shahidi: Hakuna
Mallya: pale Rau Bia wanauza au Bure?
Shahidi: Wanauza
Mallya: Wakati mnawapekua Mliwakuta na Bastola na Siyo Pesa
Shahidi: Hakuwa na Pesa
Jaji: Watakuwa walishalipaaaaaa
MAHAKAMA kichekoooooo
Mallya: zoezi la Kufanya usafi Lilichukua muda gani?
Shahidi: Kwa muda wa Kufanya Usafi kama Dakika 10
Mallya: Wakati Tukio linatoka Ulishamaliza Usafi au Ulikuwa unaendelea
Shahidi: nilikuwa naendelea ikabidi Nisimame
Mallya: Tukio la kukamatwa lilichukua Muda gani?
Shahidi: Rudia swal?
Mallya: Kitendo Cha Kukamatwa hawa watu Mpaka unaitwa kushuhudia ilichukua muda gani?
Shahidi: kama Dakika 03
Mallya: Kwa hiyo tukijumlisha Dakika 10 za Usafi na Dakika 3 wakakuita wewe Zoezi la Kusachiwa lilidumu kwa a muda gani?
Shahidi: Kwa Dakika 45
Malya: Saa Nane ilikuwa imefika
Shahidi: Kama saa Nane Kasoro
Mallya: Kwa Maelezo Yako wewe yalitolewa Umesaini Ukiwa polisi saa 7 kamili Je, tukuamini wewe au?
Shahidi: Muamini Maneno Yangu
Mallya: Tuchukue Yote.?
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Kabla ya kwenda Kwenye Tukio Siku hiyo ulikuwa wapi na wapi
Shahidi: Nilitoka Nyumbani baada ya Usafi, Nikaenda Kwa Mgonjwa na Baadae Saloon
Mallya: Umeulizwa aliyekuchukua maelezo Yako ni nani
Shahidi: Simfahamu Kwa Majina
Mallya: Hakukuonyesha Kitambulisho ndiyo Maana Humkumbuki?
Shahidi: Hapana alinitajia nimemsahau
Mallya: Kwa kutazama Kwa Macho yako sahihi yako uliyosaini Hapa na Hapa Kwenye Exibit 02 zinafanana
Shahidi: Hazifanani lakini ni sahihi zangu
Mallya: Kwenye Maelezo Yako umeeleza Mahali Kiongozi wao, Afande nani
Shahidi: Afande Jumanne
Mallya: akitokea Mtu akisema yeye ndiyo Kiongozi aliyekwepo atakuwa Muongo
Shahidi: Ndiyo
Mallya: Unamfahamu Kingai
Shahidi: Hapana
Mallya: na Ulisema Mapolisi walikuja kujitambulisha kwako.?
Shahidi: alikuja Mmoja
Mallya: Askari waliowakamata watuhumiwa walikuwangapi
Shahidi: Walikuwa watano
Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tuh
Jaji: Mnasemaje Tubreak au tuendelee
Wakili wa Serikali: Tubreak
Jaji: kwa Muda gani
Peter Kibatala: Kwa Sababu tulisha Kaa Dakika 30 tupumzike Kwa Dakika 45
Jaji: Mnasemaje Serikali
Wakili wa Serikali: Sawa
Jaji: Shahidi Tunapumzika, tunywe Maji tutarudi baadae Kidogo