Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na rushwa. Shauri kuendelea kesho Nov, 2, 2021

Yaliyojiri Kesi ya Mbowe na Wenzake Mahakama Kuu Divisheni ya Uhujumu Uchumi na rushwa. Shauri kuendelea kesho Nov, 2, 2021

"Hapana Mkuu, walikua na Bastola Means walitaka wanywe bure halafu wafyatue risasi hewani then watokomee"
Hahahahaaaa... ni full kujichanganya... kama nimesoma vyema kuna sehemu kasema saini zake huwa zinafanana akisaini akiwa mezani... lakini baadae akasema zinafanana akiwa amesimama nakutofautiana akiwa amekaa mezani...
 
Shahidi: Niliwajua Majina kabla ya Upekuzi

Mtobesya: Soma sehemu inayosema nilishuduia wakipekuliwa........ Mpaka inaisha Jina la Afande Jumanne, Soma kwa Sauti

Shahidi: Nilishuhudia Kupekuliwa kwa Vijana hao, na Kupekuliwa Mmoja wao alikutwa na Bastola yenye namba A5340 pamoja na Magazine yanye Risasi 3 .......pia alikuwa na Madawa ya Kulevya Ambae nilimfahamu kwa Jina baada ya Kuulizwa baada ya Upekuzi.

Mtobesya: Kwa hiyo Statement Ulifahamu Kabla au Baada

Shahidi: Baada ya Kupekuliwa

NB: sasa sijui mahakama itachukuwa lipi? Kaazi kweli kweli!
 
Hakuna kesi Mkuu ni ushahidi wa KUBUMBA. I hope Mbowe Xmas atailia Moshi na yule maushungi na vikaragosi vyake KUUMBUKA.

Shahidi: Niliwajua Majina kabla ya Upekuzi

Mtobesya: Soma sehemu inayosema nilishuduia wakipekuliwa........ Mpaka inaisha Jina la Afande Jumanne, Soma kwa Sauti

Shahidi: Nilishuhudia Kupekuliwa kwa Vijana hao, na Kupekuliwa Mmoja wao alikutwa na Bastola yenye namba A5340 pamoja na Magazine yanye Risasi 3 .......pia alikuwa na Madawa ya Kulevya Ambae nilimfahamu kwa Jina baada ya Kuulizwa baada ya Upekuzi.

Mtobesya: Kwa hiyo Statement Ulifahamu Kabla au Baada

Shahidi: Baada ya Kupekuliwa

NB: sasa sijui mahakama itachukuwa lipi? Kaazi kweli kweli!
 
Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea leo katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo upande wa mashitaka utaleta shahidi mwingine.

Fuatilia hapa kujua kitakachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 11/01/2021

==========

Watuhumiwa wote wamekwishawasili katika ukumbi wa mahakama tayari kuanza kwa kesi.

Jaji: Ameingia sasa

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa

Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe na wenzake

Wakili wa Serikali, Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
1. Pius Hilla
2. Abdallah Chavula,
3. Jenitreza Kitali,
4. Nasorro Katuga,
5. Esther Martin,
6. Ignasi Mwinuka
7. Tulimanywa Majige

Wakili Peter Kibatala anawatambulisha Mawakili Wa Utetezi
1.Jeremiah Mtobesya
2.Michael Mwangasa
3.Seleman Matauka
4.Nashon Nkungu
5.Alex Massaba
6.Michael Lugina
7.Maria Mushi
8.Hadija Aron
9.Dickson Matata
10.Jonathan Mndeme
11.Fredrick Kihwelo
12.John Malya

Jaji: anawait Washitakiwa 1,2,3 na 4 Wanasimama Kuitikia

Wakili wa Serikali: Kwa Upande wetu tuna shahidi Mmoja kwa Leo na tupo tayari Kuendelea Kwa Upande wetu tupo tayari kuendelea

Wakili Peter Kibatala: Tupo tayari na sisi Kuendelea

Wakili wa Serikali: Mmoja anatoka Kwenda Kumuita Shahidi Nje ya Chumba Cha Mahakama Mahakama Ipo Kimya Kidogo

Shahidi anapita ni Mdada Kajitanda Buibui na Kavaa Barakoa Kubwa sana Kumziba Sura,

Jaji: Majina Yako

Shahidi: Anita Varelian Mtali

Jaji: umri Shahidi: 45yrs

Jaji: Kabila

Shahidi: Mchaga

Jaji: Shughuli Zako

Shahidi: Nafanya Biashara

Jaji: Dini yako

Shahidi: R. C

Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii Kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni kweli, kweli tupu Eeeh Mungu nisaidie

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Shahidi Ataongozwa na Wakili Esther Martin

Wakili wa Serikali: Esther Ikumbushe Mahakama Majina yako

Shahidi: Anita Varelian Mtali

Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi

Shahidi: Moshi, RAU madukani.

Jaji: Jina lako la Tatu sijalipata Vizuri ni Mtali.?

Shahidi: Mtaro

Wakili wa Serikali: Umeishi kwa Muda gani Rau

Shahidi: Miaka 08

Wakili wa Serikali: Unafanya Shughuli gani

Shahidi: Nafanya Biashara ya Kuuza Mbege

Wakili wa Serikali: Ulianza lini Biashara yako ya Mbege

Shahidi: Miaka 08 ninayo

Wakili wa Serikali: Mbali na Biashara yako ya Mbege una bishara gani Nyingine

Shahidi: Kuna Glocery, Stationary, Banda la Tigo Pesa na Kuna Sehemu ya Kutolea Movie

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama 05 Mwezi 08 2020 ulikuwa wapi

Shahidi: Sehemu yangu ya Biashara, Nikifanya Usafi

Wakili wa Serikali: Saa ngapi

Shahidi: Saa Saba Kasoro

Wakili wa Serikali: Ya Muda gani

Shahidi: Ya Mchana

Wakili wa Serikali : Kabla ya Kufika eneo lako la Biashara ulikuwa umetoka wapi?

Shahidi: Nilikuwa Nimetoka Nyumbani Nikaenda Saloon Kuosha Nywele

Wakili wa Serikali: Na Ulipotoka Saloon kuelekea sehemu yako Kufanya Usafi

Shahidi: Nilikuta Wakaka Watatu walikuwa wamekaa Mbele Yangu walikuwa wanakunywa na Kusajili Laini

Wakili wa Serikali: Walikuwa wanakunywa nini

Shahidi: Walikuwa wanakunywa Bia

Wakili wa Serikali: Hizo laini walikuwa wanasajili wapi

Shahidi: Kuna Vijana wanapitaga Mitaani Kusajili Laini

Wakili wa Serikali: Ukiwa unafanya Usafi kitu gani Kingine ulishuhudia

Shahidi: Kuna wakaka wawili walikuwa wanapitapita wakiongea na simu, Wanaenda wanarudi wakiongea na Simu

Wakili wa Serikali: Hao wanaopita ni tofauti na wale uliposema walikuwa wanakunywa Bia

Shahidi: Hapana ni walewale

Wakili wa Serikali: Kutoka Kwako Unapofanyia Kazi Mpaka Glocery ni Umbali gani

Shahidi: Kama Hatua 10

Wakili wa Serikali: Hapo Katikati sasa, Kati ya Glocery na ulipo, pana kitu gani

Shahidi: Pana uwazi

Wakili wa Serikali: Baada ya Muda kitu gani kilitokea

Shahidi: Wakati wanaongea na Simu Walitokea watu wawili wakaongea kwa sauti kali "Mpo chini ya Ulinzi Mnahusika na Mambo ya Kigaidi, chuchumaa Chini Mikono Juu"

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kingine ulisikia

Shahidi: Chuchumaa Chini Mnahusika na Mambo ya Kigaidi Wakili wa Serikali: Ni watu gani sasa hao

Shahidi: Ni Askari

Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya nini wakati huo

Shahidi: Nafanya Usafi

Wakili wa Serikali: Pana umbali gani kutoka Walipo na Mpaka Ulipokuwa unafanya Usafi

Shahidi: Hatua 05

Wakili wa Serikali: Ulisikia nini Kingine

Shahidi: Sikusikia Kingine zaidi ya Chuchumaa Chini Nyoosha Mikono Juu

Wakili wa Serikali: Walikuwa Askari wangapi

Shahidi: Wawili

Wakili wa Serikali: Hali ya Pale ilikuwaje

Shahidi: Ilikuwa ni Utulivu

Wakili wa Serikali: Nini Kilifuata

Shahidi: Walitokea Askari Wengine watatu wakawa wamefika eneo la Tukio

Wakili wa Serikali: Ongeza Sauti

Wakili wa Serikali: Kitu gani Kiliendelea

Shahidi: Baada ya Kuwa Askari watano alitokea Mmoja akaniambia anaomba nisogee anahitaji Kuwafanyia Upekuzi

Wakili wa Serikali: Ni Askari gani huyo

Shahidi: Alinitambulisha anaitwa Askari Polisi Jumanne

Wakili wa Serikali: Ulifanya nini kujiridhisha?

Shahidi: Alitoa Kitambulisho Akanionyesha

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo nini kilifanyika

Shahidi: Alimsimamisha Mmoja

Wakili wa Serikali: Kabla ya Kumsimamisha..?

Shahidi: Afande Jumanne alijipekua kuanzia Kifuani akatoa Mifuko Nje

Wakili wa Serikali: We ulikuwa na nani wakati huo

Shahidi: Dada Mmoja anaitwa Esther

Wakili wa Serikali: Kutoka Eneo la walioambiwa Wachuchumae Chini, palikuwa na Umbali gani?

Shahidi: Kama Hatua Mbili

Wakili wa Serikali: Kuna Kitu gani Kingine

Shahidi: Raia walikuwa wamekuja

Wakili wa Serikali: Kabla ya Raia Kusogea eneo hilo palikuwa na hali gani?

Shahidi: Palikuwa na Jua

Wakili wa Serikali: ahaa ahaaa yani hali ya pale ilikuwaje?

Shahidi: Palikuwa pametulia

Wakili wa Serikali: Ikaendelea nini?

Shahidi: Alimsimamisha Mmoja akamuuliza Unaitwa nani?

Wakili wa Serikali: Akajibu anaitwa nani?

Shahidi: Adam Kasekwa

Wakili wa Serikali: Akamwambia nini?

Shahidi: Akiwa amenyoosha Mikono Juu akamwambia Geuka, akageuka

Wakili wa Serikali: Baada ya Kugeuka

Shahidi: Askari Jumanne alianza Kumpekua Kuanzia Kichwani, Mabegani, Alipofika Kiunoni alikuta Kitu kigumu

Wakili wa Serikali: Alikikuta Upande gani

Shahidi: Kushoto

Wakili wa Serikali: Maeneo Gani?

Shahidi: Niliona ni Bastola

Wakili wa Serikali: Ulijuaje kama ni Bastola?

Shahidi: Afande Jummane alituambia ni Bastola

Wakili wa Serikali: Halafu

Shahidi: akatuonyesha namba

Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni namba gani.?

Shahidi: A5340

Wakili wa Serikali: Zilikuwa kwenye nini

Shahidi: Kwenye Bastola

Wakili wa Serikali: Wakati anakuonyesha Bastola Adam alikuwa wapi?

Shahidi: Alikuwa amesimama

Wakili wa Serikali: Ukiona na nini Kingine

Shahidi: Risasi 03

Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea

Shahidi: Akaendelea na Upekuzi

Wakili wa Serikali: Nini kiliendelea

Shahidi: Akaendelea na Upekuzi, alipofika Upande wa Kulia akakuta Vitu vidogo vidogo Kwenye Karatasi ya Nailon akasema inasadikiwa ni Madawa ya Kulevya ila itajulikana Mbele.

Wakili wa Serikali: Zilikuwa ngapi Shahidi: 58

Wakili wa Serikali: ikawaje

Shahidi: Aliendelea Kumpekua akamkuta na Simu Ndogo aina ya Itel

Wakili wa Serikali: Hiyo simu akaifanyaje

Shahidi: Akatoa laini akakuta namba akaziandika

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo aliendelea na nini

Shahidi: Akamwambia Naomba fomu, .......akaleta fomu

Wakili wa Serikali: fomu ngapi

Shahidi: Zilikuwa Mbili

Wakili wa Serikali: Akafanya nini sasa Kwenye ile Fomu

Shahidi: Kaandika Vitu alivyokuwa amempekua

Wakili wa Serikali: Umesema palikuwa na fomu Mbili, fomu ya kwanza akijaza nini

Shahidi: fomu ya kwanza alijaza Bastola, Risasi na Laini

Wakili wa Serikali: Zilikuwa ni laini gani

Shahidi: Laini ya Voda na Airtel

Wakili wa Serikali: Baada ya Kumalizia fomu ya kwanza

Shahidi: alichukua fomu Nyingine

Wakili wa Serikali: Kabla ya Kujaza Fomu Nyingine

Shahidi: Alipomaliza Kujaza akampa akasaini na Baadae akasaini yeye alipo maliza Kusaini.

Wakili wa Serikali: alimpa nani

Shahidi: Alimpa Adam

Wakili wa Serikali: baada ya fomu ya kwanza nini kiliendelea

Shahidi: alichukua Fomu Nyingine

Wakili wa Serikali: alijaza nini

Shahidi: alijaza vile Vikete vidogo Vidogo

Wakili wa Serikali: Vingapi Vilikuwa Vingapi

Shahidi: Vilikuwa 58

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: akampa Adam asome alafu asaini na sisi akamtupa tusaini

Wakili wa Serikali: Wewe na nani..?

Shahidi: Mimi na Dada Esther

Wakili wa Serikali: baada Kumalizia nini kilifuata

Shahidi: akamuita Mwingine

Wakili wa Serikali: huyo Mwingine anaitwa nani

Shahidi: Mohamed Abdulahi Ling'wenya

Wakili wa Serikali: akamwambia nini

Shahidi: asimame ageuke, Baada ya kugeuka akaanza Kumpekua

Wakili wa Serikali: alianzaje Kumpekua

Shahidi: Kichwani Mikononi

Wakili wa Serikali: ilikuwaje

Shahidi: Upande wa Kulia alikuta na Vikete Vidogo Vidogo

Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi

Shahidi: 25

Wakili wa Serikali: akafanyeje

Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua

Shahidi: akavishika Akaendelea Kumpekua

Shahidi: alikuta Simu aina ya Tecno

Wakili wa Serikali: Rangi gani

Shahidi: Nyeusi

Wakili wa Serikali: akafanya nini

Shahidi: akapekua akakuta kuna laini

Wakili wa Serikali: laini gani

Shahidi: Hallotel

Wakili wa Serikali: baada ya Kupata simu akafanyeje

Shahidi: akazitoa zile Laini, Akampa yule Mwingine akazishika

Wakili wa Serikali: Na Yeye Akaendelea na nini

Shahidi: Akaendelea na Upekuzi

Wakili wa Serikali: hizo laini alikuwa anafanya nazo nini?

Shahidi: Alimpa Askari wa Pembeni akazishika

Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi

Shahidi: Aliendelea na Upekuzi lakini hakukuta kitu Kingine

Wakili wa Serikali: Baada ya Upekuzi

Shahidi: aliomba fomu Mbili


Wakili wa Serikali: fomu ya Kwanza alijaza nini

Shahidi: alijaza vile Vikete Vidogo Vidogo

Wakili wa Serikali: Vilikuwa Vingapi

Shahidi: 25

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo

Shahidi: Alimpa akasema akasaini

Wakili wa Serikali: Nani Yeye, afande Jumanne?

Shahidi: Ndiyo na Baadae Mohamed

Wakili wa Serikali: na baadae

Shahidi: tukasaini sisi

Wakili wa Serikali: Wewe na nani

Shahidi: Mimi na Dada Esther

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: Ile fomu Nyingine akajaza Simu na laini Nyingine

Wakili wa Serikali: Za Mtandao gani

Shahidi: Airtel na Hallotel

Wakili wa Serikali: Baada ya hapo

Shahidi: Alimpa Mohamed asome kisha akasaini

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: afande Jumanne alituomba na sisi tusome Kisha tusaini

Wakili wa Serikali: Wewe na nani

Shahidi: Mimi na Dada Esther

Wakili wa Serikali: baada ya Upekuzi

Shahidi: walivalishwa Pingu

Wakili wa Serikali: baada ya hapo

Shahidi: afande Jumanne akatuomba tuelekee Kituoni

Wakili wa Serikali: Hao walivalishwa Pingu walikuwa ni akina nani

Shahidi: Adam na Mohamed

Wakili wa Serikali: baada ya kuvalishwa Pingu..?

Shahidi: Wakaelekea kwenye Magari, Barabarani

Wakili wa Serikali: Palikuwa na Askari wangapi

Shahidi: Watano

Wakili wa Serikali: Walikuwa wamebeba nini

Shahidi: Wawili walikuwa wamebeba Bunduki

Wakili wa Serikali: Hali ya hewa eneo lile ilikuwaje

Shahidi: ilikuwa imetulia

Wakili wa Serikali: Hali ya hewa ilikuwaje

Shahidi: Kulikuwa na Jua na Mwanga

Wakili wa Serikali: Mlichukua Muda gani kwenye lile eneo Mpaka Mnamaliza Zoezi

Shahidi: Kama Dakika 45

Wakili wa Serikali: Baada ya Kufanya Upekuzi Kuna Vitu Vilipatikana na Kwamba Kuna fomu zilijazwa Sasa fomu ukiziona hapa utaweza Kuzitambua?

Wakili wa Serikali: sasa bada ya Kumalizia Mkaelekea kituoni, kituo gani..?

Shahidi: Central Moshi

Wakili wa Serikali: baada ya Kufika police central

Shahidi: Tuliandika Maelezo

Wakili wa Serikali: Maelezo ya nini

Shahidi: Kitu gani Kilichofanyika ......

Wakili wa Serikali: Tukianza na fomu ya Adam utaitambuaje

Shahidi: Kwa vitu vilivyoaandikwa, Jina langu na sahihi yangu

Wakili wa Serikali: Kulikuwa na nini Kingine Bastola

Wakili wa Serikali: Kingine

shahidi: Palikuwa na Risasi

Wakili wa Serikali namba gani Shahidi: A5340

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba nimpe fomu aweze Kuitambua

Wakili wa Serikali: Shika hii Karatasi iangalie kwa Makini

Shahidi: Ndiyo yenyewe

Wakili wa Serikali: Yenyewe nini

Shahidi: Fomu niliyo saini

Wakili wa Serikali: Umeitambuaje

Shahidi: Kwa Jina langu na Sehemu niliyosaini

Wakili wa Serikali: Jina lipo wapi, Ni Jina gani

Wakili Peter Kibatala: ALICHOKIFANYA DADA YANGU ESTHER HAIRUHUSIWI, ANAKWEMDA KWENYE DETAILS

Wakili wa Serikali: Sawa naondoa hilo swali

Wakili wa Serikali: Ungependa hii fomu ipokelewe Mahakamani

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi anaomba Fomu ipokelewe

Jaji: Wakili wa Mshtakiwa wa kwanza

MTOBESYA: HATUNA PINGAMIZI

Mallya: Hatuna Pingamizi Fredrik

Kiwhero: kwa Niaba ya Mshitakiwa.....wa tatu hatunapingamizi

Peter Kibatala: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Nne hatuna Pingamizi

Jaji: anaandika Kidogo

Jaji: Mahakama inaipokea kwa ID 1

Wakili wa Serikali: Shahidi pia ulisema kwenye huo Upekuzi pana Bastola na Risasi unaweza hapa Mahakamani ukavitambua Tuanze na Bastola

Shahidi: Ndiyo nitavitambua

Wakili wa Serikali: Bastola unazitambuaje

Shahidi: Kwa Namba A5340

Wakili wa Serikali: na Kwa Upande wa Risasi

Shahidi: namtambua, zilikuwa na Rangi ya Dhahabu

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Naona Exibit nimuonyeshe Shahidi

Afisa Wa Mahakama anafungua Bahasha ya Kaki Anamkabidhi Wakili wa Serikali

Wakili wa Serikali:
Hebu Kiangalie hiki kitu hapa, Iambie Mahakama ni nini

Shahidi: anaingilia bila Kushika, ni Bastola

Wakili wa Serikali: ambayo Imetoka wapi

Shahidi: Imetoka Kwa Adam

Wakili wa Serikali: Uliona wapi?

Shahidi: iliyotoka kwa Adam

Wakili wa Serikali: ni Kitu gani Kilichokufanya ukagundua

Shahidi: kwa namba

Wakili wa Serikali: Namba gani

Shahidi: A5340

Wakili wa Serikali: Umeeleza pia ulishuhudia Upekuzi wa watu wa wili ambao kwa Majina yao ni Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya, Je ukiwaona unaweza Kuwatambua

Shahidi: naweza Kuwatambua

WAKILI WA SERIKALI: WAPO HAPA MAHAKAMANI?

Shahidi: Wapo hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali: Wapo wapi

Shahidi: hapa Mbele, Mohammed amevaa Tshirt ya Amevaa Meupe Kijani na Nyeusi

Wakili wa Serikali: na Adam yupo wapi Shahidi: amevaa Shati lenye Rangi Nyeupe Nyeupe

Wakili wa Serikali: Yupo wapi hapa Mahakamani

Shahidi: Yupo pale

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu

Jaji: Upande wa Utetezi

Mtobesya:
Ndiyo Mheshimiwa Jaji

Mtobesya: naomba Nipatiwe ID 1 Mahakama Inampatia

Mtobesya: Shahidi umeomba Mahakama Ipokee Kielelezo hiki Onyesha Sehemu ipo saini

Shahidi: Nimesaini hapa

Mtobesy: Kwa Ushahidi wako Unasema ulisaini Nyaraka ngapi

Shahidi: Nne

Mtobesya: Ushahidi wako kwamba Sahihi zako Lote zinafanana

Mtobesya: Naomba kwa Kifungu 75(1) Sheria ya Ushahidi, Shahidi asaini tena sehemu Nyingine ili Mahakama iweze Kufananisha Saini zake

Jaji: Unaweza Kutusomea.? Mtobesya: anasoma Kifungu cha 75(1) cha Sheria ya Ushahidi

Jaji: hicho Kifungu kinaitaka Mahakama shahidi asaini ili iweze Kufanya ufafananisho

Mtobesya: Ndiyo ili Mahakama iweze kufananisha, kwa sababu tuna Nyaraka Nyingine inasaini yake tofauti

JAJI: lakini hiyo Nyaraka itakuwa imetengenezwa hapa, Utakuwa umeiiingiza Mhakama .....

Jaji : Bwana Matata una jambo la Ku-she na sisi

Matata: Sheria Anayosoma Wakili Mtobesya Ni Sheria inasema kuwa Shahidi anaweza kuandika sehemu tu 75(2) Mahakama inaweza Kuagiza Mtu yoyote Mahakamani Kulingananisha.

Jaji: Je hiyo inahusiana na Mahakama kumuelekeza Shahidi asaini?

Matata: ni tafasiri yangu kuwa Mahakama Inaweza Kuruhusu Shahidi Kuandika ili Kufananisha Kama alichokiandika ni sawa

Mallya: Pale kwenye 75(2) inasema any Documents haijambana wapi kwa hiyo anaweza Kusaini popote (any documents) ili Mahakama ifanye Uamuzi iwe imepata kwa Usahihi wake....kwa usahihi Kifungu cha 75 lakini siyo kwa Kumtaja Shahidi aandike

Jaji: Upande wa Mashitaka

Wakili wa Serikali: Maombi ya Mtobesya Pamoja na Kuegemea kutoka kifungu 75 cha Sheria ya Ushahidi tunaona amekimbia Sana na siyo wakati wake Lakini pangekuwa na Nyaraka Nyingine ambayo Ndiyo Ingekuwa imekuja Rasmi Mahakamani ndipo angetumia.......Njia yako ya Kutaka Shahidi Asaini Ni sahihi Kama watapinga tutashughulikia Kupinga huko wakati huo.

Jaji: Kwa tafsiri yangu Mamlaka iliyopewa Mahakama 75(2) ni naona Mahakama inayo Mamlaka kumuelekeza Mtu yoyote Kufanya Mlinganisho wa Maneno au Namba kwa Nia ya Kuiwezesha Mahakama Kufanya Ulinganisho, ila huyu Mtu aliye na maarifa Kuliko Mahakama Yenyewe. Najiuliza kama ...Leo nilikuwa na Avoid Upande wa Utetezi Kutuzuia Kutumia Nyaraka hii ambayo sisi tumeipata kwenye Comito.

Mtobesya///; Kifungu cha 47 cha Sheria ya Ushahidi ndiyo kinaruhusu Maoni ya Kitaalamu katika Ushahidi Lakini Kifungu cha 48 au 49 Sikumbuki Vizuri kinaruhusu hata mtu asiye Mbobezi Kufanya Maoni yake Hili Kifungu cha 75 chenyewe Kinataka Mahakama Kufanya Ulinganisho.

Jaji: Na Mimi na kubaliana na wewe Lakini kwenye Document uliyonayo hatujui baada ya Kumkabidhi Karatasi at asaini Sahihi gani kati ya hizo Mbili

Jaji: Ndiyo nasema wewe endelea na Jukumu lako kama Walitokea Wakapinga tutashughulikia Pingamizi hilo wakati huo ...na Sheria ya Ushahidi wa Kifungu cha 75 Vyote Vinafanya washitakiwa Kupewa Nyaraka zinazokusudiwa Kutumika dhidi yao kwenye Makosa Makubwa Kama haya kupitia Comito Kwa hiyo watupatie

Mtobesya: Asante Mheshimiwa Jaji

Mtobesya: Naomba nikabidhi iwe Nyaraka Original ya Hati ya Kuchukua Mali iliyosainiwa tarehe 25 2020 inayomhusu Mohamed Ling'wenya Kwa sababu sisi tunayo Moja

Jaji: chini ya Sheria Gani

Mtobesya: Kifungu cha 246 na 146 ya Makosa ya Jinai ...

..Angetoa basi Maombi Rasmi lakini hata kama no Original haiwezi kuitumia kwa wakati huu Haki yake ya Kuhoji aendelee nayo na anaweza Kuitumia hata sasa Sisi tuna tatizo na Procedure jinsi gani Ushahidi huu unataka Kuletwa Mahakamani

Jaji: Jamani Mmeelewa

Wakili wa Serikali: Sisi Haja yetu ni Swala la Procedure Ni kweli Tulianika Ushahidi Tutaokuja kutumia Mahakamani lakini ieleweka Kuwa Ushahidi hi ni Wa Kwetu. Hakuna mahala popote ambapo Mteja wake anaweza Kuwa na haki ya kutumia Nyaraka hizo ......

.Ubishi ulikuwa kama Mshitakiwa Alikuwa ametahiriwa au haja tahiriwa Mahakama ya Rufani ikasema kuwa Hilo ni Kubwa sana Kwake na Isingeweza Kujiingiza katika Risk. Kwa kesi hii basi Kama anataka Mahakama Ijiridhishe. Swala ni Kama Nyaraka hiyo imepokelewa na Kama .......imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki


KESI YA buying wa John dhidi ya Jamhuri criminal appeal namba 450 ya Mwaka 2017 Mahakama iliyoketi Shinyanga Katika Ukurusa wa 11 paragraph ya Mwisho ya a Ukurasa huo wa 11 Ambapo swala Lililojitokeza tangu wakati wa Trial Court na Kesi Ilikuwa ni ya Ubakaji ........

Mheshimiwa Jaji: tunatakiwa tuzingatie Mfumo wetu wa Utoaji haki, Mahakama kwa Kutimiza Wajibu wake anakuwa ni refa na siyo kwa kukaribishwa Kutaka Kufanya Uchunguzi Zoezi kama hilo ni Kuingiza Mahakama katika riski ambazo zinaweza Kuepukika.

...imekubali imeandikwa na Mtu huyu Na pia kama Nyaraka hiyo Nyingine kama Ingekuwa hapa angekuwa na Haki

Na Hilo Ndiyo Dhumuni la Comito Trial kwamba Mshitakiwa ajue anachokuja akujitetea nacho

Upande wa serikali: Sisi tunaona ni Kukiuka Procedure na Maombi hayo tunaomba uyakatae Mheshimiwa jaji Mtobesya: Tunapoteza sana Muda Mheshimiwa Jaji, Shahidi ni wa Kwao na Ushahidi ni wa Kwao Na sijui ni wakati gani tena sisi tutapata Kuwa na wasaa wa kuwa na Shahidi huyu

Na hapa swala la Copy kwa Washitakiwa halijazungumziwa wakati ni Haki kwa Mshitakiwa Kupatiwa Hiyo Nyaraka

Nashon Nkungu: Naona nisaidie Mahakama kama Afisa wa Mahakama alichosema Wakili Robert Kidando Amejieleza Kwenye Kifungu cha 76 tuh asemi kwa nini kuna Haki ya Kukabidhi wa Nyaraka za Comito Na Kingine Kifungu 30 cha Sheria inasema tupewe Copy siyo Photocopy ....

Ambapo wewe Umegundua Sahihi Katika Nyaraka hizo na Zilizopo hapa Mahakamani Sahihi zinatofautiana Kwa Maana hiyo Ukaomba Mahakama ikupatia Nakala halisi Jaji Jambo la Pili Kwakuwa wanasema Ushahidi huo watautumia basi Wahurumie Mapema ili uweze Kuutumia.

Jaji: Mtobesya

Mtobesya: naam Mheshimiwa Jaji

Jaji: hoja zako ulizijenga katika a Mazingira Matatu Haki za Mahakama Jinai hasa akatika Mahakama Kuu, amtu anasomewa na Kukabidhi wa Nyaraka Kwamba wewe Una taarifa Kwamba zipo Nyaraka wanazolenga kuzitumia Kama Ushahidi Wao

Mtobesya: Mheshimiwa nilikuwa naomba Mashauriano na Mahakama ilitusiiipe Mahakama Mzigo wa a kuandika Rulling

Jaji: mnasemaje Jamuhuri

Wakili wa Serikali: Ni Sawa Mheshimiwa

Jaji: Basi tuta Break kwa Dakika 10, tukutane pande zote pale Ofisini

Jaji: anatoka

Mawakili wamerudi

Jaji ameingia tena Saa 6 NA Dakika 24

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa tena Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe Kisha Mahakama Kimyaaaaaa

Jaji:
Muda Mfupi Uliopita Tuli-break kwa Nia ya Kuweka Sawa Mambo ya Kitaaluma Baada ya Kuyaweka Sawa na Kualika Sasa Mtobesya Kuendelea

MTOBESYA: Wakati Unaongozwa na Dada Yangu Esther Ulisema Uliandika Maelezo

Shahidi: Niliandika Tarehe 05 Mwezi 08 2020

Mtobesya: aliyeandika Maelezo yako

Shahidi: Sijui Jina lake

Shahidi: anaitwa Jumanne

Mtobesya: Ulishawahi Kukutana na Askari anaitwa Detective Coplo Francis.?

Shahidi: Sikumbuki kama nimekutana naye

Mtobesya: Lakini walikupa Maelezo Ukasoma na kisha Ukaona sawa

Shahidi Ndiyo

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Nipewe Statement (Handwritten Statement) Naomba Chini ya Kifungu Cha 164 (1h) cha Sheria ya Ushahidi

Wakili wa Serikali Wapo Kimya Jaji anawasubiri

Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi la Kumpatia hii Nyaraka

Jaji: Pokea

Mtobesya: Shahidi Unajua Kusoma na Kuandika

Shahidi: Ndiyo

MTOBESYA: Shika Karatasi zipo Mbili Soma kama Ndiyo Uliyosoma Ukasaini na Kama Kuna Majina yako na Askari aliye andika Ihakiki Kwanza

Shahidi Anaipekua, anaikazia Macho anafunua funua mara Nyingiyingi

Mtobesya: Ndiyo hiyo.?

Shahidi: Kimyaaaa anatizama tena ile Karatasi, anaipekua

Shahidi: Ndiyo Yenyewe

Mtobesya: Soma Kuanzia Juu Kwa Sauti

Shahidi: Mimi Ndiyo Mwenye Majina na anuani takwa hapo Juu Mkazi Wa Kilimanjaro Nimezaliwa Mwaka 1979 Familia ya watoto Nilikuwa naelekea Saloon Rau Madukani Na baada ya Kumalizia nilieleza Sehemu yangu ya Biashara Kufanya Usafi. Mbele Kuna Bar Na Kukikuwa na Vijana walikuwa wanakunywa Pale Sikuwa nawafahamu Kwa Maana walikuwa ni wageni

Mtobesya: Soma Kote

Shahidi: Sikuwafahamu kwa Maana walikuwa ni Wageni maeneo haya Kwa Muda Mwingi walikuwa wanaongea na simu. Kwangu Afande Mmoja akajitambulisha Jina Afande Jumanne Akaniomba niwe Shahidi huru Ambapo nilishuduia Kufanya Upekuzi Kwenye Kupekuliwa Kijana Mmoja alikuwa na Bastola Zenye nmabaA A 5340 Pia alikutwa na Kete 58 za Madawa ya Kulevya

Shahidi: Shahidi ananendelea kusoma Baada ya Muda walikuja watu watano na a Kuwafuata wale Vijana Na wakaambiwa wapo Chino ya Ulinzi Askari hao walitaka Kufanya Upekuzi ndipo walipokuka Kuni.... Kamyamaza Kidogo Askari hao walihitaji Kufanya Upekuzi ndipo walikuja.......Adam Kasekwa mbaye nilimfahamu Jina baada ya Kuulizwa Jina lake baada ya Upekuzi Na huyo Mwingine aliyekuwa naye alitaka anaitwa Mohammed Ling'wenya ambaye pia kwenye Upekuzi alikutwa na Simu Moja ya Samrt Yenye Line ya Airtel na Hallotel na Kete 21 za Madawa ya Kulevya

Watu hawa wawili nilikuwa siwafahamu Majina wala Sura niliwafahamu baada ya Kutaja Majina yao Baada ya Kukamatwa na Polisi, Askari wale nilikuwa siwafahamu Na Kiongozi wao aliyekuwa anafanya a upekuzi aliwatambulisha kwangu ASP Jumanne.

Baada ya Majina hayo Nilijaza Hati ya Upekuzi Na Kuzuia Mali Walisaini wote na Watu tulioshuhudia Na Afande Jumanne Na baada ya Upekuzi Nilijaza Hati ambayo inaonyesha Upekuzi umefanyika Ambapo tukasaini wote na tulioshuhudia Haya Ndiyo Maelezo Yangu, Sahihi Kama Nilivyoyatoa.

Mtobesya: Nitakurudisha Kwenye baadhi ya Maeneo kama Ulivyosoma

Mtobesya: Ni sahihi Katika Ushahidi wako ulisema Askari wawili walifika wakawaambia Mpo chini ya Ulinzi na Wakawatajia Makosa yao

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hapo, hayo Maneno Yapo au hayapo

Shahidi: Hayapo

Mtobesya: Nilikusikia Unasema hawa Vijana waliokamatwa wao walikuwa wanakunywa wakati wewe unafanya usafi katika Eneo lako la Biashara

Shahidi: Sahihi

Mtobesya: Kwenye Maelezo yako hiyo Taarifa ipo

Shahidi: Haipo

Mtobesya: Nilikusikia Ukisema Kwamba afande Jumanne alikuja kwako akatoa Kitambulisho

Shahidi: Ndiyo alitoa Kitambulisho

Mtobesya: Hayo Maelezo ya kutoa Kitambulisho yapo kwenye Statement yako

Shahidi: Hayapo

Mtobesya: kwenye Maelezo yako nilikusikia watuhumiwa Waliposimamishwa kabla ya Upekuzi walijitambulisha Majina yao kwa Polisi aliyekuwa anafanya Upekuzi Nitakuwa sahihi nikisema Statement Yako inasema Uliwajua Majina Baada ya Upekuzi

Shahidi: Niliwajua Majina kabla ya Upekuzi

Mtobesya: Soma sehemu inayosema nilishuduia wakipekuliwa........ Mpaka inaisha Jina la Afande Jumanne, Soma kwa Sauti

Shahidi: Nilishuhudia Kupekuliwa kwa Vijana hao, na Kupekuliwa Mmoja wao alikutwa na Bastola yenye namba A5340 pamoja na Magazine yanye Risasi 3 .......pia alikuwa na Madawa ya Kulevya Ambae nilimfahamu kwa Jina baada ya Kuulizwa baada ya Upekuzi.

Mtobesya: Kwa hiyo Statement Ulifahamu Kabla au Baada

Shahidi: Baada ya Kupekuliwa

Mtobesya: Nitakuwa sahihi, kwenye Ushahidi wako ulielezea ulisaini Nyaraka Nne za Kushuhudia Upekuzi

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Nenda Sasa baada Upekuzi huo,

Shahidi: Nilijaza Hati ya Upekuzi na Hati ya Kuzuia Mali ilionyesha Upekuzi Umefanyika, ambao tulisaini wote tulioshuhudia pale.

Mtobesya: Ishia hapo, Nitakuwa sahihi nikisema Nyaraka hiyo Uliyosoma inaonyesha ulisaini Nyaraka Moja..? Na siyo Nne kama Ulivyosema Asubuhi ya Leo

Shahidi: kwa Mujibu wa Mstari huu ni Kweli

Mtobesya: Isaidie Mahakama sehemu nataka Usome Kwa Sauti, Soma baada ya Neno Watuhumiwa wale wawili

Shahidi: Baada ya Upekuzi huo na Kusaini Hati ya Kuzuia Mali ambapo tukisaini wote.

Mtobesya: Wakati Wakili Wa Serikali Esther anakuongoza Ulisema aliyekuongoza hapo ni Jumanne

Shahidi: Nilisema ni Afande ambaye sikujua Kwa Jina

Mtobesya: Ipo Kwenye Rekodi, Jaji ataona

Shahidi: hapana

Mtobesya: Ungependa hayo Maelezo Yawe sehemu ya Ushahidi Wako Siku ya Leo

Shahidi: Ndiyo ningependa uwe Ushahidi Wangu Siku ya Leo

Wakili wa Serikali: Hatuna Pingamizi

Jaji: Mahakama imeyapokea Maelezo hayo Kama Kielelezo namba 02 kwa Upande wa Utetezi

Mtobesya: Kwa Ruhusa yako Mheshimiwa naomba Kuendelea

Mtobesya: Ulielezea Mahakama Ulisaini Nyaraka za Uzuiaji wa Mali, zaidi ya Nne

Shahidi: Ndiyo

MTOBESYA: ieleze Mahakama Hati hizo zilijazwa na nani Mpaka Nyie Mkasaini

Shahidi: Zilijazwa na Askari Jumanne

MTOBESYA: na wewe Unakumbuka ulisaini kwenye Hati zote

Shahidi: Ndiyo

MTOBESYA: Unaweza Kuisaidia Mahakama Ulisaini Upande gani

Shahidi: Pale Mwisho Kwa Pembeni

Mtobesya: Naomba Nimuonyeshe Shahidi ID 1 Nitakuwa Sahihi Nikisema Nyaraka zote Nne ulisaini hapa Kwenye Jina lako

Shahidi: Siyo zote sehemu hii, Zingine Nilisaini Upande wa Kushoto na Zingine Upande wa Kulia.

Mtobesya: Unaweza Kutuambia Ulizosaini Upande wa Kushoto zinaruhusu nani na Kwaajili ya Vifaa Vipi

Shahidi: NilizoSaini Upande wa Kushoto zilikuwa zinamhusu Adam

Mtobesya: Hizo Ulisaini Upande wa Kushoto

Shahidi: Nilisaini Upande wa Kulia

Mtobesya: na Zilizomuhusi Mohammed Ulisaini Upande gani

Shahidi: Upande WA Kushoto

Mtobesya: Ulisaini Baada au Kabla ya Jina lako

Shahidi: Nilisaini baada ya Jina langu

Mtobesya: Na Ni Ushahidi wako Mbele ya Mahakama zote Ulisaini wewe Mwenyewe na kwa Mwandiko wako

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Na Kwa Ushahidi Wako Saini zako umesaini wewe Zikiwa zinafanana

Shahidi: Kuna zingine zilikuwa hazifanani kwa sababu nilikuwa na Hali tofauti

Mtobesya: Mweleze Mheshimiwa Jaji Sasa ni hali ipi Ulikuwa nayo ikapelekea Saini zako Kutofautiana

Shahidi: Kuna saa, wakati wa Ukamataji Nilisaini wakati nimesimama na Zingine nimesaini wakati nimekaa kwenye Meza.

Mtobesya: Unaieleza Mahakama Ukisaini ukiwa umesimama na Wakati Umekaa saini lazima zitofautiane

Shahidi: Ndiyo

Mtobesya: Nilisikia wakati anakuongoza Dada Yangu Wakili wa Serikali Kuwa Mlisaini wakati Wa Tukio

Shahidi: Wakati natoa Maelezo Nilisaini Nikiwa mezani lakini Zile zingine Nilisaini nikiwa nimesimama

Mtobesya: Ni Signature zipi sasa zinazofanana ukiwa Umekaa au Umesimama

Shahidi: Nikiwa Nimekaa ndiyo zinafanana

Mtobesya: Ukiwa Umekaa umesaini Mara Ngapi na Nyaraka zipi

Shahidi: Zile ambazo nilikuwa kituoni kutoa Maelezo.

Mtobesya: Zote ambazo ulisaini Ukiwa Umekaa Zina fanana..?

Shahidi: Hapana

Mtobesya: Zote ulizoSaini Ukiwa Umesimama Zinafanana au hazifanani

Shahidi: Zinafanana

Mtobesya: Mheshimiwa Jaji naomba Kuishia Hapo

Mtobesya: naomba Kurudisha Kielelezo

Jaji: Wakili Malya unahitaji Muda gani

Mallya: Nusu saa hivi

Mallya: Bado unauza Mbege

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Mbege unayouza wewe inalewesha

Shahidi: Kuna Inayolewesha na Isiyolewesha

Mallya: Una Ndugu au Mume ambaye ni Polisi

Shahidi: Hapana

Mallya: Ulitambuaje kuwa hiki ni Kitambulisho cha Polisi?

Shahidi: Niliona Chapa ya Taifa

Mallya: Kitu gani Kingine Uliona

Shahidi: Niliona Jina lake

Mallya: Lilikuwa limeandikwaje

Shahidi: kwa kweli hapo Sikumbuki

Mallya: Umesema Wakati Unafanya Shughuli zako za Usafi na Vijana walikuwa wanakunywa Bia, Ni hatua ngapi

Shahidi: Ni hatua 10

Mallya: Napiga hatua Mahakamani

Mallya: Hapa Kuna Hatua Saba tu

Mallya: Umbali wa Hatua 10 Macho yako yanaona Vizuri

Shahidi: Yanaona Vizuri

Mallya: hapa Kuna Umbali Wa Hatua 7 tu Unasema Mtu Amevaa Tshirt yenye Rangi Nyeusi wakati ni Dark Green Je unataka Mahakama iamini kwamba unaona Vizuri?

Jaji: umeelewa swali..?

Shahidi: ..natumiaga Miwani, Sema Leo nimesahau Miwani

Mallya: Ulielezea Kuwa siku ya Tukio ulivaa a Miwani

Shahidi: Hapana

Mallya: Siku ya Tukio ulikuwa Umbali wa Mita 10 Leo Mshitakiwa yupo hatua 10 tu hakuna aliyevaa Tshirt Nyeusi, unataka Kumwambia Mheshimiwa Jaji unaona Vizuri?

Shahidi: Kimyaaaaaaaaaa

JAJI: umelielewa Swali

Shahidi: Ndiyo

JAJI: Jibu Basi

Shahidi: Kuna saa Macho yanashida.

Mallya: Wakati Unatoa Maelezo Leo Uliomba Miwani uweze Kuangalia Vizuri.?

Shahidi: Sikuomba

Mallya: Ni sahihi Kuwa Usajili wa Simu unafanya kwa Kitambulisho?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: na wewe Uliwaona watu waliopo Mahakamani walikuwa wanasajili Line za simu

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Kwenye Maelezo Yako kuna sehemu umesema Wanasajili lini?

Shahidi: Hakuna

Mallya: pale Rau Bia wanauza au Bure?

Shahidi: Wanauza

Mallya: Wakati mnawapekua Mliwakuta na Bastola na Siyo Pesa

Shahidi: Hakuwa na Pesa

Jaji: Watakuwa walishalipaaaaaa

MAHAKAMA kichekoooooo

Mallya
: zoezi la Kufanya usafi Lilichukua muda gani?

Shahidi: Kwa muda wa Kufanya Usafi kama Dakika 10

Mallya: Wakati Tukio linatoka Ulishamaliza Usafi au Ulikuwa unaendelea

Shahidi: nilikuwa naendelea ikabidi Nisimame

Mallya: Tukio la kukamatwa lilichukua Muda gani?

Shahidi: Rudia swal?

Mallya: Kitendo Cha Kukamatwa hawa watu Mpaka unaitwa kushuhudia ilichukua muda gani?

Shahidi: kama Dakika 03

Mallya: Kwa hiyo tukijumlisha Dakika 10 za Usafi na Dakika 3 wakakuita wewe Zoezi la Kusachiwa lilidumu kwa a muda gani?

Shahidi: Kwa Dakika 45

Malya: Saa Nane ilikuwa imefika

Shahidi: Kama saa Nane Kasoro

Mallya: Kwa Maelezo Yako wewe yalitolewa Umesaini Ukiwa polisi saa 7 kamili Je, tukuamini wewe au?

Shahidi: Muamini Maneno Yangu

Mallya: Tuchukue Yote.?

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Kabla ya kwenda Kwenye Tukio Siku hiyo ulikuwa wapi na wapi

Shahidi: Nilitoka Nyumbani baada ya Usafi, Nikaenda Kwa Mgonjwa na Baadae Saloon

Mallya: Umeulizwa aliyekuchukua maelezo Yako ni nani

Shahidi: Simfahamu Kwa Majina

Mallya: Hakukuonyesha Kitambulisho ndiyo Maana Humkumbuki?

Shahidi: Hapana alinitajia nimemsahau

Mallya: Kwa kutazama Kwa Macho yako sahihi yako uliyosaini Hapa na Hapa Kwenye Exibit 02 zinafanana

Shahidi: Hazifanani lakini ni sahihi zangu

Mallya: Kwenye Maelezo Yako umeeleza Mahali Kiongozi wao, Afande nani

Shahidi: Afande Jumanne

Mallya: akitokea Mtu akisema yeye ndiyo Kiongozi aliyekwepo atakuwa Muongo

Shahidi: Ndiyo

Mallya: Unamfahamu Kingai

Shahidi: Hapana

Mallya: na Ulisema Mapolisi walikuja kujitambulisha kwako.?

Shahidi: alikuja Mmoja

Mallya: Askari waliowakamata watuhumiwa walikuwangapi

Shahidi: Walikuwa watano

Mallya: Mheshimiwa Jaji ni hayo tuh

Jaji: Mnasemaje Tubreak au tuendelee

Wakili wa Serikali: Tubreak

Jaji: kwa Muda gani

Peter Kibatala: Kwa Sababu tulisha Kaa Dakika 30 tupumzike Kwa Dakika 45

Jaji: Mnasemaje Serikali

Wakili wa Serikali: Sawa

Jaji: Shahidi Tunapumzika, tunywe Maji tutarudi baadae Kidogo
 
Back
Top Bottom