Yaliyojiri: Kongamano la Katiba: 15 Januari 2011 Nkrumah UDSM

Yaliyojiri: Kongamano la Katiba: 15 Januari 2011 Nkrumah UDSM

AMA tunaomba msaada wako yaani kina Jack wanahaingaika na mobile wewe na keyboard yote hiyo..... please kuwa mzalendo... tunakuomba, hii ndio kazi ya JF kujuzana :help:
Kwanini unalazimisha hadi AMA na Zombe wakati kuna wengine wana speed zaidi yao kama kuna kitu unataka kutoka kwao wa-PM.
 
Katiba ya Soth Africa imeandaliwa kwa miaka 100..and is the best in Africa right now!
acha uzushi wewe kama imetumia miaka 100 then unamaana na sisi tutumie miaka 100 pia? kwani tuna serikali ya kikaburu mpk tutumie hiyo miaka yoote na tupe ushaidi ati ilitumia miaka mia kha! maana ninavyojua ilitumia miaka isiyozidi mitatu haswa baada ya Mandela kutoka Gerezani na 1994 serikali mpya ikaingia chini ya katiba mpya! Hiyo katiba mpya ya Tanzania inaweza kutengenezwa ndani ya mwaka mmoja kama tuna nia na maslahi ya nchi na si ya vikundi binafsi yatazingatiwa!
 
Uteuzi wa wakuu wa wilaya Dar es salaamu ni mfumo wa kikoloni.
 
Kwanini unalazimisha hadi AMA na Zombe wakati kuna wengine wana speed zaidi yake kama kuna kitu unataka kutoka kwao wa-PM.
Kina nani hao?, basi waombe na wenyewe watujuze...... does not matter nani analeta info so long as tunapata info.... hata kama wewe unacheki TV hapo please do the neadful
 
Kuwapo kwa halmashauri za wilaya ni kwa hisani ya serikali kuu!!! Jenerali anasema haya ndio mambo ya kuzungumzwa na asasi za kiraia.
Je, kuna uhalali wa kuendelea kuwa na wakuu wa mikoa na wilaya??? Huu ni mfumo tuliorithi kwa wakoloni.
Du...Ma-RC na ma-DC watapenda mjadala huu kweli?...kibarua kinachungulia kaburi!..ha ha haaa!
 
Uteuzi wa wakuu wa mikoa na wilaya wanateuliwa kwa misingi ipi! Darasa la saba, fomu four, PhD, hadi Makoplo wa jeshi.
Wengine wanateuliwa kwa sababu ni shemeji wa mtu fulani au mchumba wa wakuu.......du jenerali anaua live!!
 
Direct hit to JK au??? Eti siku hizi hadi wachumba zao ni wakuu wa wilaya!!!
 
"Ikifika wakati hata wachumba zenu ndio wanakuwa wakuu wa wilaya" -ulimwengu
 
Ukumbi umelipuka kwa furaha baada ya jamaa kuwaua wakuu wa mikoa na wilaya.................hii ishu ya kuteua wachumba wao kuwa wakuu wa wilaya na mikoa inabidi lijadiliwe....
 
Wananchi tuchague wenyewe wakuu wa wilaya na mikoa, hili lijadiliwe.
 
Mkuu usinitishe....????, if we can not get the best even a better one will do..... ? we need it quick.
Sure we need it quick...but we have to look into that quickness...Katiba huwa ina'ferment...(hii ni lugha ya pombe zaidi)..that is..inakomaa taratibu kama pombe inavyotengenezeka pale breweries!...
The older the better...(ni kama wines vile...)
 
Uteuzi wa wakuu wa mikoa na wilaya wanateuliwa kwa misingi ipi! Darasa la saba, fomu four, PhD, hadi Makoplo wa jeshi.
Wengine wanateuliwa kwa sababu ni shemeji wa mtu fulani au mchumba wa wakuu.......du jenerali anaua live!!

Makubwa leo,mbona tutajibeba tusio kuwa wachumba/shemeji za wakuu? no wonder watu wengine wana watoto kila wilaya!!!
 
Tuna mfumo usioeleweka, wa kibunge au wa kirais....................................tujadili ni mfumo upi unatufaa.
 
Katiba ya Soth Africa imeandaliwa kwa miaka 100..and is the best in Africa right now!
Miaka mia duh kwani tunaandika urithi wa sayari ya Earth tunataka kuhamia Mars hivi Kenya walitumia miaka mingapi?
 
JENERALI

Kila kilichoko chini ya ardhi na katika nchi (rasilimali ni za nani) ni za serikali au ni za wananchi? nani awe na kauli kali juu ya usimamizi wa rasimilali hizi ni nani? jamii zinazosihi karibu na rasilimali hizi zina haki gani na wajibu gani katika rasilimali hizi?


anatoa mfano wa loliondo ambako wananchi wanaonekana kuwa ndio kero kwenye rasilimali walizonazo


Vyombo vya serikali ikiwemo bunge wanapaswa kujua juu ya mikataba inayoingiwa katika nchi hii. Nasema hivi kushadidia transparency as oposed to opaque. Mfumo wa kumuachia mtu mmoja kufanya mambo mengi ni utata.


Ingekuwa vizuri kama wananchi katika maeneo yao wangechagua watawala wao, katika nafasi za kisiasa kama mkuu wa weilaya, waytu wengi hawaoni umuhimu wa nafasi kama hizi. Nafasi za polisi na nyinge waachiwe wa magogoni wateue, ila kwa swala la mtu wa kilimo n NAFASI muhimu wananchi waachiwe wachague wenyewe.


Hakuna umuhimu wa wakuu wa wilaya ila kama itaonekana na wananchi wanafaa basi wachaguliwe na wananchi na wawajaribu ili nmiaka mitano wapimwe na kama hawafai watimuliwe


Hawa nao wamelewa kama wakubwa, hawa wadogo wamelewa vijiweni na wakubwa banquet kubwa, wwanasimama mbele ya wananchi wanawaatukana na kuwaambaia hawana la kuwafanya na kama vipi wakaseme juu.


Je tunahitaji wabungfe zaidi ya 200, wakati India wanawananchi zaidi ya bilioni kadhaa, wanawabunge 500 sisi watu 40M lakini tunawabunge kibao. Sasa hivi tunamfumo koko ambao hujui ni mfume wa kiraisi au kibunge


Mwalimu aliulizwa kwa nini kateulia waziri mkuu ambae hajatajwa kwenye katiba, Mwalimu akasema haijaandikwa kwenye katiba kwamba kutakuwa n awaziri mkuu lakini pia haijasema hakutakuwa na waziri mkuu


Mijadala ya civil society izungumze juu ya utawala bora na madalaka ya umma na ni mgawanyo gani uwepo kati ya serikali kuu na serikali za mitaa


Tumesikia mara nyingi wakuu wa serikali wakionya halmahsauri msipofanya moja mbili tatu tutafuta sisi hizi halmashauri. Kwa hisyo uwepo wa halmahsauri hizi ni kwa hisani ya srikali kuu. Bila hisani hizo halmshauri hizo hazipo. Hii inatalkiwa isiwepo kwa sababu wananchi wameamua kuwa na serilkali zao za mitaa na vyombo hivyo vitakuwepo bial kujali serikali kuu ipende au ispende


Je kuna haja ya kuwa na wakuu wa wilaya na mikoa wanaoteuliwa dsm? huu ni mpangilio wa kikoloni. Gvana wa kikoloni alikuwa akikaa dsm na kuteua watu wa kwenda kusimamia na kutekeleza ukoloni wao.


Tunajua uwezo waliokuwa nao magavana ulikuwa ni katika kuwateua watu waliokuwa mahiri na wenye uwezo mkubwa sana wa kuchota mali za watanganyika na kuzipeleka nje. India na Malaysia walikuwa wakilimisha bangi, na kuuzwa china na nchi nyingine ili fedha zikipatikana waendeshe imaya zao huko india. Umahiri wao ni kuchota rasilimali zetu na hatujui wanapeleka wapi.


Sijui hawa wakuu wa wilaya wanateuliwa kwa vigezo viupi. Mana nimeona kuna alieteuliwa darasa la 7 na mwingine phd na mwingine koplo mwingine brigedia jenerali, wote wakuu wa wilaya.


Imefika mahali, ahsakum, mpaka wananchi wanajua huyu kaletwa hapa kwa kuwa ni shemeji yake fulani huko juu (ApplauseS). Zamani Mwl na Kawawa, mara nyingi walikuwa wakipeleka watu kwa kuwa ni dereva mzuri wa tanu alipewa pensheni na sio ukuu wa wilaya. Ila inapofika hata wachumba zenu ni wakuu wa wilaya sasa hapo pengine (Big applauseS)
 
Makubwa leo,mbona tutajibeba tusio kuwa wachumba/shemeji za wakuu? no wonder watu wengine wana watoto kila wilaya!!!
Nadhani Riz1 atakuwa anahitaji mke wa 2......unaweza kumfaa!!! ahahahahaaaaaaah!!!
 
Back
Top Bottom