CHADEMA
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 490
- 2,471
Mgombea Urais wa Chadema anafanya kampeni kata kwa kata. Usikose kuyasikia madini ya Lissu, leo kata ya Isman.=====
"Mafurikoo Ya Wananchi Wa Iringa Kwenye Viwanja Vya Mwembe Togwa KatiKati Ya Mji Wa Iringa.
Mheshimiwa Tundu Lissu Akiwa Jukwaa Amenadi Sera Zifuatazo...
1. Itakuwa Jambo La Neema Na Afya Kama Wagombea Wawili Wakubwa Wakikutanishwa Kwenye Mdahalo Utakaorushwa Na Vyombo Vyote Vya Habari, Leo Naomba Nitoe Rai Kwake Kwa Raisi Magufuli Tukutane Kwenye Mdahalo Huo.
2. Uchaguzi Uliopita Tulisema Tutaanzisha Elimu Bora Bure, Lakini Raisi Magufuli Alipoingia Madarakani Akaanzisha Elimu Bure, Kwa Maana Watoto Wetu wanaToka Mashuleni Wakiwa Bure, Yaan Hawana Maarifa. Basi Tunasema Na Kuhusu BIMA Ya Afya Na Wanadandia. Kama walivyokuwa Buree Kwenye Elimu Basi Na Kwenye Afya Napo Itakuwa Bureee.
3. Kuengua Engua, Wagombea 55 Walienguliwa, Na KatiKa Mkoa Wa Morogoro Majimbo 8 Wamewaengua Wagombea 5, Hivyo Ni Wazi Kabisa CCM na Magufuli Hawawezi Hushindani. CCM Imefilisika Kiasi Hicho.. Wenzetu Kwenye Mikutano Yao Lazima Abebe Watu kwenye Mabasi.
Leo Tuongelee Kuhusu Elimu Ya Juu, Mimi Na Wenzangu Pamoja Na Raisi Magufuli Tulisoma Elimu Ya Juu Kwa Kodi Za Wananchi. Lakini Leo Ona Vijana Wetu Wengi Wanakosa Haki Yakusoma Elimu Ya Juu. Vijana Wetu Wanakosa Haki yakupata Mikopo Sababu Wazazi Wao Waliowasomesha Kwenye Shule Binafsi. Ubaguzi Wakutoa Mikopo Unakosesha Vijana Wetu Haki Yakupata Elimu.
Ulipaji Wa Mikopo Umekuwa Tatizo Na Kandamizi Kwa Vijana Wetu, Zamani Ilikuwa Ukipata Kazi Unalipa 3% Lakini Leo Wamebadilisha Sheria Na Wanawakata 15% Ambapo Imekuwa Ni Mzigo Mkubwa Kwao, Serikali Ya Chadema Ikiingia Madarakani Itarudisha Sheria Ya Zamani Ya 3%.
Serikali ya Chadema Ikiingia Madarakani Itaweka Wanachi Wote Wawe Kwenye Mfuko Wa Jamii, Sababu Watu Wote Tunazeeka NA Watu Wote Tunapata Matatizo.
Tanzania Inareserve Kubwa Ya Gesi Kwenye Bahari Ya Hindi, Tanzania Imekuwa Nchi Ya Tatu Afrika Kuwa Nakiasi Kikubwa cha Gesi, Na Ndo Hapo Tutakapotokea Watanzania. Serikali Ya Chadema Inasema Utafiti Na Uendelezwaji Gesi Ulioanzishwa nA Jakaya Kikwete Tutarudisha Mchakato Uendelee, Ambapo Kwa Sasa Umesimama na Wawekezaji Wameenda Nchi Jirani. Kwahyo Sasa Jibu Ni Tutengeneze Uchumi Kwenye Gesi.
Serikali Ya Magufuli Wameifuja Mifuko Ya Jamii, Pesa Za Wafanyakazi Zimetumiaka Kwa mambo Ambayo Hayana Mahusiano Na Wafanyakazi. Walipoona Mambo Magumu Wakaleta Kikokotoo Cha Ajabu. Leo Kuna Wastaafu Hawajalipwa Mpaka Leo. Ufujaji Wa Mifuko Ya Jamii Unamuumiza Kila Mtu, Hivyo Basi Ni Tarehe 28 Piga Kura Ya Ndio Kwann Wagombea WaChadema Tuchukue Nchi Tuondoke Na Hizi Mambo.
Mwisho, Mahusiano Mabaya Na Nchi Jirani Umesababisha Kutokuwa Na Mahusiano Mazuri Kibiashara.