Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 59,045
- 94,974
Yaani kesi ya uongo ila habari ziwe za kweli?Mungu wa mbinguni akutangulie ulete habari za kweli siyo ushabiki!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yaani kesi ya uongo ila habari ziwe za kweli?Mungu wa mbinguni akutangulie ulete habari za kweli siyo ushabiki!
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Hivi kuna 31 ya June kweli? au mie ndie sielewi?Wakili wa Serikali: Unakumbuka Ilikuwa ni wakati gani?
Shahidi: (Tigo) walitaka Taarifa za mihamala ya Fedha kutoka 01 June ya 2020 Mpaka 31 June ya 2020 Nikaingia Kwenye Computer Nikaziona
Bla bla bla bla bla bla bla bla .....
Wakili wa Serikali:Shahidi tufafanulie Maneno Ya Juu kama Sender Maana yake nini
Shahidi (Tigo): Send My Op namba 0719933386 Receiver 0787555200 Miamala wa Tarehe 20 Kiasi 500,0000 Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 21na Balance Ilikuwa 2.3M
Ana ukweli gani njaa tupu inamsumbua.Hivi mbona mnataka kulaumu kila mtu? Mlitaka huyu Legal Officer akatae kweli kutoa taarifa alizoombwa? Kuna sehemu amesema uongo mpaka sasa? Ungekuwa wewe ndiyo mwajiriwa wa Tigo kwa nafasi hiyo na umetakiwa kwenda kutoa ushahidi ungekataa? Hebu tuacheni kusukuma lawama kwa kila mtu.
Ushakula ban...[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kwahiyo unadhani JF ndio inanilisha au kunifanya napumua.
Unatoa umuhimu sana kwa vitu ambavyo haviongezi uhai.
Tena kheri asingesema ni mwanasheria..Leo ni leo ..naona muda huu na mkewe anamsikiliza mume wake eskariot akiwa mahakamani ili hela wazigawane vzrShahidi wa leo naye ni mwanasheria, sasa kama alikua anaona wenzake waliomtangulia wanakosea kwasababu hawajasomea sheria ngoja asubiri zamu yake, kibatala anamlia karanga
Hatuna kitu kama hikoHivi kuna 31 ya June kweli? au mie ndie sielewi?
Jamii forum tu ndiyo wanauwezo huo wa kumtetea member wao kutoka kwenye uonevuUnataka kuwalaumu bure MIC,ulitaka wafanyeje kama wameombwa watoe hizo taarifa tena kwa barua rasmi kutoka Taasisi inayoruhusiwa kisheria kupewa hizo taarifa? Mbona Makampuni karibu yote yanafanya hivyo,pindi yanapotakiwa kutoa taarifa kwa Taasisi zinazoruhusiwa kisheria.Hakuna Kampuni yoyote hapa Nchini itakataa kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi,Mahakama na TRA.
Kampuni lakini wategemee kupungua kwa watejaHivi mbona mnataka kulaumu kila mtu? Mlitaka huyu Legal Officer akatae kweli kutoa taarifa alizoombwa? Kuna sehemu amesema uongo mpaka sasa? Ungekuwa wewe ndiyo mwajiriwa wa Tigo kwa nafasi hiyo na umetakiwa kwenda kutoa ushahidi ungekataa? Hebu tuacheni kusukuma lawama kwa kila mtu.
Kashaipata tayari, apeleke matusi yake huko facebook alipopazoea.Bado tu hujapigwa ban pamoja na matusi yako yote?
Screen short mkuu ameniudhi snKashaipata tayari, apeleke matusi yake huko facebook alipopazoea.
Mbona kwa Sabaya zilipotolewa walichekelea?Point! Silioni kosa la huyu shahidi wala Tigo wenyewe. Hili ni swala la kisheria na ni matakwa ya kisheria kwa wao kufanya hivyo kosa litakuja kama wanatoa taarifa za uongo
Kwenye nchi zetu sie mazwazwa na misukule ya CCM ndipo hizi Sheria zinafanya kazi.
Kwa wanaojielewa huu u$3ng3 haupo..
Kampuni kama apple FBI waliomba taarifa hawakupewa, just imagine FBI hawakupewa taarifa...
Mtandao kama twitter unamfungia raisi DTrump account...
Haipaswi kampuni yeyote Kutoa taarifa za mteja bila idhini yake...
Na hii michezo hata ukifahamiana tu na hao IT wa hizi kampuni, ukiomba tu taarifa za mtu fulani hata mkeo Wana print zoooteee...
Ayaaaaa mkuu ahsante kwa umakini 😂😂😂😂😂😂Hivi kuna 31 ya June kweli? au mie ndie sielewi?
Asante kwa update mkuu, kazi nzuri sana, hawa mashahidi wanatia kinyaaIkiwa leo ni tarehe 2 November 2021 , kesi hii inayobeba sehemu kubwa ya habari za Tanzania inaendelea tena Mahakamani hapo .
Baada ya ushahidi wa Muuza Mbege wa Rau Kukamilika , Leo upande wa Jamhuri utaleta shahidi wa Tano miongoni mwa wale 24 waliopangwa kutoa ushahidi huo .
Kama kawaida JF itakuletea moja kwa moja kesi hii kutoka Mahakamani , usiondoke .
===========
Jaji ameingia Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe Imeshatajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando Anatambulisha
1.Pius Hilla
2.Nassoro Katuga
3,Abdallah Chavula
4.Ester Martin
5.Jenitreza Kitali
6.Tulimanywa Majige
Kibatala anatambulisha Jopo lake
1. Michael Mwangasa
2.Seleman Matauka
3.Nashon Nkungu
4.Alex Massaba
5.Michael Lugina
6.Maria Mushi
7.Hadija Aron
8.Dickson Matata
9.Jonathan Mndeme
10.Fredrick Kihwelo
11. John Malya
Jaji Mashtakiwa 1,2,3 na 4 Wananyanyuka kuashiria uwepo wao
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Tunashahidi Mmoja Kwa Leo Lakini Kabla ya Kuendelea Leo tuna ombi, Na Maombi yetu yatamuhusu Shahidi Wa Leo Mheshimiwa
Jaji: Wakati wa Kufile Mashahidi tuliorodhesha Majina Kama Frank Kapala
Jaji: Ndiyo
Wakili wa Serikali: na Kule Kwenye Comito Proceedings Katika Ukusara wa 32 wa zile proceeding za Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zilitaja Kama Frank Kapala Lakin kama tulivyo leta information Barua ya 11 August 2021 Ndiyo alitaja kama Frank Kapala Mheshimiwa Jaji Kwa Usahihi ....Shahidi huyu anaitwa Frank kapara.
Wakili wa serikali: Kwa hiyo tunaomba Kumbukumbu sahihi za Mahakama zi-note kama Frank Kapara Kwa kifungu 264 Sura ya 20 cha CPA Rev Ya 2009 Na Kwa sababu Ushahidi wa Shahidi huyu ulisomwa wakati wa Comito Proceedings tunaomba turuhusiwe Kuendelea na Shahidi huyu.
Jaji: Kifungu gani?
Wakili wa Serikali: 264 Sura ya 20 kama Ilivyofanyiwa marekebisho Mwaka 2009
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Maombi yetu ni hayo tu
Mtobesya: Tumesikia Maombi ya Upande wa Mashitaka na Kwa sababu Wanasema Substance ndiyo Iliyo contain Ushahidi Wake tangu Maelezo yake Polisi. Kwa Upande wetu hatuoni Kama inaathiri Haki za Mteja wetu, Hatupingi hilo Ombi Kwa niaba ya Mshitakiwa Wa Kwanza, Asante.
Wakili John Mallya: Kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili hatuna Pingamizi.
Wakili Fredrick Kihwelo: hatuna Pingamizi Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu.
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi Kwakuwa wameleta Maombi Rasmi.
Jaji: Samahani Kidogo, Unachotaka Kirekebishwe Unaweza Ku-Spell
Wakili wa Serikali: FREDY KAPALA
Jaji: Basi maombi ambayo yameletwa Kurekebisha Kumbukumbu za Mahakama Kuwa Shahidi alikuwa Frank Kampala na Sasa atafahamika kuwa ni FREDY Kapala Na hiyo ndiyo Itakuwa kumbukumbu Mpya ya Mahakama, NATOA AMRI. Mawakili wote Wananyuka na Kukubaliana na Jaji.
JAJI: Shahidi aletwe sasa
Wakili wa Serikali: Ameenda Kuitwa
Jaji: Anakuwa Shahidi Wa Ngapi huyo
Wakili wa Serikali: Shahidi 05
Jaji: Utetezi Ndiyo..?
Kibatala: Ndiyo
Jaji: Majina yako
Shahidi: Naitwa Afredy Kapala
Jaji: Umri
Shahidi: 38yr
Jaji: kabila
Shahidi: Mpare
Jaji: Shughuli yako
Shahidi: Nimeajiriwa na kampuni ya Tigo
Jaji: Dini yako
Shahidi: Mkristo
Shahidi: Naapa Mbele ya Mahakama hii kuwa Ushahidi nitakao toa utakuwa ni Kweli, kweli tupu Eenheeeee Mwenyezi Mungu nisaidie.
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Wakili Nasorro Katuga atamuongoza
Wakili wa Serikali Nasorro: Nitakuuliza Maswali
Wakili wa Serikali: Umesema Unashughulika na nini?
Shahidi: Nimeajiriwa na kampuni ya kibiashara inaitwa TIGO
Wakili wa Serikali: Kwanini Unasema Kampuni ya kibiashara
Shahidi: Kwa sababu kampuni iliyosainiwa Brela ni MIC Tanzania
Wakili wa Serikali: Jina la Kibiashara ndiyo
Shahidi: Tigo
Wakili wa Serikali: Kampuni ya MIC Tanzania Ltd Inafanya Shughuli gani?
Shahidi: Mawasiliano ya Simu pamoja na Mihamala ya Kifedha
Wakili wa Serikali: Mwambie Mheshimiwa Jaji Umeajiriwa lini
Shahidi: March Mwaka 2012
Wakili wa Serikali: Umeajiriwa kama nani?
Shahidi: Kama Mwanasheria wa Tigo
Wakili wa Serikali: Katika Kitengo Kipi
Shahidi: Kitengo cha Sheria
Wakili wa Serikali: Umesema Kampuni yako inajishughulisha Kutoa Mawasiliano ya Simu na Mihamala ya kifedha Iambie Mahakama kwa nani?
Shahidi: Kwa Wateja Ambao wanamiliki line za Mitandao ya Simu
Wakili wa Serikali: Hawa wateja Wa Tigo Wanapatikana Vipi?
Shahidi: Wanapatikana Kwa Kununua line za Tigo na Wakaitumia basi Wanakuwa Wateja wetu. Na ili ifanye kazi lazima ifanyiwe Usajili.
Wakili wa Serikali: Kwenye Kusajili mnasajili Kitu gani?
Shahidi: Kwa mtu ambaye ana kitambukisho cha NIDA tunatumia NATIONAL IDENTIFICATION NUMBER. Mtu anaye sajili ataingiza Namba ya Kitambulisho Cha Taifa Itasoma Taarifa.
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama process za Manunuzi ya Line kama zipo?
Shahidi: Mtu yoyote anaweza Kufika kwenye Duka au sehemu ambayo kuna Wakala anauza hizo line za Tigo akiwa na Kitambulisho Cha Taifa, Lakini pia Kuna Wageni ambao wanatakiwa kutumia passport....
Wakili wa Serikali: Mtu anaye jua atafanya nini?
Shahidi: Ataweke Kidole Kigumba, Zitasoma Taarifa zote ambazo zipo Kwenye NIDA, Kama Jina Na tarehe ya kuzaliwa Kwa hiyo Taarifa hiyo itachukuliwa Na kuhifadhiwa Kwenye Mfumo wa Tigo kama Taarifa za Owner au Mtumiaji wa hiyo line.
Wakili wa Serikali: Mtu asiyejua NIDA, unaposema Zinaenda Kutally na Taarifa za NIDA unamaanisha Nini?
Shahidi: NIDA nimfumo wa Usajili wa Vitambulisho Vya Taifa ambao unatunzwa na Authority
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama unaposema Taarifa zile zitachukukiwa na Kuhifadhiwa Tigo, Nani atazichukua
Shahidi: Tunasema Ki Electronic kuna Mfumo wetu ikizipata na Ikatally inatunza Kwetu, Kwa hiyo Mifumo inawasiliana
Wakili wa Serikali: Jinsi ya Kusajili line Taratibu ziko Vipi
Shahidi: Ukishanunua Laini na Kwamba wewe sasa Unawasiliana, Tuna kutumia Meseji Kuwa kama Unataka Kutumia huduma ya Mihamala ya Fedha, Ukisema Okey tunakupa Vigezo na Masharti.
Wakili wa Serikali: Hiko Kitendo Mnakiitaje?
Shahidi: Umejiregister Kwenye Huduma ya Tigopesa
Wakili wa Serikali: Nikurudiahe kwako sasa wewe Mwenyewe, Tigo Umeajiriwa kama Mwanasheria Je Majukumu yako ni Yapi
Shahidi: Kushauri Viongozi Maswala Yanayohusu Sheria, Kutengeneza Kusoma, kupitia na Kusaini Mikataba Kufuatilia, Kusimamia Kesi zote zinazohusiana na Tigo ...Kumsaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama Katika Kupata Taarifa Mbalimbali Kutoka kwa Wateja zinapohitajika.
Wakili wa Serikali: Jingine, Baada ya kutoa hizo Taarifa
Shahidi: Kama Kuna Jinsi Yoyote Kusaidia Chombo chochote Katika Kutafuta Taarifa, Naweza Kusaidia Siyo VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama tu Bali hata Mtu Binafsi anaweza kupata Msaada wangu.
Wakili wa Serikali: Ni Vipi Mtu Binafsi, Mtu X anaweza kupata Taarifa za Mtu Y
Shahidi: Mtu Mmoja Kupata Taarifa za mtu Mwingine HAIWEZEKANI
Wakili wa Serikali: Kwa mujukumu hayo uliyoyataja, Unamajukumu gani au Ujuzi gani inayo Kusaidia katika Kutekeleza Majukumu yako
Shahidi: Kama Mwanasheria wa kampuni Nina Digrii ya Sheria, Nimesomea India JSS law college. Under MYSORI University, Ambayo niliipata 2009 Nilisoma Pia Advanced Computer Course, MYSORI University India 2007. Nilisoma Pia Advanced Diploma in Practice Nilimaliza Mwaka 2012 Baada ya hapo Kuna Training mbalimbali ambazo Nimezipata Nikiwa kazini 2012 nilipoanza Kazi
Wakili wa Serikali: Zitaje Training gani
Shahidi: Nilipopata kazi ilikuwa ni Majukumu yangu Nilikuwa nimeingia Kampuni ya Telecom Nilipata Training Ya Mwezi na nusu
Wakili wa Serikali: Ulisomea nini ktk hiyo Training
Shahidi: Mifumo ya Kujifunza Kutumia, ilikupata Taarifa Wa kwanza ni oracle Wa Kusaidia Kupata Taarifa mbalimbali zilizopo Sehemu za Kazi.
Shahidi: Kuna system Nyingine ambayo CONVIVER iliyokuwa Inasaidia Kupata Mihamala Yote ni soft ware BILL QUERY Iilikuwq Inasaidia Kujua matumizi Mbalimbali ya Mteja Upande wa Vocha Na SMAP ni Mfumo Sawa QUERY Kwa hiyo nilikuwa nasaidia VYOMBO Vya Ulinzi Na Usalama Kupata ...Information
Wakili wa Serikali: Unaweza Kukumbuka Ulikuwa unafanyiwa na nani
Shahidi: Ofisini na Mtu anaitwa Mr.....
Wakili wa Serikali: Ofisi za Tigo ziko wapi
Shahidi: Ofisi za Tigo Zipo Makumbusho DERM COMPLEX
Wakili wa Serikali: Unakumbuka Training Nyingine
Shahidi: 2015 palikuwa na Training Nyingine Baada ya Mifumo Kubadilika Baada ya oracle ikaja SQL Server CONVIVER ikaja Kubadirishwa Ikaja TELVIVER IKAJA ENVIVER ambayo sasa Ikaja Information Mbayo Ukiingia Unaona Matumizi ...na Kila Kitu. Wanakufundisha Kule Unakoenda Kuchukua zile Information Siyo Kila amtu anaruhusiwa Kwenda Kuchukua Unafundishwa Jinsi gani ya Kuzilinda.
Wakili wa Serikali: Baada ya Mifumo Kubadilika sasa
Shahidi: Ikabidi tupate Training, Jinsi zinavyofanya kazi na Tabia zake
Wakili wa Serikali: Katika Training zako ulipata Lolote Kuhusiana na Information ambazo unaenda kufanyia Kazi
Shahidi: Wanakufundisha General Overview
Wakili wa Serikali: Umetaja Training za 2012 na 2015 Je una Training Nyingine
Shahidi: Zipo Nyingine hizo ni Major Kila Siku Dunia Ikileta System Mpya tutaambiwa tu Kuna Training za Kila Siku Katika Majukumu ya kazi
Wakili wa Serikali: Nikurudishe Nyuma Wakati Unataja Majukumu Yako Unasema Unasaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama. Je Ni VYOMBO gani
Shahidi: VYOMBO Vyote Vya Usalama Ukijumlisha Polisi, Jeshi, Kama ni Anga kama ni Ardhi na VYOMBO Vyote Vinavyofanya Uchunguzi wa Kisayansi. 2.Taarifa za Mihamala ya Fedha, Kutuma na Kupokea fedha 3. Kuna Recharge ya Vocha na Kutumia pamoja na Matumizi yake 4. Taarifa za Usajili 5. Taarifa Nyingine zote zinazoambatana Kama NIDA, LOCATIONS, BILL MBALIMBALI ANAZOLIPA
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama sasa Unawasaidia Kuwapa Taarifa, Je ni Taarifa zipi Mnawapa, ulikuwa unatumia Neno zinazoruhusiwa Kisheria
Shahidi: Zozote ambazo zitakuwa zinahitajika sisi tunazo 1.Kuna Kupiga na Kupokea Simu, Za wateja wetu zinaitwa Call Details ...
Wakili wa Serikali: Shahidi Iambie Mahakama Hizo Taarifa wewe unazitoa wapi
Shahidi: (Tigo) Taarifa zote za kampuni pamoja na Wateja wake Zinakuwa Stored Kwenye Server
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Nani anaitoa Taarifa kwenye Server
Shahidi: (Tigo) Taarifa zote Zinakuwa Served Automatically Mtu anapo piga Simu Mnara Unasima na Taarifa zinashuka na Zina switch kwenda Automatically Kwenda Kwenye Server Kuwa stored. Lakini pia Kuna watu ambao ni Observers wa kungalia na Ku Audit kazi Nzima ya Server
Wakili wa Serikali: hizo Taarifa unazozitoa Unasema Zinakuwa self Generated, Je kiuadilifu kuwa hizi ni zile zilizojitengeneza, Uadilifu wake kwenye Server?
Shahidi: (Tigo) Kama kampuni ina Mifumo ya tofauti ilitengenezwa Mahususi Kulinda hizi Server na The Whole System
Wakili wa Serikali: Unaweza kuwa unaijua hiyo Mifumo
Shahidi: (Tigo) Yeah Naweza kukujibu Kuna Mfumo Obeservit, Server au Kutoka Kwenye Switch yanyewe inakuwa na Catalist Na Kuna HUAWEI pia
Wakili wa Serikali: Unajishughulisha na nini na unafanyaje kazi?
Shahidi: (Tigo) ni software ambayo kazi yake ni Kucheki Kama Kuna Mtu au kitu kili Intend Kuingia. Kuna Firewall ni Mfumo wa kuulinzi Pale kwetu wanatumia SISQO Kuchuja kinachoingia Na Kutoka Kwenda kwenye ....
Shahidi: (Tigo) Kuna Kitu Kinaitwa AUDIT Kuangalia nani na nani Kachukua nini na Kapita wapi Kingine kuna VAPT Volumeability Acess And Penetration Test Hizi Test zinafanywa na Watu ambao ni Very Profesional lakini ni Independent Office ambapo Mnawapa Kazi Ya Kuingia .... Kwenye Mifumo yenu So It's the test Ukitaka Unamleta Unamwambia Vunja Mifumo yako Akijaribu anakwambia Wapi pana Udhaifu na wapi Mtu anaweza Kupita Inabidi Kufanya Test Mara kwa mara ili Ujue.
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Ili Usitujaze sana, Wewe Umeyajuaje
Shahidi: (Tigo) Training niliyopata, Kazi nilizofanya, uzoefu niliyopata, na Matatizo ya kila Siku (Challenge).
Wakili wa Serikali: Unaiambia Mahakama ndiyo yaliyokupa Ujuzi
SHAHIDI: (Tigo) Training, Experience ya 9yrs na Matatizo Computer nitakayopewa, nitapewa Acess kwa kuombewa Access Kwamba Mtu tuliyemuajiri anahitaji Kupata Access ili utendaji wake wa Kazi uwe Rahisi
Wakili Wa Serikali: Iambie Mahakama wewe Kwakuisaidia VYOMBO Pelelezi au VYOMBO Vya Ulinzi wewe Unafanyeje
Shahidi: (Tigo) Ukipata Kazi tuh, Kwa Maana ya kuajiriwa Kuna Vitendea Kazi kama Computer na simu ya Kwanza, Ni Vitu Vinavyo Configure Namaanisha Simu nitakayopewa na ..
Wakili wa Serikali: Unapoombewa Acess Unapewa Vitu gani?
Shahidi: (Tigo) wakati Unapewa Access Kuna SERVICE NOW system ambayo inampa Ruhusa Boss wako Ruhusa ya kuthibitisha kwamba unakuja Kufanya Kazi Fulani Kuna watu ambao ni IT security wanatakiwa kuangalia. Naingia Mara ya Kwanza Kwa Laptop lakini Kuna System Nyingine itaniambia Kama tunataka Password Yako Kuverify Either Inipigie Simu au Itumie sms, itatuma Alafu itatuma sasa Code ili niweze Kufungua Sasa Kwenye System.
Wakili wa Serikali: Sasa Umeshakuwa Approved Kwamba Huyu Mtu anafaa, Iambie Mahakama sasa Vitu gani Unakabidhiwa
Shahidi: (Tigo) Laptop Ukishapewa na Simu Kuna Vitu Vinakuwa vinawekwa ndani ya Laptop ambapo Kuna System Nyingine itaniruhusu Mimi Kuingia Mimi kwenye hiyo Computer.
Wakili wa Serikali: Code Unapewa Mara Moja unapo ajiriwa.?
Shahidi: (Tigo) Kila Ninapotaka Kuingia
Wakili wa Serikali: Nini Kitafuata
Shahidi: (Tigo) ndiyo nitakuwa na Uwezo wa Ku Access Emails, Kufungua Systems yoyote ile
Wakili wa Serikali: Nataka Kujua Sasa Jinsi ya Kuingia Kwenye Server
Shahidi: (Tigo) Kuna Mifumo sasa Nilitaja Mfumo wa SQL Itanisaidia ku-Commicate Kupata Taarifa mbalimbali
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Unaweza Je Kujua hapa umezipata na Utafanya nini
Shahidi: (Tigo) nikishaingia na kama nimezipata Kuna Button ya ku-Execute itazileta Kwenye Screen ya Laptop Yangu Kwamba naziona lakini siwezi ku-editi (READ ONLY) Kwamba naweza Kuziona tu ..nikitaka itaniruhusu Kuzi Print
Wakili wa Serikali: Ishu ya kuvisaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama Utaratibu Ukoje
Shahidi: (Tigo) Kila Chombo Cha Ulinzi Kinahitaji Kuwa na Hizo Document iwe Amri au Ombi lazima iwe In Writing
Wakili wa Serikali: In Writing Unamaanisha nini?
Shahidi: (Tigo) iwe na Proper heading, naIwe na Nini wanataka
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo ni Barua, lazima iwe hivyo
Shahidi: (Tigo) NI Barua au Order ya Mahakama
Wakili wa Serikali: Kwa kumbukumbu zako Mnamo tarehe 02 Mwezi 07 2021 ulikuwa wapi
Shahidi: (Tigo) nilipata Barua Mbalimbali za Maombi, Katika Barua hizo Kuna Barua ilitoka Kwa Kamishina wa Upelelezi wa Kisayansi Ikihitaji Taarifa za Namba ya mteja.
Wakili wa Serikali: Ulisema kuna aina Mbili Za Maombi kuwa kuna Maombi na Amri. Je hiyo ilikuwa nini?
Shahidi: (Tigo) Ilikuwa ni Requeast
Wakili wa Serikali: Unaweza Kukumbuka Ilikuja kwa Maombi Ya Kuomba Taarifa fulani za Namba fulani, Je unaweza Kukumbuka.? Hiyo namba uliyoombewa Kwenye Hiyo barua
Shahidi: (Tigo) Baada ya Kuifikiria Sana anaitaja 0719933386
Wakili wa Serikali: hilo Ombi lilikuwa ni Maombi Mangapi
Shahidi: (Tigo) yalikuwa Maombi ya Mihamala ya Fedha na KYC
Wakili wa Serikali: KYC unamaanisha nini
Shahidi: (Tigo) Usajili.
Wakili wa Serikali: baada ya Kupokea Sasa, Nini Ulifanya Kuhusiana na Ombi hilo
Shahidi: (Tigo) nilipopokea ombi Kutoka kwa kamishina, Niliingia Kwenye Computer yangu Nikaweka Credentials Zangu Nikafunga Screen Server Nikaingiza namba ya Simu kwenye Procedure Ambayo...Inaniruhusu Kupata Tigo Pesa.
Wakili wa Serikali: Unakumbuka Ilikuwa ni wakati gani?
Shahidi: (Tigo) walitaka Taarifa za mihamala ya Fedha kutoka 01 June ya 2020 Mpaka 31 June ya 2020 Nikaingia Kwenye Computer Nikaziona
Wakili wa Serikali: Baada Ya Kuziona
Shahidi: (Tigo): Nikaziprint
Wakili wa Serikali: Kabla ya kuziprint
Shahidi (Tigo): nili-execute Kuona Ni Yenyewe Nikaingiza Namba sehemu ambayo itanipa Usajili. Server yenyewe ilitoa Majibu Ambapo Taarifa Inapokaa iliweza Kutoa hiyo Taarifa ambayo niliweza Kuiomba.
Wakili wa Serikali: Na huko Unatumia Mfumo gani?
Shahidi(Tigo): SQL server
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Utendaji kazi wa Siku hiyo Ulikuwaje
Shahidi (Tigo): Laptop yangu ilikuwa Kwenye condition Nzuri Inafanya kazi Kawaida SQL sever ilikuwa Inafanya kazi Vizuri ....
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama hicho ulichokifanya, watu wapi wa Kitengo gani wanaweza Kuwa na Access ya Server kama wapo?
Shahidi: (Tigo) kila Mtu anapata Access Kutokana na Kazi anayoifanya ambapo Kuna watu wanaangalia ile server Kama Inapata Moto Kila wakati ili iweze Kufanya kazi yake
Wakili wa Serikali: Kama watu gani?
Shahidi (Tigo): Kama Legal Department Ambapo tulipaswa Kuwa na Access Ya Kuingia Kutokana na Order za Mahakama ni watu tunaoweza Kufanyia Kazi Haraka Kuna watu Wanaitwa Order Audit, Watu wa IT security Kuna watu pia wa Data warehouse ...
Wakili wa Serikali: Nyinyi Legal Department Mnapewa Access ya Kufanyaje
Shahidi (Tigo): Kusaidia VYOMBO Vya Ulinzi na Usalama na lazima Muhuri wa MIC Tanzania Ltd
Wakili wa Serikali: Turudi Kwenye namba uliyotaja, Baada ya kuprint Ukafanya nini?
Shahidi (Tigo): Niliandika Barua kumjibu Kamishina wa Makosa ya kisayansi alichokuwa anakitafuta, nikamrudishia Katika Barua nilisha Print lazima Nigonge Muhuri na Signature yangu ....
Wakili wa Serikali: Ukiambatanisha na nini hiyo Barua?
Shahidi (Tigo): Cover later, Barua ya kamishina, Mihamala ya kifedha na KYC
Wakili wa Serikali: Ukafanya nini?
Shahidi (Tigo): Nikazipeleka Ofisi ya Cyber
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Leo hii Ukionyeshwa hiyo Barua na Hizo Print Out kama utaweza Kuzikumbuka.
Shahidi (Tigo): naweza Kuzimbuka kwa Barua yangu ambapo Cover later ipo kwenye headed Paper. Cover later Ya Tigo Nimesaini Nimegonga na Muhuri
Wakili wa Serikali: Barua Ukiona Utakumbuka
Shahidi (Tigo): Nitakumbuka kwa namba Niliyofanyia Kazi
Wakili wa Serikali: Namba ngapi
Shahidi (Tigo): Nimesahau
Wakili wa Serikali: Tarehe?
Shahidi (Tigo): Nimesahau ila ni 2020
Wakili wa Serikali: ambapo ulisema hiyo namba ni ngapi
Shahidi (Tigo): 0719933386
Wakili wa Serikali: Kingine
Shahidi (Tigo): Mihamala ya Fedha pia ninaweza kutambua Kwa sababu niligonga Muhuri wa MIC Tanzania Ltd
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Kwa ridhaa ya Mahakama naomba nimuonyeshe Shahidi Documents fulani Kama anaweza Kuzitambua.
Wakili wa Serikali: Anamkabidhi Makaratasi
Wakili wa Serikali: Nakupa hii Nyaraka Ishike iangalie Moja badala ya Nyingine
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Kama umeweza Kuitambua
Shahidi (Tigo): nimetambua Barua ya juu ambayo ni Cover later ambapo ina later Head ya Tigo
Wakili wa Serikali: Kingine
Shahidi (Tigo): Nimeona Muhuri Niliogonga na namba ambavyo Nililetewa kwenye Barua ya kamishina
Wakili wa Serikali: na KYC
Shahidi (Tigo): Same same Ina namba na pia nimegonga Muhuri za Usajili wa namba hiyo, Ziwe Kielelezo katika Kesi hii
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama Sasa Unaiomba nini Mahakama
Shahidi (Tigo): Naomba Mahakama hii Ipokee Barua niliyoandika kwa kamishina Uchunguzi wa Kisayansi, Barua iliyokuwa inahitaji Taarifa alizokuwa akihitaji Mihamala ya Fedha ya namba iliyokuwa anaiombea na Taarifa ...
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Kwa niaba ya Mshitakiwa wa kwanza hatuna Pingamizi
Malya: kwa niaba ya Mshitakiwa wa Pili hatuna Pingamizi
Fredrick Kihwelo: hatuna Pingamizi Kwa Niaba ya Mshitakiwa wa tatu
Peter Kibatala: na sisi pia kwa niaba ya Mshitakiwa wa Nne hatuna Pingamizi
Jaji: tunaweza Kukiita Kielelezo namba ngapi
Wakili wa Serikali: Namba 05 Mheshimiwa jaji
Mahakama ipo Kimya kwa Dakika 10 Sasa
Jaji: Mahakama Imepokea Barua ilivyoandikwa Kutaka Taarifa ya Uchunguzi wa Kisayansi kama Kielelezo namba 06 Napokea Barua ya Tigo, Majibu yao Kama Kielelezo namba 07 Napokea Print Out Kama Kielelezo namba 08 Na Mwisho Nyaraka ya KYC kama Kielelezo Namba 09.
Jaji: Sasa Naomba Shahidi utusomee Kila Kielelezo
Shahidi (Tigo): anasoma Barua ya Ombi la Kupatiwa Uchunguzi wa Kisayansi
Shahidi (Tigo): anasoma Barua ya majibu yao Kwa Kamishina wa Upelelezi wa Kisayansi Kwa niaba ya MIC Tanzania Ltd Ni matumaini Yangu Taarifa tuliyowapatia Itawasaidia
Shahidi (Tigo): anasoma Taarifa ya Mihamala ya Kifedha.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji nafikiri Shahidi (Tigo) hawezi Kusoma hiyo Nyaraka yote tutakesha hapa Wao Wamuongoze na Kisha Tukubaliane kuwa Nyaraka ilisomwa.
Jaji: upande wa serikali
Wakili wa Serikali: Sawa Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali:Shahidi tufafanulie Maneno Ya Juu kama Sender Maana yake nini
Shahidi (Tigo): Send My Op namba 0719933386 Receiver 0787555200 Miamala wa Tarehe 20 Kiasi 500,0000 Tarehe 20 July 2020 Saa 2 na Dakika 21na Balance Ilikuwa 2.3M
Wakili wa Serikali: Twende kwenye hii KYC Kielelezo namba 09
Shahidi (Tigo): Imeanza na namba pale Juu Jina la Kwanza Jina la Katika, Taifa, Jenda na Vitu Vinginevyo Mstari unaofuata 0719933386 Jina Freeman Last name Mbowe Nationality Tanzanian From Kilimanjaro
Shahidi (Tigo): Kuna namba ya Tigo ya O719933386 imetuma kiasi cha fedha Tsh 500,000 kwenda kwa namba ya Airtel namba 0787555200
Wakili wa Serikali: IOP Maana Yake nini?
Shahidi (Tigo): Kitu Kimetumwa kutoka Namba hiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa hayo ndiyo maeneo ambayo tulikuwa tunaomba Shahidi ayasome
Wakili wa Serikali:Kielelezo namba 7 iambie Mahakama ni nini?
Shahidi (Tigo): Barua iliyotoka kwa Kamishina Ikiwa inataka taarifa za mteja
Wakili wa Serikali: Tarehe 20.7.2020 inaonekana nini.
Wakili wa Serikali: Sender City maana yake nini?
Shahidi: Mnara wa mtu aliyetuma Pesa alikuwa wapi?
Wakili wa Serikali: Fafanua Sender One Mikocheni
Shahidi: aliyetuma fedha alikuwa Mikocheni na alikuwa Kinondoni
Wakili wa Serikali: Fafanua hapo Kwamba Mikocheni ipo Kinondoni
Shahidi (Tigo): hapana, MIKOCHENI ni KITONGOJI
Wakili wa Serikali: Kielelezo namba 9 Kuna Kitu Umesema First name na Middle name Na ulianzana namba
Shahidi: 0719933386 ni namba ya Tigo
Shahidi: First name Freeman, Middle name Aikael, Last name Mbowe
Wakili wa Serikali: Maana yake
Shahidi (Tigo): namba inamilikiwa na Mtu anaitwa Freeman Aikael Mbowe
Wakili wa Serikali: chini ni nini
Shahidi (Tigo): Tarehe ya kuzaliwa
Wakili wa Serikali: ID proof Maana yake nini?
Shahidi (Tigo): Kitambulisho kilichotumika Kusajilia namba
WS: Mwenye namba hii alisajili kwa alama za Vidole tarehe ngapi?
Shahidi (Tigo): 16.9.2019
Wakili wa Serikali: hizi Null Null Null fafanua kidogo
Shahidi (Tigo): System haipati Taarifa za Usajili wa wakati Ule wa zamani
Kwa CCM inawezekanaAyaaaaa mkuu ahsante kwa umakini 😂😂😂😂😂😂
Sasa hapa elements za ugaidi zipo wapi jamani???? Yaani mtu kuntumia mwenzie pesa ni ugaidi????Tunaleta kama zilivyo kutoka mahakamani .