Kibatala: Kwa hiyo wewe ulimruhusu Bwire Waendelee na Mipango yao, Mipango ipi
Shahidi: Waendelee na Mipango yao ya Kumdhuru Sabaya, Kama Wakiweza
Kibatala: kwa hiyo Baada ya Kumdhuru Sabaya Walitakiwa Kuriport Kwako tena
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Kwa hiyo Wewe Luteni Wa Jeshi la Wananchi Tanzania, uliwaruhusu Kwamba wakatekeleze Mpango wa Kumdhuru Sabaya Kwa sababu wapo Ground?
Shahidi: Ningefanyaje sasa na Watu wapo Ground
Kibatala: Kwani Wakati huo walikuwa weshamdhuru au Bado
Shahidi: Walikuwa Bado, Ndiyo Wapo Kwenye Mpango
Kibatala: Je Baada ya Bwire Ku Confess Kwako, Ulimwambia Afande Kingai
Shahidi: Sikumwambia