WanaJF
Karibuni kufuatilia mapokezi makubwa ya Mgombea Urais CHADEMA Tundu Lissu hapa mjini Shinyanga.
Lissu anatarajiwa kuhutubia mkutano Mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Joshoni ikiwa ni uzinduzi wa kampeni kwa Kanda ya Serengeti.
Mgombea huyo wa Urais anaambatana na Mgombea Mwenza Salum Mwalimu na Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe
Sisi wa Molemo Media tumesafiri usiku kucha kutokea Mwanza na tupo hapa Shinyanga kuihabarisha dunia.
View attachment 1556310
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu ameingia Kanda ya Serengeti (Mara, Shinyanga & Simiyu) ambapo leo atakuwepo Shinyanga Mjini akiambatana na Mgombea-mwenza, Salum Mwalim pamoja na Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe