WanaJF
Karibuni kufuatilia mapokezi makubwa ya Mgombea Urais CHADEMA Tundu Lissu hapa mjini Shinyanga.
Lissu anatarajiwa kuhutubia mkutano Mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Joshoni ikiwa ni uzinduzi wa kampeni kwa Kanda ya Serengeti.
Mgombea huyo wa Urais anaambatana na Mgombea Mwenza Salum Mwalimu na Mwenyekiti wa Taifa Freeman Mbowe
Sisi wa Molemo Media tumesafiri usiku kucha kutokea Mwanza na tupo hapa Shinyanga kuihabarisha dunia.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CHADEMA, Tundu Lissu ameingia Kanda ya Serengeti (Mara, Shinyanga & Simiyu) ambapo leo atakuwepo Shinyanga Mjini akiambatana na Mgombea-mwenza, Salum Mwalim pamoja na Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe
Picha zikionesha msafara wa Mgombea Urais wa JMT kwa Tiketi ya Chadema, Mhe. Tundu Lissu tangu alipotua Uwanja wa Ndege wa Kahama leo asubuhi. Kisha kuanza safari ya kuelekea Shinyanga mjini ambapo alilazimika kusimama mara kadhaa sehemu mbalimbali kuwasalimia mamia ya wananchi waliosimama barabarani kuzuia msafara wakiomba awahutubie.
=========
Mnyika: Naomba mjiandae kwa sababu safari hii wamedhamiria kudhibiti mawakala wetu wasiingie vituoni, nyinyi wananchi kwa nguvu ya umma kabla ya kupiga kura awepo ndani ya kituo cha kupigia kura.
Wamejiandaa safari hii, ni hiari kumpa nakala ya matokeo ya uchaguzi wakala wa CHADEMA kwenye kituo cha kupigia kura, nawaambia mapema ili nyinyi wananchi muungane na sisi kwa pamoja katika ulinzi wa kura zetu kuhakikisha kila kituo cha kupigia kura tunapata nakala ya matokeo iliyoonesha Lissu ameshinda na inabandikwa kituoni..
Nimeshangazwa huyu Rais dikteta, Rais anayejiita mbabe, anayejiita jiwe eti leo anawawekea mabango Magufuli ni mtu mnyenyekevu kwelikweli, sasa basi.
Mbowe: Leo tunazungumza baada ya miaka mitano ya kufungwa midomo, mtakumbuka CHADEMA tulikuwa tunakuja Shinyanga mara kwa mara lakini leo tunaenda kucheza mchezo baada ya kukaa miaka mitano bila mazoezi, alafu alietufungia kwa miaka matano naye atakuja kesho, atabeba watu kutoka mikoa mbalimbali kwa matrekta, punda, malori
Hakuna kitu kibaya kama mtu kukunyima uhuru wako, miaka mitano tunashindwa kuzungumza. Unapiga marufu mikutano ya vyama vingine shindani, unaruhusu mikutano ya watu wako. Hii si haki na lazima tuoneshe hasira tarehe 28/10 siku ya kupiga kura.
Tumeona miaka matano ya udikteta katika nchi yetu kwamba kiongozi mkubwa ambae ni Rais anataka kuzungumza peke yake. Amefunga vyombo vyote vya habari vimsifie yeye. Vyo mbo sio vyake, sio vya ukoo wake, ni vyombo vya umma vinavyoendeshwa kwa kodi za watanzania.
Rais wetu anaendesha hii nchi kama ya ukoo wake, hii nchi inaendeshwa kwa katiba na inastahili kuheshimu katiba. Hata Raisi wetu tnaomba mumchague tarehe 28, tunategemea ataiongoza kwa misingi ya katiba na sheria.
View attachment 1556422View attachment 1556423View attachment 1556431