Yaliyotokea Kariakoo ni ukumbusho kuwa Amani hulevya Ujinga

Yaliyotokea Kariakoo ni ukumbusho kuwa Amani hulevya Ujinga

Tanzania Tatizo hawataki Kuambiwa Ukweli ila hakuna Haja ya Jeshi la Zimamoto maana Halina Linachofanya mpaka Sasa hivi..

Halina Vifaa wala halina Nyendo za Kufanya kazi zaidi ya Maji na Vigali vyao vyekundu..

Ila Mimi Naona Walihalalishe Jeshi la Kujenga Taifa Liwe Jeshi rasmi...Waliondoe Kwenye Militia ili ndo Liwe Jeshi la Uokoaji..
Na Lipewe bajeti ya Kutosha
Imagine kila goli wanalofunga yanga na simba Rais alikuwa anatoa million 5, pesa zote tulizochea kule zingenunua hata gari moja la uokoaji
 
Kukaa sana kwa amani tunalewa sio polisi, uhamiaji, JW au wapi tuko vizuri. Tatizo ni kukaa na imani kwamba jeshi ni kwa ajili ya vita tu, zana (sio silaha) za kijeshi zina dual use ukiwa nazo zitatumika sana kwa civilians kuliko mara moja kwa miaka kadhaa usubiri vita.

Jana nimeona mabasi ya JWTZ yamejaza wanajeshi wakashuka mikono mitupu, sanasana walichosaidia ni kusogeza watu pembeni ili magari ya wagonjwa na viongozi wapite. Jambo ambalo mgambo anaweza.

Nchi zenye majeshi yenye bajeti, zilizokaa chonjo unakuta military ina search and rescue helicopters kadhaa za nchi kavu na majini, ikitokea mafuriko au meli kuzama wanajeshi wanawahi. Kule Bukoba ajari ya ndege tungeona Navy wanatumia ujuzi wao kama wangekuwa na small base Bukoba au Mwanza, badala yake wavaa yeboyebo kina Majaliwa ndio walionekana.
Hizohizo helicopters zinatumika kuzima moto mkubwa ukiwaka mjini, au milimani kama Kilimanjaro kule moto huwaka mara nyingi.

Hapa kwenye hili jengo tungeona Engineering Brigade ambayo imefundishwa vitu kama kutengeneza airstrip ya haraka wakati wa vita, kurekebisha barabara na madaraja kama Bailey bridge, kuwa na floating piers kusafirisha mizigo ya dharura kwenye mito, kujenga base kwa haraka, kufanya demolition au kuokoa kama strategic factories, buildings zimeharibiwa na adui.

Ingekuwa hivyo tungeona jeshi wanafika na zana zao wanafanya kazi kwa haraka na kwa ufanisi zaidi maana discipline ya kuwa haraka wanakuwa nayo, mafunzo ya gharama kubwa wanayo, vifaa vya uwezo zaidi wanavyo.
Sasa bongo bajeti kama hiyo haitengwi.
Tofautisha uokozi we eneo la vita na uokozi kwenye domestic settings.
Gaza walianza kuwa effective baada ya matukio mangapi??
Ni mashirika mangapi ya kimataifa yapo kwa kazi hiyo??
Unakumbuka Ilichukua siku ngapi kumtoa Yesser Arrafat chini ya kifusi??
 
Hivi makomandoo wetu hawaezi kupenya penya kama miners taratibu kwa kutambaa na vifaa vidogo vidogo kama vya wachimbaji wadogo wadogo wa madini..... Taratibu sana kupenya kama nyoka.....
Sijui lakini... Nawaza TU. SI kwa ubaya
😅 😅

Hao wadau ndio mmoja wao alitumwa akabaka binti
 
Ina maana tusiwe na jeshi la akiba?...

Ni vyema hili jeshi la zimamoto na uokoaji liboreshwe zaidi...(Vifaa )
Hili Jeshi la Zimamoto halifai Wengi ni waoga Sana kufanya Uokoaji Wamezoea Luxury sana..

Unaposema kusiwe na Jeshi la akiba unamaanisha nini?

JKT sio Jeshi la Akiba..
Jeshi la Akiba Ni Mgambo na Mgambo wanaruhusiwa
 
Tofautisha uokozi we eneo la vita na uokozi kwenye domestic settings.
Gaza walianza kuwa effective baada ya matukio mangapi??
Ni mashirika mangapi ya kimataifa yapo kwa kazi hiyo??
Unakumbuka Ilichukua siku ngapi kumtoa Yesser Arrafat chini ya kifusi??
Hoja ya msingi hapa ni maandalizi yetu katika majanga na allocation of resources.
 
Hili Jeshi la Zimamoto halifai Wengi ni waoga Sana kufanya Uokoaji Wamezoea Luxury sana..

Unaposema kusiwe na Jeshi la akiba unamaanisha nini?

JKT sio Jeshi la Akiba..
Jeshi la Akiba Ni Mgambo na Mgambo wanaruhusiwa
Jeshi la zimamoto lipo vizuri tu kwenye uokoaji tatizo ni vifaa tu.
 
😅 😅

Hao wadau ndio mmoja wao alitumwa akabaka binti
Dah. Inasikitisha sana. Maana mahali kama hapa ndio pa kuonyesha weledi.
Kuna mwamba namuona huko mitandaoni Jana kapenyapenya katoa watano. Kuamkia Leo saa sita ya usiku ameenda huko mpaka alfajiri katoa wengine watatu. Na ni msela TU wa huko mtaani, ,,Sasa unaona!!!!
 
Vile vifaa vina gharama mkuu
Vifaa Vyote Nchi nzima Havidi Trilion 3..
Kwa supply ya Kila Mkoa..
Ukiangalia Goli la Mama, Malipo Mechi za K.O za Ngumi na Pesa Nyingi zinazotumika Kwenye Vitu visivyo vya Msingi...

Juzi Juzi bunge linaidhinisha Manunuzi ya ndege Nyingine ya Viongozi inayocost Bilions of Money..
Bajeti ya Mwaka huu inakaribia trilion 40 kwanini Tusitumia trilion 3 Kuboresha Jeshi linaloweza Kuokoa Maisha?
 
Hivi makomandoo wetu hawaezi kupenya penya kama miners taratibu kwa kutambaa na vifaa vidogo vidogo kama vya wachimbaji wadogo wadogo wa madini..... Taratibu sana kupenya kama nyoka.....
Sijui lakini... Nawaza TU. SI kwa ubaya
Unaonaje ungeenda kupenya wewe mkuu...
Si kwa ubaya lakin
 
Vile vifaa vina gharama mkuu
nimejaribu kugoogle vifaa used

Hao mawaziri walioenda hapo kila mmoja gari lake ni angalau mara 10 ya Caterpillar moja hapa.

Tanzania hadi Kesho tumeshindwa kukubaliana dhidi ya wabunge 19 ambao mishahara yao ingetumika sehemu husika tusinge poteza baadhi ya watu jana
Screenshot 2024-11-17 125309.png
 
Mimi ni mshabiki namba moja wa Israel, ila nimeguswa na tukio la kuanguka kwa Jengo Kariakoo, Jitihada tuliyoweka katika uokozi ni aibu kwetu hasa sisi Watanzania tunaomini sio Nyani.

Gaza kwao kuanguka kwa majengo ni kila siku tena kwa mabomu na sio uzembe, lakini Watu wake na mifumo yao ya uokozi imepunguza Idadi ya vifo hadi 40, 000 pekee, Kama sisi Jengo moja tumetumia siku 2 na bado hatujamaliza, basi kwenye Majanga makubwa ya Vita au asili tunaweza kupoteza watu zaidi ya laki moja kwa wiki,

Ifike hatua tuiwajibishe serikali ya CCM kwa kuiweka pembeni tuanze upya, ni aibu kuona viongozi wa Serikali wanaenda eneo la maafa na magari ya zaidi ya billioni 3 alafu wanashindwa kuwa na vifaa vya uokozi visivyozidi billion 1.
Yaani hilo balaa kama la Gaza kwetu tuombe lituepuke kwa sababu ikitokea jengo limepigwa bomu basi nyie mliofukiwa mjihesabu mmekufa hamtomuona mtu kuja kushughulika na nyie.
Hapa kwetu tukivamiwa na adui ndani ya saa 24 adui keshajichukulia nchi kiubwete kabisa tulivyokuwa waoga wa kufa utafikiri tutaishi milele ndiyo maana hata hawa vibwengo wanatutesa watakavyo kwa sababu wanajua Wabongo ni waoga sana.
 
Hapana Hilo Nitakupinga Mkuu..

Kuna Wakati tu tuseme Ukweli..
Kwenye matukio makubwa Jeshi la zimamoto mara zote husaidiwa na JWTZ na JKT sasa kwanini Tusirasimishe Uokoaji uwe Chinu ya Idara ya JWTZ kupitia Idara ya Jeshi ya JKT
Hili jeshi la zimamoto na uokoaji linahitaji maboresho tu mkuu hasa kwenye vifaa sio wabaya kiasi unachodhani.....huko kusaidiwa na majeshi mengine sio jambo baya ni kuongeza nguvu tu.

Hao zimamoto ndio wanapaswa kuwa mstari wa mbele kwenye uokoaji tatizo vifaa vya kutosha hawana isitoshe wanahitaji bajeti ya kutosha.
 
Unaonaje ungeenda kupenya wewe mkuu...
Si kwa ubaya lakin
Hii SI ligi Mangi. Embu kuweni na akili.... Hata kama wazo langu ni ujinga lakini angalau nimefikiria....
Kwani masharti ya kujiunga na hicho chama ni ubongo wako uutupe au..... Huwa siwaelewi.
 
Jeshi la Netflix ( Zimamoto ) halina maana kabisa Mana kwenye Moto maji hawana kwenye vifusi wanakuja Kama vibodi warriors.....Hawaeleweki.
 
Back
Top Bottom