Yanayoendelea ndani ya uongozi wa CCM na serikali yanatafakarisha

Yanayoendelea ndani ya uongozi wa CCM na serikali yanatafakarisha

Kuna siasa za majibizano zinaendelea ndani ya uongozi wa juu kabisa wa CCM na serikali kuu. Mheshimiwa Nchimbi haonekani kufurahishwa na hulka za kikazi za RC wa Arusha na hakai na kitu moyoni mwake, anaweka wazi kabisa kutofurahishwa na kauli pamoja na tabia za Paul Makonda.

Wakati Makonda akifanya kazi nzuri mkoa wa Dar Mheshimiwa Nchimbi alikuwa nje ya nchi akifanya shughuli za ubalozi, Samia alikuwa msaidizi wa moja kwa moja hayati JPM hivyo anamfahamu vyema Makonda.

Naamini Samia anawavuta vijana wa hayati JPM karibu yake wakiwa na uwezo wa kujilipua na hawana aibu kabisa wakiwa kazini. Ni utamaduni mpya wa hayati ambao kwa serikali ya Samia ni wa kawaida kabisa.

Hata kutolewa kwake nafasi ya uenezi ni kwa shinikisho la wakubwa ndani ya CCM wakongwe hawaonekani kufurahishwa na hulka za vijana wa kisasa kina Makonda na wenzake wote wa rika lake na Nchimbi anawakilisha siasa za umri fulani wenye kuheshimu busara na hekima kabla ya kutoa hotuba na baada ya hapo.

Kitendo cha Rais Samia kufurahia namna Makonda alivyokipeleka mchakamchaka chama katika kipindi cha muda mfupi ni ushahidi wa uwepo wa sintofahamu ya chini kwa chini katika uongozi wa juu wa serikali na CCM.

Nchimbi akiwa katibu mkuu wa CCM anapopingana katika hotuba na bosi wake Samia juu ya hulka za kikazi za Makonda sio suala lenye afya nzuri ya kisiasa kwa maana ya muelekeo mzima wa serikali. Nchimbi hana la kufanya vinginevyo Makonda angeondolewa kabisa kutoka kwenye serikali na kurudi mtaani.

Na mpaka muda huu Mzee Kikwete bado ana nguvu ndani ya serikali na anaonekana ni mtu mwenye kupenda sana kuwa karibu na kila kinachoendelea, kule kuombwa kushauri na kutumwa kwenye mikutano mikubwa huko ughaibuni ni ushahidi wa kuhitajika kama mshauri wa masuala nyeti na yenye kuhitaji uzoefu.

Anatumia huko kuhitajika kwake kama tiketi ya kuingiza ushauri wake katika shughuli za kila siku, ni hapa tunapoona namna ambavyo Rais aliyepo madarakani anavyokwazwa na mstaafu anayekuwa nje ya ofisi. Sioni namna yoyote ambayo Nchimbi anakuwa na uhuru wa kufanya kazi pasipo maamuzi yake kutokuwa na chembechembe za hisia za Jakaya Kikwete.

Maamuzi ni yake kumhusu Makonda, Sabaya na Biteko ambao ni masalia halisi ya Bosi wake wa zamani hayati JPM, aendelee kuwa karibu nao kikazi akiwa anaujua uwezo wao au aachane nao kwani Mstaafu Kikwete na kund lake kubwa hawapendi hulka zao za kikazi.

Kinachofikirisha ni ukweli kwamba Kikwete akiwa Rais hakuingiliwa kwa namna yoyote ile na Hayati Mkapa, haonekani kuondoka kabisa kwenye duru za kisiasa akihitajika kwa uzoefu wa ushauri wake na wakati huo huo akiwa na hulka ya kupenda kuhusika kwenye mengi zaidi ya ustaafu wake.


Si mkajadiliane huko haya mambo yenu ya familia?
 
Ukiona hivyo ujue bado hujaelewa dhima ya mchora katuni.
Dhima ya mchora katuni imeishia kwenye Ccm/Chadema na mgao wa sahani za ubwabwa kwa wapiga kura.
Lakini nyumba na ghorofa za nyasi tupu hata wewe ulikuwa haujazitafakari.
 
Leo hii ukimuweka hapa Nchimbi na Makonda ktk sanduku la kura na uwaache wapige kampeni, Makonda atashinda mchana kweupe. Ninyi na akina Nchimbi msichokielewa ni kuwa Tanzania ya sasa siyo ile ya miaka ya tisoni! Na kumbuka, Dkt Magufuli alitembea kila sehemu ya hii nchi wakiwa na Dkt Samia.

Dkt Magufuli alikuwa sikio la kila mtanzania kila pahala alipotembelea na Dkt Samia alipendwa sana na watanzania baada ya msiba ila yeye ndiye aliyeharibu kwa kujionesha kiasi kwamba leo hii ukienda vijijini wanajua yeye ndiye aliyehusika na kifo na hilo mtu pekee aliyeanza kufuta hayo mawazo alikuwa Makonda.

Kibaya ya manchojidanganya nikudhani kura zinapigwa na watu wa mjini, hahaha hapana. Sisi wa mwenye mitandao siyo wapiga kura na mtu kama Mange na kundi lake siyo wapiga kura kabisa. Na ukitaka kujua Makonda anapendwa tizama alivyokuwa anajaza watu na wanamlilia.

Dkt Nchimbi na kundi lake ni kama sikio la kufa, maana wangeusoma mchezo walipaswa kuona namna nzuri ya kuendelea kumtumia Makonda CCM Kujisafisha na kuondokana na dhana potofu inayoendelea mtaani ya CCM kumuua Dkt Magufuli ili ufisadi uendelee.
Wewe ndiye mdau Jf unayeielewa vizuri hali halisi ya Tz na raia wake ilivyo.

Kama ulivyokwisha kusema 'kupendwa' huonekana kwa mwitikio wa raia, hizo zingine ni ngonjera, chuki zao, kununuliwa au kampeni chafu.

Kiuhalisia Makonda ni kiongozi mzuri na mwenye uwezo wa kutatua changamoto na ni mtu anayekubalika sana, hilo wakubali ama wakatae lakini ukweli unabaki pale pale.
 
Hakuna tatizo la Kikwete au Makonda.
Hayo 'mapungufu ya Samia kama anavyoyasema Mange Kimambi yamesababishwa vipi na Kikwete?
Kuhusu Makonda ameshawekwa pembeni,lakini inamchukua muda mrefu kuelewa yeye basi tena.
Yeye ahangaike na Wameru,basi.
Na huyu Mange Kimambi amefanya analysis nzuri ya matatizo ya nchi. Nadhani amewafurahisha sana washauri wa rais .
"Ametukana" lakini picha ya rais ni nzuri.
Kikwete ni tatizo linawazidi uwezo wa kulitatua kwa sasa, ni tatizo linalochanganyika na suluhisho la matatizo ya kiuongozi ya juu kabisa.

Anategemewa na anajua kuwa anategemewa hivyo anayo nguvu ya kufanya kazi nyingi nyuma ya Rais Samia, kwa ufupi ushawishi wake haukwepeki, tunaishi kwa kutegemea fadhila zake na hilo kwa muda mrefu ujao ni suala baya kwa mustakabali mzima wa Tanzania.
 
Ni vizuri sana anavyofanya Nchimbi kumpinga Makonda kwani huyu bwana akili zake ni mbovu kabisa na wote wananwona anafaa akili zao pia ni mbovu kabisa.
Anajirekodi akisikiliza taarabu ya kumpamba Samia, huwezi kumuona mkuu wa mkoa yoyote akifanya ujinga wa namna hiyo.

Ni masuala ya kitoto na inaonekana anamjua boss wake vizuri na anafanya hivyo akijua muitikio wake utakuwa vipi kuhusu hiyo video.
 
Mtakuja kutuambia. Hii Secretariat ya Nchimbi ni mbovu kuwahi kutokea. Ni zaidi ya ile ya Wilson Mkama. Picha linaanza wanafanya kazi na kutoa hotuba kama vile ni watumishi wa umma(civil servants). Wamegeuka wasemaji wa maafisa masuhuli na Mawaziri katika maeneo tofauti tofauti. Nadhani hili limechangiwa pia name ukweli kwamba wengi wao wamezoea kuwa watendaji katika maeneo kadha waliopita.
Makonda ndiye anajua na alijua kutafsiri maana halisi ya chama cha siasa, chama tawala na maana ya chama kuunda serikali.

Chama tawala hakipaswi kujiunga katika mlolongo wa Government Bureaucratic system but it should commands the system. Nchimbi and Co. ndio kwanza wameanza ziara ya kwanza lkn kwa jicho la tatu, wanafanya kazi kama bureaucrats wa serikali.

Wanashindwa kutafsiri majukumu yao kwa niaba ya chama. Wanashindwa kutafsiri supremacy ya chama over the govt system. Wanashindwa kukaa upande wa Wananchi ama kuvaa viatu vya wananchi. Wasipobadilika, itakuja kuwa Secretariat Mbovu kuwahi kutokea ndani ya chama cha mapinduzi.
Kuongea kwa niaba ya wananchi sio hulka ya CCM hii yenye ushawishi wa JK, hata kidogo hawana sifa ya aina hiyo.

JPM alipendwa na kuaminiwa kwa sababu alijua kujiweka karibu na mwananchi wa kawaida kwa vitendo, hakuonyesha kutawaliwa na kuitukuza mali ya dunia hii ambayo anakufa na kuiacha. Aliifahamu hekima ya kiuongozi na akajitahidi kuiishi japo ubinadamu ulimzidi nguvu.

JK na Samia wana hulka ya kuiabudu dunia na anasa zake ambayo ina msingi wa tamaduni za kwao za asili yaani wamelelewa hivyo tangu utotoni. Hawana uwezo wa kuzitumikia mali na wakati huo huo wakamtumikia Mungu {kwa maana ya kuwa mtumishi wa watu}.
 
Wewe ndiye mdau Jf unayeielewa vizuri hali halisi ya Tz na raia wake ilivyo.

Kama ulivyokwisha kusema 'kupendwa' huonekana kwa mwitikio wa raia, hizo zingine ni ngonjera, chuki zao, kununuliwa au kampeni chafu.

Kiuhalisia Makonda ni kiongozi mzuri na mwenye uwezo wa kutatua changamoto na ni mtu anayekubalika sana, hilo wakubali ama wakatae lakini ukweli unabaki pale pale.
Kabisa mkuu, ni kama ilivyokuwa 2015, bila Dkt Magufuli CCM tulikuwa tumepoteza uchaguzi tena bila chenga maana kila mpiga kura aliamini ni Dkt Magufuli pekee anaweza kuivusha CCM. Same kwa Makonda tangu alipoteuliwa uenezi alionesha matumaini kwa wapiga kura tena kwa mwitikio ambao hata Dkt Samia Mwenyekiti wetu hawezi kumfikia, ilikuwa salama ya CCM kuhakikisha Makonda wanamtumia kukihuisha Chama. Ila kwa sasa nakuhakikishia CCM bila watu kama akina Makonda haibebeki, maana wapiga kura kule vijijini wanaamini CCM hao hao baadhi ya viongozi wa juu walimuua Dkt Magufuli ili waibe, na kuuza rasilimali za nchi. Na moto wa akina Mbowe na kampeni zao siyo za kudharau wananchi wanaelewa kabisa. Sijui kama CCM itapata mwenye akili ya kujua kesho yake 2025. Na kibaya zaidi tena kibaya zaidi ni kundi kubwa la Dkt Magufuli kupitia wabunge aliowaweka bungeni kwa mkono wake na lile kundi alilolikata Dkt Magufuli kwa mkono wake wa chuma, hayo ni makundi nayaita Dynamics “ukilizingua kundi mojawapo” linahamia chadema na kila kundi lina ajenda ya udhaifu wa serikali ya Dkt Samia na dhihaka dhidi ya mpendwa wao Dkt Magufuli, kwa hiyo 2025 tutegemee chochote kutokea. Mtu pekee anayeweza kuivusha CCM ni Paul Makonda tena akiwa kama Katibu Mkuu wa CCM chama kinaweza kuvuka kwa sababu Dkt Nchimbi hana ushawishi kwa wapiga kura, yes anaweza kuwa na ushawishi ndani ya CCM na mfumo ila hana ushawishi kwa masikini. Na akitaka kujilinganisha na Dkt Kikwete atakosea, kikwete 2005 na alikuwa na popularity ya ajabu yaani watu walimpenda bila hata kuongea, ila baada ya Kikwete kushidwa kuzuia wizi alichukiwa mpaka leo na wapiga kura wa leo wanataka kiongozi anayekemea wizi, anawajibisha na analinda maslahi wa walio wengi kwa kuhakikisha wachache pia maslahi yao yanakuwa second priority.
 
Kuna siasa za majibizano zinaendelea ndani ya uongozi wa juu kabisa wa CCM na serikali kuu. Mheshimiwa Nchimbi haonekani kufurahishwa na hulka za kikazi za RC wa Arusha na hakai na kitu moyoni mwake, anaweka wazi kabisa kutofurahishwa na kauli pamoja na tabia za Paul Makonda.

Wakati Makonda akifanya kazi nzuri mkoa wa Dar Mheshimiwa Nchimbi alikuwa nje ya nchi akifanya shughuli za ubalozi, Samia alikuwa msaidizi wa moja kwa moja hayati JPM hivyo anamfahamu vyema Makonda.

Naamini Samia anawavuta vijana wa hayati JPM karibu yake wakiwa na uwezo wa kujilipua na hawana aibu kabisa wakiwa kazini. Ni utamaduni mpya wa hayati ambao kwa serikali ya Samia ni wa kawaida kabisa.

Hata kutolewa kwake nafasi ya uenezi ni kwa shinikisho la wakubwa ndani ya CCM wakongwe hawaonekani kufurahishwa na hulka za vijana wa kisasa kina Makonda na wenzake wote wa rika lake na Nchimbi anawakilisha siasa za umri fulani wenye kuheshimu busara na hekima kabla ya kutoa hotuba na baada ya hapo.

Kitendo cha Rais Samia kufurahia namna Makonda alivyokipeleka mchakamchaka chama katika kipindi cha muda mfupi ni ushahidi wa uwepo wa sintofahamu ya chini kwa chini katika uongozi wa juu wa serikali na CCM.

Nchimbi akiwa katibu mkuu wa CCM anapopingana katika hotuba na bosi wake Samia juu ya hulka za kikazi za Makonda sio suala lenye afya nzuri ya kisiasa kwa maana ya muelekeo mzima wa serikali. Nchimbi hana la kufanya vinginevyo Makonda angeondolewa kabisa kutoka kwenye serikali na kurudi mtaani.

Na mpaka muda huu Mzee Kikwete bado ana nguvu ndani ya serikali na anaonekana ni mtu mwenye kupenda sana kuwa karibu na kila kinachoendelea, kule kuombwa kushauri na kutumwa kwenye mikutano mikubwa huko ughaibuni ni ushahidi wa kuhitajika kama mshauri wa masuala nyeti na yenye kuhitaji uzoefu.

Anatumia huko kuhitajika kwake kama tiketi ya kuingiza ushauri wake katika shughuli za kila siku, ni hapa tunapoona namna ambavyo Rais aliyepo madarakani anavyokwazwa na mstaafu anayekuwa nje ya ofisi. Sioni namna yoyote ambayo Nchimbi anakuwa na uhuru wa kufanya kazi pasipo maamuzi yake kutokuwa na chembechembe za hisia za Jakaya Kikwete.

Maamuzi ni yake kumhusu Makonda, Sabaya na Biteko ambao ni masalia halisi ya Bosi wake wa zamani hayati JPM, aendelee kuwa karibu nao kikazi akiwa anaujua uwezo wao au aachane nao kwani Mstaafu Kikwete na kund lake kubwa hawapendi hulka zao za kikazi.

Kinachofikirisha ni ukweli kwamba Kikwete akiwa Rais hakuingiliwa kwa namna yoyote ile na Hayati Mkapa, haonekani kuondoka kabisa kwenye duru za kisiasa akihitajika kwa uzoefu wa ushauri wake na wakati huo huo akiwa na hulka ya kupenda kuhusika kwenye mengi zaidi ya ustaafu wake.
Mkiwa na Rais mwanamke wa nchi kama ya Tanganyika yenye taasisi kama Bunge, mahakama, TISS, PCCB, AG nk dhaifu katika kusimamia utendaji wa serikali mnategemea nini?

Ni lazima mambo yawe hovyo tu kwa sababu pembeni mwa mwanamke huyu lazima atakuwepo mshauri au kundi la washauri wanaume waovu kadhaa kumshauri na kumwelekeza kusimamia mambo vile watakavyo wao kwa manufaa yao na sio ya nchi...

Lakini inakuwa ni hatari zaidi mambo hayo anayoshauriwa yanapokuwa yanaihusu nchi na ustawi wa wananchi...

Kwa hiyo shida hapa ni "Rais Mwanamke" na sio kitu kingine chochote..

Hao kina Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli hawakuwategemea wala ku - rely kwenye ushauri wa watangulizi wao ktk kufanya maamuzi kuhusu nchi kwa sababu walikuwa ni wanaume - free & independent men...

Bila shaka mmenielewa japo kuna baadhi wanaweza kudhani siwapendi wanawake au nadharau uwezo wao. Ukweli ni kuwa Nawapenda sana wanawake, siwadharau wanawake lakini ukweli ni kuwa hakuna mwanamke wa kuweza kubeba jukumu la uongozi mkuu wa nchi hususani ya kwetu Tanganyika.!!
 
Kabisa mkuu, ni kama ilivyokuwa 2015, bila Dkt Magufuli CCM tulikuwa tumepoteza uchaguzi tena bila chenga maana kila mpiga kura aliamini ni Dkt Magufuli pekee anaweza kuivusha CCM. Same kwa Makonda tangu alipoteuliwa uenezi alionesha matumaini kwa wapiga kura tena kwa mwitikio ambao hata Dkt Samia Mwenyekiti wetu hawezi kumfikia, ilikuwa salama ya CCM kuhakikisha Makonda wanamtumia kukihuisha Chama. Ila kwa sasa nakuhakikishia CCM bila watu kama akina Makonda haibebeki, maana wapiga kura kule vijijini wanaamini CCM hao hao baadhi ya viongozi wa juu walimuua Dkt Magufuli ili waibe, na kuuza rasilimali za nchi. Na moto wa akina Mbowe na kampeni zao siyo za kudharau wananchi wanaelewa kabisa. Sijui kama CCM itapata mwenye akili ya kujua kesho yake 2025. Na kibaya zaidi tena kibaya zaidi ni kundi kubwa la Dkt Magufuli kupitia wabunge aliowaweka bungeni kwa mkono wake na lile kundi alilolikata Dkt Magufuli kwa mkono wake wa chuma, hayo ni makundi nayaita Dynamics “ukilizingua kundi mojawapo” linahamia chadema na kila kundi lina ajenda ya udhaifu wa serikali ya Dkt Samia na dhihaka dhidi ya mpendwa wao Dkt Magufuli, kwa hiyo 2025 tutegemee chochote kutokea. Mtu pekee anayeweza kuivusha CCM ni Paul Makonda tena akiwa kama Katibu Mkuu wa CCM chama kinaweza kuvuka kwa sababu Dkt Nchimbi hana ushawishi kwa wapiga kura, yes anaweza kuwa na ushawishi ndani ya CCM na mfumo ila hana ushawishi kwa masikini. Na akitaka kujilinganisha na Dkt Kikwete atakosea, kikwete 2005 na alikuwa na popularity ya ajabu yaani watu walimpenda bila hata kuongea, ila baada ya Kikwete kushidwa kuzuia wizi alichukiwa mpaka leo na wapiga kura wa leo wanataka kiongozi anayekemea wizi, anawajibisha na analinda maslahi wa walio wengi kwa kuhakikisha wachache pia maslahi yao yanakuwa second priority.
Uliyoongea ni madini matupu umetema.

Ninaona Samia anayumbishwa na kakikundi ama mtu fulani, hatawali kufuata falsafa zake na utashi wake.
.
Kila nikiigeuza geuza orodha ya ninaowajua walioko juu huko, ninashindwa kumhisi mchawi kwa kuona kila sura hapo Samia anaimudu kwa kuifanya lolote apendavyo.

Ukija na uchawa wao, kila mtu kuanzia Pm ni kusifia na kuabudu, ndiyo hapo ninavurugwa napotezwa.

Kwa utata na mkoroganyo huu, ndiyo maana watu wanamhisi Jk kuendelea kututawala kwa remote control.

Haiwezekani mtu kakiheshimisha chama kwa muda mfupi na matokeo ya raia kukikubali chama halafu aondolewe ghafla!

Hako kakikundi ama ni mtu basi ana nguvu sana kuliko Samia mwenyewe kwenye maamuzi nchi hii.
 
Mkiwa na Rais mwanamke wa nchi kama ya Tanganyika yenye taasisi kama Bunge, mahakama, TISS, PCCB, AG nk dhaifu katika kusimamia utendaji wa serikali mnategemea nini?

Ni lazima mambo yawe hovyo tu kwa sababu pembeni mwa mwanamke huyu lazima atakuwepo mshauri au kundi la washauri wanaume waovu kadhaa kumshauri na kumwelekeza kusimamia mambo vile watakavyo wao kwa manufaa yao na sio ya nchi...

Lakini inakuwa ni hatari zaidi mambo hayo anayoshauriwa yanapokuwa yanaihusu nchi na ustawi wa wananchi...

Kwa hiyo shida hapa ni "Rais Mwanamke" na sio kitu kingine chochote..

Hao kina Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli hawakuwategemea wala ku - rely kwenye ushauri wa watangulizi wao ktk kufanya maamuzi kuhusu nchi kwa sababu walikuwa ni wanaume - free & independent men...

Bila shaka mmenielewa japo kuna baadhi wanaweza kudhani siwapendi wanawake au nadharau uwezo wao. Ukweli ni kuwa Nawapenda sana wanawake, siwadharau wanawake lakini ukweli ni kuwa hakuna mwanamke wa kuweza kubeba jukumu la uongozi mkuu wa nchi hususani ya kwetu Tanganyika.!!
Huyo mwanamke angekuwa mpaka leo hii ni makamu iwapo Magufuli angekuwa anaishi mpaka dakika hii, tukumbuke ni mpango wa Mungu. Kwa matakwa yetu ya kibinadamu Magufuli angeachia madaraka mwaka 2025.

Hivyo tusiegemee kwenye hoja ya uanamke wa Samia, waliopendekeza jina lake ni binadamu kama mimi na wewe na hawakuona kwa namna yoyote ile kuwa mwisho wa JPM ungekuwa ni March 17 2021.

Huyo huyo mwanamke amekuwa na bahati mbaya ya kuletwa huku bara na kupewa cheo na JK, kwake JK ni sawa na kiongozi anayeendelea kuwa hai miaka na miaka, hawezi kuusahau mchango wa JK katika uongozi wake hata akija kustaafu.

Tatizo ni mipango ya Mungu namna inavyofanya kazi, alitaka mpaka muda huu wastaafu wote isipokuwa JK wawe wameshatangulia mbele ya haki, tatizo lipo kwa hiyo JK namna asivyoonekana kujali wala kuguswa na vilio vya watu huku mtaani.

Ana unafiki kwa kumuangalia tu akiwa anaongea majukwaani. Hajali na haonyeshi kabisa kujali n mtu yupo kwa ajili ya tabaka fulani la juu.
 
Kabisa mkuu, ni kama ilivyokuwa 2015, bila Dkt Magufuli CCM tulikuwa tumepoteza uchaguzi tena bila chenga maana kila mpiga kura aliamini ni Dkt Magufuli pekee anaweza kuivusha CCM. Same kwa Makonda tangu alipoteuliwa uenezi alionesha matumaini kwa wapiga kura tena kwa mwitikio ambao hata Dkt Samia Mwenyekiti wetu hawezi kumfikia, ilikuwa salama ya CCM kuhakikisha Makonda wanamtumia kukihuisha Chama. Ila kwa sasa nakuhakikishia CCM bila watu kama akina Makonda haibebeki, maana wapiga kura kule vijijini wanaamini CCM hao hao baadhi ya viongozi wa juu walimuua Dkt Magufuli ili waibe, na kuuza rasilimali za nchi. Na moto wa akina Mbowe na kampeni zao siyo za kudharau wananchi wanaelewa kabisa. Sijui kama CCM itapata mwenye akili ya kujua kesho yake 2025. Na kibaya zaidi tena kibaya zaidi ni kundi kubwa la Dkt Magufuli kupitia wabunge aliowaweka bungeni kwa mkono wake na lile kundi alilolikata Dkt Magufuli kwa mkono wake wa chuma, hayo ni makundi nayaita Dynamics “ukilizingua kundi mojawapo” linahamia chadema na kila kundi lina ajenda ya udhaifu wa serikali ya Dkt Samia na dhihaka dhidi ya mpendwa wao Dkt Magufuli, kwa hiyo 2025 tutegemee chochote kutokea. Mtu pekee anayeweza kuivusha CCM ni Paul Makonda tena akiwa kama Katibu Mkuu wa CCM chama kinaweza kuvuka kwa sababu Dkt Nchimbi hana ushawishi kwa wapiga kura, yes anaweza kuwa na ushawishi ndani ya CCM na mfumo ila hana ushawishi kwa masikini. Na akitaka kujilinganisha na Dkt Kikwete atakosea, kikwete 2005 na alikuwa na popularity ya ajabu yaani watu walimpenda bila hata kuongea, ila baada ya Kikwete kushidwa kuzuia wizi alichukiwa mpaka leo na wapiga kura wa leo wanataka kiongozi anayekemea wizi, anawajibisha na analinda maslahi wa walio wengi kwa kuhakikisha wachache pia maslahi yao yanakuwa second priority.
Makonda anauweza uongozi kwa maana ya ufuatlliaji wa maagizo ya kiserikali lakini hana kabisa busara wala hekima.

Alimsingizia Lowassa kwamba ana mtoto wa nje, ili amchafue tu. Akaenda msibani kule Arusha akisahau kuwa anayemzika ni yule yule aliyemtungia uongo.

JPM alianzisha siasa za kibabe na za ajabu sana hivyo Sabaya, Makonda na Hapi wakawa wanaingia moja kwa moja kwenye siasa hizo chafu.

Kuamini kwamba Makonda eti anaweza kuivusha CCM ni sawa na kufilisika kabisa kimtazamo.

Hana hoja za kwake mwenyewe za maana. Ni mtu anayetumika kuanzisha 'michezo' ya kisiasa ya kuhamisha akili za jamii wakati serikali ikiwa inataka kufunika suala fulani lenye kuhojiwa kwa kina na jamii.
 
Makonda anauweza uongozi kwa maana ya ufuatlliaji wa maagizo ya kiserikali lakini hana kabisa busara wala hekima.

Alimsingizia Lowassa kwamba ana mtoto wa nje, ili amchafue tu. Akaenda msibani kule Arusha akisahau kuwa anayemzika ni yule yule aliyemtungia uongo.

JPM alianzisha siasa za kibabe na za ajabu sana hivyo Sabaya, Makonda na Hapi wakawa wanaingia moja kwa moja kwenye siasa hizo chafu.

Kuamini kwamba Makonda eti anaweza kuivusha CCM ni sawa na kufilisika kabisa kimtazamo.

Hana hoja za kwake mwenyewe za maana. Ni mtu anayetumika kuanzisha 'michezo' ya kisiasa ya kuhamisha akili za jamii wakati serikali ikiwa inataka kufunika suala fulani lenye kuhojiwa kwa kina na jamii.
Upo sawa ila ukiangalia kwa jicho la pembeni utagundua kizazi kilichopo kinahitaji mtu wa aina gani ili wampigie kura. Ndiyo maana nchi kama Ukraine wanachagua rais eti muigizaji matokeo yake wapo vitani mpaka leo. Kwa ufupi mfumo unatakiwa ufanye kazi kuhakikisha nchi inapata viongozi sahihi. Na ndiyo maana cde Dkt Nchimbi naona kabisa hana agenda ktk nafasi ya KM ila kwingine anaweza faa sana hasa nafasi ya Makamu wa rais etc ila kwenye CCM inahitaji mikikimikiki ambayo kwa upole wake na hekima naona kabisa ni ngumu sana CCM kutoboa
 
Upo sawa ila ukiangalia kwa jicho la pembeni utagundua kizazi kilichopo kinahitaji mtu wa aina gani ili wampigie kura. Ndiyo maana nchi kama Ukraine wanachagua rais eti muigizaji matokeo yake wapo vitani mpaka leo. Kwa ufupi mfumo unatakiwa ufanye kazi kuhakikisha nchi inapata viongozi sahihi. Na ndiyo maana cde Dkt Nchimbi naona kabisa hana agenda ktk nafasi ya KM ila kwingine anaweza faa sana hasa nafasi ya Makamu wa rais etc ila kwenye CCM inahitaji mikikimikiki ambayo kwa upole wake na hekima naona kabisa ni ngumu sana CCM kutoboa
Makonda na Nchimbi ni wanasiasa wa marika mawili tofauti na wana misingi tofauti ya ukuaji wao.

Nchimbi ana hoja kwa watu wa rika lake na makuzi aliyopitia pia Makonda ana hoja kwa watu wa rika lake.

Rais SSH katizama mvuto wa Makonda kwa watu wanaomuelewa anapozungumza. Mzee Kikwete bado ana nguvu na ushawishi kwenye siasa za Tanzania na anao uwezo wa kuzima kabisa ndoto za Rais Samia. Mtandao wake kautengeneza kwa miaka mingi, japo kiuhalisia simuoni akikubali kuonekana mbaya wakati historia ya nchi hii itakapokuwa ikiandikwa.
 
Makonda ni WA kutumika ni chawa kama chawa wengine,anaweza ahidiwa Uongozi ila baada ya 2025 habari yake inaweza Isiwe na umuhimu japo itategemeana na Nguvu za Kambi na upepe wa Kisiasa.

Mwisho Huwa sipendi kujadili mambo ya Kisiasa ila masuala ya Uchumi so endeleeni na mijadala yenu.
Uchomoe kama unakuwasha kwani lazina ubebe mimba husiyopenda baba yake?
 
Mkuu andiko lako kimsingi linamuhusu JK, tunakuomba uthibitishe jinsi JK anavyoingilia maamuzi ya Raisi aliyepo sasa hivi. Punguza chuki mkuu.
Jk inajulikana na kiongozi mroho hajawai tokea kwenye ili bara la Afrika....keshajimilikisha kila kitu ila hatosheki...kaona haifai sasa anatumia vijana wake mkumtusi mama...Na sisi tukiwa bega kwa bega na Makonda wala hatuwezi kubali.
 
Makonda na Nchimbi ni wanasiasa wa marika mawili tofauti na wana misingi tofauti ya ukuaji wao.

Nchimbi ana hoja kwa watu wa rika lake na makuzi aliyopitia pia Makonda ana hoja kwa watu wa rika lake.

Rais SSH katizama mvuto wa Makonda kwa watu wanaomuelewa anapozungumza. Mzee Kikwete bado ana nguvu na ushawishi kwenye siasa za Tanzania na anao uwezo wa kuzima kabisa ndoto za Rais Samia. Mtandao wake kautengeneza kwa miaka mingi, japo kiuhalisia simuoni akikubali kuonekana mbaya wakati historia ya nchi hii itakapokuwa ikiandikwa.
Ni hakika umegonga penyewe, na ndiyo maana vyama vikongwe hushindwa uchaguzi. Ktk mambo ya uongozi wa biashara huwa tunasema biashara huzaliwa na kukua kupitia wateja kupenda product na inafika wakati unahitaji kubadili mbinu ili kuweza kuendana na matakwa ya wateja, Dkt Nchimbi na Dkt Kikwete hawaoni kabisa ila Dkt Magufuli aliona mapema ndiyo maana akawa adui yao. Ila nakuhakikishia kama wakiendelea hivi kuelekea uchaguzi, aisee hali itakuwa ngumu sana tena itakuwa zaidi ya 2010 na 2015, maana wapiga kura wa sasa ni kile kizazi kinachoelewa CCM ni chama cha kulinda mafisadi etc, yaani ukikiambia eti Amani hakijui maana mauaji ya Rwanda na Burundi haviyajui. Dkt Samia namshauri bora aahirishe uchaguzi, katiba mpya ipatikane na asigombee!
 
Back
Top Bottom