Yanayoendelea sasa hivi nchini ni hatari kwa uhai wa chama kilichopo madarakani na baadhi ya viongozi waliopo Serikalini

Kwa hiyo raisi apate wakati mgumu kwa sababu ya kumuumbua Meko na viongozi wengine walafi?Come on..Sisi wananchi tulio wengi tunamsapoti mother!!!!

Sema sisi mijizi tulio kuwa tumethibitiwa na mwenda zake tuna msupport mother. Huoni wezenu walio kimbia waneitwa warudi shamba la Bibi.
 
Kwa hiyo raisi apate wakati mgumu kwa sababu ya kumuumbua Meko na viongozi wengine walafi?Come on..Sisi wananchi tulio wengi tunamsapoti mother!!!!

Jibu la hapa ni neno moja tu muda.
 
Sisi bado ni CCM hatariii gani unaosema hapa tunazungumza walichokifanya waliokuwepo madarakani ya kuiba ma pesa bila Huruma. Hatuna shida na serikali ya Mama Samia.
Majizi nyie,mnanuka ufisadi kila kona, mtoto wa mkulima anaishi kwa mlo mmoja kwa siku nyie mnafisadi mamilioni ya pesa hamna hata aibu
 
Usihofu; hakuna anayechafuliwa. Mengi yanayoongelewa ni kutokana na ripoti ya CAG.
Ofisi, shughuli na ukaguzi wa CAG uko mwa mujibu wa sheria na taratibu; na ripoti za ukaguzi huo hazipaswi kufichwa bali kuwekwa wazi kwani zina manufaa kwa ajili ya Serikali kujipima, kurekebisha na kuchukua hatua stahiki.
Afterall ni pesa za walipa kodi.
Haiwezekani mambo yakaachwa yaende kienyeji.
Kama vile yanavyoongelewa mazuri vivyo hivyo na mabaya yataongelewa.
(Always remember that there are two sides of a Coin).
 
Rais aseme ni Kwa nini Serikali yake, ambayo awali alikuwa Makamu wa Rais imegubikwa na Ufisadi huu wa kutisha?
Pia atupe mikakati yake ya kukomesha Ufisadi kwenye Serikali yake, na hatua ambazo atachukua kwa Taasisi/Mashirika na Watuhumiwa wote wa Ufisadi.

Mwisho, kama ana nia ya dhati na Tanzania, hana haja ya kuendelea kuyafungia Magazeti ya Uchunguzi. Tumeona tamko lake la kufungulia Vyombo vya Habari ilikuwa geresha tu.
 
Kabisa nashangaa kuona lawama anatupiwa mtu mmoja, wakati hata yeye alikua anahangaika sana kuyaondoa haya matatizo..
Wanamuonea kwa vile wanajua hili swala hata likifika mbele ya kamati za bunge au mahakamani, mtuhumiwa ambae ni marehemu hatokuwepo kujitetea
 
Kinachosikitisha ni kuona kila ufisadi au kila jambo baya lililofanyika, au lililofanywa na kiongozi au mtu yoyote aliekuwa katika serikali ya awamu ya tano lawama zote anabebeshwa hayati Magufuli.
Alikosea kubeba mzigo wa TANZANIA peke ake

Alikosea kufunika baadhi ya vitu kwa nguvu kubwa ikiwemo kuvitungia sheria sasa watu wanaona ni mapya.

Aliumiza kundi kubwa la raia (watumishi & wafanyabiashara) hili lilikua swala la muda tu wangelipuka.

Vijana ambao wengi ni Jamuhuri ya internet waliumizwa zaidi kwa kunyimwa ajira kwa muda mrefu na walipojiajiri kutoboa ilikua ngumu wakaishia kuitwa WANYONGE.

TATIZO KUBWA ALIJIPA USAFI ulopitiliza mbele ya watu akasahau ana watendaji wachumia tumbo hivyo kwa kipindi chote alikua kafunika kinyesi kwa bakuli wapo waloisikia harufu wakasema kilichofuata tunakijua ambao hawakusikia bakuli limeanza kufunuliwa unategemea nn??

Mwisho wa siku ana mengi mezuri na alipigana vita vyake kwa kiwango chake na wengine waanzie hapo....

JIANDAENI BOMU LINAKUJA MEIMOSI LINAWEZA KUFUTA MAZURI YAKE YOTE.
 
Makamu qa Rais hana Say kwaio lawama zinaendelea kwenda kwa Mwendazake
Ikiwa raisi anapaswa kuwajibika kwa ufisadi, wizi au uchafu wowote unaofanyika chini ya uongozi wake ni kwann mwaka 2008, mzee Lowasa alijiuzulu badala ya Kikwete? Pia mzee Mwinyi aliwahi kujiuzulu kwa kashfa iliyotokea chini ya uongozi wa mwalimu Nyerere?
 
ccm wengi wamekubali kucheza mchezo wa mafisadi na tayari wameingia kingi vibaya.Kama hawawezi japo kujitoa mhanga kupambana mitandaoni kuna anguko linakuja si kutoka vyama vya upinzani maana vyama ni dhaifu bali ni ccm kukatika mara mbili. Nyerere alishatabili na lazima utokee.Kukatika kwa ccm kutakuja kwa njia ya ukabila. watu wanasahangilia kabila la wasukuma kushambuliwa sababu ni la Magufuli hawa sasa wamejikunyata wanatafutatana na mkumbuke ni 1/3 ya nchi bila kujumlisha wajomba wanyamwezi.Endeleeeni kushangilia ya kenya yatapiga hodi
 
ilikuwa ni serikali ya one-man show.Alitaka kujiuzulu mara nyingi sababu ya kutokubaliana na meko.
Alitaka? Kwanini basi hakufanya hivyo kabisa?

Je, alitokea hata popote na kusema sikubaliani na hili na hili?

Ila kinachofurahisha ni kwamba wapinzani ndio wanaoishangilia ccm kwa sasa
 
Samia ili kulinda heshima yake angejiuzulu
 
Wewe ni Polepole au? Tulia basi dawa ikuingie, huyo Mwendazake kama alikuwa mwizi tuko tayari kumwambia Gwajima amfufue ili tumfungulie mashtaka[emoji16]
 
Magufuli aliwazodoa sana watu kwa minajili ya kupinga ufisadi, hivyo na yeye akionekana alikuwa anafuga ufisadi ni sawa tu azodolewe.

Waswahili wanasema, ukiishi kwa upanga, utakufa kwa upanga.
 
Lawama zinaelekezwa kwake kwasababu moja tu.
Yeye alituaminisha kwamba chini ya uongozi wake hakuna ufisadi au fisadi yeyote ange survive. Na alijitapa kwamba amedhibiti rushwa na ufisadi kwa kiwango kikubwa.

Lakini pia kama kuna kitu ambacho hawezi kukwepa lawama hizi ni kitendo chake cha kujitoa kwenye mkataba wa kuendesha serikali kwa uwazi.
Kama akili inafanyakazi lazima utajiuliza lengo hapa lilikuwa ni nini?
Je alikusudia kuficha nini?

Je kwanini alizuia uhuru wa vyombo vya habari hasa vile vilionekana kufichua maovu?

Je kwanini aliwachukia wapinzani na hata kuhakikisha kwenye uchaguzi wa 2020 hawarudi bungeni wakati wapinzani walikuwa whistleblowers wa kufichua maovu ambayo wana ccm hawezi kuyafichua?

Je alifanya yote hayo ili afiche nini?
Kwahiyo lawama zinapoelekezwa kwake usishangae.
 
Kwanini hamkutaka CAG asome madudu yenu kwa undani, 2016-2019,hamkutaka tujue kwamba mnatupiga,mlikataza pia vyombo vya uchunguzi ili vizisiwachunguze mkatengeneza na kikundi cha watu wasiojulikana ambacho hadi leo hamjataka wajulikane
 
Kama na wewe ni great thinker, basi Taifa hili bado lina safari ndefu. Muda huu uliotumia kuandika pumba hizi ni Heri ungelimsaidia mkeo kuchambua mchele.
Pumba kivipi kijana.. kwamb hakuna ufisadi uliyofanyika? Kwamba hakuna viongozi wengine nje ya hayati Magufuli waliohusika na ufisadi huo? Na kama wapo kwann lawama abebeshwe marehemu tu?
 
Nashukuru sana kwa mchango wako mkubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…