"NAAAM....!
Miradi yake mingine inaleta foleni kubwa kabisa kuwahi kutokea, haina maana ni hasara? Mbona ni rahisi tu, kwa nini tuendelee na Ma-foleni na Ma-hasara? Nashauri Vunjeni Madaraja na Flyovers zote, Ng'oeni reli zote hasahasa ya SGR, uzeni Ndege zote na vivuko vyote nchini, Uza Meli zote Mpya zilizozinduliwa kule ziwa Nyasa, simamisheni Ujenzi wa Bwawa la umeme tununue majenerata kwa wahindi tupate kodi, Gaweni Migodi yote kwa wawekezaji uchumi ukue, Binafsisheni Milima, Maziwa na Mbuga kwa watu binafsi tupate faida Bomoa Bandari zote zilizoboreshwa ikiwemo Mtwara, Tanga na Dar, Jengeni moja ya Wachina Bagamoyo kwa mkataba wa miaka 100. Rudisheni Ada mashuleni walimu walipwe vizuri tukuze uchumi, Wapeni Matajiri misamaha ya kodi waongeze mzunguko wa pesa, Ruhusuni Makinikia na gesi kwenda nje wawekezaji waongezeke zaidi tupate pesa, Vunjeni Masoko mapya ya Madini mikoani yakauziwe nje huko, Charaza Bakora Machinga mjini waache kusumbua watu, Mwaga wali wa Mama Ntilie wasituchafulie jiji, Vunja vyama vya wakulima na utaratibu wa stakabadhi ghalani umepitwa na wakati, Ruhusuni Uhuru wa Mashoga nao wana haki kama wengine, ruhusuni Chanjo ya Corona wasije wakatutenga, Msitumie nguvu kukabiliana na majangiri wa tembo tutafukuza watalii, Uhuru wa mateja kwa wingi mtaani nao ni ndugu zetu, Madawa ya kulevya sio yote yanalevya mengine yanalewesha tu kama bia n.k. Pia Msisahau kuifunga ile Mahakama ya Mafisadi sab ufisadi hauta isha hata hivyo, Kwa uchache tu Hakika hapo sasa pengine Tanzania itakuwa kama ULAYA, Tanzania ya Asali na Maziwa!.