Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Na bado hapo Serikali haijamuibia huyo mfanyakazi kwa kupitia PAYE, magumashi ya bima ya afya, magumashi ya mafao na vikokotoo vyao. Inasikitisha.
 
ongeza bidii katika kufanya kazi kwani mtaji ulionao ni nguvu zako mwenyewe🐒

ukijipanga na kasavingi kidogo, njoo shamba msimu wa kilimo, na ndio itakua mwisho wa manung'uniko na malalamiko bali long smile na kicheko cha haja baada ya muda mfup tu 🐒
 
Hebu tuacheni unafiki

Kwani mmelazimishwa kufanya hizo kazi?

Utalipwa kutokana na thamani yako , ukiona mshahara hautoshi jiongezee thamani .

Tafuta fani ya ufundi , jifunze endeshea maisha..

Sio lazima mrundikane wote kiwandani.
 
Aisee ndio maana tunatakiwa kumshukuru MUNGU sana kwa kile unachokipata hasa wale waajiriwa wenye mishahara inayoanzia 500k kwenda juu.

Unakuta mtu anafanya kazi ngumu NON STOP.. RISK telee

Kumbuka hapo akijichanganya akaingiza miguu/mikono kwenye mashine hiyo ni juu yake.. Mwajiri kesho analeta PUNDA mwingine apige kazi ww utajuana na ndugu zako huko.
 
haya mambo wazungu walipitia mwaka 1600 to 1800 mwishoni huko ndio kulikuwa na unyonyaji wa design hizi huko ulaya maana hakukuwa na sera wala sheria za kuwalinda wafanyakazi.

ila cha ajabu sasa leo mwaka 2024 nchi yetu inasera, miongozo na sheria za kuwalinda wafanyakazi hawa lakini wamiliki wa hivyo viwanda bado wameachwa wafanye wanavyotaka mafano kima cha chini kwa sasa kwa siku kwenye viwanda kwa mijibu wa serikali ni tsh. 5,770 kwa siku. kwa wiki 34,618 na kwa mwezi 150,000= bado unajiuliza inakuwaje mhindi mmoja mjinga tu amelowea hapa nchini anawatumikisha ndugu zetu kwa ujira wa 3,500/= kwa siku na bado anakenuliwa meno na viongozi wetu.

je hawa viongozi wetu waliojaa kama utiriri kuanzia serikali za mitaa, kata, tarafa, wilaya, mkoa wanatusaliti au ni wamelogwa au ni nini!

pia hii sheria inatakiwa itamke wazi kabisa haya malipo ni kwa masaa mangapi maana ukisema kwa siku mwingine anawafanyisha watu kazi saa moja asubh hadi saa moja jioni nayo ni siku sheria zetu wenyewe zinatukandamiza haya ni maajabu kabisa.

hivi hakuna wanasheria wanaweza kujitolea kusimamia hivi vitu ili wananchi wanyonge wapate haki yao.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-03-15 at 15.48.51.jpeg
    64.1 KB · Views: 12
Utumwa .
Yaani serikali ndio kibaraka wa utumwa
 
Forgotten mbona unaongea maneno kama mungu mjomba Ako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…