Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Yanayofanyika viwandani Tanzania ni utumwa. Kazi ngumu, maslahi duni. Serikali haina mpango na wananchi wake, inachoangalia ni kodi tu

Kuna kiwanda kiko Pale Keko karibu na ukumbi wa DDC nadhani ni cha cello. Malipo kwa siku ni sh. 3500 kwa siku ilikuwa kwa muda mrefu. Sasa ni sh. 4000, kazi masaa 12 yaani lisaa limoja sh. Mia tatu na centi.

Viwanda vingi malipo ni sh. Elfu 5000 kwa siku, hii maana yake lisaa limoja la kazi ni sh. 400. Viwanda vyenye majina makubwa malipo kwa siku ni sh. 7000 hii maana yake lisaa limoja sh mia 6.

Hata kama ni non skilled labor ni haki Mtanzania alipwe sh. Mia 4 kwa lisaa limoja? Ni utumwa wa wazi uliopata baraka za serikali.

Hawa mabilionea wetu akina Bakhressa na Mo huwabebesha Watanzania viroba vya unga wa ngano kwa sh. 50 au pungufu kwa kiroba kimoja. Ni utumwa.

Nimewahi kufanya kazi siku moja tu kwa wahindi Kariakoo ni zaidi ya utumwa , kula juu yangu, nauli juu yangu malipo 7500 kwa siku na kazi very risk. Kazi ya kupeleka mizigo ghorofa ya 12 kutoka chini. Sikurudi tena.
Vijana wa kiafrika katika kusaka Hela. Huwa ni sawa tuko jehanamu. Kazi tunazozifanya hazilingani na kipato kunachokipata. Ni maumivu makubwa sana Tena Sana.
 
Hebu tuacheni unafiki

Kwani mmelazimishwa kufanya hizo kazi?

Utalipwa kutokana na thamani yako , ukiona mshahara hautoshi jiongezee thamani .

Tafuta fani ya ufundi , jifunze endeshea maisha..

Sio lazima mrundikane wote kiwandani.
Nyie ndo wale wale chawa wa ccm.. mnaojitoa ufahamu wa akili mkiwa chawa. Unafikiri watu wote wanaweza kujiajiri? Hujui nafasi ya serikali katika hili..
 
Mkuu hio upo dunia nzima, unaposikia Wazungu wanakimbilia china kwa ajiili ya cheap labor ndio kama hao, saizi wanatoka china wanaenda India kwa ajiili ya watu kana hao,
Unskilled labor dunia nzima mishahara yao ni mbuzi tu, mana wanakuwa hawana mikataba, day worker tu,

Kwa kusema hivyo tuhimizane ndugu zangu kusoma sanaa

Kwa maana hiyo Elimu ndio kipimo cha Utu?

Elimu unayopewa na binaadam Kama wewe inapita vipi kiwango cha Utu ulichoumbwa nacho?
 
Once you are born in Africa life is automatically leading you 1-0.

And if you are not educated that's 2-0.

At this point you have no option than hustling like a donkey.

Educated in what sense?

Knowledge will take you even further n Life, places no amount of education you receive could ever afford them.

Knowledge illuminates all beings equally while Greed & Misconceptions portrays man made Education as reality.

Knowledge flows naturally, only to beings with open currents and free from brainwashing systems called education.

Knowledge has no limit nor boundaries.
 
Hebu tuacheni unafiki

Kwani mmelazimishwa kufanya hizo kazi?

Utalipwa kutokana na thamani yako , ukiona mshahara hautoshi jiongezee thamani .

Tafuta fani ya ufundi , jifunze endeshea maisha..

Sio lazima mrundikane wote kiwandani.

Kwahiyo wale wasioweza kuzitambua thamani zao waachwe waangamie?

Kuna dhambi gani kila binaadam akapata thamani Sawa na nafasi Sawa katika kujipambania katika uhai wake?

Kwamba akilipwa kila saa elf 5 badala ya Mia 5 huyo bilionea akashuka kuwa milionea na dunia ikatulia, shida itakua nini?

Binaadam tunatengeneza madaraja kati yetu tena kwa kupenda wenyewe lakini yakitukuta maafa tunaanza kutafuta mchawi.
 
Sad truth, maisha hayaangalii process,
Ni kweli wanatafuta hela ya kujisomesha, ila hapo wapo kama unskilled labor, na issue ya wao kutokwenda shule sio kesi ya mwenye kiwanda ni kesi yao wenyewe, hapo watalipwa pesa ya siku,

Kwenye maisha hulipwi ili kutimiza ndoto zako, unalipwa kwa kiasi cha value unayo add, mwajiri hakulipi ili uende shule, analipa kwa kile unampa kwenye biashara yake,

Huu ni ukweli mbaya, hausound vema ila ndivyo ilivyo

Lakini bila huyo “unskilled person” huyo tajiri si chochote.

Kimsingi huyo unskilled person ndio engine ya kiwanda lakini anafanywa kama ndio dekio la kiwanda.

Ni ukweli uliopo lakini haina maana kwamba ndio Ukweli sahihi na unaopaswa kuwapo.
 
Mimi naona huu ni mpango wa serikali wa makusudi kabisa. Kuwafanya wananchi wake kuwa watumwa kwa kutumikishwa bila kujaali kwamba watanufaika au laa. Sio viwandani tu bali pia sehemu zote mishahara ni midogo sana angalia hata kazi za ulinzi watu wanalipwa kidogo sana.

Wakati mwingine hata hizi sera za siasa kwa pande zote mbili yaaani wapinzani na wanaotawala hakuna hata mmoja ambaye kipindi cha kampeni atagusia kuhusu ajira na malipo kwa wananchi wanaoingia kwenye ajira. Kwamba watashighulikia badala yake husema tu tutaongeza ajira bila kusema namna ya kuboresha maslahi kwanza.

Nchi yetu ipo kwenye wakati mgumu sana kuhusu maendeleo ya watu wake ndiyo maana ni rushwa na ujanja mwingi maeneo mengi ya kazi. Haiwezekani eti mtu analipwa kwa siku 5000 au laki Moja na nusu kwa mwezi.
 
Mkuu hio upo dunia nzima, unaposikia Wazungu wanakimbilia china kwa ajiili ya cheap labor ndio kama hao, saizi wanatoka china wanaenda India kwa ajiili ya watu kana hao,
Unskilled labor dunia nzima mishahara yao ni mbuzi tu, mana wanakuwa hawana mikataba, day worker tu,

Kwa kusema hivyo tuhimizane ndugu zangu kusoma sanaa
Sasa mkuu unaposema hivyo, sio sahihi, kwani sasa hivi hata huyo aliyesoma sana, naye kipato anacholipwa ukiangalia kimahesabu ni sawa tu na huyo casual labour!! Juzi waziri wa kilimo anasifia kuwa sasa wahitimu wa SUA, watakuwa wanaajiriwa moja kwa moja kwenye makampuni ya pamba kwa mshahara wa tsh. 500,000 kwa mwezi sawa na karibia 17,000 kwa siku!! Hii si hatari?!!
 
Mimi naona huu ni mpango wa serikali wa makusudi kabisa. Kuwafanya wananchi wake kuwa watumwa kwa kutumikishwa bila kujaali kwamba watanufaika au laa. Sio viwandani tu bali pia sehemu zote mishahara ni midogo sana angalia hata kazi za ulinzi watu wanalipwa kidogo sana.

Wakati mwingine hata hizi sera za siasa kwa pande zote mbili yaaani wapinzani na wanaotawala hakuna hata mmoja ambaye kipindi cha kampeni atagusia kuhusu ajira na malipo kwa wananchi wanaoingia kwenye ajira. Kwamba watashighulikia badala yake husema tu tutaongeza ajira bila kusema namna ya kuboresha maslahi kwanza.

Nchi yetu ipo kwenye wakati mgumu sana kuhusu maendeleo ya watu wake ndiyo maana ni rushwa na ujanja mwingi maeneo mengi ya kazi. Haiwezekani eti mtu analipwa kwa siku 5000 au laki Moja na nusu kwa mwezi.
Kweli. Rushwa na ufisadi ni kama vina baraka kutoka serikalini.
Mtu ana familia laki na nusu inamtosha kufanyia nini?
Hata kula mtu mmoja kwa mwezi haitoshi.
 
Sasa mkuu unaposema hivyo, sio sahihi, kwani sasa hivi hata huyo aliyesoma sana, naye kipato anacholipwa ukiangalia kimahesabu ni sawa tu na huyo casual labour!! Juzi waziri wa kilimo anasifia kuwa sasa wahitimu wa SUA, watakuwa wanaajiriwa moja kwa moja kwenye makampuni ya pamba kwa mshahara wa tsh. 500,000 kwa mwezi sawa na karibia 17,000 kwa siku!! Hii si hatari?!!
Kibongo bongo 500k ni mshahara mkubwa,
Walimu ndio wanakunja hio,
Polisi wanakunja hio,
 
Mkuu hio upo dunia nzima, unaposikia Wazungu wanakimbilia china kwa ajiili ya cheap labor ndio kama hao, saizi wanatoka china wanaenda India kwa ajiili ya watu kana hao,
Unskilled labor dunia nzima mishahara yao ni mbuzi tu, mana wanakuwa hawana mikataba, day worker tu,

Kwa kusema hivyo tuhimizane ndugu zangu kusoma sanaa
Na huko wanalipa Tsh 400 kwa saa?
 
Kuna kiwanda kiko Pale Keko karibu na ukumbi wa DDC nadhani ni cha cello. Malipo kwa siku ni sh. 3500 kwa siku ilikuwa kwa muda mrefu. Sasa ni sh. 4000, kazi masaa 12 yaani lisaa limoja sh. Mia tatu na centi.

Viwanda vingi malipo ni sh. Elfu 5000 kwa siku, hii maana yake lisaa limoja la kazi ni sh. 400. Viwanda vyenye majina makubwa malipo kwa siku ni sh. 7000 hii maana yake lisaa limoja sh mia 6.

Hata kama ni non skilled labor ni haki Mtanzania alipwe sh. Mia 4 kwa lisaa limoja? Ni utumwa wa wazi uliopata baraka za serikali.

Hawa mabilionea wetu akina Bakhressa na Mo huwabebesha Watanzania viroba vya unga wa ngano kwa sh. 50 au pungufu kwa kiroba kimoja. Ni utumwa.

Nimewahi kufanya kazi siku moja tu kwa wahindi Kariakoo ni zaidi ya utumwa , kula juu yangu, nauli juu yangu malipo 7500 kwa siku na kazi very risk. Kazi ya kupeleka mizigo ghorofa ya 12 kutoka chini. Sikurudi tena.
Kama ndoo ya plastiki ya cello inauzwa 2500 kariakoo kiwandani inauzwa shs ngapi? Unadhani gharama ya kuzalisha ndoo moja ni shs ngapi? Halafu wewe wakulipe shs ngapi? Muda mwingine mtumie vichwa vyenye nywele kufikiri, hiyo kazi ya elfu tatu kuna watu wamejenga na kusomesha watoto kwa hiyihiyo kazi na kuna watu wanahonga pesa kuipata hiyo kazi, uwe na adabu nyoko
 
Kama ndoo ya plastiki ya cello inauzwa 2500 kariakoo kiwandani inauzwa shs ngapi? Unadhani gharama ya kuzalisha ndoo moja ni shs ngapi? Halafu wewe wakulipe shs ngapi? Muda mwingine mtumie vichwa vyenye nywele kufikiri, hiyo kazi ya elfu tatu kuna watu wamejenga na kusomesha watoto kwa hiyihiyo kazi na kuna watu wanahonga pesa kuipata hiyo kazi, uwe na adabu nyoko
Kujenga na kusomesha??😉😉
 
Kama ndoo ya plastiki ya cello inauzwa 2500 kariakoo kiwandani inauzwa shs ngapi? Unadhani gharama ya kuzalisha ndoo moja ni shs ngapi? Halafu wewe wakulipe shs ngapi? Muda mwingine mtumie vichwa vyenye nywele kufikiri, hiyo kazi ya elfu tatu kuna watu wamejenga na kusomesha watoto kwa hiyihiyo kazi na kuna watu wanahonga pesa kuipata hiyo kazi, uwe na adabu nyoko
Wanazalisha ndoo moja kwa siku?
 
Kama ndoo ya plastiki ya cello inauzwa 2500 kariakoo kiwandani inauzwa shs ngapi? Unadhani gharama ya kuzalisha ndoo moja ni shs ngapi? Halafu wewe wakulipe shs ngapi? Muda mwingine mtumie vichwa vyenye nywele kufikiri, hiyo kazi ya elfu tatu kuna watu wamejenga na kusomesha watoto kwa hiyihiyo kazi na kuna watu wanahonga pesa kuipata hiyo kazi, uwe na adabu nyoko
Mtumwa anaposifia utumwa.
Kama mfanyakazi wa kiwandani anajenga huyo ni aidha mwizi au hana akili yaani hali kama anavyopaswa kula mwanadamu na badala yake anaweka akiba sehemu ambayo hakupaswa kuwekwa akiba
 
Back
Top Bottom