Uchaguzi 2020 Yanayojiri kwenye kampeni za Mgombea Urais wa CHADEMA Tundu Lissu kwenye Mikoa ya Kilimanjaro na Tanga

Aiseee mpaka Tanga wanataka mabadiliko? Kweli Lissu ni shujaa wa kizazi hiki.
CCM wanashangaa Lissu anapataje watu kwenye mikutano yake wakati hatangazwi na main stream media yoyote.

Cha kushangaza zaidi ni zile impromptu gatherings kwenye vijiji mbali mbali ambazo zilikuwa zinajitokeza wakati anatumia usafiri wa gari.
 
Ni ngumu sana kuitoa ccm madarakani,wana miziz mikubwa kama miti ya mibuyu,na hata ukitanzama kwa jicho la mbali bado itatawala sana,zile 58% alizopata Magu mwaka 2015 zinaongezeka mara dufu mwaka huu,ni uchaguz mwees sana kwa CCM,,

Na mbaya zaid hata ukiangalia upande wa pili ni watu ambao hata wakipewa nchi ni ngumu sana kuunda serikali maana kule makarai ni mengi mno
 
Kwa kuiba tu sio kwa uhalali.
 
Kwenda kwenye mkutano wa Magufuli Kilimanjaro dau limeongezwa kutoka elfu tano walizotoa Mkoa wa Tanga hadi elfu kumi kwa Mkoa wa Kilimanjaro

Swell langu Mbona Watumishi wa Serikali hawaongezewi Mishahara wakati fedha zinachezewa na hawa Wanasiasa?

CCM wanajua fika kuwa Wananchi watakula hizo fedha na kura watampa Lissu sasa je Polepole bado anamdanganya Mwenyekiti wake?
 
Una akili timamu ?
 

Najua inauma sana ila imesalia wiki tu maumivu yaishe.

Kawatia adabu, zile kelele za upinzani umekufa cjui hatuna mgombea, cjui picha za 2015 kwishaaaaaaa
 
Nimemsikiliza Lissu leo. Amechanganya vijembe na sera. Safi sana. Mwambieni aendelee hivyo hivyo hadi mwisho. Vijembe na sera, vijembe na sera...

Kitu kingine ahakikishe karatasi ya kura kama itabaki hivyo hivyo ilivyoonyeshwa na Tume. Akisha hakikisha, aanze kuhamashisha wapigakura kwenda moja kwa moja pale MWISHO kabisa alipowekwa Lissu na Mwalimu. Na wakiweka tiki iwe fupi ili mkia wa tiki usiingie kwenye boksi la mgombea mwingine. Tiki ndefu zinaweza kuleta figisu kwa vile NEC na CCM wanawafuta kwa udi na uvumba.
hakuna ubishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…