LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

LIVE Yanayojiri vita ya Israel dhidi ya Palestina na HAMAS

Live coverage on JamiiForums
Silaha hizo zinafahamika kama "white phosphorus bombs" ni aina ya incendiary weapons ambazo zina madhara makubwa ya kusabisha moto katika kila kitu itakachogusa na kukiyeyusha hata iwe chuma cha pua. Kwa binadamu madhara yake hayaelezeki.

Silaha hizo ni moja kati ya silaha zilizopigwa marufuku kutumika katika makazi wanamoishi watu au vitani na Umoja wa mataifa (UN).

Hii ni mara ya pili kwa Israel kutumia silaha hiyo ukanda wa Gaza. Mara ya kwanza ilikuwa ni katika mapigano ya 2008-2009 (Rain of Fire: Israel's Unlawful Use of White Phosphorus in Gaza)


View attachment 2776905View attachment 2776907View attachment 2776908View attachment 2776921View attachment 2776922

Source: PTVBreaking
Hata kama ni kweli, wamechelewa kuzitumia ikiwa ndiyo njia ya kuwamaliza magaidi
 
Israel njooni tuwape eneo zuri kusini uko...lina gas na linafaa kwa kilimo...
Mtatupa umeme..maji na kutujengea miundombinu mingine, achaneni na palestina uko
 
Hapa Sasa Kuna tatizo, maana ulikuwa unaelezea historia halafu reference Yako ni Quran, nimechallenge tu kuhusu tarehe ya matukio unayoelezea na tarehe ya QURAN umesema nikawaulize tena hao Wana wa israel. Wakati Mimi nimekuuliza Wewe uliyekuwa unaelezea historia.

Tafadhali Nielezee kwa ushahidi hiyo historia.
Believe me, Mimi sio biased kivyovyote vile maana Sina interest na upande wowote hapo. I'm Purely Afrocentric.
Kwangu Mimi Quran,Biblia,Veda nk. Ni vitabu tu kama vitabu vya Shaban Robert au Ngugi wa thiong'
Sasa mkuu hata nikueleze kwa kihebrania chenyewe umeshasema unachukulia ni kama vitabu vya kina shaaban robert unataka nikwambie nini tena? ilhali hiyo Qur'an ni uteremsho kutoka kwa mola wa walimwengu wote, na imeeleza habari za tangu kabla ya baba wa wanadamu ambaye ni aadam amani iwe juu yake, sembuse habari za wajukuu wa ibraahim wa hapa majuzi?.

Pili sikukwambia wewe ndo uwaulize hujanisoma tu vizuri, anyway tusiharibu uzi tuendelee kupeana updates.
 
Hio Strategy itasababisha vifo vingi sana,na wengi watakufa kwa Njaa.
Inasikitisha sana.

Nadhani hao Palestinian walio wengi wakiulizwa kama wanazipenda harakati za hao Hizbulah sijui Hamas hakuna anaewaunga mkono maana mara nyingi makosa wanayoyafanya wakidhani wanaokoa nchi yao matokeo yake yanawaumiza wasiokuwepo.
 
Jeshi lolote linalo tumia chakula kama silaha vitani ni jeshi daifu na,ni jeshi la hovyo kabisa ,yaani mnajiita mna jeshi bora kimapambano alafu mnategemea njaa iwasaidie kwenye mapambano.
alafu hii sio mara ya kwanza kwa Israel kupigana na Hamas na ikafunga mipaka lakini wapalestina wali ishi.
Wapelekeeni chakula, maji, umeme, silaha nk.
 
Yaani mshambulie kwa maroketi mkijibiwa mnaanza kuandika andika filosofia...
Mimi ni MKRISTO PURE toka ninazaliwa, tumefundishwa anayeibariki Israel atabarikiwa na anayeilaani atalaaniwa.


Hapo nimeongea madhara yatokanayo na vita pasipokujalisha vita hiyo inapiganwa Israel/Africa/Ukraine/Palestine au Bolivia.
 
Mkuu ,kijiji chako hakuna maji Safi na salama,umeme hakuna, huduma za Afya ni shida ,ujinga na umasikini umetamalaki, pigania hayo!,mambo ya middle east watching wenyewe!,elewa pamoja na juhudi zote ilizozifanya Tanzania, still Mozambique walituwekea visa,SA visa na sasa Kenya wanafanya biashara kubwa na SA kuliko sisi, na juzi kati wamepewa e visa !,angalia ya kwako hapa nchini
 
IMG_20231009_171306_020.jpg

I am drafted as well to serve and defend my country Israel. 🇮🇱

I said goodbye to my wife India, who sent me with blessings and protection of God. From now on she will be managing and posting on my behalf so be nice to her. 😉🇮🇱😊
 
UN,wako wapi? Hizi ndiyo kazi zao,Sasa wako wapi au Kwa kuwa Israel ni mshirika wao.
Papa Yuko wapi mbona Yuko kimya, viongozi wakubwa wako wapi duniani kusulihisha hili jambo.
Nchi za G8 ziko wapi mbona ziko kimya au Israel na Palestine migogoro Yao hawa wasuluhishi hawaruhusiwi kuingilia na kutatua?
 
IMG_20231009_171649_440.jpg

Senior Hamas commander Raafat Abu Hilal was reported killed in an airstrike on the Bashit camp in Rafah, south of the Gaza Strip.
 
Kabla ya Isaka kuna mtoto alizaliwa tena wa kiume, unaweza kutueleza alienda wapi? Je alirithi nini?? La pili, Yakobo na kizazi chake walienda Misri, je kizazi cha Essau kilienda wapi?? Kumbuka mtoto wa kwanza wa Ibrahim naye alipata uzao.
Kabla ya Isaka mtoto Alie zaliwa alikua anaitwa Ishmael ambaye Ibrahim alizaa na kijakazi wake ambaye alikua akiitwa hajira
Soma👇
Mwanzo 16 : 2 Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, Bwana amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai.
Mwanzo 16 : 15 Hajiri akamzalia Abramu mwana wa kiume; Abramu akamwita jina lake Ishmaeli, yule mwanawe, ambaye Hajiri alimzaa.

Baada ya hapo Sarah akamchukia Yule kijakazi ambaye ni Hajira akamtesa mpaka yule Kijakazi akakimbia lakin hata hivyo Biblia inasema Mungu alimrudisha.
So Kibiblia haionyeshi alienda wapi Ishmael alienda wapi lakin ukisoma history yake alienda inaonyesha Ishamel aliishi pande za Shuru kuelekea Misri!! Soma👇
Mwanzo 25 : 17 Na hii ndiyo miaka ya maisha ya Ishmaeli, miaka mia na thelathini na saba. Akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake.
Mwanzo 25 : 18 Wakakaa toka Havila mpaka Shuri, unaoelekea Misri, kwa njia ya kwenda Ashuru. Akakaa katikati ya ndugu zake wote.
Hapa inaonyesha baada ya kufa so alipo zikwa Sasa na hii inaonyesha hayo ndo makao yake na kunaa baadhi ya Wana theology huwa wanasema Ishmael ndo alikua Babu wa Mohammad yule wa Waislamu na ndo Chimbuko la Kislmu limetokea hapo na pia wanasema ndo mtu wa kwanza Kuzungumzia Ki-arabu.


Kuhusu Urithi wa Ishmael Mungu alimbariki sana alimpa aridhi na aliapa atamfanya Kuwa Taifa kubwa soma👇
Mwanzo 17 : 20 - Na kwa habari za Ishmaeli nimekusikia, nimembariki, nitamzidisha, nami nitamwongeza sana sana. Atazaa maseyidi kumi na wawili, nami nitamfanya awe taifa kuu.
Lakini pia unaweza soma Mwanzo hiyo Sura 25 nzima utaona uzao wa Ishmael
Unaweza fuatilia Mkuu Ili ujue kiundani zaidi.

Esau inaonyesha baada ya Kuwa na Ugomvi Mkubwa na ndugue Esau alihama kutoa nchi ya ndugue akaelekea katika Nchi ya Seiri katika Nyika ya Edomu ambayo kwa Sasa ipo Yordani .
Soma👇
Mwanzo 36 : 8 Esau akakaa katika mlima Seiri, Esau ndiye Edomu.
Piah ukisoma hapa inaonyesha Kuwa Ujumbe unatumwa kwenda Esau ambaye alikua ktka makazi yake.
Mwanzo 32 : 3 Basi, Yakobo akapeleka wajumbe mbele yake kwenda kwa Esau nduguye mpaka nchi ya Seiri katika nyika ya Edomu.

Unaweza fuatilia ujue zaidi Mkuu
 
Mkuu ni ukweli tunajua kuwa palestina anaonewa lakin hii haifanyi sote tuunge mkono upumbavu wa Hamas unaoenda kusababisha vifo vya watu wengi wa palestina wasio na hatia.
this time we are almost there,, this has been planned with tactical mastermind IRAN. we angalia alafu uone wapalastina washakufa sana this time i promise you shit is real.
 
Israel na US wanalazumisha WWIII kama ilivyotaviriwa na Notradame kuwa itaanzia mashariki ya kati 2025. Huyu alitabiri pia WWI na II exactly Miaka Zaidi ya 400 iliyopita. Baada ya kufurumushwa na Russia kwenye mgogoro WA Syria bado hawajaridhika.
 
Back
Top Bottom