Uchaguzi 2020 Yanayotokea Tanzania Leo yalitokea Indonesia 1998

Uchaguzi 2020 Yanayotokea Tanzania Leo yalitokea Indonesia 1998

Waliorogwa kama wewe wapo wachache,
ila tulio upinga urozi wa CCM tupo wengi na sasa tunakwenda kuandika historia mpya "ni yeye"
Tutamchagua NI YEYE TUNDU LISU
mimi ni mzalendo na wala si mtumwa wa vyama kama unavyo dhania mkuu, tatizo la tanzania na nchi za afrika lipo katika mifumo ya kiutawala na si kubadili kiongozi...

kwa mtizamo wangu kabla ya uchaguzi kungefanywa mabadiliko ya mifumo ya kiutawala, yaani tukawa na demokrasia inayoakisi matakwa ya watanzania na sio hii inayoakisi matakwa ya mabeberu na kuendelea kutugawa na vyama vyote vingeshiriki katika huu mchakato.

ni mifumo hii tunayotumia kisiasa ni ngumu sana watanzania kua wamoja coz upande wa shilingi unavibaraka ambao wanavujisha siri za taifa kwa maslahi yao bt wakiwa kwa camera wanakaza mishipa ya shingo kudai haki.
 
Nikweli but just think Lisu Kuwa Rais? Or Member? Nadhan nibora tuongozwe na Jiwe Tu. Tunasafari ndefu Sana bado vyama vya upinzani Kuwa vyenye uwezo kutuongoza. Tutakuwa tumepoteza

Huu ni mtazamo wa kiccm. Wakati KANU inaongoza hapo Kenya kwa mabavu, wapambe wa chama hicho walikuwa wanahadaa umma kuwa hakuna chama kinaweza kuongoza nchi hiyo. Lakini mpaka leo KANU haiko madarakani, na bado Kenya inaoongoza kiuchumi kwenye ukanda huu wa Afrika mashariki. Kama ccm na wizi wao wameweza kukaa madarakani muda wote huo, hakuna chama chochote kitashindwa kuongoza nchi hii.
 
Indonesia ilikuwa na utawala uliojulikana kama New Order ulioendeshwa na Rais Surharto. New Order ili dumu madarakani kwa miongo mitatu, watawala walikuwa wamepumzika na hawakuangalia tena matatizo ya wananchi walala hoi.

Mwaka 1998 upinzani ulifanya campeni ya nguvu. Pamoja na New Order kuwa na jeshi, polisi na Usalama wa Taifa, ushindi wa upinzani ulikuwa mkubwa mno.

Mabadiliko makubwa ya kiutawala yalifanywa na Upinzani ulipoingia madarakani. Haikua kazi rahisi na walipitia mwaka mzima wa mtikisiko wa kuichumi. Baada ya hapo mpaka sasa hali ya siasa a uchumi iko shwari.

Mnaopenda kusoma zaidi nendeni Wikipedia msome The history of Indonesia.
Mwaka 1998 upinzani ulifanya campeni ya nguvu. Pamoja na New Order kuwa na jeshi, polisi na Usalama wa Taifa, ushindi wa upinzani ulikuwa mkubwa mno.[emoji1548][emoji1548][emoji1548][emoji1534][emoji1534][emoji1534]

Jr[emoji769]
 
Hakuna mpinzani atampigia Membe wakati Lisu yupo. Hata 2015 ilisemekana kura za wapinzani zitagawanywa na ACT, lakini kura alizopata mama Anna hata milioni hazikufika.
mama mgwira hakuwa na nguvu kama membe
 
Indonesia ilikuwa na utawala uliojulikana kama New Order ulioendeshwa na Rais Surharto. New Order ili dumu madarakani kwa miongo mitatu, watawala walikuwa wamepumzika na hawakuangalia tena matatizo ya wananchi walala hoi.

Mwaka 1998 upinzani ulifanya campeni ya nguvu. Pamoja na New Order kuwa na jeshi, polisi na Usalama wa Taifa, ushindi wa upinzani ulikuwa mkubwa mno.

Mabadiliko makubwa ya kiutawala yalifanywa na Upinzani ulipoingia madarakani. Haikua kazi rahisi na walipitia mwaka mzima wa mtikisiko wa kuichumi. Baada ya hapo mpaka sasa hali ya siasa a uchumi iko shwari.

Mnaopenda kusoma zaidi nendeni Wikipedia msome The history of Indonesia.
Hii inatukumbusha kuwa hakuna marefu yasiyo na ncha.
 
Hizo propaganda Hazina nafasi Kwani alieuza hii nchi rasilimali zake miaka yote hii ni wapinzani hiyo mikataba mibovu waliingia wapinzani hata Magufuli huwa anakili kuwa nchi yetu imeliwa sana ni wapinzani ndiyo wamesababisha, si ni serikali ya CCM ndiyo imeendelea kuuza nchi miaka 59. Ati mabeberu wakileta misaada wadau wa maendeleo sijui huu ujinga utaisha lini. Na hizo flyover miaka yote 59 mbona hazikujengwa na hizo Ndege Nyerere alinunua zilikwenda wapi na tunauhakika gani na hizo kama hazitaishia huko huko kwenye ufisadi. Tumechoka na hizo propaganda za kila siku.
laiti hayo unayoyasema angeyaendeleza magufuli point yako ingekua na mashiko bt yote kayafyekelea mbali na mabeberu wamekosa upenyo ndo maana wamerudi kupitia mlango wa nyuma wapinzani..

mkuu kubali kataa mabadiliko tunayoyataka kwa sasa waafrika ili tujikomboe ni kubadili hiyo mifumo ya mabeberu wanayotuimbisha daily ajili ya maslah yao.
 
Sijui kama watakuelewa.
Lissu hafai kuwa raisi hata kwa mwezi mmoja tu.
Akishinda uraisi itakuwa janga kwa taifa. Sijamsikia akiongea mambo yoyote ya maendeleo na huduma za kijamii.
Hadi sasa sijui kwa hakika dira au sera za chama chake ni zipi. Angalau Membe na ACT nimewasikia wakigusia mambo kadhaa muhimu tatizo utekelezaji wake utakuwa mgumu kama atafungulia kila kitu na kurudisha kama ilivyokuwa awamu ya nne.
They are just unrealistic goals.

Kwani hao wanaoongelea mambo ya maendelea kila siku wameleta maendeleo gani. Hapa tunahitaji mtu wa kubadilisha mfumo mzima wa utawala ili watu waogope sheria siyo kuogopa mtu na hili linawezekana kama tutakuwa na mihimili iliyo imara isiyoegemea muhimili mwengine yakitatuliwa hayo ndipo tutapata maendeo. Huku kutiana hofu na kunyamazisha vyombo vya habari hakuwezi kutufikisha tunakokwenda. Tunataka maendeleo ya watu na hayawezi kupatikana kama watu hawaishi kwa uhuru katika nchi yao.
 
Membe ana wafuasi kutoka ccm, ungeeleweka kama ungesema kuwa kura za mgombea wa ccm zitapunguzwa na Membe.
Kura za Lissu zitapunguzwa na Membe
Kwa kifupi upinzani unajitafuna wenyewe
 
Hao ndiyo chanzo cha kifo cha ccm
Endelea kujifariji wakati kuna wakulima, Askari, watumishi wa umma, vijana kila mmoja amekata tamaa ya maisha katika serikali hii.
 
Hawajawekeza kwenye media kwa maana ya uwekezaji, bali media zote wamezitia hofu kupitia madaraka ya rais yanayotumika vibaya. Ukijaribu kufuatilia vizuri utaona kabisa kuwa ccm sio chama imara, ila kina mwenyekiti anayetumia madaraka yake kibabe, na kumuonea yoyote asiyemsujudia au kuisujudia ccm. Kwahiyo utawala huu wa mabavu na shuruti umetengeneza kukubalika bandia, kisha ndio kugeuzwa kuitwa uimara wa ccm.

Vyama vyote vinavyoongozwa na marais madictator hupewa sifa bandia kuwa ni imara, na huhakikisha washindani wao wote hawapati covarage kwenye media, ili wao tu ndio wasikike na kujifanya wanakubalika.
Hii ndiyo tunaita kujifariji au kukariri.
Media maarufu zenye subscribers wengi karibu zote zinapiga safari hadi miakoani kuonesha miradi iliyofanywa na jamaa kisha wanarusha kila kitu kila kona. Wanarusha hadi miradi ya choo au jiko la shule au zahanati.
Unafikiri mtu anaye fanya hivyo ametishwa?
Fedha za hizo safari anatoa wapi?

Media zote zinafanya live coverage ya matukio ya zinduzi zote za wale wa ngazi za juu kila kona ya nchi, unataka kusema wanafanya hivyo sababu wametishwa?

Hujaliona hilo jambo toka miaka angalau mitatu iliyopita? Watu wanakula mahindi, madafu, mapapai kule forodhani ufukweni, watu wanakaa chini na walemavu wajane, wazee, migogoro ya ardhi inatolewa maamuzi papo hapo kwenye misafara, teuzi katikati ya mikutano au hotuba.

Watu wanaongeza umiliki wa media za chama kama 'Channel Kumi', n.k. wewe bado unahisi vitisho tu?

Je ninyi upinzani mmewekeza angalau redio moja ya chama ya kurusha live matangazo hadi vijijini ambako wengi hawana smart phones hawaingii mitandaoni? Msifikiri watanzania wengi wana vifaa vya kuingia na kuona matangazo mitandaoni.
Kuna mikoa maskini huko wengi hawana simu wala computer.

Hiyo ya media kutorusha mambo ya chama chenu kwenye media inaweza kuwa hoja yako na mimi naikubali huenda ni vitisho, lakini tujiulize swali.
Hivi kama media flani ina mkataba wa ku-brand chama flani na mgombea wake, na katika Terms za mkataba wao wamekubaliana ili tukupe dau hili basi usitangaze brand ya mpinzani wetu hiyo ni kosa kibiashara?
Ukumbuke media nyingi binafsi zinaendeshwa kibiashara kama biashara zingine. Ni kama vile Emirates wanafadhili Arsenal wanaweka mashariti uwanja wenu na jezi zenu marufuku kuweka au kutangaza wapinzani wetu kama Qatar au KLM, n.k.
Je, utawalaumu Arsenal kwa kutoweka matangazo ya brand hizo zingine uwanjani kwao na kwenye vipindi vya TV zao?

MY TAKE: Kutangazwa na media flani siyo hisani bali ni biashara ambayo lazima uingie gharama kubwa kushinda dau la mshindani wako.
 
Wanakijiji huko siku wakiona vyombo vya ulinzi wafugaji washafanya yao kwenye mashamba na jamaa wanaenda kutuliza halo au wanataka ardhi isiyoendelezwa Kingui polisi wanaenda kuweka mambo shwari.

Siku zingine zote shida zao zote zilizobaki wanazipeleka kwa mwenyekiti wa kijiji, diwani au ofisi ya wilaya ivyo vyombo vya ulinzi wala hawana shughuli navyo na wala awakumbani navyo on daily basis. Na hawa ndio watanzania walio wengi.

Halafu wee uende huko uwaambie story zako sijui hawapo huru chini ya serikali ya sasa polisi wananyanyasa raia (vyombo ambavyo wakiviona sababu ni migogoro walioanzishiana wenyewe) sijui habari za vyombo vya habari kufungiwa; watu ambao wanataka ardhi, maji, umeme, barabara, uwatoe wamang’ati kwenye mashamba yao.

Wakati Magufuli amejiandaa kwenda kutatua changamoto zao za kila siku na nyingi tayari keshazifanyia kazi.

CDM wajiandae wanashindwa huu uchaguzi mchana kweuoe kwa sera zao wenyewe, wasitunge story tu ya kupeleka kwa mabeberu ikifika November.

Sisi tunaishi huku vijijini ndiyo tunafahamu umasikini wa kipato ulivyoongezeka ni kweli vyama vya upinzani vijiji vingine haviko lakini wakifika kufanya kampeni wanachukuwa kura zote watu wamechoka na huu utawala hakuna mfano tusubiri kampeni zianze ndo ukweli utajulikana wazi huu ndo mwisho wa CCM watu wana maisha magumu hakuna mfano. Ukiongea na wananchi wa kawaida wamekata tamaa kabisa ya kuishi sasa hivi sababu ya ugumu wa maisha.
 
Back
Top Bottom