SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Hili ni jambo la kusikitisha sana na najua wanayanga wengi limewafedhehesha.
ASAS Djibouti au kwa jina lingine "AS Ali Sabieh" ni timu ambayo msimu uliopita ilimaliza nafasi ya pili katika ligi ndogo na dhaifu ya Djibouti lakini jana imeisumbua sana Yanga. Ingekuwa na mshambuliaji mmoja wa kati mzuri, kuna watu jana wangelia.
ASAS pia walinyimwa penati ya wazi baada ya Diara kupigwa chenga akaamua kumsukumia mbali mshambuliaji wa ASAS tena mbele ya refa. Yule jamaa anayeripoti matukio ya mpira na kupeleka UN na Interpol asilisahau na hili tukio.
Kwa kumalizia Yanga isiseme ilikuwa ugenini wakati tiketi za mechi iliuza yenyewe na hata bei ya tiketi inaonyesha ilipangwa na Yanga, umbali kutoka Chamazi hadi Kimbiji ni mfupi kuliko wao kutoka Chamazi kurudi kwao. Pia sitashangaa kama hata malazi mliwapa nyie. Najua mechi ya pili mtajipigia tu hao wasomali ila round ijayo hamtoboi.
ASAS Djibouti au kwa jina lingine "AS Ali Sabieh" ni timu ambayo msimu uliopita ilimaliza nafasi ya pili katika ligi ndogo na dhaifu ya Djibouti lakini jana imeisumbua sana Yanga. Ingekuwa na mshambuliaji mmoja wa kati mzuri, kuna watu jana wangelia.
ASAS pia walinyimwa penati ya wazi baada ya Diara kupigwa chenga akaamua kumsukumia mbali mshambuliaji wa ASAS tena mbele ya refa. Yule jamaa anayeripoti matukio ya mpira na kupeleka UN na Interpol asilisahau na hili tukio.
Kwa kumalizia Yanga isiseme ilikuwa ugenini wakati tiketi za mechi iliuza yenyewe na hata bei ya tiketi inaonyesha ilipangwa na Yanga, umbali kutoka Chamazi hadi Kimbiji ni mfupi kuliko wao kutoka Chamazi kurudi kwao. Pia sitashangaa kama hata malazi mliwapa nyie. Najua mechi ya pili mtajipigia tu hao wasomali ila round ijayo hamtoboi.