Kwani feitoto hajafuata mkataba?
Mkataba umeweka vigezo vya kuuvunja ni fei kulipa million 100 na mshahara wa miezi mitatu
Kuna utaratibu gani tena?
Hujauona mkataba wa Fei waliuweka humu jf Wewe ulikuwa Bado unanyonya!
Mkataba niliusoma humu JF ni very tight na umefungwa na kufuli la Solex na key iko Jangwani , yaani kwa Fei Mwenye elimu ya Madrasa Jambiani na elimu ya msingi Mfereji wa Wima primary mara Sijui form four Mchambawima skuli basi alisaini bila kuuelewa kama stori ya Chief Mangungo au sisi wabongo tunaotekeleza siasa ya ujamaa bila kuifahamu kuwa it is something Utopian , bullshit, bogus and unrealistic!
Mkataba unasema Feitoto anatakiwa akishalipa hizo pesa 100m za usajili na mishahara 3 kisha ataje na sababu "za maana" za kuvunja mkataba km kutopangwa, kutotibiwa, kutolipwa , sababu ambazo kiukweli Hana hata moja na hakutaja na mkataba unasema Yanga Wana haki kisheria ya kuzikubali au kuzikataa sababu za Fei-kubwa maana dogo keshaota mapembe ATI. Yaani hata angetaja sababu za kutoka mbinguni Yanga bado wangesema "Si za maana" na wangetoa sababu zingine na wangeshinda kesi , Fei ni Mtoto mdogo asie na elimu ya sheria msaidieni kwa kumwambia awalete warubuni wake Mezani walipe hiyo bei ya kumuuza ni 1B wasepe nae kwa Mpalanger, Fei na wachezaji wengine wanapaswa kujua uhuni Huwa Hauna nafasi mbele ya sheria!
Wanayanga ni vizuri tutajiwe aliempa Feitoto Ile milioni 100 ni haki yetu wanautopolo kumjua in exchange with our paying members subscription fee and coming to support our team pale Chamazi. Kuna mganga Pemba wa kushughulikia vivuruge hawa.
Hivi Utopoloni kuchukua makombe yote miaka miwili mfululizo na kupiga BOLI la kideoni kuzidi hata Brazil mbona Makolo inawauma sana yani imewashinda kabisa kumeza hawatulii hawapoi Kila kukicha wanafanya njama za kuibomoa Yanga. Kwa Dickson Job wamefeli, Mayele wamegonga mwamba basi walipomrubuni Fei maana ni Mtoto walirukaruka wakijua wameimaliza Yanga mara kaletwa Mudathir na Musonda Ngoma Inogile!
Yanga bin Utopoloni tunapanda juu kileleni mara paaap tunapishana na Simba bin Mikia aka Zuwena wanashuka chini , Utopoloni tunasalimia Makolo nayo hata kupokea salamu tu hayataki! Mikia mtakufa Bure na presha za kujitakia , kubalini tu this is Utopolo Era wengine Wote mnatusindikiza na kutupepea.
Fei katuparura nasi twamparura, jino kwa jino!!