Yanga SC Inawachezaji wengi wanaotoka kwenye mataifa makubwa kimpira. Ndio maana hawaitwi katika timu zao za taifa

Yanga SC Inawachezaji wengi wanaotoka kwenye mataifa makubwa kimpira. Ndio maana hawaitwi katika timu zao za taifa

Naona umetuwekea kinyesi kwenye hotpot halafu unasema karibuni pilau
Na ulivyokuwa Inteligent ukafunua na hotpot lenyewe na hata Ukanusa kilichomo na ukagundua kuwa ni Kinyesi.

Kwanini hukuamini macho yako?
 
Hivi Kama wewe ungekua Kocha wa Congo ungemwita Moloco ukawaacha Wachezaji wanacheza Belgium, France ama England!?

Kinachofanywa Morisson asiitwe Ghana, ni hicho hicho kina apply kwa DR CONGO.
Wachambuzi wa kibongo wanaipongeza Simba SC kwa kutoa mcheza ambaye ameitwa Timu ya Taifa ya Rwanda & Malawi. 😂
 
Kuna Mjadara Unzazungumzwa Sana Pasi na Kuangaliwa na Kutazamwa Kwa Jicho la Ziada.

Suala la Idadi kubwa ya wachezaji wa Simba SC kuitwa kwenye Timu za Taifa.

Kiufupi iko hivi:-
Dar es Salaam Young Africans SC Ina Idadi Kubwa ya wachezaji wanaotokea katika Mataifa yaliyopiga hatua kubwa sana kimpira ukilinganisha Simba SC. Idadi kubwa ya wachezaji ya kigeni walioko Simba SC wanatokea katika mataifa yasiyo juu katika viwango vya soka. Hali inayopelekea kupata nafasi katika timu zao kwa sababu ya kutokuwapo na ushindani wa namba na wachezaji wanao cheza nje ya Bara la Africa.

Jangwani:-

Mabingwa wa Kihistoria wana wachezaji kutoka Mataifa tofauti manne (4) ambayo kati ya hayo manne ni matatu (3) tu ambayo ni mataifa yaliyoendelea kisoka na yana historia yao katika mpira wa kiafrika. Yanga wana mchezaji mmoja tu kutoka kwenye taifa lenye kiwango cha wastani Kimpira.
1. DR Congo - Wengine 9
2. Mali - Djigui Diarra
3. Burkina Faso - Yacouba Sogne
4. Uganda - Khalid Aucho

Hayo mataifa ambayo nimeyawekea rangi nyekundu ni mataifa Makubwa kimpira. Ukiingia na kuanza kufanya tathmini ya vikosi vyao utagundua wachezaji wengi wanatokea katika Ligi Maarufu barani Ulaya.
Je ni mchezaji gani wa kigeni kutoka Simba SC ambaye angeweza kupata nafasi katika timu ya Taifa ya Congo, Mali au Burkinabe?

Yanga ina jumla ya wachezaji 11 ambao hawana uhakika na matarajio makubwa ya kuitwa kwenye mataifa yao Ukiachana na Khalid Aucho ambaye panga pangua ni lazima aanze kwenye kikosi cha timu ya taifa cha Uganda kutokana na ukweli kuwa hakuna mchezaji wa Calibre yake anayeweza kumfikia uwezo.

Msimbazi:-

Simba SC ina wachezaji kutoka Mataifa tofauti manne (10) ambayo kati ya hayo manne ni matatu (5) tu ambayo ni mataifa yaliyoendelea kisoka na yana historia yao katika mpira wa kiafrika. Kati ya wachezaji 12 wa kigeni Simba SC wana wachezaji (6) tu kutoka kwenye mataifa yenye viwango cha wastani Kimpira.

Je katika mazingira kama haya Simba SC inashindwaje kupeleka wachezaji wengi wa kimataifa kwenye Timu zao za Taifa? Kumbuka kuwa Yanga SC ina mchezaji mmoja tu kutoka taifa lenye rank ya wastani kimpira wakati huo huo Simba ina wachezaji sita kutoka taifa lenye rank ya wastani kimpira.

1. Malawi -2
2. Zambia - 1
3. Rwanda - 1
4. Kenya - 1
5. Uganda - 1
6. DR Congo - 2
7. Ghana - 1
8. Ivory Coast - 1
9. Senegal - 1
10. Mali - 1

Je Simba SC ingekuwa na wachezaji 11 kutoka mataifa ya Congo DR, Mali & Burkina Faso - ni wangapi wangepata kuitwa katika timu zao za Taifa?
Hawatakuelewa humu hata kidogo japo ndo ukweli wenyewe.
 
Tukitumia mizania ya namba.

Asilimia ipi ya uwezekano wa takribani wachezaji 9 wa kikongo walioko Yanga kuitwa ukilinganisha na mchezaji 1 aliyeko Simba?

Tusisahau hata Tonombe aliitwa May 2021.
Unatumia takwimu za May au October ?
 
Ogopa matapeli Inonga yupo Bunju huko kwenye mazoezi, Angekuwa kaitwa angekuwa Congo huko now
 
sasa ndo wakongo wote mlionao asiitwe hata moja ?
Hilo sio jambo la kushangaza mkuu, Timu ya pili kwa ubora Congo As vita haina mchezaji hata mmoja timu ya Taifa, na hiyo Tp mazembe imetoa wachezaji 3 tu na hakuna hata mmoja ataweza ku feature kwenye first eleven
 
Bla bla nyingi halafu wachezaji wote wa kigeni hamna hata moja aliyeitwa timu ya taifa ,Utopolo ni Utopolo tu
Khalid Aucho
Djigui Diaara
Yacouba Sogne
Saido Ntibanzonkiza
 
Ebu ngoja hapo hapo pa aucho, huyo kibopa amepaishwa sana humu na ana record mbaya sana huko national team. Na hata angepata nafasi basi angeenda kuandika record mbovu nyingine

Na wala sio mara yake ya kwanza kua excluded kwenye squad
 
Mechezaji gani wa Simba wa Kikongo ameitwa timu ya Taifa ya Kongo?
Orodha ya wachezaji walio itwa Kongo.
1. Mandanda Parfait
2. Kiassumbwa Joël
3. Mpasi Nzau Lionel
4. Lomboto Hervé
5. Ngonda Muzinga
6. Mbemba Chancel
7. Nathan Idumba
8. Zola Arsène
9. Kayembe Edo
10. Okita Jonathan
11. Muleka Jackson
12. Moutoussamy Samuel
13. Akolo Chadrac
14. Dieumerci Mbokani
15. Ben Malango
16. Cédric Bakambu
17. Samuel Bastien
1. Nsakala Fabrice
2. Luyidama Christian
3. Mukoko Amale
4. Ngoma Fabrice

Tusisahau hata Tonombe aliwahi kuitwa May 2021.
Hapo kuna mchezaji 1 tu wa Tp mazembe ambaye ni Arsene Zolla ila As vita hakuna player hata mmoja, halafu ndo uje uulize wachezaji wa kutoka simba na Yanga kutoka congo yenye player kibao wanacheza Ufaransa na Ubelgiji
 
Bla bla nyingi halafu wachezaji wote wa kigeni hamna hata moja aliyeitwa timu ya taifa ,Utopolo ni Utopolo tu
Swali ni hili...

Je kuna mchezaji yeyote kutoka Simba SC angepata hata kuitwa timu ya Taifa kama angekuwa Mkongo, M'bukina Faso au M'mali? Yanga ina wachezaji takriban 1O kutoka mataifa hayo bora kisoka barani Afrika.

Ukishindwa kulielewa swali nijuze nikufafanulie zaidi.
 
Ebu ngoja hapo hapo pa aucho, huyo kibopa amepaishwa sana humu na ana record mbaya sana huko national team. Na hata angepata nafasi basi angeenda kuandika record mbovu nyingine

Na wala sio mara yake ya kwanza kua excluded kwenye squad
Broo, it seems u know nothing about football nowadays

Khalid Aucho kapewa Ucaptain jana wa timu taifa baada ya Okwi kutoitwa timu ya taifa coz now mwamba hana timu anayo chezea kwahyo level yake ya competition ni ndogo
 
Kwa hiyo yanga haijapeleka mchezaji hata mmoja national team ukiachana na wachezaji wa hapa ndani?
 
Back
Top Bottom