Abuu Kauthar
JF-Expert Member
- Jul 10, 2011
- 4,296
- 6,492
Mimi ni shabiki wa yanga. Ila nakataa kwamba yanga bado hatujafikia stage ya kutwaa ubingwa wa champions league. Sisi tuwaze nusu kwanza.
Mamelodi sundowns wametengeneza kikosi cha zaidi ya bilioni 90. Wamenunua wachezaji mpaka south america wa bilioni 6. Ila bado anafeli kubeba Caf champions league kila msimu.
Kutwaa ligi ya mabingwa africa sio kazi nyepesi.
Timu pekee yenye uhakika kutwaa hilo kombe kwa urahisi ni Al ahly peke yake ( kama Real madrid anavyobeba uefa kwa urahisi )
Wengine wote huwa wanalibeba kwa mbinde sana.
Yanga kwanza afike nusu fainali.. kabla hajawaza kubeba kombe
Kuna timu kama Esperence, Raja Casablanca, hizo timu hata zikicheza hovyo hovyo tu kipuuzi huwa hazitolewi na timu level ya yanga.
Muulize mamelodi sundowns ama Petro Luanda shughuli ya kuvuka nusu fainali ilivyo ngumu.
Yanga malengo ya msimu huu ni robo fainali, msimu uliopita ilikuwa makundi