Yanga yaipeleka ligi kuu Tanzania Top Ten Africa

technically

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2016
Posts
12,706
Reaction score
52,355
Baada ya ushindi wa Jumatano kwa kasi sana Yanga imetoka nafasi ya 75 mpaka nafasi ya 46 Afrika na kuifanya Ligi ya Tanzania kutoka nafasi ya 11 mpaka nafasi ya 9.

Haya ni mafanikio ya Yanga wachambuzi uchwara hawasemi mpaka Sasa wapo kimya Ila Yanga ikifungwa tu kelele zinaanza.

Yanga ndio habari ya mjini nimetazama wiki hii vyombo vya habari vya waarabu kule Egypt, Morocco,Algeria na Tunisia Wana discuss Yanga .

Na kutoa tahadhari kwa timu ambazo bado zipo shirikisho kutoka kwenye nchi zao huenda zikakumbana na alichokumbana nacho Club Africain
 
🤔🤔🤔🤔🤔 kuna ukweli nauona katika hii post
 
Source please
 
Hili ni jambo jema sana kwenye ukuaji wa soka la Tanzania. Ila nina uhakika 98% ya wapenzi wa Yanga walikuwa wanajua Yanga angefungwa kule Tunisia. Lakini kwa ushindi ule kwa sasa wanajiamini sana na kwamba timu yao inaweza kumfunga yeyote mahali popote. Hakuna cha home au away. Ukiwa na timu nzuri lazima Mwananchi uvimbe. Huu ni wakati wenu wa kutamba sasa.
Hongereni sana watani wetu wa jadi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…