Yanga yupo kwenye kundi gumu ila fixture inaweza kumbeba

Yanga yupo kwenye kundi gumu ila fixture inaweza kumbeba

vibertz

JF-Expert Member
Joined
Mar 15, 2022
Posts
2,474
Reaction score
4,726
Jana Yanga wamepoteza dhidi ya Belouizdad kwa kufungwa goli tatu kwa bila. Kimpira, Yanga alicheza soka safi sana na walikuwa wanapiga mipira ya kasi sana ila safu ya ulinzi ikawa inajisahau sana kurudi, magoli wamefungwa ya counter attacks nadhani ni somo kwao ni vitu vidogo sana vilivyowangusha.

Kuna watu wamewachukulia poa Belouizdad ila kama timu ya wazee wangecheza na hawa jamaa pengine ingejirudia ya zama za magoli matano. Jamaa wanajua kuzitumia nafasi chache wanazozipata. Ili Yanga aweze kufuzu ni lazima, tena lazima apate alama tatu dhidi ya Al Ahly kwa Mkapa.

Kwanini fixture ipo upande wa Yanga?
Yanga atacheza mechi yake ya pili dhidi ya Al Ahly, kama atashinda atakuwa na point 3.Mechi mbili zinafuata zote ni dhidi ya Medeama, hapo inatakiwa Yanga apate point zote sita kwa Medeama. Ili imfanye kufikisha point 9 huku akibakisha michezo miwili (mmoja home na mmoja away).

Kwenye michuano ya klabu huwa mara nyingi sana timu zilizopo pot 3 zinasonga mbele hatua inayofuata kwasababu mpangilio wa mechi zinawabeba sana.
 
Jana Yanga wamepoteza dhidi ya Belouizdad kwa kufungwa goli tatu kwa bila. Kimpira, Yanga alicheza soka safi sana na walikuwa wanapiga mipira ya kasi sana ila safu ya ulinzi ikawa inajisahau sana kurudi, magoli wamefungwa ya counter
Walisema jipeni moyo Leo ndo umejua kundi gumu mlikuwa mnatamba eti Al Ahly atapigwa nje ndani ,hii ndo Champions league siyo lile kombe la losers
 
1700885218475.jpg
hizo habari za kuanza kuandika mlicheza mpira wa kasi sijui nini ni kelele tuu, mmepigwa subirini vipigo vingine
 
Yanga Champions league bado mwaka jana alipata bahati ya kucheza na timu nyingi zilizokuwa hazina ubora mechi inayo fuata atapigwa na Al Ahyl na kinachomuangusha Yanga anacheza bila malengo wakati hii ni Champions League ligi ya kikubwa asipokuwa makini mechi ijayo ndio inaweza kumaliza kundi mapema maaana Al Ahyl anaweza shinda na Wababe wa Uto wanaweza shinda shughuli ikaisha hapo walivyokuwa wanaona Simba anaishia robo wakazani ni rahisi na bado mtapigwa sana Champions league unaenda ugenini kucheza na timu za warabu huku unajishaua badala ya kucheza kwa malengo unawachukulia poa watakukanda sana usipobadilika kima wee
 
Utopwingo aka Kujifariji FC mna nini? Eti Counter attack! Mlitegemea kabisaa mumfunge mwarabu kindezi? thubutuuu.


Tar 2/12 tuwaone tena!
 
Mlisema Simba inaishia robo na mkaibatiza mwakarobo kwenye Klabu Bingwa
Sasa ninyi Uto nendeni hadi fainali kama Shirikisho,maana mmezoe kukariri.
Nawashauri:Uto ijikaze la sivyo itaishia ilipoanzia.
 
Yanga Champions league bado mwaka jana alipata bahati ya kucheza na timu nyingi zilizokuwa hazina ubora mechi inayo fuata atapigwa na Al Ahyl na kinachomuangusha Yanga anacheza bila malengo wakati hii ni Champions League ligi ya kikubwa asipokuwa makini mechi ijayo ndio inaweza kumaliza kundi mapema maaana Al Ahyl anaweza shinda na Wababe wa Uto wanaweza shinda shughuli ikaisha hapo walivyokuwa wanaona Simba anaishia robo wakazani ni rahisi na bado mtapigwa sana Champions league unaenda ugenini kucheza na timu za warabu huku unajishaua badala ya kucheza kwa malengo unawachukulia poa watakukanda sana usipobadilika kima wee

Hiyo Al Ahly wangeomba kwa CAF ibadilishwe icheze na Simba maana Simba ndiyo wanawamudu Al Ahly ndani nje. Kwa Yanga ni kinyume, itakuwa mvua ya magoli ndani nje!
Kifupi tu niseme ‘asanteni utopolo kwa kushiriki’ CAF 2023/24
 
Mwisho wa siku ni matokeo ya mwisho ndiyo kipimo cha kucheza vizuri au vibaya!

Hii michuano matokeo ya nyumbani ndiyo kila kitu,wakaze tu viuno kwa Mkapa.
 
Back
Top Bottom