Yaya Toure akosoa uwepo wa Fainali 2 kwenye Michuano ya Afrika

Yaya Toure akosoa uwepo wa Fainali 2 kwenye Michuano ya Afrika

Smart codetz

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2023
Posts
218
Reaction score
875
C8FCADE4-07BF-4A8B-8EFC-D892C9F6C01A.jpeg


Ujumbe wa nyota wa zamani wa Barcelona na Man City, Yaya TOURE juu ya uwepo wa fainali mbili kwenye michuano ya Afrika.

Wakati umefika kwa mashabiki wa soka wa nchi zetu barani Afrika kudai HAKI YA MICHEZO kwa kuitaka CAF kuwa na mechi moja pekee ya fainali kwenye uwanja wa usiofungamana na upande wowote (neutral) au fainali mbili kwenye Uwanja wa neutral.

Ni aibu kwa bara letu kuona unyonge wa mchezo bora pendwa wa fainali ya soka duniani (ukitazamwa na mamilioni ya watu duniani) kushuhudia udhalilishaji wa timu ya ugenini kukumbana na mashambulizi ya kuvizia kwa fataki nyakati za usiku wakiwa wamepumzika katika uwanja wao wakiwa hotelini.

Kana kwamba haitoshi, wakati wa mchezo tulishuhudia (vijana waokota mipira (ball boys) wakirusha mipira mingi kwa wakati mmoja ili kupoteza muda kwa ajili ya timu za nyumbani, zaidi ya fataki mbili nzito zilipigwa kiasi cha kupelekea mechi kusimamishwa (mara tatu) ili kuruhusu moshi huo kutoweka, yote haya yalifanywa mbele ya rais wa CAF na ulimwengu mzima wa mashabiki wa soka wakitazama.

Hii sio mara ya kwanza barani Afrika Basi aibu kwenu CAF & FIFA kwa kujua haya yote yatatokea na bila kufanya lolote ila kukaa tu na kutazama onyesho la kupendeza la uharamu na kumtawaza mpiga picha na kombe la ubingwa akiota na kufikiria kuwa hii ingekoma?

Natumai FIFA ingefanya soka kuwa mchezo mzuri tena.

9875C8CE-6556-4151-9244-70F81035ECE4.jpeg
 
Motsepe aliwai kuifafanua hii kwamba ikiwa final mechi moja itapigwa uwanja wa neutral mashabiki wengi awana msuli wa pesa,Africa njaa waya mkali mashabiki watashindwa gharama za kukwea pipa,gharama za hoteli n,k

mfano final iwe Yanga Vs Usm Alger alafu mbungi ikapigwe Lagos mashabiki wangapi wataenda Lagos Nigeria kucheki game!
 
Picha linaanza muda wa nyongeza ni dakika 6 wakati mpira ulisimama zaidi ya hizo dakika.
Picha lilianza kwa kuweka watu wa VAR wote wanatokea Misri. Nakumbuka kucomment mechi ilipokuwa inaanza kuwa Yanga kazi wanayo.

Kawaida huwa wanachanganya watu kutoka maeneo tofauti. Ndiyo maana ukaona mara VAR haifanyi kazi, mara imerudi hewani. Ila kimaamuzi refa jana alikuwa fair sana.
 
Picha lilianza kwa kuweka watu wa VAR wote wanatokea Misri. Nakumbuka kucomment mechi ilipokuwa inaanza kuwa Yanga kazi wanayo. Kawaida huwa wanachanganya watu kutoka maeneo tofauti. Ndiyo maana ukaona mara VAR haifanyi kazi, mara imerudi hewani. Ila kimaamuzi refa jana alikuwa fair sana.
Refa alikuwa very fair ila ile additional time hapana kabisa ni ya mchongo. Mpira ulisimama sana haikustahili kuwa dakika 6 tu.
 
Refa alikuwa very fair ila ile additional time hapana kabisa ni ya mchongo. Mpira ulisimama sana haikustahili kuwa dakika 6 tu.
Lakini mpira ilisimama vipindi vyote viwili. Ulivyosimama kipindi cha kwanza, muda uliopotea ulifidiwa kabla ya mapumziko. Dakika 5 sijui 6 zilizoongezwa kipindi cha pili ni fair kwa muda uliopotea kipindi cha pili kwa sababu nadhani haukusimama kwa zaidi ya dakika 2. Kama unashindwa kufunga kwa dakika 90 toka goli la kwanza, kulilia dakika 3 za nyongeza ni kutafuta kisingizio tu.

Kawaida mashindano haya, tegemea timu ya nyumbani kupata favour fulani. Hata Yanga game ya kwanza alipewa dakika 10 za nyongeza. Je alistahili? Na hili nililisema mapema msitegemee nyongeza za namna hiyo kule nikaonekana sina akili.
 
Lakini mpira ilisimama vipindi vyote viwili. Ulivyosimama kipindi cha kwanza, muda uliopotea ulifidiwa kabla ya mapumziko. Dakika 5 sijui 6 zilizoongezwa kipindi cha pili...
unasema kama umeshindwa kufunga dakika 90 tatu ndio utaweza? Ka angalie mechi ya KRC Genk Vs Royal Antwerp uone dakika 1 tu imenyima watu ubingwa, Real Madrid Vs Atletico Madrid final UCL, Manchester United Vs Bayern Munich UCL, kwenye mpira dakika moja ni kubwa sana na ina badili kila kitu
 
Back
Top Bottom