Yesu alikuwa mfanyabiashara, Mohammed alikuwa mfanyabiashara: Kwanini wafanyabiashara wakristo na waislam wengi sio waaminifu?

Yesu alikuwa mfanyabiashara, Mohammed alikuwa mfanyabiashara: Kwanini wafanyabiashara wakristo na waislam wengi sio waaminifu?

Umeanza kufeli kwa kututapeli Yesu alikuwa mfanyabiashara. Utakuwa mfanyabiashara mmojawapo kati ya wanaolalamikiwa na wewe. Anza kwanza kuwa mwaminifu na unayosema na kuandika kwanza...

Mathayo 8:18-20
"Naye Yesu alipoona makutano mengi wakimzunguka, aliamuru kuvuka kwenda ng’ambo. Mwandishi mmoja akamwendea, akamwambia, Mwalimu, nitakufuata ko kote uendako. Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake"
Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake"

Hapa Yesu alimaanisha nini?
 
Tujadili kidogo.

Wafanyabiashara wengi Kama sio waislam ni wakristo.

Lakini wengi sio waaminifu. Wanatumia juju na uchawi, wanaforce kupata faida isivyo halali, kukwepa Kodi na kukwepa taratibu rasmi

TATIZO linatoka wapi ikiwa Yesu alikuwa mfanyabiashara wa samani(furniture) lakini hakutenda dhambi?

Marko 6:3
[3]Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake.
Is not this the carpenter, the son of Mary, the brother of James, and Joses, and of Juda, and Simon? and are not his sisters here with us? And they were offended at him.

Mtume Mohammad SAW alikuwa mfanyabiashara muaminifu Sana chini ya Khadija. Akifanya Biashara Kati ya saudia na Syria. Alikuwa amenyooka.

Tunafeli wapi wakuu.

Karibuni
Ukumbuke mtume aliashinza kikundi cha maharamia wakaanza kuwaibia watu wa Makka wakina Faisal
 
Naona watu bado wanaendelea kukaza mafuvu kwa mada rahisi kama hii.

Kwani kufanya kazi au kufanya biashara ni dhambi hadi mmushambulie mleta mada kiasi hicho?

Baba wa imani Ibrahim mbona alikuwa mfugaji na mkulima mkubwa sana alie ajiri mamia ya wafanya kazi, kwahiyo nae akija mtu hapa kutaka tuwe kama alivyokuwa Ibrahim kwenye kazi zake napo tutamshambulia?

Mbona hata Mungu ameweka clear kabisa kuhusu mwanadamu kufanya kazi, kipi kigumu kwenu kueleweka? Hebu tuanze kuona maagizo ya mwanzo kabisa ya Mungu kwa mwanadamu ambae ni Adam yalikuwa ni yapi;
●Adam alipoumbwa aliambiwa ailime bustani na kuitunza, amri ya nne inasema Siku sita FANYA KAZI, na siku ya saba pumzika. Je kama kufanya kazi halali ni dhihaka (kwa mjibu wenu) kwahiyo hiyo amri ya Mungu nayo ni dhihaka?

Tuje kwenye injili ya Paul kuhusu kufanya kazi alisema je?
●Mwishoni katika 3:6-15 Paulo anawahimiza watu waendelee na kazi zao katika jumuiya. Maneno ya Paulo “Asiyefanya kazi, asile” (3:10) yanamtahadharisha msomaji asikubali kupotoshwa na mawazo yanayochanganya imani na fikira zisizo sawa za kutowajibika.

Haya sasa naomba mrudi kwenye maana halisi ya mada, kwanini katika kazi zenu na biashara zenu zimejaa skendo na makando kando mengi licha ya kuwa wafuasi wazuri wa Adam(mkulima na mtunza bustan ya eden), Ibrahim (Mkulima na mfugaji mkubwa), Yesu Mwana wa Adam(Seremala kwa mjibu wa Mk 6:3 SUV)Mtume Muhammad (mfanya biashara wa masafa marefu kwa mjibu wa hadithi mbalia mbali).
 
Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake"

Hapa Yesu alimaanisha nini?
Jamaa haelewi.
Yesu aliulizwa na wanafunzi wa Yohana anaishi wapi?
Wanafunzi akawaambia nifuateni. Walipofika hawakuwahi kurudi Tena kwa Yohana

Yesu alikuwa na makazi Bora , sema alitaka Kuna kwenye reli huyo mjinga
 
Naona watu bado wanaendelea kukaza mafuvu kwa mada rahisi kama hii.

Kwani kufanya kazi au kufanya biashara ni dhambi hadi mmushambulie mleta mada kiasi hicho?

Baba wa imani Ibrahim mbona alikuwa mfugaji na mkulima mkubwa sana alie ajiri mamia ya wafanya kazi, kwahiyo nae akija mtu hapa kutaka tuwe kama alivyokuwa Ibrahim kwenye kazi zake napo tutamshambulia?

Mbona hata Mungu ameweka clear kabisa kuhusu mwanadamu kufanya kazi, kipi kigumu kwenu kueleweka? Hebu tuanze kuona maagizo ya mwanzo kabisa ya Mungu kwa mwanadamu ambae ni Adam yalikuwa ni yapi;
●Adam alipoumbwa aliambiwa ailime bustani na kuitunza, amri ya nne inasema Siku sita FANYA KAZI, na siku ya saba pumzika. Je kama kufanya kazi halali ni dhihaka (kwa mjibu wenu) kwahiyo hiyo amri ya Mungu nayo ni dhihaka?

Tuje kwenye injili ya Paul kuhusu kufanya kazi alisema je?
●Mwishoni katika 3:6-15 Paulo anawahimiza watu waendelee na kazi zao katika jumuiya. Maneno ya Paulo “Asiyefanya kazi, asile” (3:10) yanamtahadharisha msomaji asikubali kupotoshwa na mawazo yanayochanganya imani na fikira zisizo sawa za kutowajibika.

Haya sasa naomba mrudi kwenye maana halisi ya mada, kwanini katika kazi zenu na biashara zenu zimejaa skendo na makando kando mengi licha ya kuwa wafuasi wazuri wa Adam(mkulima na mtunza bustan ya eden), Ibrahim (Mkulima na mfugaji mkubwa), Yesu Mwana wa Adam(Seremala kwa mjibu wa Mk 6:3 SUV)Mtume Muhammad (mfanya biashara wa masafa marefu kwa mjibu wa hadithi mbalia mbali).
Mungu akuongezee siku za maisha
 
Yesu kafanya Sana Biashara ya furniture. Maana hata kazi za kiroho alianza akiwa na takribani miaka 27.

Nazareti nzima walimjua Kama fundi. Alikuwa atengenezi vya kutumia. Alikuwa anauza.

Kwa sasa tuseme angekuwa ni wamiliki maduka makubwa ya furniture.
Hebu tuweke sawa hapa. Yesu hakuwa mfanyabiashara, na wala hakuja duniani kwa lengo hilo. Yesu alikuja duniani kwa lengo moja tu, nalo ni ukombozi. Mambo mengine aliyofanya, alifanya kama binadamu anavyofanya shughuli za kila siku, maana alikuja duniani kama binadamu, lakini akiwa na Uungu.

Kuzaliwa katika familia ya Yosefu, ukoo wa Daudi, ilimpasa kufuata mila na desturi za ukoo huo, ikiwa ni pamoja na kushiriki katika shughuli mbalimbali. Baba yake (mrithi) alikuwa seremala, na kama ilivyo ada, mafundi seremala huuza samani wanazotengeneza ili kujipatia kipato. Hivyo, kuna wakati Yosefu alimtuma Yesu kupeleka samani hizo mahali zilipohitajika.

Akiwa katika umri mdogo, Yesu aliishi maisha ya kawaida kama walivyoishi wazazi wake (Yosefu na Maria). Inasemekana, wakati mwingine walikutana na wakati mgumu, hata samani alizotengeneza Yosefu hazikupata wateja na kupelekea kushindwa kununua chakula, hivyo wote kulala njaa. Hivyo, Yesu kama binadamu (maana ni Mungu pia), aliishi kama binadamu wengine.
 
Hebu tuweke sawa hapa. Yesu hakuwa mfanyabiashara, na wala hakuja duniani kwa lengo hilo. Yesu alikuja duniani kwa lengo moja tu, nalo ni ukombozi. Mambo mengine aliyofanya, alifanya kama binadamu anavyofanya shughuli za kila siku, maana alikuja duniani kama binadamu, lakini akiwa na Uungu.

Kuzaliwa katika familia ya Yosefu, ukoo wa Daudi, ilimpasa kufuata mila na desturi za ukoo huo, ikiwa ni pamoja na kushiriki katika shughuli mbalimbali. Baba yake (mrithi) alikuwa seremala, na kama ilivyo ada, mafundi seremala huuza samani wanazotengeneza ili kujipatia kipato. Hivyo, kuna wakati Yosefu alimtuma Yesu kupeleka samani hizo mahali zilipohitajika.

Akiwa katika umri mdogo, Yesu aliishi maisha ya kawaida kama walivyoishi wazazi wake (Yosefu na Maria). Inasemekana, wakati mwingine walikutana na wakati mgumu, hata samani alizotengeneza Yosefu hazikupata wateja na kupelekea kushindwa kununua chakula, hivyo wote kulala njaa. Hivyo, Yesu kama binadamu (maana ni Mungu pia), aliishi kama binadamu wengine.
Kwa nini unadhani wakina Yesu walikuwa ni familia ya kimasikini hivyo hadi Biashara yao iwe ni ya kkungaunga.?


Yesu alikuwa selemala Mwana wa selemala sio saidia fundi Kama unavyomuhafifisha.


Kazi zake hazihafifishi utumishi wake na shughuli yao ya ukombozi
 
Yesu alkua anafanya biashara Gani???
Huyu jamaa ni muongo mpaka anakera. Ilikuwa inatosha tu kusema Mtume Muhammad SAW alikuwa mfanyabiashara.

Hakuwa na ulazima wa kumhusisha Yesu. Kuwa mtoto wa seremala hakumfanyi mtu kuwa mfanyabiashara.

Maana hiyo ilikuwa ni shughuli ya kawaida kabisa (shughuli ya mtu wa kipato cha chini) katika jamii ya wakati huo.
 
Lengo la huu uzi ni lipi? Kila mtu anajadili jambo lake tofauti! Ni mparanganyiko mtupu
 
Huyu jamaa ni muongo mpaka anakera. Ilikuwa inatosha tu kusema Mtume Muhammad SAW alikuwa mfanyabiashara.

Hakuwa na ulazima wa kumhusisha Yesu. Kuwa mtoto wa seremala hakumfanyi mtu kuwa mfanyabiashara.

Maana hiyo ilikuwa ni shughuli ya kawaida kabisa (shughuli ya mtu wa kipato cha chini) katika jamii ya wakati huo.
Unaargue kupitia biblia au Kanisa.?
Yesu alikuwa Selemala. Fungu lipo kwenye Uzi. Yesu akisema fanyeni Biashara hata nitakapokuja. Unataka kupotosha akifanya Biashara duniduni wakati yeye anasisitiza tufanye Mambo makubwa kuliko yeye.?

Acha kumuhafifisha masihi mkuu
 
Lengo la huu uzi ni lipi? Kila mtu anajadili jambo lake tofauti! Ni mparanganyiko mtupu
Kwa nini wafuasi wa viongozi waliowahi kufanya Biashara Biashara zinawashinda au wanakuwa na ujanjaujanja.
Mfano anamuamini mganga ambaye hajawahi kuwa hata na duka la Pemba Ila hamuamini Yesu aliyewahi kufanya Biashara kabla ya utume
 
Kwa nini unadhani wakina Yesu walikuwa ni familia ya kimasikini hivyo hadi Biashara yao iwe ni ya kkungaunga.?


Yesu alikuwa selemala Mwana wa selemala sio saidia fundi Kama unavyomuhafifisha.


Kazi zake hazihafifishi utumishi wake na shughuli yao ya ukombozi
Kwa nini unadhani wakina Yesu walikuwa ni familia ya kimasikini hivyo hadi Biashara yao iwe ni ya kkungaunga.?

Ukiniuliza hivyo mimi nakujibu kuwa huo ulikuwa ni mpango wa Mungu kuhusiana na suala zima la ukombozi. Tunajua ya kuwa hatuwezi kumuona Mungu kwa macho, isipokuwa ni kwa imani tu. Yesu kuja duniani kwa namna hiyo, ilikuwa kupima imani ya binadamu.

Utakumbuka hata mahali alipozaliwa Yesu palikuwa duni, maana tunaambiwa alizaliwa katika zizi la ng'ombe, huko Bethrehem. Hapa ukichunguza, utaona kuwa kuna dhana iliyojificha ili kukamilisha tukio fulani (tuhoji, ni nini?).

Unaweza kuona safari ya ukombozi ya Yesu ilivyopata upinzani mkubwa. Hii ilitokana na Yesu kuzaliwa na kuishi kama binadamu wa kawaida na hivyo watu waliomzunguka kumwona wa kawaida. Watu hawa hawakuamini walipoambiwa kuwa huyo waliyeiashi naye alikuwa mwana wa Mungu.

Hata watu wa nyumbani kwake alikozaliwa hawakuamini kama Yesu alikuwa mwana wa Mungu, kwani walisema, wewe tumekuona umezaliwa hapa, baba yako ni Yosefu fundi seremala na mama ni Maria, leo unatuambiaje ni mwana Mungu? Licha ya kufanya ishara nyingi, lakini walimkatalia. Tunapimwa na kipimo kidogo lakini tunashindwa. Kumbe tunafundishwa tusidharau watu kimuonekano.
 
Kwa nini unadhani wakina Yesu walikuwa ni familia ya kimasikini hivyo hadi Biashara yao iwe ni ya kkungaunga.?

Ukiniuliza hivyo mimi nakujibu kuwa huo ulikuwa ni mpango wa Mungu kuhusiana na suala zima la ukombozi. Tunajua ya kuwa hatuwezi kumuona Mungu kwa macho, isipokuwa ni kwa imani tu. Yesu kuja duniani kwa namna hiyo, ilikuwa kupima imani ya binadamu.

Utakumbuka hata mahali alipozaliwa Yesu palikuwa duni, maana tunaambiwa alizaliwa katika zizi la ng'ombe, huko Bethrehem. Hapa ukichunguza, utaona kuwa kuna dhana iliyojificha ili kukamilisha tukio fulani (tuhoji, ni nini?).

Unaweza kuona safari ya ukombozi ya Yesu ilivyopata upinzani mkubwa. Hii ilitokana na Yesu kuzaliwa na kuishi kama binadamu wa kawaida na hivyo watu waliomzunguka kumwona wa kawaida. Watu hawa hawakuamini walipoambiwa kuwa huyo waliyeiashi naye alikuwa mwana wa Mungu.

Hata watu wa nyumbani kwake alikozaliwa hawakuamini kama Yesu alikuwa mwana wa Mungu, kwani walisema, wewe tumekuona umezaliwa hapa, baba yako ni Yosefu fundi seremala na mama ni Maria, leo unatuambiaje ni mwana Mungu? Licha ya kufanya ishara nyingi, lakini walimkatalia. Tunapimwa na kipimo kidogo lakini tunashindwa. Kumbe tunafundishwa tusidharau watu kimuonekano.
Nikurekebishe kidogo.
Yesu hakuzaliwa zizini mwa ng'ombe kwa sababu hawakuwa na pesa.

Ni kwa sababu Lorge zilikuwa zimejaa. Ni sawa na mtu kulala stand baadae kukosa gesti siku ya mechi ya Simba na Madrid maana wageni wamekuwa wengi alafu useme jamaa no masikini.
 
Unakoswa kuchukua mafungu ya wakati Yesu kaacha active business kahamia kwenye ualimu kada tofauti. Kabadilisha taaluma na hii kaifanya sio zaidi ya miaka mitatu ya maisha yake.
Boss naona unaruka kipengele cha biashara. Hiyo biashara aliianza lini na kuacha lini? Hili swali tu hujanijibu. Mi ukiniletea andiko, hata kama linasema aliuza genge la nyanya sitakataa. Ila leta kwanza andiko la Biblia twende sawa kuwa alikuwa mfanyabiashara was samani!
 
Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota; lakini Mwana wa Adamu hana pa kulaza kichwa chake"

Hapa Yesu alimaanisha nini?
Hakuwa na makazi ya kudumu kama wengine. Alikuwa anatembea na kufundisha, kambi popote!
 
Nikurekebishe kidogo.
Yesu hakuzaliwa zizini mwa ng'ombe kwa sababu hawakuwa na pesa.

Ni kwa sababu Lorge zilikuwa zimejaa. Ni sawa na mtu kulala stand baadae kukosa gesti siku ya mechi ya Simba na Madrid maana wageni wamekuwa wengi alafu useme jamaa no masikini.
Ndugu, usiwe mzito kuelewa. Kwa Mungu hakuna linaloshindikana, kukuta lodge zimejaa, that was a cause to go to the hut, lakini wangeweza kukuta vyumba bado vipo kwenye lodge. Kwa hiyo hapa ilikuwa shabaha ya Mungu itimie!
 
Back
Top Bottom