Yesu ni Mungu. Kwanini alijalibiwa na kiumbe alichokiumba (shetani) Huoni kama alionyesha udhaifu wake?

Yesu ni Mungu. Kwanini alijalibiwa na kiumbe alichokiumba (shetani) Huoni kama alionyesha udhaifu wake?

Nadhani mali zote za thamani zilizopo hapa duniani ni mali ya shetani
Shetani Hana Mali yoyote, ni maskini wa kutupwa, na Mali zake ni za feki na maigizo.

Shetani hakuumba hata jiwe, Yeye ni mwongo na muharibifu tangu mwanzo,

Mali zote ni za Mungu aliyeziumba, akamkabidhi Adam azitawale, shetani akampora Kwa kupitia uongo pale Eden.

Sasa Mungu akashuka katika mwili wa mwanadamu amrudishie Mali zake.
Sasa wote wamwaminio Yesu wamerudishiwa Mali zao, ukitenda dhambi, unampa shetani kibali kuchukua baraka zako Ili awape wanaomwamini akiwaaminisha ni zake kumbe sio.

Shetani ni jizi na baba wa wizi!!

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
 
18 Kiongozi mmoja akamwuliza Yesu, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?”

19 Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mwema? Hakuna mtu aliye mwema ila Mungu peke yake.
Mungu akivaa mwili ni LAZIMA ajishushe, afiche identity yake halisi,

Ungekuwa jasusi ungeelewa kirahisi, mtanzania kwenda kuipelekeza ug huendi na identity Yako halisi, unaenda kificho, likewise Mungu kuja duniani katika mwili wa mwanadamu ni LAZIMA afiche identity yake.

Malaika walimjia Abraham kama WANADAMU na hawakujutambulisha kuwa ni Malaika,

Mapepo na majini yajapo katika miili ya WANADAMU huja kificho sababu Dunia alikabidhiwa mwanadamu aitawale.

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
 
Shetani Hana Mali yoyote, ni maskini wa kutupwa, na Mali zake ni za feki na maigizo.

Shetani hakuumba hata jiwe, Yeye ni mwongo na muharibifu tangu mwanzo,

Mali zote ni za Mungu aliyeziumba, akamkabidhi Adam azitawale, shetani akampora Kwa kupitia uongo pale Eden.

Sasa Mungu akashuka katika mwili wa mwanadamu amrudishie Mali zake.
Sasa wote wamwaminio Yesu wamerudishiwa Mali zao, ukitenda dhambi, unampa shetani kibali kuchukua baraka zako Ili awape wanaomwamini akiwaaminisha ni zake kumbe sio.

Shetani ni jizi na baba wa wizi!!

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
Kwahiyo yesu ni Mungu tena

Tambua mimi sio muislam wala mkristo
 
(Yeremia 22:5)

Naapa Kwa NAFSI yangu asema BWANA.

Wanaosema Mungu ana NAFSI tatu hawana support ya maandiko.

Mungu ni MMOJA,

Ndiye Mungu BABA akiwa KITI Cha Enzi,

Ni Mungu Mwana alipokuwa duniani katika mwili Kwa KAZI ya kumuokoa mwanadamu. Na ndiye huyo huyo aliyeumba Ulimwengu akitambulika kama " NENO / Logos.

Ni Mungu huyo huyo Roho mtakatifu akaae ndani ya wote wamwaminio.

Mungu ni MMOJA NAFSI Moja,anatambulika Kwa Majina tofauti kulingana na KAZI na majukumu kiofisi,

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
Ok
 
Wakati YESU anajaribiwa na Shetani,alikua ni Binadamu wa kawaida kama wewe asiyekua na Uungu.
 
Kwahiyo yesu ni Mungu tena

Tambua mimi sio muislam wala mkristo
Ndio Yesu ni Mungu aliyeumba mbingu na Nchi aliyekuja duniani katika mwili wa mwanadamu kijasusi Kwa mission maalum ya kumwokoa mwanadamu, na kumrudishia mwanadamu utawala wa vyote vilivyoko duniani ambavyo aliporwa na shetani.

Ikiwa hujui Yesu ni Mungu aje, soma Kuzaliwa kwake,

Bikra alichukua mimba Kwa uwezo wa Roho mtakatifu, ndipo ujue Yesu Hana baba Wala mama.

Ndiye Mungu baba,

Ndiye Mungu Mwana,

Tena ndiye huyo huyo Mungu Roho mtakatifu.

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
 
Ndio Yesu ni Mungu aliyeumba mbingu na Nchi aliyekuja duniani katika mwili wa mwanadamu kijasusi Kwa mission maalum ya kumwokoa mwanadamu, na kumrudishia mwanadamu utawala wa vyote vilivyoko duniani ambavyo aliporwa na shetani.

Ikiwa hujui Yesu ni Mungu aje, soma Kuzaliwa kwake,

Bikra alichukua mimba Kwa uwezo wa Roho mtakatifu, ndipo ujue Yesu Hana baba Wala mama.

Ndiye Mungu baba,

Ndiye Mungu Mwana,

Tena ndiye huyo huyo Mungu Roho mtakatifu.

Mungu ni MMOJA na YESU KRISTO/YESHUA HAMASHIACH ndilo JINA lake. Amen
Sawa asante sana kwa neno
 
Upuuzi mtupu


Unaleta maneno ya kupambiza tu mara kijasusi,mission maalumu

Kama yesu mwenyewe anakataa kuitwa mwema anasema mungu pekee ndo anastahili kuitwa mwema, halafu wew wasema yesu ni mungu ??
Yesu anaenda kusali muda mfupi tu kabla ya kifo, alikua anasali kwa nani?

Malaika wanashuka kuja kumfariji, saa ilipofika ya kuuwawa,mungu gani anafarijiwa na malaika wake?

Anajaribiwa na ibilisi ,yesu anamjibu shetani mungu ndo hupaswa kuabudiwa, yaani yesu anasema mungu tu ndo nitakaemwinamia !
 
1.Kama wewe ni mwana wa Mungu geuza jiwe kuwa mkate
2. Ukinisujudia nitakupa mali zote za ulimwengu

Mali zote ni za Mungu kwani Shetani ampe Mungu ahadi na masharti yote hayo?
Hapo hapo unasema kama wewe ni mwana wa Mungu
 
Majaribu yaliwekwa ili kuona kama mwana wa MUNGU (YESU) Imani yake Iko thabiti akiwa katika umbile la kibinadamu na ili kuwatengenezea wanadamu namna wanatakiwa wawe kiimani
Ko yesu yaan huyo mungu alikuwa anafanya drama sio? Alikua anajifanyisha kuvaa ubinadamu sio?

Sauti inatoka mbinguni inasema huyu ni mwanangu mpendwa niliyemchagua, ni maigizo maana mungu yupo duniani na ndo yesu huyo huyo?

Mnapotosha watu kwenye ukristo na mapokeo ya kipagani
 
Siku zote huwa najiuliza mkristo mwenye imani anamshawishi vipi mtu wa imani nyingine au mtu asiye na imani

Kwa hoja za yesu alikua ni mungu kwa 100% pia ni mtu kwa 100% na akakubaliana na hiyo imani.

Kwa maana hilo jambo haliingii akilini kwa mtu yeyote mwenye akili timamu.
Kazi kwelikweli
 
Sasa Kwa mantiki hiyo hiyo,

Iweje wayahudi kutaka kumwua Yesu Kwa kujiita Messiah, mwana wa Mungu aliye juu?

Rudi hapo kwenye mwana wa Mungu ufikiri UPYA,

Yesu ni Mwana wa Mungu asiye na baba wa kimwili, na ndio Hasa walitaka kumwua wakiamini Yusufu ni babaye wa kumzaa kimwili.

Ukifikia hapo, utajua kwanini Shetani alisema ikiwa u "Mwana wa Mungu "!
Karibu 🙏
Kwani adamu ana baba wa kimwili?
Eva ana baba wa komwili?

Wao kutaka kumuua au hata wangemkubali kuwa masihi wasingeongeza wala kupunguza chochote katika kibali alichopewa.
Na kuhusu kukataliwa hata nuhu alikataliwa,yusuph aliuzwa adi kuuzwa,lakini matendo hayo ya watu dhidi yao hayakuondoa utume wao the same applies to yesu!

na Sio tu walitaka kumuua,walimuua kweli! Kwahiyo unataka kusema mungu alikufa!
Hivi kwani wewe sio mwana wa mungu? Na kama sio acha kumuita mungu baba!
 
yesu ni mtoto pekee aliyeumbwa kwanza yeye kabla ya vitu vingine na viumbe wengine kwahiyo akasaidiaa uumbaji wa viumbe vingine na vitu vingine kwahiyo lazima apewe kipaumbele
Hii tena mpya na kali kuliko zote.

Kwamba suala la Adam kuwa kiumbe wa kwanza kuumbwa ni fix tu au?

Halafu Yesu anamsaidiaje Mungu katika uumbaji wa viumbe vingine ina maana Mungu muweza wa yote alihitaji msaada?

Ninavyojua mimi Mungu ni muweza wa yote na akisema kuwa basi inakuwa.

Nipe andiko linalosema Yesu aliumbwa kama binadamu wa kwanza na jukumu lake lilikuwa kumsaidia Mungu katika uumbaji tafadhali. 🙏
 
Wakati nasoma Sunday School na kujisomea biblia nilijua Yesu (mwana wa Mungu) ni Yesu na Mungu ni Mungu. Baadae ukubwani nakuja kuambiwa Yesu ndio Mungu. Nikachoka. Itabidi nirudi tena kusoma
 
Wakati nasoma Sunday School na kujisomea biblia nilijua Yesu (mwana wa Mungu) ni Yesu na Mungu ni Mungu. Baadae ukubwani nakuja kuambiwa Yesu ndio Mungu. Nikachoka. Itabidi nirudi tena kusoma
Kwahyo mkuu uliamua kushika kipi sasa kati ya hivyo?
 
Upuuzi mtupu


Unaleta maneno ya kupambiza tu mara kijasusi,mission maalumu

Kama yesu mwenyewe anakataa kuitwa mwema anasema mungu pekee ndo anastahili kuitwa mwema, halafu wew wasema yesu ni mungu ??
Yesu anaenda kusali muda mfupi tu kabla ya kifo, alikua anasali kwa nani?

Malaika wanashuka kuja kumfariji, saa ilipofika ya kuuwawa,mungu gani anafarijiwa na malaika wake?

Anajaribiwa na ibilisi ,yesu anamjibu shetani mungu ndo hupaswa kuabudiwa, yaani yesu anasema mungu tu ndo nitakaemwinamia !
Mkuu Pesawebz maswali yako magumu sana
 
Back
Top Bottom