Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Sasa mbona mechi yenyewe haioneshwi live kupitia luninga kama ilivyotangazwa hapo awali? Maana siyo wote tunaishi Dar es Salaam! Yaani muda huu nimelazimika kuwaangalia Simba badala ya Yanga!

Au ndiyo uswahili ule ule wa miaka nenda wa viongozi wetu, wa kujifanya wanazikwepa fitna za Waarabu? Halafu siku ya mechi unakuta wachezaji wenyewe akina Ali Ali wanaruka ruka tu uwanjani na kuchomesha!
 
Sababu kuu ilikuwa ni hii hapa. 👇👇👇
 

MJUE MWINYI ZAHERA

Anaitwa Mwinyi Zahera alizaliwa Oktoba 19, mwaka 1962. Ilipofika mwaka 1975 Zahera alianza kucheza mpira akiwa na miaka 13 katika klabu ya Bankin ya Goma, Kaskazini mwa jimbo la Kivu, DRC hadi mwaka1980.

Baada ya hapo akaenda Kinshasa kucheza soka na kujiendeleza kielimu,
Akajiunga na chuo cha Teknolojia(ISTA) huku akichezea klabu ya Sozacom hadi alipokutana na wakala wa wachezaji, Mbelgiji Mr. Karl Broken aliyemchukua na kumpeleka Ulaya kucheza soka la kulipwa. .

Alifika Ulaya na kusajiliwa na Antwerp Fc ya Ubelgiji alicheza kwa miaka miwili kabla ya kumaliza mkataba wake kumalizika na kwenda Ufaransa alikocheza katika timu za daraja la pili Amiens Fc, Beauvais Fc kisha Abbeville hadi alipostaafu soka.

Baada ya hapo Zahera alianza mafunzo ya Ukocha ambako alitunukiwa Diploma na Leseni A ya Shirikisho la soka Ulaya(UEFA) baadae akaenda kuifundisha klabu ya SC Feignies ya Ufaransa kwa mafanikio makubwa kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2010 kisha akatimkia Ubelgiji kwenda kuifundisha AFC Tubize kwa msimu mmoja na baadaye kurudi tena Ufaransa akiifundisha klabu ya Douai Fc kwa misimu miwili kabla hajarejea tena AFC Tubize kama kaimu kocha mkuu wa klabu hiyo ilipofika mwaka 2014 alirejea nchini kwao Congo DR na kuifundisha klabu ya DC Motema Pembe mpaka mwaka 2016.

Tar. 30 September/2017 Zahera alitangazwa kuwa kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Congo DR akiwa chini ya kocha mkuu Frolent Ibenge Na ilipofika 25April 2018 Zahera alijiunga rasmi Dar es Salaam Young Africans Sports Clubs "Yanga Sc" kama kocha mkuu akirithi mikoba ya kocha George Lwandamina(Chicken) .

Huyu ndio Papaa Mwinyi Zahera Mcongoman mwenye uraia wa Ufaransa kwa sasa ana miaka 56, Usisahau Oktoba19 ni birthday yake. Natumai sasa walau umemjua vema kocha wetu.

yangaafuldozz
 
ISSA BIGIRIMANA NA DEUS KASEKE WAUNGANA NA WENZAO.

Nyota Yanga waliokuwa majeruhi Issa Bigirimana na Deus Kaseke wamerejea uwanjani wakiungana na waliorejea juzi kwenye mchezo wa kirafiki wa Yanga dhidi ya Friends Rangers akiwamo Mrisho Ngassa, Sadney Urikhob, Papy Tshishimbi, Patrick Sibomana, Paul Godfrey ‘Boxer’ na Lamine Moro,

Wachezaji hao wameanza kupiga tizi na wenzao na kazi sasa kubaki kwa Kelvin Yondani, Ally Mtoni ‘Sonso’, Juma Mahadhi, Mohammed Issa ‘Banka’ na Cleofas Sospeter ambao hali zao inaelezwa bado.

Yanga inakabiliwa na mechi mbili ngumu jijini Mwanza - moja ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbao FC na nyingine dhidi ya Waarabu wa Pyramids - zote zikitarajiwa kuchezwa Uwanja wa CCM Kirumba.

@Yangasoccer
 
ZAHERA AREJEA KUONGOZA MAANDALIZI MECHI DHIDI YA MBAO FC

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera tayari amerejea nchini akitokea DR Congo alikokuwa akikabiliwa na majukumu ya timu ya Taifa

Leo Mcongomani huyo anatarajiwa kuendelea na majukumu ya kukiandaa kikosi chake kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbao Fc ambao utapigwa Oktoba 22

Zahera amesema mechi dhidi ya Mbao huwa na ushindani mkali lakini wamejipanga kuweza kushinda ili kuwajengea kujiamini wachezaji kuelekea mchezo dhidi ya Pyramids Fc.

Yangasoccer
 
MASHABIKI KANDA YA ZIWA WAISUBIRI YANGA

Uamuzi wa kuupeleka jijini Mwanza mchezo wa kombe la Shirikisho kati ya Yanga dhidi ya Pyramids Fc, umepokewa kwa furaha na mashabiki wa timu hiyo kanda ya ziwa ambao wamejipanga kuandika historia

Wakati kikosi cha Yanga kikitarajiwa kuwasili jijini Mwanza Jumapili, mashabiki wameanza mapema mikakati ya kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi uwanja wa CCM Kirumba kuipa sapoti timu yao ili iweze kushinda mchezo huo utakaopigwa Jumapili ya Oktoba 27

Mashabiki kutoka mikoa ya Mara, Shinyanga na Tabora tayari wameanza mipango ya maandalizi ya kuelekea jijini Mwanza

Pamoja na kuwa bado zoezi la uuzwaji tiketi halijaanza, mashabiki wameonyesha utayari wakisubiri kutangazwa kwa viingilio pamoja na uuzwaji wa tiketi

Uongozi wa Yanga umesema tiketi zitaanza kuuzwa mapema kuhakikisha mashabiki wote wanakuwa na tiketi siku tatu kabla ya mchezo. Hakuna tiketi zitakazouzwa siku ya mchezo

Shamrashamra kuanza mechi dhidi ya Mbao Fc

Viongozi wa Matawi ya Yanga jijini Mwanza wamesema shamrashamra za maandalizi ya mchezo dhidi ya Pyramids Fc zitaanza Oktoba 22 Yanga itakapocheza na Mbao Fc mchezo wa ligi kuu

Yangafuldozz
 
Mwenyekiti wa Yanga Dk Mshindo Msolla amesema hawatakuwa na tatizo kumrejesha kiungo wao wa zamani Haruna Niyonzima kama kocha Mwinyi Zahera atamuhitaji

Baada ya hivi karibuni Niyonzima kukutana na mmoja wadau wakubwa wa yanga sc Abdallah Bin Kleb, kumekuwa na taarifa kuwa Niyonzima anaweza kurejeshwa wakati wa usajili wa dirisha

Mwenyewe Niyonzima ameeleza kuwa tayari kurejea Yanga, akikiri kuwa ni klabu aliyoitumikia kwa mapenzi makubwa

Dk Msolla amesema pamoja na kuvutiwa na kiwango cha nyota huyo, hatma yake iko mikononi mwa Zahera "Ipo wazi Niyonzima aliitumikia Yanga kwa mapenzi yote na alifurahia uwepo wake katika klabu" "Suala la kama tutamsajili au la litategemea na maoni ya kocha kwani yeye ndiye anayefahamu mapungufu ya timu yake"

Kwa mara ya kwanza, Niyonzima alitua Yanga mwaka 2012 akitokea APR na kufanikiwa kushinda mataji manne ya ligi kuu

Mwaka 2017 alijiunga na Simba klabu aliyoitumikia kwa misimu miwili na kuongeza mataji mengine mawili ya ligi kuu
 
TUKO TAYARI KUIKABILI MBAO "MWINYI ZAHERA'

Kocha Mkuu wa Yanga Mwinyi Zahera amesema wamejiandaa kikamilifu kuelekea mchezo dhidi ya Mbao Fc ligi kuu ya Vodacom ambao utapigwa Jumanne, Oktoba 22

Akizungumza baada ya kuwasili jijini Mwanza, Zahera amesema kikosi chake kimefanya maandalizi ya kutosha "Tumejipanga kucheza kufuatana na wapinzani wetu tutakaokabiliana nao, tupo tayari kucheza na Mbao," alisema Zahera "Tumekuja na wachezaji wetu wote waliotimamu ambapo wale wawili (Abdulaziz Makame na Metacha) waliopo Taifa Stars watawasili nao hapa Mwanza, hivyo tutaanza mazoezi tayari kuelekea michezo ijayo"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…