Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

20191204_085450.jpg
 
WINGA WA COASTAL AJIPELEKA YANGA

KUELEKEA usajili wa dirisha dogo, winga wa timu ya Coastal Union, James Kihimba, ametamba kuwa na namba katika kikosi cha Yanga baada ya kuanza kunyemelewa na viongozi wa klabu hiyo.

Kihimba ambaye msimu uliopita alichezea Biashara United, mkataba wake na Coastal Union unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.

Akizungumza na BINGWA jana, mchezaji huyo alisema, kuna mazungumzo yanaendelea kati yake na Yanga, endapo mambo yatakwenda vizuri hatasita kujiunga na timu hiyo kwa sababu ni moja ya ndoto zake.

Alisema aliwahi kuzungumza na Mwenyekiti wa Yanga, Dkt. Mshindo Msolla, siku walipocheza na Wanajangwani hao katika mechi ya kirafiki hivi karibuni. “Siku ile tuliyocheza na Yanga pale Taifa, mechi ilivyoisha yule mwenyekiti wao (Dk. Msolla), alinifuata na kuniambia nimefanya kazi nzuri, tena kama kutakuwa na uwezekano dirisha dogo watanichukua,” alisema. “Yanga kuna wachezaji wengi lakini nafasi yakucheza naona ipo kwa sababu najua ninachokitafuta, nitakomaa hadi nipate namba kikosi cha kwanza, muhimu ni kujituma tu na maelekezo ya mwaliamu,” alisema.

Alieleza kuwa hakuna kitakachomzuia kutoka Coasta Union kwa sababu mkataba wake una kipengere cha kumruhusu kuondoka muda wowote. “Nina mkataba wa mwaka mmoja, unamalizika msimu huu lakini una kipengele kinachoniruhusu kuondoka, nimefanya hivyo kwa sababu mara kwa mara naenda kufanya majaribio nje ya nchi,” alisema.

@Yangafulldozz
 
20191204_090226.jpg
NINJA ASHANGAA MECHI YA YANGA DHIDI YA KMC

Beki wa LA Galaxy ya Marekani, Abdallah Shaibu 'Ninja' juzi alikuwepo jukwaani akishuhudia Yanga ikilazimishwa sare 1-1 na KMC

Ameeleza kushangazwa jinsi timu yake hiyo ya zamani ilivyocheza soka la kupooza.

Ninja aliyeichezea Yanga kabla ya kujiunga na LA Galaxy mwanzoni mwa msimu amerejea nchini katika mapumziko wakati huu Ligi ya Marekani imesimama kupisha majira ya baridi.

Akizungumzia mechi hiyo, Ninja alisema katika mchezo huo ameona walikuwa wanacheza kwa kupooza kama vile wachezaji wamechoka, kitu ambacho si kizuri kwa Yanga inayohitaji ubingwa. "Si Yanga wala KMC, walicheza kwa kupooza sana, imeonekana kama wachezaji wamechoka pengine ratiba ya ligi inawabana, ila wanahitaji kujitofautisha na timu nyingine ili kuchukua ubingwa," "Wachezaji wazawa wajaribu kuwapa nafasi, kwani wanakuwa wanajua ligi ilivyo kuliko wageni ambao nimeona wanakwama kidogo," alisema Ninja.

Jambo lingine ambalo alikuwa makini sana kulifafanua kwamba hataki kuingilia majukumu ya benchi la ufundi ila alishauri wachezaji wangecheza kwenye namba zao akimtolea mfano Jafary Mohamed

Mwanaspoti
 
NINJA ASHANGAA MECHI YA YANGA DHIDI YA KMC

Beki wa LA Galaxy ya Marekani, Abdallah Shaibu 'Ninja' juzi alikuwepo jukwaani akishuhudia Yanga ikilazimishwa sare 1-1 na KMC

Ameeleza kushangazwa jinsi timu yake hiyo ya zamani ilivyocheza soka la kupooza.

Ninja aliyeichezea Yanga kabla ya kujiunga na LA Galaxy mwanzoni mwa msimu amerejea nchini katika mapumziko wakati huu Ligi ya Marekani imesimama kupisha majira ya baridi.

Akizungumzia mechi hiyo, Ninja alisema katika mchezo huo ameona walikuwa wanacheza kwa kupooza kama vile wachezaji wamechoka, kitu ambacho si kizuri kwa Yanga inayohitaji ubingwa. "Si Yanga wala KMC, walicheza kwa kupooza sana, imeonekana kama wachezaji wamechoka pengine ratiba ya ligi inawabana, ila wanahitaji kujitofautisha na timu nyingine ili kuchukua ubingwa," "Wachezaji wazawa wajaribu kuwapa nafasi, kwani wanakuwa wanajua ligi ilivyo kuliko wageni ambao nimeona wanakwama kidogo," alisema Ninja.

Jambo lingine ambalo alikuwa makini sana kulifafanua kwamba hataki kuingilia majukumu ya benchi la ufundi ila alishauri wachezaji wangecheza kwenye namba zao akimtolea mfano Jafary Mohamed

Mwanaspoti

Naomba uniunge kwny group la yanga...0717550291
 
MATOKEO DROO YA RAUNDI YA TATU ASFC.

Droo imeshirikisha jumla ya timu 64: Timu 20 zinatoka ligi kuu, timu 24 kutoka ligi daraja la kwanza na timu 20 zilizofuzu kutoka madaraja ya chini

Yanga watakuwa wenyeji wa Iringa United.

Mechi hizi zitapigwa kati ya tarehe 22 na 28 mwezi Desemba mwaka huu.

Kwa mujibu wa droo hiyo iliyofanyika mubashara kupitia Azam Sports , mechi 32 za raundi ya tatu ziko hivi.

1. Migombani vs Mbeya City
2. Polisi Tanzania vs Top Boys
3. Mwadui FC vs Mkamba Rangers.
4. Tukuyu Stars vs Singida United.
5. Mbuni FC vs KMC
6. Alliance vs Transit Camp
7. Ndanda SC vs Cosmo Politan.
8. Milambo FC vs Ruvu Shooting.
9. Mbao FC vs Stand United.
10. Nyamongo vs Biashara United.
11. Mawenzi Market vs Mtwivila.
12. Mpwapwa United vs Kitayosa.
13. Talinega FC vs Friends United.
14. Ihefu vs Kasulu Red Star
15. Toto Africans vs Gipco.
16. Mighty Elephant vs Mashujaa FC
17. Jeshi Warriors vs Dodoma FC
18. Majimaji FC vs Pamba SC
19. Panama FC vs Area C
20. Gwambina FC vs Mbeya Kwanza.
21. Pan African vs Geita Gold.
22. Njombe Mji vs Sahare All Stars.
23. Lipuli FC vs Dar City.
24. Kagera Sugar vs Rufiji United.
25. Tanzania Prisons vs Mlale FC.
26. Mtibwa Sugar vs Rhino Rangers.
27. Simba SC vs Arusha FC.
28. Yanga SC vs Iringa United.
29. Coastal Union vs African Sports.
30. Namungo FC vs Green Warriors.
31. JKT Tanzania vs Boma FC
32. Azam FC vs African Lyon.

@Yangafulldozz
 
YANGA KUFANYA ZIARA YA MECHI ZA KIRAFIKI NJE YA JIJI

Mashabiki wa Yanga wa nje ya jiji la Dar es salaam wamekuwa na shauku ya kuiona timu yao kwani kwa baadhi ya mikoa wanapata nafasi hiyo mara moja tu huku mikoa mingine ambayo haina timu zinazoshiriki ligi kuu wakiishia kuwaona kupitia runinga

Habari njema wakati huu ambao ligi imesimama, Yanga itafanya ziara mikoani kucheza mechi za kirafiki ambazo zitakuwa sehemu ya maandalizi ya mchezo wa kombe la FA dhidi ya Iringa United na ule wa watani wa jadi dhidi ya Simba

Afisa Mhamasishaji wa Yanga Antonio Nugaz amesema baada ya wachezaji kurejea kutoka mapumziko, wataweka hadharani ratiba ya program nzima ya maandalizi

Baada ya mchezo dhidi ya KMC, wachezaji walipewa mapumziko ya siku mbili na wanatarajiwa kurejea mazoezini kesho Alhamisi

Wakazi wa mikoa ambayo haina timu zinazoshiriki ligi kuu kama Dodoma, Kigoma, Rukwa na kwingineko huenda wakapata nafasi ya kutembelewa na mabingwa hao wa kihistoria.

@Yangafulldozz
 
TANZIA:
Mchezaji wetu wa zamani Ally Yusuf ‘Tigana’ amefariki dunia l

Tigana aliichezea Yanga kwa vipindi viwili aliingia mwaka 1994 -1995 baadae mwaka 2001-2004.

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema Peponi.
Amina
FB_IMG_1575568326193.jpg
FB_IMG_1575568290417.jpg
 
HATMA YA KOCHA MSAIDIZI KUFAHAMIKA MWISHONI MWA WIKI

Kamati ya Ufundi ya klabu ya Yanga itakutana mwishoni mwa wiki kupitisha jina la kocha msaidizi wa timu hiyo, imefahamika

Tangu alipoteuliwa Charles Mkwasa kuwa Kaimu kocha Mkuu mwezi uliopita, amekuwa akisaidiana na Said Maulid (SMG) ambaye ni mkufunzi wa timu ya vijana pamoja na Dismas Ten ambaye ni Meneja wa timu

Hata hivyo pamoja na kuwa mchakato wa kusaka kocha mkuu haujakamilika, uongozi wa Yanga umeamua kumaliza mchakato wa kocha msaidizi kwanza

Upo uwezekano Mkwasa ataendelea kuinoa Yanga mpaka mwishoni mwa msimu

Kocha wa Kagera Sugar Mexime ndiye anaetajwa zaidi kuwa anaweza kutua kwa mabingwa hao wa kihistoria

Mexime amesema kuwa yuko tayari kujiunga na Yanga kama watafikia makubaliano

Mwingine anayetajwa ni Kalimangonga Ongala aliyewahi kuzinoa klabu za Azam Fc na Majimaji ya Songea.

@Yangadaima.
 
SADNEY,BALINYA MTEGONI

Mashabiki wa Yanga walikuwa na matarajio makubwa kutoka kwa washambuliaji Sadney Urikhob na Juma Balinya ambao walitua Yanga kwenye usajili wa msimu huu

Balinya alitua kwa mbwembwe siku ya KUBWA KULIKO akitambulishwa ukumbini sambamba na kiungo Abdulaziz Makame 'Bui'

Sadney alichelewa kidogo lakini mashabiki walipagawa na 'mavitu' aliyokuwa akiyafanya kupitia video zake Youtube

Baada ya Yanga kumuuza Heritier Makambo aliyekuwa kinara wa kuzifumania nyavu, wengi waliamini kuwa wachezaji hao wangefanya zaidi ya kile kilichofanywa na Makambo msimu uliopita

Hata hivyo mambo yamekuwa tofauti, washambuliaji hao mpaka sasa kila mmoja amefunga bao moja tu kwenye ligi 

Wakati kocha Charles Mkwasa akitangaza kufanyia maboresho safu yake ya ushambuliaji wakati wa dirisha dogo, pengine ni wakati wao kujitathimini

Hakuna shaka Yanga itawapa nafasi hadi mwishoni mwa msimu ili waonyeshe kama wanastahili kuendelea kuichezea Yanga

Lakini kama mambo yataendelea kuwa yalivyo, huenda wakaitumikia Yanga kwa msimu mmoja tu

Kwa sasa Yanga inamtegemea zaidi mshambuliaji David Molinga ambaye pamoja na kuwa nae hajaonyesha ubora ambao wengi wanautaka, lakini ameonyesha utofauti

Mabao manne aliyofunga kwenye ligi mpaka sasa yanadhihirisha kuwa yuko vizuri zaidi

Pengine usajili wa washambuliaji wapya utakuwa chachu kwa nyota hao kuimarisha viwango vyao ili wawanie nafasi kwenye kikosi cha kwanza.

@Yangadaima
 
WINGA WA COASTAL AJIPELEKA YANGA

KUELEKEA usajili wa dirisha dogo, winga wa timu ya Coastal Union, James Kihimba, ametamba kuwa na namba katika kikosi cha Yanga baada ya kuanza kunyemelewa na viongozi wa klabu hiyo.

Kihimba ambaye msimu uliopita alichezea Biashara United, mkataba wake na Coastal Union unatarajiwa kumalizika mwishoni mwa msimu huu.

Akizungumza na BINGWA jana, mchezaji huyo alisema, kuna mazungumzo yanaendelea kati yake na Yanga, endapo mambo yatakwenda vizuri hatasita kujiunga na timu hiyo kwa sababu ni moja ya ndoto zake.

Alisema aliwahi kuzungumza na Mwenyekiti wa Yanga, Dkt. Mshindo Msolla, siku walipocheza na Wanajangwani hao katika mechi ya kirafiki hivi karibuni. “Siku ile tuliyocheza na Yanga pale Taifa, mechi ilivyoisha yule mwenyekiti wao (Dk. Msolla), alinifuata na kuniambia nimefanya kazi nzuri, tena kama kutakuwa na uwezekano dirisha dogo watanichukua,” alisema. “Yanga kuna wachezaji wengi lakini nafasi yakucheza naona ipo kwa sababu najua ninachokitafuta, nitakomaa hadi nipate namba kikosi cha kwanza, muhimu ni kujituma tu na maelekezo ya mwaliamu,” alisema.

Alieleza kuwa hakuna kitakachomzuia kutoka Coasta Union kwa sababu mkataba wake una kipengere cha kumruhusu kuondoka muda wowote. “Nina mkataba wa mwaka mmoja, unamalizika msimu huu lakini una kipengele kinachoniruhusu kuondoka, nimefanya hivyo kwa sababu mara kwa mara naenda kufanya majaribio nje ya nchi,” alisema.

@Yangafulldozz
Mchukuweni na Ally Kiba basi Shadeeya ni winga hatari sana tena ni shabiki lialia wa Chura FC
 
TPLB YASISITIZA MECHI YA WATANI WA JADI ITAPIGWA JANUARY 4

Pamoja na uwepo wa michuano ya kombe la Mapinduzi mwanzoni mwa mwaka, Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara imesisitiza haitafanya mabadiliko ya tarehe ya mchezo wa kwanza wa watani wa jadi kati ya Simba dhidi ya Yanga

Mchezo huo umepangwa kupigwa January 04 2020 kwenye uwanja wa Taifa

Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Stephen Mguto amesema wamepeleka mapendekezo kwa waandaaji wa michuano ya kombe la Mapinduzi ili ichezwe kwa mfumo wa mtoano

Hata hivyo amesema vilabu vya Simba na Yanga vitalazimika kurejea nchini kucheza mchezo baina yao January 04 "Tulichofanya sisi ni kuwasiliana na viongozi wa kamati ya maalum inayosimamia michuano ya Mapinduzi, ili watupe maoni yao kuhusu tariba ya ligi hapa Tanzania Bara," amesema Mguto "Tumeomba michuano ya Mapinduzi iwe ya mtoano ili timu za huku ziweze kucheza mechi zake mara zitakapotoka, lakini kwa Simba na Yanga hata kama zitaingia hatua ya nusu fainali au robo zitatakiwa zirudi Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo huo, hivyo hatutabadilisha"
 
TPLB YASISITIZA MECHI YA WATANI WA JADI ITAPIGWA JANUARY 4

Pamoja na uwepo wa michuano ya kombe la Mapinduzi mwanzoni mwa mwaka, Bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara imesisitiza haitafanya mabadiliko ya tarehe ya mchezo wa kwanza wa watani wa jadi kati ya Simba dhidi ya Yanga

Mchezo huo umepangwa kupigwa January 04 2020 kwenye uwanja wa Taifa

Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Stephen Mguto amesema wamepeleka mapendekezo kwa waandaaji wa michuano ya kombe la Mapinduzi ili ichezwe kwa mfumo wa mtoano

Hata hivyo amesema vilabu vya Simba na Yanga vitalazimika kurejea nchini kucheza mchezo baina yao January 04 "Tulichofanya sisi ni kuwasiliana na viongozi wa kamati ya maalum inayosimamia michuano ya Mapinduzi, ili watupe maoni yao kuhusu tariba ya ligi hapa Tanzania Bara," amesema Mguto "Tumeomba michuano ya Mapinduzi iwe ya mtoano ili timu za huku ziweze kucheza mechi zake mara zitakapotoka, lakini kwa Simba na Yanga hata kama zitaingia hatua ya nusu fainali au robo zitatakiwa zirudi Dar es Salaam kwa ajili ya mchezo huo, hivyo hatutabadilisha"
Lengo la TFF ni kupiga pesa tu
 
20191208_071329.jpg
ZIARA YA MKOANI KIGOMA

Timu ya Wananchi itafanya ziara mkoani Kigoma na kucheza mechi mbili za kirafiki. Timu itaondoka Alhamisi ya tarehe 12/12/2019, mchezo wa awali utachezwa tarehe 13/12/2019 dhidi ya Mwamgongo FC na mwingine ni 15/12/2019 dhidi ya MBAO FC.

Michezo yote hii miwili itachezwa Uwanja wa Lake Tanganyika.
 
Back
Top Bottom