Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Halafu nasikia eti juzi baada ya kutolewa akaingizwa Tarik Seif nasikia Molinga aliliamsha sana dude kwa Kocha. Hivi ni ukweli au ndio stori za Mitandaoni?
Ni kweli,jamaa halafu hiyo ni Mara ya pili kuleta ghadhabu zake. Kuna siku mwanza pia aliwahi kuzingua hivyohivyo,anajiona anapaswa kucheza dk zote hata akichemsha. Juzi baada ya kutolewa alichukia akaamua kuondoka na bodaboda
 
Ni kweli,jamaa halafu hiyo ni Mara ya pili kuleta ghadhabu zake. Kuna siku mwanza pia aliwahi kuzingua hivyohivyo,anajiona anapaswa kucheza dk zote hata akichemsha. Juzi baada ya kutolewa alichukia akaamua kuondoka na bodaboda
Aongezage bidii akiyataka hayo yote sababu kikawaida siku zote timu inahitaji matokeo. Nje ya hapo haya ayatarajie.
 
20200102_064036.jpg

Shirikisho la Soka nchini @tanfootball limemtangaza Jonesia Rukyaa kuwa mwamuzi wa kati mechi ya watani wa jadi Simba na Yanga itakayopigwa Januari 4. Waamuzi wasaidizi ni Sudi Lila, Hamis Chang’walu na mwamuzi wa akiba ni Elly Sasii.

azamtv
 
JANUARY 4 TUNAKUJA KIVINGINE 'MKWASA'

Kaimu Kocha Mkuu wa Yanga Charles Mkwasa amesema kikosi chake kitakuwa sawa kuelekea mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba ambao utapigwa Jumamosi, Januari 04 uwanja wa Taifa.

Mkwasa amesema mpaka kufikia Jumamosi, wachezaji wake watakuwa wamepata muda wa kutosha kuweka sawa miili baada ya uchovu wa kucheza mfululizo "Kwa wanaodhani mchezo dhidi ya Simba tutacheza kama tulivyocheza na Biashara United wanajidanganya. Tuna siku tatu za kujiandaa na mchezo huo, tunahitaji kushinda hivyo tutapambana" "Wanachohitaji wachezaji wangu ni mapumziko ili kupoza miili yao. Tutakuwa tukifanya mazoezi lakini zaidi yatakuwa ya kufanya miili ya wachezaji irudi kwenye hali yake," amesema Mkwasa "Ninachowaambia mashabiki wa Yanga wasiwe na wasiwasi, timu itakuwa tofauti kabisa Januari 04".

Tariq, Nchimbi, Yikpe waongeza nguvu.
Jana TFF imeachia leseni ya Ditram nchimbi hivyo atakuwa na ruksa ya kucheza mchezo wa Jumamosi.

Lakini pia ITC ya mshambuliaji Yikpe Gnamien inatarajiwa kuwasili wakati wowote na hivyo nae atakuwa na nafasi ya kucheza mchezo huo.

Kuongezeka kwa washambuliaji hao kutabadili kabisa sura ya safu ya ushambuliaji ya Yanga.

@Yangafulldozz
 
Uongozi yanga wakati mwingine unashusha hadhi ya timu. Hivi haruna hadi sasa hajafika na ndo mchezaji ambae wanataka wamtegemee jumamosi na yeye ndo abebe show nzima. Walisema angefika Jana na Leo wanadai atafika Leo. Yaani wanaifanya yanga kama ndanda kwamba mchezaji anaweza akasajiliwa na akaingia kwenye kikosi moja kwa moja hata bila ya kufanya mazoezi na wenzake
 
Back
Top Bottom