Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Young Africans Sports Club (Yanga) | Special Thread

Yanga 3-1 Mtibwa...
The Sagga continua
Who'z next?????????????
 
Hivi ule nao unaita uwanja? Kama mna uwanja kwa nini mnaenda kufanyia mazoezi Uhuru?
Klabu kubwa haipimwi kwa mechi za mchangani bali kwa mashindano ya kimataifa ambayo mnyama ndio mwenyewe. Yebo yebo ni michuano gani ya kimataifa ambayo wamewahi kufika japo nusu fainali?
Kutembeza bakuli yebo yebo ndio wenyewe au umesahau wakati Ngozoma Matunda alipoomba timu ichangiwe mchele na maharagwe?

Mbona matajiri Simba walidaiwa CHAPATI 20 walizo kopa kwa Kaduguda ehhh
 
Umenifurahisha sana umezungumza mambo ya msingi, Yanga ni kiboko
 
Waungwana wa Yanga na wandugu toka vilabu vingine, haswa wale wanaoshindwa kupaka hata chokaa jengo lao, nawakaribisha kesho ktk uwanja wa Taifa ili tuwe mashuhuda wa mtanange kati ya Yanga na wakata viuno toka DRC...

Yanga imara.
Yanga daima mbele, nyuma mwiko.
 
Mwenzetu kweli mwana historia kama darasani ungekuwa na kumbukumbu namna hii mwenzetu ungekuwa unafanya kazi NASA!
 
Papic ajitosa rasmi kumrithi Maximo
papicmwalusako.jpg
Kocha wa Yanga Kostadin Papic akizungumza na katibu wa Yanga Lawrence Mwalusako nje ya ofisi za Shirikisho la soka Tanzania (TFF) jijini Dar es Salaam jana mara baada ya kutoa taarifa ya kutaka kuwasilisha barua ya maombi ya kazi ya kukinoa kikosi cha Taifa StarsSosthenes Nyoni

KOCHA wa Yanga, Kostadin Papic jana aliwasilisha rasmi barua ya maombi ya kazi Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) kuwania nafasi ya kumrithi Mbrazil Marcio Maximo anayemaliza mkataba wake wa kuifundisha Taifa Stars mwezi Julai.

Papic ambaye aliweka bayana dhamira yake hiyo ya kuwania kuifundisha Taifa Stars pale tu TFF ilipotangaza kuanza mchakato wa kumtafuta kocha mpya, aliwasili katika ofisi za shirikisho hilo majira ya saa 5:30 asubuhi akisindikizwa na katibu mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako.

Akizungumza na Mwananchi mara baada ya kukabidhi barua yake, Papic alisema amefikia uamuzi huo kutokana na kuamini kuwa ana vigezo vyote vinavyomwezesha kuwa kocha wa Taifa Stars.

"Bila shaka niliweka wazi kwamba nitaomba kazi ya kufundisha Taifa Stars na leo nimeleta rasmi maombi yangu hapa kwa kuwa najiamini kutokana na vigezo vilivyotolewa ninavyo,"alisema Mserbia huyo.

Aliongeza kuwa ameshafanya kazi ya kufundisha soka sehemu mbalimbali akiwa na timu kubwa na kuziletea mafanikio, hivyo hana wasiwasi wa kuimudu vema Taifa Stars.

Akizungumzia mustakabali wake na Yanga ikiwa atakabidhiwa nafasi ya kuifundisha Taita Stars, alisema kwa sasa hakuna tatizo hasa kwa kuwa mkataba wake na Yanga unamalizika mwezi Juni na kuongeza kuwa kama atafanikiwa pia anaweza kuwasaidia kutafuta kocha mwingine ikiwa watapenda.

"Mkataba wangu unamalizika Juni hivyo kwa sasa sioni tatizo na kama nitafanikiwa katika hili ninaweza pia kuwasaidia Yanga kutafuta kocha mwingine kama watapenda," alisema Papic maarufu kama Clinton.

Endapo Papic atafanikiwa kuchukua nafasi ya kuinoa Stars, itakuwa zamu ya Yanga kutoa kocha wao kuifundisha timu hiyo ya taifa kwa kuwa mara nyingi makocha wa Stars pindi wanapomaliza mikataba yao ndipo wanaamua kufundisha klabu hiyo ya mtaa wa Jangwani na Twiga.

Makocha waliowahi kuifundisha Taifa Stars na baada ya kumaliza mkataba wao kujiunga na Yanga ni pamoja na Rudi Gutadrf mwaka 1982, Joel Bendera (1986) kwa sasa Naibu Waziri wa Habari na Utamaduni akiwa kocha wa Stars aliombwa kuisaidia klabu hiyo kwenye michuano ya Afrika mashariki na kati. Mwaka 1996, Yanga ilifanikiwa kumnasa Sunday Kayuni aliyekuwa kocha msaidizi wa timu ya Tanzania Bara.

Katika hatua nyingine Papic alisema kuwa maandalizi ya kikosi chake kinachojiandaa na mpambano wa Michuano ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya FC Eloi Limpopo yanaendelea vizuri ingawa ana majeruhi wawili.

"Tupo vizuri ingawa nina majeruhi wawili ambao tayari hawatakuwepo katika kikosi cha Jumamosi, hawa ni Obren Curkovic aliyeumia katika mchezo wetu wa mwisho na Kabongo Honore aliyefanyiwa upasuaji wa goti,ukiondoa hao wengine wako vizuri." "Ninajua itakuwa mechi ngumu siwezi kuwazungumzia sana wapinzani wetu kwa kuwa hata nilipoenda kule walichezesha kikosi cha pili,lakini pia siwezi kuwadharau kwa kutambua timu ile haijacheza mashindano haya kwa miaka mitatu, sasa huwezi kujua watakuja na nguvu kiasi gani, tutakachofanya ni kuwasoma kwanza,"alisema Papic
 
Papic ajitosa rasmi kumrithi Maximo
papicmwalusako.jpg
Kocha wa Yanga Kostadin Papic akizungumza na katibu wa Yanga Lawrence Mwalusako nje ya ofisi za Shirikisho la soka Tanzania (TFF) jijini Dar es Salaam jana mara baada ya kutoa taarifa ya kutaka kuwasilisha barua ya maombi ya kazi ya kukinoa kikosi cha Taifa StarsSosthenes Nyoni

KOCHA wa Yanga, Kostadin Papic jana aliwasilisha rasmi barua ya maombi ya kazi Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) kuwania nafasi ya kumrithi Mbrazil Marcio Maximo anayemaliza mkataba wake wa kuifundisha Taifa Stars mwezi Julai.

Papic ambaye aliweka bayana dhamira yake hiyo ya kuwania kuifundisha Taifa Stars pale tu TFF ilipotangaza kuanza mchakato wa kumtafuta kocha mpya, aliwasili katika ofisi za shirikisho hilo majira ya saa 5:30 asubuhi akisindikizwa na katibu mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako.

Akizungumza na Mwananchi mara baada ya kukabidhi barua yake, Papic alisema amefikia uamuzi huo kutokana na kuamini kuwa ana vigezo vyote vinavyomwezesha kuwa kocha wa Taifa Stars.

"Bila shaka niliweka wazi kwamba nitaomba kazi ya kufundisha Taifa Stars na leo nimeleta rasmi maombi yangu hapa kwa kuwa najiamini kutokana na vigezo vilivyotolewa ninavyo,"alisema Mserbia huyo.

Aliongeza kuwa ameshafanya kazi ya kufundisha soka sehemu mbalimbali akiwa na timu kubwa na kuziletea mafanikio, hivyo hana wasiwasi wa kuimudu vema Taifa Stars.

Akizungumzia mustakabali wake na Yanga ikiwa atakabidhiwa nafasi ya kuifundisha Taita Stars, alisema kwa sasa hakuna tatizo hasa kwa kuwa mkataba wake na Yanga unamalizika mwezi Juni na kuongeza kuwa kama atafanikiwa pia anaweza kuwasaidia kutafuta kocha mwingine ikiwa watapenda.

"Mkataba wangu unamalizika Juni hivyo kwa sasa sioni tatizo na kama nitafanikiwa katika hili ninaweza pia kuwasaidia Yanga kutafuta kocha mwingine kama watapenda," alisema Papic maarufu kama Clinton.

Endapo Papic atafanikiwa kuchukua nafasi ya kuinoa Stars, itakuwa zamu ya Yanga kutoa kocha wao kuifundisha timu hiyo ya taifa kwa kuwa mara nyingi makocha wa Stars pindi wanapomaliza mikataba yao ndipo wanaamua kufundisha klabu hiyo ya mtaa wa Jangwani na Twiga.

Makocha waliowahi kuifundisha Taifa Stars na baada ya kumaliza mkataba wao kujiunga na Yanga ni pamoja na Rudi Gutadrf mwaka 1982, Joel Bendera (1986) kwa sasa Naibu Waziri wa Habari na Utamaduni akiwa kocha wa Stars aliombwa kuisaidia klabu hiyo kwenye michuano ya Afrika mashariki na kati. Mwaka 1996, Yanga ilifanikiwa kumnasa Sunday Kayuni aliyekuwa kocha msaidizi wa timu ya Tanzania Bara.

Katika hatua nyingine Papic alisema kuwa maandalizi ya kikosi chake kinachojiandaa na mpambano wa Michuano ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya FC Eloi Limpopo yanaendelea vizuri ingawa ana majeruhi wawili.

"Tupo vizuri ingawa nina majeruhi wawili ambao tayari hawatakuwepo katika kikosi cha Jumamosi, hawa ni Obren Curkovic aliyeumia katika mchezo wetu wa mwisho na Kabongo Honore aliyefanyiwa upasuaji wa goti,ukiondoa hao wengine wako vizuri." "Ninajua itakuwa mechi ngumu siwezi kuwazungumzia sana wapinzani wetu kwa kuwa hata nilipoenda kule walichezesha kikosi cha pili,lakini pia siwezi kuwadharau kwa kutambua timu ile haijacheza mashindano haya kwa miaka mitatu, sasa huwezi kujua watakuja na nguvu kiasi gani, tutakachofanya ni kuwasoma kwanza,"alisema Papic

Huyu jamaa anaweza kazi.
Na kama ataaminiwa na kuachiwa basi Taifa Stars itafika mbaali sana.

Huyu Maximo hana jipya.
Bora arudi alikotoka akaendelee kuchoma chapati.
 
Yanga vs FC Lupopo
FC_Saint_Eloi_Lupopo.jpg

Safari ya wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Klabu Bingwa Afrika - Yanga inaanza leo kwa kupambana na timu ya FC Saint Eloi Lupopo ya DRC kwenye uwanja wa Taifa Dar.


Yanga inatakiwa ishinde mchezo wa leo ili kujiweka katika mazingira katika mchezo wa marudiano utakaopigwa huko Lubumbashi wiki mbili zijazo.

Mchezaji pekee ambaye ni majeruhi kwa upande wa Yanga ni winga Kabongo Honore ambaye alifanyiwa upasuaji wa goti mwanzoni mwa mwaka huu.


Kocha Kostadin Papic anatarajiwa kuteremsha kikosi chake kamili ambacho kimefanya vizuri katika mechi zake tano za mzunguko wa pili wa ligi kuu ya Vodacom. Papic alifunga safari hadi Lubumbashi mwishoni mwa wiki iliyopita ili kusoma mfumo wa uchezaji wa timu hiyo ya DRC.

Kwa upande wao FC Lupopo wanadai wameisoma vizuri Yanga na walituma wawakilishi wao kuja kutazama mechi ya mwisho ya ligi dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo Yanga iliibuka na ushindi wa 3-1.

Tusubiri dakika 90 na kama kawaida tutafahamishana kinachoendelea kutoka uwanja wa Taifa.

Pamoja na kufungwa tunatumai tutawafunga kwao kwa tofauti ya mabao mawili na kusonga mbele pia pateni mipicha ya siku mtanange huo ulipopigwa jumamosi iliyopita...
IMG00267-20100213-1546.jpg
IMG00269-20100213-1608.jpg
IMG00268-20100213-1546.jpg
IMG00262-20100213-1539.jpg
IMG00259-20100213-1538.jpg
IMG00272-20100213-1617.jpg
IMG00272-20100213-1617.jpg
IMG00270-20100213-1610.jpg
IMG00260-20100213-1538.jpg
IMG00264-20100213-1541.jpg
 
picture.php

Sijaona update nyingi za sredi hii tangu Yanga ilipofungwa na SEFC Lupopo, ndo maana nimeamua niweke picha ya mshambuliaji Ntombo Lutete alipokuwa akiipangua ngome ya Yanga. Ni wakati wa majonzi, lakini tusifiche habari kwani kwa mtindo huo hatutajua tulipokosea.
 
picture.php

Sijaona update nyingi za sredi hii tangu Yanga ilipofungwa na SEFC Lupopo, ndo maana nimeamua niweke picha ya mshambuliaji Ntombo Lutete alipokuwa akiipangua ngome ya Yanga. Ni wakati wa majonzi, lakini tusifiche habari kwani kwa mtindo huo hatutajua tulipokosea.

Hili Jukwaa Limelala sana inabidi mara moja moja tuwe tunaingia kuwaamsha akina Balantanda, Gang Chomba na ndugu zao
 
Hili Jukwaa Limelala sana inabidi mara moja moja tuwe tunaingia kuwaamsha akina Balantanda, Gang Chomba na ndugu zao
Huku kumekuwa kuchungu, nimeona Gang Chomba ameanzisha thread ya AC Milan na Man U kule.
 
asalaaam aleykum kandambili wote.... ninawapa pole kwa kuwakosa wakongo lakini nategemea yule beki wa malawi hamtampanga tena..
 
asalaaam aleykum kandambili wote.... ninawapa pole kwa kuwakosa wakongo lakini nategemea yule beki wa malawi hamtampanga tena..
Yule jamaa majeruhi , ila ni beki wa ukweli
 
Back
Top Bottom