Kama kawaida yetu tunaongelea vitu kwa upeo mfupi umeona nilochosema..., Unless Otherwise Viwanda vya ndani ambavyo havipo na quality yake leaves a lot to be desired itapelekea watu kuvaa midabwada (hii sio theory tu it happened hapo nyuma) kwahio sitetei mitumba ila mimi ni muumini wa bottom up approach anza kwanza vutia watu vitu vyako; quality na taste (kuna kipindi watu walipenda kuvaa mavitenge (though they were not cheap) watu wanavaa mitumba sio sababu tu imetoka nje bali quality na uniqueness..., Leo hii dada anauza nyanya kipato chake cha kuunga unga ila akienda mnadani anatoka na kupendeza hata Beyonce haoni ndani..., Kutokana na Economy of Scale ni ngumu kwa nguo ya ndani kushindana na price ya hio mitumba....(we are not there yet) Unaweza ukasema kwanini wanunue cheap na wasinunue za gharama (swali linakuja watu wako wana- sufficient income) ?
Issue sio kuzoea tu issue / fashion ni taste na uniqueness hata huku kuna kipindi watu walikuwa wanavaa nguo saresare; au kule China kuna kipindi cha kufunga mikanda walikuwa wanavaa manguo yao fulani ya kufanana na viatu vya kamba za katani - lakini leo giving them a choice kila mtu anafanya anachofanya (To each their own)
Kwani hata bila kuboreshwa ni baya na unaongelea vazi material au kufunga lubega (hio sio mmasai tu ni kabila nyingi tu) ila nakuuliza hilo vazi la mmasai wakiboresha unadhani litacost kiasi gani kwenye market value kwa viwanda vyetu hivi vinavyotegemea umeme wa Makamba ?
Kumbe hujui midabwada ni nini midabwada ni viraka watu wanakosa pesa za kununua nguo hence wanashona na kuweka viraka..., mafundi viatu watarudi kushona viatu sababu ukinunua kimoja unakibembeleza kisiishe au wote kuvaa Bata na Bora / Sare Sare usiongelee Nike na Adidas au Puma hao wakija huku hakuna pesa (pesa zako za madafu kwao ni hasara)
Unajua hata kabla ya Rambo na vifugashio tulikuwa tunaishi na mifuko ya karatasi (ila ukweli ndio huo hizo plastics ni cheaper) kwahio wakiacha rambo sio kwamba watu wanatumia mifuko mingine ambayo ni expensive ila inawafundisha Reuse (katika ile 3Rs)
Nimekujibu hapo juu mifuko / plastics ni cheaper ndio maana imesambaa sana ila inaharibu mazingira balaa...., ndio maana hata ulaya wanataka kufanya hivyo Ni manufaa kwa mazingira ila ni kipigo kwa mifuko ya watu / Pesa
Usingoje mitumba ipigwe marufuku kuza sekta ya nguo za ndani zikiwa nzuri watu watanunua ni utamaduni..., Uganda watu wanapenda kuvaa nguo za kushona huku nguo za kushona sio kivile (pia quality ni mbovu unavaa nguo mara moja inapauka ikipigwa upepo) hio sio huku tu hata original za China unadhani kwanini kuna watu wanachukua kiatu dukani wanasugua soli chini ionekane ni mtumba, ili wakuuzie kama mtumba ?
Mgeni aje awekeze ili alipwe nini wakati watu wamepigika ? Hivi ushajiuliza kwanini wawekezaji wengi wa vitu ambavyo ni fashion hawaji kuwekeza huku ? Jibu watu hawana buying power.....
Huo ubunifu unasubiri nini . Si wabuni waende kuwauzia diaspora waliopo ulaya ?
Anza ila kuanza sio kwa kupiga siasa anza kwa kuzalisha quality kutoka viwanda vya ndani promote nguo zako ili kina mama Aisha na Mwajuma na Neema wapende kuvaa kitu kutoka Mwatex na sio Mombasa hio ndio njia sahihi sio kulazimisha watu
Unadhani hio pamba yako ukishamaliza kuitengeneza na kuwa-refined kwa umeme huu wa Makamba na ukatoa nguo itakuwa bei gani ? Ushajiuliza kwanini kuna vitu vinatoka ulaya vinakuwa na bei ndogo kuliko vitu vya ndani ? Jibu ni Economy of Scale - Pile it High.., Sell it Cheap.......; Na kama soko lako ni la kuokoteleza volume unazotoa hazitafanya bei iwe chini - Anza kidogo waambie watoto wa shule, wanajeshi n.k. wavae nguo made in Tanzania (ila utashangaa mzazi itabidi atoe mara tatu ya bei aliyokuwa anatoa jana)
Watetezi wa magharibi hamjawahi kosa hoja za kuuendeleza na umagharibi.
Fashion ni propaganda za kimagharibi hakuna la zaidi.
Kadeti ya mwaka 90 wala haina tofauti sana na ya mwaka 2023 ni uongouongo wa kibiashara tu.
Kitambaa cha mchelemchele kuna yofauti gani na hivi vitambaa vya mafuta vya siku hizi ?
Jambo ka pili kupiga marufuku mitumba haina maana kupiga marufiku nguo mpya kutoka nje. Wewe unaemependa fasheni utanunua fasheni mpya au kuagiza duka la mtandaoni.
Ndugu yangu kwenye mitumba kuna fasheni gani? Mitumba si ni fashion iliopitwa na wakati !
Nyerere aliopozuia mitumba ni zama tofauti na leo.
Leo kuna mashine za kiviwabda huitaji mabilioni ya fedha kuvijenga na ndio maana ASIA wameweza kujitosheleza nguo na kuuza nguo dunia nzima.
Kama Malaysia,Thailand , Vietnam nk wameweza sisi tunashindwa nini ?
Unafikiri China iliwainua watu wake ghafla na kwa mpigo kwenda kipato cha kati na juu ?
Tanzania tunatakiwa tuende kwenye vitendo badala ya maneno .
Nakuhakikishia Uganda wala hawata tembea uchi kisa kuzuia mitumba na tutaenda kujifunza kwao miaja si mingi.
China inazalisha nguo kwa bei rahisi sana. Kwa nini tuendelee kuvaa mitumba?
Hayo malonya waliotupa wazungu ni midabwada acha kuyapamba.
Tunavaa mitumba muda mwingine ni kwa sababu ya mazoea na hatutaki kufikiri wenyewe, wazungu wafikiri kwa niaba yetu, mpaka lini.
Wewe na mimi tuchukue hatua ya kubadirika kwanza kifikra, kufanya linaloshindikana liwezekane.
Ifike mwisho sasa kulaumu tu wabna siasa , mbona kina mengi waliweza sisi tunashindwa nini? Kaxi kulaumu laumu tu.
Tulaumu huku tukichukua hatua ktk kika jambo.
Tumekuwa watu wa kulaumu huku tunajua tunaowalaumu hawatabadiri chochote.