Yupi ni kocha bora wa kigeni kuwahi kufundisha ligi ya Bongo?

Yupi ni kocha bora wa kigeni kuwahi kufundisha ligi ya Bongo?

Huyo Edil Silva aliwafundisha 'Samba na Diagonal' Simba ilikuwa ukiwatazama unafurahi na roho yako.
Dah umenikumbusha mbali, hiyo ilikuwa mwaka 1983, Simba ya kina Lilla, Mogella, Malota, Innocent Haule, Mkandawire baada ya kwenda Brazil mwezi mzima pre season wakiwa chini ya kocha Mbrazil Edil Silva, Simba ilirejea imeiva kweli kweli na mechi ya kwanza wakapangiwa CDA wakati huo wanajulikana kama watoto wa nyumbani, moto kweli kweli akina Mgodo, Mgeni, Nyuki, Adolph Kondo, Simfukwe, CDA walilala 2 - 0 lakini walipigiwa diagonal acha mchezo. Wakati huo Rage kiongozi wa Simba alikuwa na rap Manara cha mtoto, lakini hiyo diagonal na baadaye samba zilidumu miezi mitatu tu, Simba ikapoteza mwelekeo, na Silva akaondoka kimya kimya, mwishoni mwa msimu Yanga bingwa.
 
Dah umenikumbusha mbali, hiyo ilikuwa mwaka 1983, Simba ya kina Lilla, Mogella, Malota, Innocent Haule, Mkandawire baada ya kwenda Brazil mwezi mzima pre season wakiwa chini ya kocha Mbrazil Edil Silva, Simba ilirejea imeiva kweli kweli na mechi ya kwanza wakapangiwa CDA wakati huo wanajulikana kama watoto wa nyumbani, moto kweli kweli akina Mgodo, Mgeni, Nyuki, Adolph Kondo, Simfukwe, CDA walilala 2 - 0 lakini walipigiwa diagonal acha mchezo. Wakati huo Rage kiongozi wa Simba alikuwa na rap Manara cha mtoto, lakini hiyo diagonal na baadaye samba zilidumu miezi mitatu tu, Simba ikapoteza mwelekeo, na Silva akaondoka kimya kimya, mwishoni mwa msimu Yanga bingwa.
Silver na msaidizi wake akiitwa Paul Nivo walifundisha Original Diagonal na Samba baada ya kua wamekaa Brazil kwa siku 45

Mechi ya pili baada ya kucheza na CDA walicheza na Tumbaku ya Morogoro Simba wakashinda 3-0

Baada ya hapo kukazuka mgogoro ambao ulianza kuiathiri timu na kupelekea kutoka sare ya bila kufungana na Yanga ya kina Athuman Juma Chama liyokua na wachezaji wengi majeruhi. Mgogoro huo ndio hatimaye ulisababisha makocha hao wakaondoka kurudi kwao Brazil

Mechi ya marudiano na Yanga Lunyasi alichezea kichapo cha kama sio 1-0 basi ni 3-0 na Yanga wakanyakua ndoo mwaka huo

Lakini kikosi hicho kilikaa pamoja kwa muda mrefu na mwaka unaofuata yaani 1984 Simba walifanya vizuri katika mashindano ya CECAFA yaliyofanyika Khartom na kutolewa na AFC Leopards ya Kenya kwenye nusu fainali, na hata kwenye Klabu bingwa Afrika Simba walitingisha kwa kuichapa Nationa Al Ahly ya Misri 2-1 pale CCM Kirumba Mwanza kwa mabao ya Mogella na Mtemi Tamadhani
 
Nabby Camara alikuwa kocha aliyetengeneza defense ya SSC iliyokaa zaidi ya miaka 5 wakati huo Yanga ikiwa na forward kali iliyotengenezwa na Tambwe Leya . Hawa walikuja fukuzwa nchini kwa repatriation ya saa 24 na serikali , then Simba walipata wabrazil Edil da Silva nadhani walipata kocha bora kabisa wakamtimua baada ya kushindwana itikadi
Yanga walikuwa na Tambwe na pia Shungu wakiwa makocha wazuri mno huku mtangulizi wao Victor Stanslous akiwa kinara
Victor stantclaus, Tambwe Leya,Raul Shungu,Rudi Guntendorf, Micho, Plujim(Yanga),/Nabi Camara,Samsorov,Edil Silva, Popadi, Sianga, Patrick Phiri,Omog, Lenchentre na Patrick Aussem( Simba)
 
Shida ilikuwa kamati ya ufundi hakuikubali
Dah umenikumbusha mbali, hiyo ilikuwa mwaka 1983, Simba ya kina Lilla, Mogella, Malota, Innocent Haule, Mkandawire baada ya kwenda Brazil mwezi mzima pre season wakiwa chini ya kocha Mbrazil Edil Silva, Simba ilirejea imeiva kweli kweli na mechi ya kwanza wakapangiwa CDA wakati huo wanajulikana kama watoto wa nyumbani, moto kweli kweli akina Mgodo, Mgeni, Nyuki, Adolph Kondo, Simfukwe, CDA walilala 2 - 0 lakini walipigiwa diagonal acha mchezo. Wakati huo Rage kiongozi wa Simba alikuwa na rap Manara cha mtoto, lakini hiyo diagonal na baadaye samba zilidumu miezi mitatu tu, Simba ikapoteza mwelekeo, na Silva akaondoka kimya kimya, mwishoni mwa msimu Yanga bingwa.
 
Kama wana Yanga wamemsahau Prof Dusan Condic basi atakuwa hawana shukrani.

Huyu mchawi wa kiserbia ndiyo aliyekuja kuwapa Yanga ubingwa baada ya kuukosa Miaka mingi mfululizo.

Lakini huyu jamaa ndiye aliyekuja kuufuta uteja wa Yanga kwa Simba uliodumu kwa miaka 12 mfululizo.

Kumbukeni kikosi cha Yanga cha kina
Obren cirkovic
Ivo Mapunda
Shadrack Nsajigwa
Godfrey Bonny
Rashid Gumbo
Wisdom ndlovu
James chilaponda
Credo mwaipopo
Fred Mbuna
Shamte Ally
Nabir cannavaro
Boniface Ambani
George Owino
John Baraza
Edwin Bukenya
Athuman Idd chuji
Gaudence mwaikimba
Ndiyo nilikuwa kikosi Bora kabisa cha Yanga cha karne ya 21.

Tuweke kumbukumbu sawa sawa Zahera hajafikia hata mafanikio ya Sam Timbe au Hans Van del pluijm.
 
My list
1 James Siang'a
2 Patrick Aussems
3 Hans van De pluijm
4 Stewart John Hall
5 Milovan Cirkovic
6 Patrick Phiri
7 Milutin Micho
8 Dragan Popadic
9 Raul Shungu
10 Dusan Condic
11 Tom Olaba
12 pierre Lechantre
13 Sam Timbe
14 Mario's Omog
15 Jack Chamangwana
16 Tambwe Leya
17 George Lwandamina
18 Clasmir Berzinsk
19 Moses Basena
20 Masoud Djuma.
Nikipima kwa vigezk vya mafanikio
James siang'a na Patric Ausesm kwa upande wa vilabu wao ni bora..!

kwa timu ya Taifa Amunike kufuzu Afcon...!

Nje ya hapo ni upenzi tu...lakin hakuna kocha aliefikia level hizo.!
 
Afu hakuwa kocha wa football, alijishughulisha na Netball

Mkuu huyo alikua mkurugenzi msaidizi wa michezo wizara ya habari utamaduni na michezo, alifariki lini? Alikua chini ya Leonard Thadeyo
 
Kocha bora hupimwa na mafanikio yake, hebu tuache kujibu maswali kama wanafunzi wa shule za msingi, unapotaja kocha fulani ni bora, utaje na mafanikio yake, hapo ndipo utastahili kujiona GT na kujitofautisha na wale wa shule za msingi.

Kwangu kocha bora wa kigeni ni James Siang'a ambaye aliifikisha Simba fainali ya kombe la Shirikisho la CAF. Anayefuatia ni Patrick Aussems ambaye aliifikisha Simba robo fainali ya Ligi ya Mabingwa ya CAF.

Huyu papa Zahera, tumpe muda maana ndio anaanza safari kwenye kombe la mabingwa is CAF.


Vv

Hiyo fainali mlicheza na nani? Acheni kuropoka muwe mnauliza
 
Back
Top Bottom