Zaidi ya KM 2000 za barabara kuanza kujengwa kwa mtindo wa EPC +F. Serikali yasema hazitalipiwa Tozo

Hapo Masasi,Nachingwea-,Liwale wangeunganisha na Nangurukulu ingeleta maana kubwa sana..kuishia Liwale sioni kama itasaidia kitu..bado itakuwa hujafungua huo ukanda.
Au ingeanzia Nangurukulu,Liwale Nachingwea- kwa maana kipande cha Nachingwea- Masasi ni kifupi na angalau kinapitika.
 
Luhaga Mpina ana roho mbaya na unyonge mwingi wa nafsi. Anajua kuwa anao wafuasi na hata akiandika upupu atapata tu wa kumuunga mkono.

Hawa ndio wacheleweshaji wenyewe wa maendeleo halisi.
 
Wamekusikia watakufikia
 
Yaani yule Mwehu aliwaweza aisee Kwa propaganda mliiva haswaaa 😁😁😁

Ni vile wengi wenu mkisafiri sana mnaishia Gongo la Mboto 🤪🤪

Sasa angekuwa amejenga zote hizo Tzn yote si ingekuwa Ina lami Sasa manaa kati ya hizo Barabara ulizotaja nusu ni vumi,robo zilikamiloka kipindi Cha Kikwete na kiasi kilichosalia ni Barabara alijojenga hazikuzisi km 2500 Kwa miaka 5 ya Uongozi wake.

Yaani wadanganye wengine Mimi nazunguka Tzn hii nazijua hizo Barabara karibu zote.
 
Mbarawa siyo wa kumuamini. Kama kauza Bandari unadhani anashindwa kubadili gia angani?
 
iv) Barabara ya Igawa – Songwe – Tunduma (njia nne) (km 237.9) inapita katika Mikoa ya Mbeya na Songwe na inapita katika Majimbo ya Mbarali, Mbeya Vijijini, Mbeya Mjini, Mbozi, Vwawa na Tunduma;

Katika zote hizo, hii iwe ya kwanza kujengwa....

Katika barabara yote ya Tanzam, hiki ndio kipande kibovu kuliko vyote na ni lami ya miaka mingi mno...
 

Ukweli lazima usemwe.

Serikali iliyoko madarakani imetimiza zaidi ya miaka 2, lakini ilichoweza kufanya ni kuendeleza, tena kwa kuchelewesha, miradi ya Awamu iliyopita (SGR, Bwawa la Nyerere, Daraja la Tanzanite, Daraja la Busisi, Kuboresha shule kongwe, Zahanati, Vituo vya afya, barabara kuu km upanuzi wa barabara kutoka Ubungo kwa njia 4, nk). Ucheleweshaji huo hautokani na kukosekana fedha, la hasha, kwani hii Serikali ilipoingia madarakani imeweka tozo kibao, kukopa kwa wingi na misaada kibao.

Hivyo tutegemee mwendelezo wa ahadi hewa za maneno matamu (KAZI IENDELEE) huku viongozi wakijipendekeza na kutoa sifa, mwanzo mwisho, kwa mamlaka ya uteuzi wao.

Matokeo yake, tunashuhudia utayarishaji wa mikataba ya ulaghai na ufisadi (mfano ni wa Bandari - IGA, na hii ya barabara - EPC+F). Maana yake Serikali inakiri kuwa haina viongozi wa kufikiri kutumia, wataalamu wetu wenyewe na utajiri wa maliasili tulio nao, ila kuwakaribisha wageni, kwa kile inachokiita "Demokrasia ya Uchumi".

Hakika ANAUPIGA MWINGI
 
Katika zote hizo, hii iwe ya kwanza kujengwa....

Katika barabara yote ya Tanzam, hiki ndio kipande kibovu kuliko vyote na ni lami ya miaka mingi mno...
Zote zitajengwa Kwa pamoja na zote zinatakiwa Kukamilika 2027 japo Kuna nyingine xitawahi
 
Makampuni yote ni ya China.
Ina maana hakuna local engineering company ya kuweza kujenga barabara?

Huu ni uhuni na uhaini kabisa.
Siyo local tu, yaani hakuna wakandarasi kutoka nchi nyingine zaidi ya China tu?
 
Makampuni yote ni ya China.
Ina maana hakuna local engineering company ya kuweza kujenga barabara?

Huu ni uhuni na uhaini kabisa.

..mkandarasi ndiye anayesanifu, kutafuta fedha, na kujenga.

..serikali inakabidhiwa mradi ukiwa umekamilika na kumlipa mkandarasI.

..Nadhani hii ni sawa na kumkopa mkandarasi badala ya kukopa benki.

..kwa hiyo utaona ugumu wa wakandarasi wa Tanzania kushiriki. Labda kutakuwa na kazi za SUB-CONTRACTORS.
 

Ile ya Morogoro Songea nayo ipo?
 
Mtu yeyote aliyewahi kutumbuliwa na JPM ujue ana walakini.

..wakandarasi ni Wachina peke yao.

..mimi ninachotaka ufafanuzi ni terms za MKOPO wa ujenzi.

..utaratibu unaotumika ni wa kumkopa MKANDARASI badala ya kukopa BENKI.

..Je, tuko salama kiasi gani?


..Je, ina maana tumekopa sana, sasa tunayakwepa mabenki?

Cc Wo shi niubi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…